Chahali na Uenyekiti wa Mbowe CHADEMA

Chahali na Uenyekiti wa Mbowe CHADEMA

Unazungumzia kipindi tumetoka kupata uhuru nionavyo mimi b4 tanzania ikombolewe ikombolewe kwanza chadema kutoka mikononi mwa familia kiwe chama huru cha wanachama
Isiishie hapo tu! kuwa huru, namaanisha kutoka SACCOS ya familia ya kaskazini hadi chama cha siasa!
Je kunatofauti yoyote ya ile benki ya Kilimanjaro iliyofungiwa na hii saccos inayojiita chama cha siasa?
 
Kukalia madaraka kwa muda mrefu kama anavyofanya Mbowe si sahihi kwenye zama hizi ambazo Demokrasia inapiganiwa nchini Tanzania.ni kweli kuwa Mbowe amefanya mageuzi makubwa ndani ya chama hicho, lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya yeye kuwa mwenyekiti wa maisha. Chadema ni taasisi, tunaamini ndani ya chadema kuna watu wengi wenye uwezo wa kufanya mageuzi zaidi ili kuipeleka mbele zaidi chadema
 
Isiishie hapo tu! kuwa huru, namaanisha kutoka SACCOS ya familia ya kaskazini hadi chama cha siasa!
Je kunatofauti yoyote ya ile benki ya Kilimanjaro iliyofungiwa na hii saccos inayojiita chama cha siasa?
Sioni tofauti mkuu sasa naona wanajaribu kumbadilisha kenge kuwa samaki kwamba keshotoka nchi kavu kaingia majini kwamba haruhusiwi tena kutoka majini vinginevyo amuone papa ampe viza
 
Billicanas hajaporwa ni kujigeuzia mali ya umma kuwa ya kwake kwa kutegemea huruma za wananchi! Eti Mwenyekiti afu hutaki lipa kodi!
Suala la kujichukulia maamuzi ya kulima kwenye catchment area siliungi mkono hata kidogo.
Suala la muundo wa upatikanaji kiongozi lisikupe shaka ni desturi ya chama kupokezana vijiti kila ufikapo ukomo wa uongozi na inafahamika hivyo na iko wazi katika katiba ya chama!

HOJA: Niambie uongozi wa CHADEMA katika nafasi ya uenyekiti ni miaka mingapi mingapi kwa muhula mmoja?
Ni lini amewahi itisha hata uchaguzi wa uongo uongo ili mpige kura ya kuchagua au kupendekeza mwenyekiti?
NI muundo upi wa demokrasia unayoizungumzia mliyoitumia kumpitisha LOWASA kuwa mgombea wenu wa uraisi kupitia CHADEMA na UKAWA kwa ujumla?
Tuwekee hapa kipengele cha katiba ya ccm kinachoruhusu uhuni huu wa kutokuwa na uchaguzi wa ushindani ndani ya ccm ngazi ya Taifa.

Pili tueleze Mtuliabna Dr Mollel ni lini walichukuwa fomu zankuomba kugombea ubunge na lini kura za maoni zilipigwa na ni lini kikao cha kamati kuu ya ccm kilikaa kufanya uteuzi?

Na kwenye chama hakuna kitu kinachoitwa utamaduni, chama kinaendeshwa kwa katiba na kanuni zake.

Upuuzi huu wa utamaduni waeleze mazuzu wenzako wanaotumia tumbo kufikiri ambao wanawahubiria vijana kujiajiri wakati wao wenyewe ni majobles wanaishi kwa kitegemea kujipendekeza uvccm ili wapate posho na ukatibu wa wilaya.
 
Bora huyo, ila kuna yule mnyama mwenda pole, siku asipokuwepo kanisani basi waumini hupata mahubiri kupitia runinga hana msaidizi wake wa kutoa neno kanisani yeye ndo Alfa na Omega (nisikiavyo mtaani)
Hahahaa....... Umenikumbusha Zitto " alipoutamani" uenyekiti pale Ufipa kilichomkuta hatakaa asahau!!
 
Mrema, Lipumba, Cheyo na Mbatia mwenyeviti toka mimi sijaanza la kwanza mpaka leo nimekuwa babu, mbona hamuwasemi? shame on you

Kutokana na tatizo hilo hilo la uenyekiti wa milele ndio maana vyama hivyo vimebakia na bendera zao tu watanzania waliokuwepo huko wengi wameenda chadema. Sasa wanapokuta ugonjwa lie ule uliowaua marehemu wale wengine wasiseme?

Angalau huku ni chama cha demokrasia na maendeleo vingine vile ni vyama vya wananchi, labour na mageuzi. Angalau demokrasia ionekane basi na si demokrasia ya kutembea na yeyote umpendae, demokrasia ya kubadilisha uongozi ili mgonjwa asife na ugonjwa ule ule! Tujifunze kwa makosa yetu wenyewe
 
"Kirefu cha CHADEMA ni Chama cha DEMOKRASIA na Maendeleo. Sasa ni demokrasia gani hiyo ambayo inaruhusu mwenyekiti mmoja kuwa madarakani milele? What if “uenyekiti wa milele” ni miongoni mwa vikwazo kwa maendeleo ya chama hicho?" Evarist Chahali
Jamani kwani Mbowe ni mwenyekiti wa CCM? Mbona roho zinawauma sana??
Mbowe is there to stay forever.
 
Mshana unalidhika na muda wa mwenyekiti mamlakani?, ni Kweli Mbowe si kikwazo kwa maendeleo ya chadema Kwa sasa?, du!
Samahani mkuu,naomba tu nimjibie shemeji mshana. Asiporidhika labda akapewa yeye ataweza?
 
Isiishie hapo tu! kuwa huru, namaanisha kutoka SACCOS ya familia ya kaskazini hadi chama cha siasa!
Je kunatofauti yoyote ya ile benki ya Kilimanjaro iliyofungiwa na hii saccos inayojiita chama cha siasa?
Na hiyo CCM ni Kikoba cha usukumani au?
 
Kuna watu wengine Akili zao zinawatosha wenyewe mimi nilidhani wangemwaga Povu kwa ccm kutawala kwa mkono wa Chuma tangu Uhuru
Kumbe hiyo kwao sio Shida ni Mwenyekiti wa Chama duh...
Charity begins at home mkuu, wala hajakosea...
 
Mwwnyekiti wa kwanza wa Chadema ni Edwin Mtei, Mwenyekiti wa pili ni Bob Makani, Mwenyekiti wa tatu ni Freeman Mbowe na ndiye mwenyekiti mwenye mafaniko zaidi ya wote, ni kwa nini huyu anawanyima usingizi?

Mmepora Billicanas hajaunga mkono juhudi za Magufuli, mmeharibu green house yake Hai bado hataki kuunga mkono juhudi za Magufuli sasa mnaingilia hata maamuzi ya chama chake, je mmewahi kuwauliza ccm ni kwa nini haifanyi uchaguzi kupata uongozi wa ngazi ya Taifa? Au yale maigizo yanayofanyika Dodoma ya mgombea mmoja kupata 100% kwa 100% ndio uchaguzi? Ni lini ccm itajifunza kwa ANC jinsi inavyoendesha chaguzi za kweli na za wanachama kushindana kugombea uongozi?

wanampora mpaka wabunge!
 
Back
Top Bottom