Chahali na Uenyekiti wa Mbowe CHADEMA

Chahali na Uenyekiti wa Mbowe CHADEMA

"Kirefu cha CHADEMA ni Chama cha DEMOKRASIA na Maendeleo. Sasa ni demokrasia gani hiyo ambayo inaruhusu mwenyekiti mmoja kuwa madarakani milele? What if “uenyekiti wa milele” ni miongoni mwa vikwazo kwa maendeleo ya chama hicho?" Evarist Chahali
Mwwnyekiti wa kwanza wa Chadema ni Edwin Mtei, Mwenyekiti wa pili ni Bob Makani, Mwenyekiti wa tatu ni Freeman Mbowe na ndiye mwenyekiti mwenye mafaniko zaidi ya wote, ni kwa nini huyu anawanyima usingizi?

Mmepora Billicanas hajaunga mkono juhudi za Magufuli, mmeharibu green house yake Hai bado hataki kuunga mkono juhudi za Magufuli sasa mnaingilia hata maamuzi ya chama chake, je mmewahi kuwauliza ccm ni kwa nini haifanyi uchaguzi kupata uongozi wa ngazi ya Taifa? Au yale maigizo yanayofanyika Dodoma ya mgombea mmoja kupata 100% kwa 100% ndio uchaguzi? Ni lini ccm itajifunza kwa ANC jinsi inavyoendesha chaguzi za kweli na za wanachama kushindana kugombea uongozi?
Mshana unalidhika na muda wa mwenyekiti mamlakani?, ni Kweli Mbowe si kikwazo kwa maendeleo ya chadema Kwa sasa?, du!
 
"Kirefu cha CHADEMA ni Chama cha DEMOKRASIA na Maendeleo. Sasa ni demokrasia gani hiyo ambayo inaruhusu mwenyekiti mmoja kuwa madarakani milele? What if “uenyekiti wa milele” ni miongoni mwa vikwazo kwa maendeleo ya chama hicho?" Evarist Chahali
Chadema ni kama kanisa la kilokole, mwenye kanisa ndio askofu wa maisha. Kwa mfano unamtofautishaje Mbowe na Gwajima?!......wote ni viongozi wa kudumu!
 
Mwwnyekiti wa kwanza wa Chadema ni Edwin Mtei, Mwenyekiti wa pili ni Bob Makani, Mwenyekiti wa tatu ni Freeman Mbowe na ndiye mwenyekiti mwenye mafaniko zaidi ya wote, ni kwa nini huyu anawanyima usingizi?

Mmepora Billicanas hajaunga mkono juhudi za Magufuli, mmeharibu green house yake Hai bado hataki kuunga mkono juhudi za Magufuli sasa mnaingilia hata maamuzi ya chama chake, je mmewahi kuwauliza ccm ni kwa nini haifanyi uchaguzi kupata uongozi wa ngazi ya Taifa? Au yale maigizo yanayofanyika Dodoma ya mgombea mmoja kupata 100% kwa 100% ndio uchaguzi? Ni lini ccm itajifunza kwa ANC jinsi inavyoendesha chaguzi za kweli na za wanachama kushindana kugombea uongozi?
Billicanas hajaporwa ni kujigeuzia mali ya umma kuwa ya kwake kwa kutegemea huruma za wananchi! Eti Mwenyekiti afu hutaki lipa kodi!
Suala la kujichukulia maamuzi ya kulima kwenye catchment area siliungi mkono hata kidogo.
Suala la muundo wa upatikanaji kiongozi lisikupe shaka ni desturi ya chama kupokezana vijiti kila ufikapo ukomo wa uongozi na inafahamika hivyo na iko wazi katika katiba ya chama!

HOJA: Niambie uongozi wa CHADEMA katika nafasi ya uenyekiti ni miaka mingapi mingapi kwa muhula mmoja?
Ni lini amewahi itisha hata uchaguzi wa uongo uongo ili mpige kura ya kuchagua au kupendekeza mwenyekiti?
NI muundo upi wa demokrasia unayoizungumzia mliyoitumia kumpitisha LOWASA kuwa mgombea wenu wa uraisi kupitia CHADEMA na UKAWA kwa ujumla?
 
Mbowe kawashika pabaya sana.. Amekuwa mbigili kali kwao hivyo mizengwe haitisha

Tatizo la kushabikia kuabudu watu badala ya kuimarisha na kujenga imani katika mfumo kutatufikisha mbali sana, maana tutabadilishia gia angani kila kukicha hatimae tutatalii dunia nzima na lengo letu la kuzurura zurura litatimia.
 
Mrema, Lipumba, Cheyo na Mbatia mwenyeviti toka mimi sijaanza la kwanza mpaka leo nimekuwa babu, mbona hamuwasemi? shame on you
Kwa hiyo kwa kuwa Vyama vingine vimefanya makosa na nini mmehalalisha? Mbona hivyo Vyama vinapoisifia CCM nyie mnaviita vibaraka hadi mnataka kumtoa roho kipenzi cha wanamageuzi waliojaa huko eti tu kamsifia the real and only one @MagufuliJP?
 
Chadema ni kama kanisa la kilokole, mwenye kanisa ndio askofu wa maisha. Kwa mfano unamtofautishaje Mbowe na Gwajima?!......wote ni viongozi wa kudumu!
Bora huyo, ila kuna yule mnyama mwenda pole, siku asipokuwepo kanisani basi waumini hupata mahubiri kupitia runinga hana msaidizi wake wa kutoa neno kanisani yeye ndo Alfa na Omega (nisikiavyo mtaani)
 
Kuna watu wengine Akili zao zinawatosha wenyewe mimi nilidhani wangemwaga Povu kwa ccm kutawala kwa mkono wa Chuma tangu Uhuru
Kumbe hiyo kwao sio Shida ni Mwenyekiti wa Chama duh...
Sijui kwanini, wanadili na chama cha siasa kisichowaho kushika madaraka. Sijui ni upofu au? Lakini babu yangu aliniambia, ukiona unasifiwa ujue una kasolo.
 
Back
Top Bottom