Chagulani: Wenje ni chanzo cha migogoro Mwanza

Siyo kazi ya Chadema kujenga chochote maana hiyo ni kazi ya serikali iliyoko madarakani. Uongozi wa chadema mwanza ni wa kisiasa tu ila maendeleo yanaletwa na serikali iliyoko madarakani. Magamba wanavuruga halmashauri za chadema wakidhani kuwa watapata kura 2015 kumbe ndo wanapoteza zaidi. Nenda kamuulize mtoto wa mkulima kilichomtokea MZ kama anahamu hata ya kurudi kule kuomba kura 2015. Hata kama wananchi watakosa maendeleo kwa ukandamizaji wa kimagamba kisa halimashauri zile zinaongozwa na chadema bado hawawezi kurudisha ccm tena! Nenda Arusha, Moshi,mbeya kama na kote ambako watu walisha ng'oa ccm kaulize kama wa na juta kwa uamuzi huo? ni bora kukaa bila maendeleo kuliko kuongozwa na ccm!

Kazi ya Chadema ni nini ufisadi na madiwani kuuziana viwanja na kutafuna ruzuku? ebu jiulize kwa nini Meya wa Chadema alivuliwa cheo chake.
 
Tatizo wa bongo mgao Kama haujaenda vizuri lazima makelele yatasikika
 
Tatizo wa bongo mgao Kama haujaenda vizuri lazima makelele yatasikika
"Majugu si Mtaji"
Nilipofika mwz nilishauriwa kupima sana marafiki wa kuwa nao, kwani ni mkoa wenye majungu sana.Hapo awali sikuliona hilo lakini muda unavyokwenda nazidi kuamini.Vijiwe vya Majungu mwanza viko,Mwanza Institute, Shooters, Kirumba Resort.(Hiki cha Kirumba resort kinabeba wana ccm wengi hasa Vijana,Shooters kinabeba wachezaji wastaafu na vijana wapenda mpira na pamoja na wanaccm-kwa mtizamo wangu,Mwanza Institute hiki ni mchanganyiko wa vijana -madreva taxi,wafanyakazi, wafanya biashara na baadhi ya wafanyakazi, ijapokua kimechoka kidogo siku hizi.Hivyo ni vijiwe ambavyo ukipita tu,ushafahamika.Nilifika Mwanza siku ya kwanza usiku nikapelekwa na mwenyeji wangu Villa.Kesho kutwa yake niliporipoti ofcn kujitambulisha kwa boss ,akaniambia umeonekana viwanja kadhaa vya jijini mwz.I was surprised.

back to Ulingo wa siasa,habari za Wenje kutokushinda 2015,ukipita kwenye hivi vijiwe utazipata, kwa mara ya kwanza nilizipata, Ile siku CCM walipobeba watu kwa Malori kusherehekea kuzaliwa kwao,maana tulipata msosi katika kijiwe cha Shooters.lakini ukijaribu kuangalia kiini hasa cha kulaumiwa hukipati zaidi ya kusema ,siku hizi anafanya biashara za kwenda nje ya nchi,mara alishinda kwa ajili tu ya kupata mtaji hata yeye anajua na mengine mengi.

Nilichojifunza ni hawa madiwani wawili, walikua wakijitahidi kumpiga sana majungu huyu bwana kwa kushirikiana na madiwani wa CCM.Niliwahi kuandika humu ndani siku moja nilipokutana na huyo diwani kwa mara ya kwanza,akiwa na dogo mmoja aliyetambulishwa kwangu kama katibu wa Chacha Wangwe R.I.P, na walikua na jamaa mwingine ambaye ni mwl.Adam naye alijitambulisha kama mwalimu wa shule ya Nganza.walipiga majungu kuhusiana na uongzi wa CDM.

Juzi usiku hawamadiwani walikua katika hotel ya Sparrow Ghana, wakamwita rafiki yangu niliyekua naye kwa furaha huku Adam akimwambia huyo rafiki yangu," Umeona Highness alivyo jificha chini ya meza?" huyo rafiki akamwambia sikuona,akamwambia hujaona taarifa ya habari?wakati huo walikua wakiongea na yule mmiliki wa hiyo hotel.Nikajaribu kuunganisha Dots zangu, mmiliki huyo wa hotel kwa redio mbao ni rafiki wa Ritz1 ,alifahamiana naye kupitia kuunganishwa na jamaa wa Villa Park.Na pale hotel walikua wakiongelea kuhusiana na hayo mambo ya kisiasa, kwa hiyo ni ka hisi kuna uwezekano haya mambo yanafanyika kwa kusaidiwa na watu fulani.

Kwa ujumla hawa watu hawafai.Nilipenda kauli ya CDM ilikua very straight kwamba ,wamefukuzwa kwa kwa kukihujumu chama,hilo nilikubaliana nalo na nikaamini CDM wanapata taarifa sahihi.

lengo langu ni kuwafahamisha wana jf kuwa siasa za mwanza ziko kimajungu majungu sana, hivyo muwe makini sana mnapopata taarifa za mwz wakati wa kuzijadili.
 
Ni mtu mjinga pekee anayeweza kumlamu Wenje.Wenje ni Katapila linaloangusha vibaraka wote wa ufisadi.

umeona jina na cheo/wadhifa wa alieandika hii?ana akili kuliko wewe na ana madaraka ya juu hapa mkoani,sasa wewe unaongea kutoka wapi?
 
Chadema wameonyesha udhaifu wa hali ya juu katika masuala ya utawala katika Jiji la Mwanza, wakazi wa Mwanza waliwapa kura kwa imani mtaijenga Mwanza kinyume chake ni ufisadi tu na vita vya kugombea madaraka.

Haijalishi lakini siyo ccm, imetosha ccm afadhali hata fisi au jiwe
 
Chagulani kaa utulie ili upate busara ya kufanya maamuzi yenye faida kwa ajili ya mustakabali wako wa kisiasa. Leo hii ndio unapata akili ya kumuandikia mwenyekiti malalamiko haya wakati ulipewa kila nafsi ya kuyasema lakini hukuweza.

Hii tabia ya kudhani kwamba unaweza ukagain political popularity kwa kumshambulia Wenje haitakusaidia kamwe. Alishindwa Masha utaweza wewe mtoto mdogo ambae bado unajifundisha siasa. Hao watu wa ccm wanaokudanganya wanakupoteza na mwisho wako kisiasa hauko mbali kama hautobadilika. Zile siasa za vyuoni zilishakwisha ni wengi tulizifanya lakini tulipofika mtaani tukaswitch kuendana na hali halisi ya maisha na siasa za nchi hii.

Na mwanachadema yeyote anayeshabikia huu upuuzi wa chagulani atambue kwamba hatutamuonea haya katu, lazima atawajibika kwa matendo yake.

Mbona wewe uliuza jimbo la tarime na bado tumekuacha ndani ya chama na sasa umekuwa kuhadi wa slaa.
 
umeona jina na cheo/wadhifa wa alieandika hii?ana akili kuliko wewe na ana madaraka ya juu hapa mkoani,sasa wewe unaongea kutoka wapi?

Molemo ni mkurugenzi wa halmashauri na bunge pale makao makuu cdm lakini hana uongozi wowote zaidi ya ukabila na kubebwa na mbowe.
Na anatabia ya kupiga mizinga wabunge na nazani atakuwa kampiga sana mizinga wenje kwa hio analipa fadhila.
 
chanzo cha Migogoro ni wewe mwenyewe na kujua kwako kwingi.. unapong'ang'ania kumtoa MEYA so what? badala ya kufind solution within chama u ar comming JF
 
mwanza wanajuta kumchagua wenje,ni mlafi.mroho wa madaraka,na mla rushwa mkubwasana,anajifanya kama watu wote wa mwanza kawaweka kiganjani kwake,asitarajie kabisa kupata tena kura mwanza labda akagombee ubunge kwao ujaluoni kenya,watu wamechoka na usanii na utapeliwake,hakuna ahadi hata moja aliyotekeleza,kaiba hela zamadawati 78milioni na ushahidi upo,hata matata kasema,wenje kupata tena ubunge nyamagana ni sawa na nguruwe kuingia msikitini,amalizie utapeliwake aondoke,mwanza wanajuta kuchagua muhuni na tapeli.

nyie vijana mliokosa vyeo CDM mna shida sana na hampati kitu pumbavu nyie.
 
Wewe lazima amekutuma umtete humu, mwanza walimchagua baada ya kuona udhaifu wa masha na hawakua na choice nyingine. Huyu kijana alianza kwa kasi lakini na yeye ametulizwa, hizi hadithi za kusema alipewa mamilioni anazo wahadithia ziko kichwani kwake tu. 2015 huyu dogo ni miguu juu. Hapati ubunge Mwanza.

Kwa sababu wewe ndiye unaetoa ubunge Mwanza?
 
Wewe endelea kuendekaza upambe kwa Dr Slaa na Mbowe, Wenje hana nafasi tena ya kuwa mbunge wa Nyamagana, eti Chagulani mtoto mdogo hawezi kushinda na Wenje, muulize Wenje, zipo wapi Milioni 78 za madawati walizochanga wakazi wa Mwanza, safari hii wakazi wa Mwanza wanataka Mbunge mzawa, Msukuma mwana Mwanza, Wenje akagombee kwao Kenya.
na ushahidi upo,wenje kaiba pesa za walalahoi milion 78 walizochangishwa pale sahara,kama ana ubavu aje akanushe tumuumbue,watu wana data na ushahidi kamili,huyu ni tapeli tu aende kwao kenya akafanye utapeli huko kwa mwanza wamemshtukia ana tamaa kuliko fisi.akipata tena ubunge mje mnikate kichwa changu hadharani,mwanza wanajuta tena sana,pita mitaa yamwanza uwaskie wana mwanza wanavomkandia wenje tapeli waliokua hawajamjua wakampa kura.
 
MUSTAKABALI WA CHADEMA MWANZA.
- Waswahili hunena, ”ukikosea fomula hakika jibu sahihi halipatikani” Wana Mwanza kwa pamoja tunawapongeza ninyi binafsi na Kamati kuu ya chama kwa kuhakikisha ya kuwa chama kinaendeshwa katika misingi inayokubalika kwa mujibu wa katiba ya chama toleo la mwaka 2006, mmefanya maamuzi magumu ambayo hayakutegemewa, yalikuwa magumu lakini yenye maslahi kwa chama na taifa kwa ujumla. Wafuasi watano Yuda Iskariote waliokuwa Arusha walipata hukumu ya haki. HERI HAMSINI NZIMA KULIKO MIA MBOVU.

MADIWANI NA WABUNGE WETU
- Mara nyingi donda lililo kichwani muuguzi wake huwa ni mkono ikumbukwe yakuwa tarehe 21/01/2011 viwanja vya furahisha katibu mkuu alitamka ya kwamba, atawasimamia Madiwani wetu wa jiji la Mwanza kuhakikisha yakuwa wananchi waone tofauti ya utawala wa kisanii na utawala makini. - Pia ikumbukwe kuwa kabla ya chadema kushinda Mwanza tulikuwa tukisema mambo kama Tarime & Karatu, kesho tulitegemea tuseme mabo kama Mwanza tukifika Sengerema, Buchosa, Sumve, Kwimba & Magu.

Takribani sasa Mwaka unakatika wa wawakilishi wetu hawa hawana sauti moja, chakushangaza na kusikitisha zaidi wamepitia mgongo wa watu wengine kushika “Tender” za Halimashauri ya Jiji! Watahoji nini? Watu kunena wana Mwanza hawakuifukuza CCM jijini Mwanza kama mlaji wa zamani, na wala hawakuichagua chadema kama mlaji mpya!

Bali walihitaji mabadiliko ya kivitendo na wala si ya kinadharia. Huenda makamanda mtashtuka kusikia maneno haya, hata kama chungu tunywe kwa kuwa inatibu. Mabadaliko Mwanza bado hayajaja kwa kuwa wawikilishi wetu hawa wanatenda kimazoea wakiongozwa na hisia zao binafsi zaidi kuliko ilani ya chadema waliyokuwa wakiinadi majukwaani. Wawakilishi wetu hawa hawana sauti moja, kila mmoja anatafuta umaarufu binafsi wamekisahau chama. makamanda wakalisheni kitako waseme tatizo ni nini?

Kwanini wavutane na kulumbana wao kwa wao?wamesahu ya kuwa vita ya panzi ni furaha kwa kunguru? Kwanini hawa wasusie kikao cha baraza la Madiwani? Na kwanini hao wabaki? kajua ndo haka.
- Tusipouanika mapema, itatulazimu tuutwange mbichi. Siku 340 wametenda au kubadilisha lipi Mwanza?

Wakati ndani ya siku mia moja mgombea urais (Dr. Slaa) alikuwa ametuahidi makuu likiwemo suala tete kwa sasa la katiba mpya!
- Mbunge aliahidi ada na stahili za wanafunzi, lakini kwa leo wanafunzi na wazazi wanadaiwa madawati. Mpango wa kuomba kibali kukata miti Misitu ya Kigoma kupitia kwa wadau wa chama waliopo Jijini Mwanza wanaofahamiana na Dr. Felician Kilahama mpaka leo hii Mbunge huyu bado hajalifanyia kazi, wakati uwezekano wa kumaliza tatizo hilo lipo. Mbunge huyu wa Nyamagana haambiliki. Watoto hawa 905 anaowasomesha Rushwa imetembezwa hadharani na wafanyakazi wa ofisi yake, wengi wao hawatoki mazingira magumu na wala si yatima kama alivyoaminishwa.

Huenda hizi sifa binafsi ndizo zinamfanya Wenje akwamishe ilani ya Chama ya Elimu bure kwa wote.Chadema tunawabunifu wepesi wa kusahau.
- Wenje anamfumbia au hupuuza taarifa anazopewa ndani ya Jiji (zero response). Akipewa taarifa hazifuatilii, huenda anakwamishwa na deni alilonalo kwa mkurugenzi baada ya kumkopesha pesa za kulipia watoto 905. tulipanga tupate utafiti wa mapato halisi ya Jiji ili bajeti inapokuja tufanye uwiano halisi Mbunge huyu bado haonyeshi ushirikiano.

Hivyo hivyo na katibu wa chama mkoa yuko tayari kuomba au kufuata mchango wa fedha lakini mchango wa kimawazo kama ujenzi wa ofisi ya mkoa hayuko tayari.
- Wenje alipewa majinaya madiwani kadhaa wa chadema ambao tayari mkurugenzi wa jiji amekwishawakamata kwenye himaya yake Mbunge huyu hakufuatilia. - Tax property na service levy ni pesa ambazo bado Kabwe (Mkurugenzi Jiji la Mwanza) anakula na wawakilishi wetu hawajui zinakusanywa kiasi gani. Hata ukiwauliza mmoja mmoja nyumba ngapi kwenye kata yake zinalipa kodi Halmashauri na kiasi gani kinapatikana bado kazi ipo.

Chukulia mfano mabilioni ya fedha yaliyotolewa na EU (jumuia ya ulaya) ili kuziunganisha nyumba 5,000 kwenye mfumo wa maji taka Jijini Mwanza ni nyumba 1200 tu ndizo zilizounganishwa.
- Kauli za Wenje kuhusu machinga Mwanza ndizo zinazochochea vurugu. Mbunge huyu ni tatizo kwa chama mkoa. Wenje amepoteza mwelekeo, anahamasisha uvunjaji wa sheria akiwalazimisha wananchi kujichukulia sheria mkononi. Suala la machinga na suala la sharifu wanaofanya kazi ya kuzoa taka na usafi wa mazingira aliwahamasisha wananchi wawapige mawe pindi waingiapo kwenye nyumba zao kufanya ukaguzi akisahu kuwa sisi chadema tunaongoza Halmashauri.

Wajumbe huenda wawakilishi wetu hawakujiandaakuongoza ndiyo maana wanapuyanga. Diwani wa viti maalumu ambaye pia ni mwenyekiti wa BAWACHA Jimbo la Nyamagana ni tatizo katika Chama, mamlaka haya anayatoa wapi? Yatupasa tutanabaishe kama yeye ni kiongozi wa Chama Proper, BARAZA au ni katibu wa ofisi ya Mbunge? Mamlaka haya yanatoka wapi nayeye kuwa juu ya viongozi wa nafasi husika?

MIGOGORO YA CHAMA
- Niliposoma gazeti la majira la tarehe 20/08/2011 lenye kichwa cha habari kilichosomeka, “MONGELA AMWEKEA PINGAMIZI MACHEMLI” nilifadhahika kukuta taarifa za kujihuzulu kwa viongozi wote wa Wilaya ya Ukerewe na Kamati tendaji. Chanzo walidai mgombea wao Bw. Simon Mabagala Mtobesya kukataliwa na Kamati kuu ya Chama. Namshukuru Mungu kwa chadema Kusimama imara na kushinda kiti cha Ubunge na kuiongoza Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe.

- Mtaalamu mmoja wa masuala ya Uongozi na Utawala aliwahi kuainisha baadhi ya vyanzo vya Migogoro kwamba ni pamoja na ukiukaji wa kanuni na taratibu ndani ya Chama (Katiba), uongozi wa kibabe, ubinafsi, na upendeleo bila kufuata kanuni (sisi tumesema), na kutowajibika kwa viongozi wa Chama.

Haya yaliyosemwa na mtaalamu huyu japo si yote au zaidi ya haya yaliyosemwa mtaalamu huyu ndiyo chanzo cha migogoro katika chama ndani ya mkoa wa Mwanza. Majimbo ya Magu Buchosa, Nyamagana na Sengerema uongozi unayumba. Hii isimaanishe ya kwamba majimbo mengine hayana migogoro, la hasha, iliyotajwa imefikia kukipa chama doa katika jamii.

CHANZO CHA MIGOGORO
a) Uteuzi wa Madiwani viti maalumu umejenga majeraha na kuacha makovu ambayo hayatafutika. Ikumbukwe ya kuwa kovu la utotoni hufifia au huisha kabisa, lakini kovu la utu uzima hudumu daima. Makovu haya yapo Magu, Sengerema na Nyamagana, Mbaya zaidi viongozi wa chama tena siyo BAWACHA ndiyo waliyohusika kuyajenga. Bila ya kumung’unya maneno tunamtaja katibu wa Mkoa Ndugu Wilson Mushumbusi kuhusika moja kwa moja katika mizozo hii.

Makamanda leo jimbo la Magu linaviongozi waliosimamishwa na mkoa na wale waliosimikwa na mkoa wote wanafanmya kazi ofisi mbili tofauti. Hivyo hivyo na Nyamagana ambapo katika jimbo hili nafsi ya uongozi ina viongozi wawili kila upande ukiita mwingine Batili. Katibu wa mkoa anadai Kamati kuu ilifuta uongozi wa Wilaya ya Nyamagana. Hii inamaanisha Mushumbusi aliachiwa Fredy Lukanga(katibu wa baraza la wazee) peke yake kama kiongozi aliyepatikana kwa njia halali wakati huo huo alidai Kata zote za Nyamagana zilikuwa hazijafanya uchaguzi na Mkoa, Nyamagana haikuhusika? Na kama ilihusika na Mushumbusi haoni hata yeye amechaguliwa na wajumbe Batili?


b) Viongozi kuwa na makundi: hii imewajengea dhana kuamini ya kwamba baadhi ya wanachama ni wasaliti au hawana nidhamu, hivyo hata wanaposimama katika haki wao siku zote huwa ni wakosaji tu. Lakini yatupasa kuelewa yakuwa hata saa mbovu kuna kipindi husema ukweli, tujenge urafiki na wala si uadui ndani ya chama.

Kiongozi anayejenga migogoro anahitaji kuwatawanya ili awatawale viiongozi wa namna hii wamegundua ya kuwa wamepoteza mwelekeo, wanatafuta sifa binafsi ya kujilundikia mali kwa kuwa hawajui mustakabali wao ndani ya Chama kwenye nyadhifa zao.


c)
Njaa za viongozi: viongozi wengi wa Chama wanaishi kwa kuchungulia mifuko ya wawakilishi wetu, hii imewanyanga’anya wao fursa ya kusimamia kanuni, taratibu na maadili ya Chama kwa kushindwa kuwakemea wafadhili. Wameshindwa kutoa maamuzi sahihi au kukemea kutokana na kuwekwa mifukoni na wawakilishi wetu. Hii nayo imechangia kuzua migogoro miongoni mwa wanachama wetu.

d)
Upangaji safu ya wanaotajaria kugombea Ubunge & Udiwani 2015, huku wakijenga kupenyeza propaganda zenye kuchafua na kujenga mgawanyiko, kukatisha tamaa na hata kutishia kufukuzwa wanachama kwa wale wanaoonekana kukinzana na matakwa yao. Ya nini kugombania fito wakati wote tunajenga nyumba moja? Upi ni uongozi halali wa Nyamagana?

e) Wawakilishi kuwa juu ya viongozi wa Chama: viongozi wetu wa chama mkoa wamekosa sauti juu ya aidha Wabunge au Madiwani wetu wa Jiji la Mwanza. Wawakilishi hawa wamekuwa wakipanga nini chama kifanye na wale si Chama kuwapangia wao nini wafanye. Chama sasa kinawajibika kwa wawakilishi hawa.

f) Kupwaya kwa Baraza la uongozi Mkoa: huenda unusu wa baraza hili au kufanya kazi kimezoea leo hii takribani mwezi mmoja sasa chama kinachoenda kushika Dola 2015 hakina ofisi ya chama Mkoa. Katiba ya chama toleo la 2006 ibara ya 7.8.1.4 & 7.8.1.5 zinatamka bayana kuwepo ofisi ambayo Mkoa utawajibika kulipa gharama ya pango.

Licha ibara ya 7.8.3.2 kuhitaji ofisi za wilaya na Mikoa ziwe angalau na mtu mmoja na wakudumu wakufunga na kufungua ofisi kila siku Mwanza hili halijawahi kutendeka. Huenda kutokuwepo kwa M/kiti wa chama Mkoa na M/kiti wa BAWACHA kwa kipindi kirefu sasa huku Finias Magesa akitumia “remote control” kuongoza Mkoa kumechangia Mkoa kuyumba, kukosa ofisi na hata kutoa maamuzi yanayokinzana na katiba katika suala la kesi ya Diwani viti maalumu Sengerema.

Katiba ya Chadema uk 95 kipengele cha X kinazuia matatizo ya chama kupelekwa mahakamani, lakini cha ajabu kesi ilifunguliwa Nov, 2010, Baraza la uongozi tarehe 14/07/2011, Magnum Hotel Baraza la Mkoa lilitoa siku 14 kesi hiyo iwe imeondolewa makamani ama sivyo wahusika bila kuwataja hadharani wangechukuliwa hatua. maamuzi haya yalitoka kifungu kipi cha katiba? Huku Magesa akijinasibu ya kwamba, familia isiyo na utaratibu lazima itasambaratika.

Pamoja na siku hizo 14 kesi haikufutwa hadi mwezi Septemba ndipo ilipofutwa uongozi wa Wilaya ya Sengerema ilijinasibu ya kuwa Dr. Slaa ametoa “Go ahead” Dr. Slaa haijui katiba ya Chadema! Kumrudisha M/kiti wa (J) Sengerema aliyejihuzulu kwa hiyari yake,bila yeye mwenyewe kuomba kurejea kwa zaidi ya kipindi cha mwaka mmoja Baraza la uongozi mkoa halikusoma barua iliyotajwa na CC juu ya viongozi wa Wilaya ya Ukerewe waliojuhuzulu au baraza la uongozi mkoa linatenda kwa mazoea.

SULUHISHO LA MGOGORO

- lazima tubadilishe mtazamo kwa sasa, heri tulinde kiwanda chetu hata kwa mabomu kuliko kukisahau tukalinda kwa rada magari yaliyozalishwa na kiwanda chetu. Tujenge chama kuliko kumjenga mtu ambaye leo tunaye na kesho hatunaye - wawakilishi wetu wapewe mafunzo na semina wajue chama hakikutokana na wao bali wao ndio wametokana na chama hivyo popote penye mgogoro au mvutano chama kitatamalaki wajue upi ni wajibu wao kwa chama na ipi haki yao kutoka kwenye chama.

- Mushumbusi na Wenje ni chanzo cha Migogoro Mwanza, wanakwamisha kukua na kuenea kwa Chama, hivyo wakae wajitathimini ama sivyo waachie ngazi kwani siasa siyo hisia binasfi, bali ni utashi wenye kushirikisha mawazo ya wengine – waswahili husema “mjinga wa kweli huwa hajui kama ni mjinga hivyo hajui anachokipoteza” - Ili kubaini ukweli na kupata ufumbuzi viongozi wa kata zote za Jiji Wakutanishwe kubaini kinachoendelea na kiini cha migogoro wakutanishwe na viongozi wakuu.

RAI

- Uchaguzi wa viongozi ufanyike haraka kwenye majimbo yenye migogoro na yasiyo na uongozi kabisa kama jimbo la Sumve, ili kazi ya kukieneza chama ianze haraka iwezekanavyo. Pia Uongozi wa Mkoa ambao kwa sasa unapwaya aidha uvunjwe na uchaguzi uitishwe au nafasi zinazopwaya kwa sasa zijazwe.

- Iletwe semina ya viongozi wa Chama ngazi ya Jimbo, Wilaya na Mikoa ili kuwajengea uwezo wa kufanya kazi wakijua mipaka yao kwani inajidhihilisha yakuwa migogoro mingi inatokana na ukiukwaji wa katiba huku ule utendaji wa kimazoea ukipewa kipaumbele - Tunaomba Madiwani wakutanishwe na uongozi wa Wilaya hizi mbili yaani Ilemela na Nyamagana,pia katibu mkuu ahamishe ofisi yake DAR kwa muda na aje awasimamie Madiwani wetu hawa.

- Meya wa Jiji aondolewe kwa maana ameshindwa kujirekebisha nakuisimamia Halmashauri - Wakurugenzi wa chama Taifa nao ni tatizo, kwani hawarejeshi taarifa sahihi na halisi wanazokuja kutafiti majimboni. Hutumiwa na baadhi ya watu kupika repoti. Taarifa zao ziwe zinachujwa. Rejea Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Mwanza na uchaguzi wa chama Ukerewe 5/01/2011. Benson alionywa akakaidi, lakini matokeo ya utemi wake aliyaona.rejeeni pia ripoti yake kuhusu uchunguzi wa uhalali wa viongozi wa Nyamagana alimhoji nani, lini, na wapi kubaini kama uchaguzi haukufanyika.

- Ofisi ya chama Taifa izingatie haki za wanachama kwani hata maonyo yanatolewa kimya kimya yanawavunja nguvu wanachama. Katiba ya chama toleo la 2006 ibara 6.3.6 (a) – (f) imekuwa ikikiukwa sana na chama, kiongozi wa Jimbo/Wilaya anasimamishwa uongozi na katibu Mkuu kwa katiba ipi na ibara ipi inayompa mamlaka kutenda hayo?

Pia ubatirishaji wa uteuzi wa wawakilishi wa chama kama wabunge CC iwe inawapa taarifa walioenguliwa na sababu za kuwaengua. Rejea yaliyotokea kwa NYAMAGANA(Chacha Okong’o).

- Chama kimekuwa na mfumo mbovu wa mawasiliano, kwani mawasiliano yanatoka chini kwenda juu. Wabunge wetu wamekuwa wakitumia nafasi ya ukaribu na ukatibu mkuu kuwakandamiza wale wasio na nafasi ya karibu kuongea na katibu mkuu, huku wakitoa taarifa zenye kupotosha. Shilingi ina pande 2.

- Makamanda pigieni kelele wafadhili wanapotoa fedha zisiingie hazina, badala yake ziingie mfuko maalumu ili usimamizi uwe wa makini kuliko sasa, kwani zinatumiwa vibaya na serikali ikibidi hata walete msimamizi wao kama MCC.

- Wadau wa Chadema Mwanza wakutanishwe na Viongozi wakuu (viongozi) ilikusikia nao wanatushauri yapi ili kukipeleka chama mbele maana viongozi wetu hawasemi ukweli wa yale yanayojili.

- makamanda, hata asiye na kiuno huvua mbele yawengine, nasi tumevua, popote palipo na mvutano au migogoro baina ya pande mbili historia itatuhukumu na wakati utatuambia nani Alikuwa sahihi na nani hakuwa sahihi.
Wasalaam

Katibu (BAVICHA) Mkoa wa Mwanza Naibu katibu Baraza la Wazee Wilaya
ya Nyamagana

………………………………….. ………………………………………
SALVATORY MAGAFU PATRICK SAMSON


Nakala

- Mwenyekiti wa Taifa
- Katibu taifa
- Naibu katibu mkuu taifa bara na visiwani
- Wajumbe wa Kamati kuu.
- Makamu mwenyekiti bara na Zanzibari.



CHADEMA VEMA
PEOPLE’S POWER

Kazi ya namna hii inaweza kufanywa na watu wasiojua katiba ya chama, kanuni, miongozo na taratibu. Lakini kuna vitu viwili hapa wala kwa kuanzia, ukiachia kujichanganya kwa mwandishi kwa kiasi kikubwa sana kwa sababu kutumia nguvu nyingi za mikono kulazimisha kile anachokitaka yeye ndiyo kiingie na kuaminiwa na watu wengine. Hapo chini kwenye signature mbona inaonekana imesainiwa na mtu mmoja mwenye vyeo viwili tofauti kabisa kama mbingu na ardhi. Unless hii the so called barua au maelezo yamefojiwa, lakini ABADANI HAIWEZEKANI mtu akawa kiongozi aw BAVICHA pia akawa kiongozi wa Baraza la Wazee. Ndani ya CHADEMA mtu anaweza kuwa kiongozi BAVICHA na BAWACHA at once, lakini is kwa namna ya huyo aliyeandika hayo maelezo anayoyaita ni barua.

Pili chanzo cha barua hii...mpaka hapo unaweza kuelewa. Fumbo mfumbieni mjinga... Wapenzi wa akina Chagulani na Matata watafuteni kila siku munywe nao chai, kama mnawapenda sana. Lakini kwa staili hii ya kuwatetea KUPATA TENA UANACHAMA kwa mgongo wa kuwatungia tuhuma watu wengine, haitawasaidia zaidi ya kujikuta mkifanya double mistaking. Tulieni mtumikie watu kupata CHADEMA.
 
na ushahidi upo,wenje kaiba pesa za walalahoi milion 78 walizochangishwa pale sahara,kama ana ubavu aje akanushe tumuumbue,watu wana data na ushahidi kamili,huyu ni tapeli tu aende kwao kenya akafanye utapeli huko kwa mwanza wamemshtukia ana tamaa kuliko fisi.akipata tena ubunge mje mnikate kichwa changu hadharani,mwanza wanajuta tena sana,pita mitaa yamwanza uwaskie wana mwanza wanavomkandia wenje tapeli waliokua hawajamjua wakampa kura.

Mnaweza kuwa wasemaji wazuri wa kifisadi na ufisadi lakini kamwe hamtaweza kuwa wasemaji wa watu wa Mwanza. Watu wa Mwanza wanaokipenda chama chao hawafanyi uhuni wa namna hii, tena kwa kuzungumza lugha za CCM za ukabila, ukanda na mengine. Kwa lugha hiyo na maneno hayo watu makini hapa wanayo haki ya kukupuuza. Nawapatia pole waliokuamini kuwafanyia hii kazi. Hawakuweza kupata mtu mwingine smart huko uliko wewe?
 
Njaa bana kitu cha ajabu kwelix2,hapa hamna kitu ni njaa tu ndizo zinazowasumbua.Upuuzi mtupu huu kwani alimwaga mboga wakamwaga ugali kaaazii kwelix2.huyu jamaa anafikiria uongozi ni kukurupukax2 tu kwenye media,atulie afanye mambo mengine.
 
Chagulani kaa utulie ili upate busara ya kufanya maamuzi yenye faida kwa ajili ya mustakabali wako wa kisiasa. Leo hii ndio unapata akili ya kumuandikia mwenyekiti malalamiko haya wakati ulipewa kila nafsi ya kuyasema lakini hukuweza.

Hii tabia ya kudhani kwamba unaweza ukagain political popularity kwa kumshambulia Wenje haitakusaidia kamwe. Alishindwa Masha utaweza wewe mtoto mdogo ambae bado unajifundisha siasa. Hao watu wa ccm wanaokudanganya wanakupoteza na mwisho wako kisiasa hauko mbali kama hautobadilika. Zile siasa za vyuoni zilishakwisha ni wengi tulizifanya lakini tulipofika mtaani tukaswitch kuendana na hali halisi ya maisha na siasa za nchi hii.

Na mwanachadema yeyote anayeshabikia huu upuuzi wa chagulani atambue kwamba hatutamuonea haya katu, lazima atawajibika kwa matendo yake.

Umesema kweli. Watu wa aina hiyo huishia kuwa kama Dr. W. Kabourou (Kaburu) ambaye aliitikisa ccm Kigoma na leo jina lake limepitishwa kugombea uwenyekiti wa Magamba Mkoa wa Kigoma. Mitume wa Magamba kuua CDM ni wengi. Lakini wanajisumbua. CHADEMA daima Mbele, Nyuma mwiko.
 
Wenye kupenda kitu hawai empty tin, kama mtu umeweza kusoma kwa kiwango cha degree huwezi kushuka ukawa mwehu wa kulalamika na kutafuta njia za kujitoa unadhani huyo unayemsema kwa kumsingle out Wenje inamsaidia au ndio inamuonyesha kwamba kicha chake ni cha samaki hafikirii
Kwenye barua amemcopy Katibu mkuu huyu alishusha uzi hapa akisema ni dictator,hafai hata kuwa Raisi vipi leo amuone wa maana watu wanafuatlia maandiko yake yanaaonyesha jinsi alivyochanganyikiwa na hana namna ya kujikwamua,chama chenyewe alikitukana sasa kinachomfanya leo aone kina mfumo wa kuwajibishana ameyatoa wapi
he is just a looser vinginevyo atafakari akae chini upepo upite aombe radhi aendeleze gurudumu la mabadiriko kutapatapa hakumsaidii sana
.. sina mengi ya kuwaambia ila PASIPOZIBWA UFA, UTAJENGWA UKUTA!
aidha tubaki na huyu ANAWEZA na YULE HAWEZI tukisubiri MATOKEO!
 
Back
Top Bottom