Mkuu wa Operesheni ya polisi Chagonja amesema kwamba Polisi hawana "ROHO MBAYA NA YA KIKATILI" kama Mtawala wa zamani Adolf Hitla ,ila wanachofanya ni kulinda Raia na mali zao.
Source: Radio free Afrika.
Maswali ya kujiuliza:
(1) Ikiwa ni kweli polisi hawana Roho ya kikatili kama Adolf Hitla, iweje sasa polisi wawapige risasi wananchi wasio kua hata na fimbo siku bomu lilipo rushwa ktk mkutano wa CHADEMA?
(2) Kama ni kweli wao Polisi ni walinzi wa Raia na mali zao ilikuaje juzi baada ya kuwatawanya watu kwa Mabomu yao na risasi na kukimbia(nikiwemo mimi) na kuacha magari na pikipiki, mbona polisi mlivunjavunja pikipiki na kupiga magari risasi matairi na kuvunja vioo?
Binafsi nilikua na gari pale mbali kidogo na uwanja ila wakati watu wanakimbia nilishindwa kuondoa kwa kuogopa kukanyaga watu waliokua wanaanguka hovyo.
Matokeo yake Polisi walitoboa matairi yote manne na kuvunja Sait mirror zote. Cha kushangaza hadi gari linaondolewa pale kwa break down mida ya saa moja lilikua na vioo vyote. Jana asubuhi kwenda kuliangalia polisi tayari kioo cha nyuma kimevunjwa. Nadhani lengo la walio vunja kioo cha nyuma ni walijua labda kuna fedha huko ndani.Kwani gari lenyewe ni jipya na la garama kubwa.
Sio hilo tu lakini magari mengi likiwemo la Diwani wa kata ya Olturoto Mh,Gipson Meseyeki aina ya JEEP limeharibiwa vibaya sana kiasi kwamba halifai tena. Je kwa haya machache tu CHAGONJA yupo sahihi kusema kwamba polisi hawana roho ya Kikatili kama Adolf Hitla?
Source: Radio free Afrika.
Maswali ya kujiuliza:
(1) Ikiwa ni kweli polisi hawana Roho ya kikatili kama Adolf Hitla, iweje sasa polisi wawapige risasi wananchi wasio kua hata na fimbo siku bomu lilipo rushwa ktk mkutano wa CHADEMA?
(2) Kama ni kweli wao Polisi ni walinzi wa Raia na mali zao ilikuaje juzi baada ya kuwatawanya watu kwa Mabomu yao na risasi na kukimbia(nikiwemo mimi) na kuacha magari na pikipiki, mbona polisi mlivunjavunja pikipiki na kupiga magari risasi matairi na kuvunja vioo?
Binafsi nilikua na gari pale mbali kidogo na uwanja ila wakati watu wanakimbia nilishindwa kuondoa kwa kuogopa kukanyaga watu waliokua wanaanguka hovyo.
Matokeo yake Polisi walitoboa matairi yote manne na kuvunja Sait mirror zote. Cha kushangaza hadi gari linaondolewa pale kwa break down mida ya saa moja lilikua na vioo vyote. Jana asubuhi kwenda kuliangalia polisi tayari kioo cha nyuma kimevunjwa. Nadhani lengo la walio vunja kioo cha nyuma ni walijua labda kuna fedha huko ndani.Kwani gari lenyewe ni jipya na la garama kubwa.
Sio hilo tu lakini magari mengi likiwemo la Diwani wa kata ya Olturoto Mh,Gipson Meseyeki aina ya JEEP limeharibiwa vibaya sana kiasi kwamba halifai tena. Je kwa haya machache tu CHAGONJA yupo sahihi kusema kwamba polisi hawana roho ya Kikatili kama Adolf Hitla?