SI KWELI CHADEMA yatoa pole kufuatia kifo cha Hafidh Ameir

SI KWELI CHADEMA yatoa pole kufuatia kifo cha Hafidh Ameir

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #2
View Source #2
Kumekuwepo na picha inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikidaiwa kuwa ni taarifa kwa umma iliyotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuhusu kutoa salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mume wake, Hafidh Ameir.
Chdmsm.jpg
 
Tunachokijua
Kumekuwepo na picha inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikidaiwa kuwa ni taarifa kwa umma iliyotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuhusu kutoa salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mume wake, Hafidh Ameir.

Katika taarifa hiyo, imeelezwa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Mhe. Tundu Lissu, ametoa salamu za pole kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia msiba huo. Aidha, taarifa hiyo inasema Mhe. Lissu alitoa maelekezo ya kufikisha salamu zake za pole kupitia Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, alipokutana naye mahakamani wakati wa kuendelea kwa kesi.

Taarifa hiyo pia inadai kuwa, kwa niaba ya wanachama wote wa CHADEMA, chama hicho kimetoa salamu za pole kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, familia, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba wa Hafidh Ameir.

Hata hivyo, ufuatiliaji wa maneno muhimu pamoja kurasa rasmi za CHADEMA zimebaini kuwa chama hicho hakijatoa taarifa kwa umma yenye maudhui hayo, Aidha, ukurasa na kupitia Instagram, umekanusha taarifa hiyo.

Aidha kupitia ukurasa rasmi wa instagram wa Brenda Rupia, ambaye Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA,umekanusha taarifa kwa kuandika kuwa taarifa hizo ni potoshi

Taarifa hiii inajiri ambapo Tundu Lissu akiwa mahakamani aliuliza iwapo ujumbe wake wa pole alioutuma kwa familia ya marehemu ulikuwa umewafikia wafiwa.
Unafiki, unafiki, unafiki.

Dr Samia Suluhu Hassan, The Mother of Modern Tanzania, atupilie mbali ujinga wao huu.
 
... Mwenyekiti akiwa kizimbani, for the sake of humanity na akijua ndio njia yetu sote, ameelekeza zitumwe.
 
Juzi na Jana baadhi ya wanazi wa CHADEMA walimshambulia Mh F Mbowe kwenda kutoa pole huko Zanzibar kwa Mh Rais Samia.

Mh Mbowe alikemewa,alibagazwa na kutupiwa kila aina ya kejeli.

Ningependa watu wale wale waanze kumkejeli Mh Lissu.

Ngongo kwasasa Tungu,Zanzibar.
 
Juzi na Jana baadhi ya wanazi wa CHADEMA walimshambulia Mh F Mbowe kwenda kutoa pole huko Zanzibar kwa Mh Rais Samia.

Mh Mbowe alikemewa,alibagazwa na kutupiwa kila aina ya kejeli.

Ningependa watu wale wale waanze kumkejeli Mh Lissu.

Ngongo kwasasa Tungu,Zanzibar.
Ngongo bado huamini mabadiliko?
 
Back
Top Bottom