CHADEMA yaonywa na JWTZ 'Leave us alone" - Army

CHADEMA yaonywa na JWTZ 'Leave us alone" - Army

Hawa wanasemaje kuhusu hili?
 

Attachments

  • 1439843883676.jpg
    1439843883676.jpg
    67.3 KB · Views: 638
Hii ina ushahidi gani kama imetoka FFU, mbona limeandikwa kama tangazo la kuuza viwanja huko mbande na sio amri,tuache kupanda chuki tuweke ukweli hapa.Nimekaa JKT miaka miwili, sijawahi kuona hawa jamaa wakitumia neno tangazo, labda mtu binafsi anauza kitu chake ndiyo huweka tangazo

IGP amekiri kuwa ni kweli wamefanya zoez hili.
una swali la ziada?
 
"Mwnyekiti wa chama cha
CHADEMA Freeman Mbowe
amesema kuna vijana watatu
wametoka jeshini wataalamu
wa mambo ya Kompyuta
wamenda Tume ya Taifa
Uchaguzi kushughulika na
BVR na wakiwa pale
hawajitambulishi kama
wanajeshi".
Mbowe amesema ushahidi
upo na kama Mwamunyange
akibisha atamuekekeza kambi
wanaotoka, wameanza kazi
tarehe ngapi na majina yao
na wapo NEC kwa kazi ipi.
Amesema jaji Lubuva naye
ajitokeze asema vijana hao
wako ofisini kwake kwa
malengo yapi..
Mbowe aliyasema hayo
alipokuwa kwenye mkutano
wa kutambulisha mgombea
urais kwa tiketi ya CHADEMA
Edward Lowasa jana kwenye
uwanja wa furahisha
ulioudhuriwa na umati
mkubwa sana wa watu.
Chanzo: Tanzania Daima
 
Waache waendelee kuropoka dawa yao ipo jikoni... kwa style hii hata wafanyeje hawatakaa wainufaishe nchi ni wapuuzi sana hawa jamaa kila kukicha heshima yangu kwao inashuka kwasababu ya ujinga kama huu. Sijui lowassa kawapa nini walahi siwezi toa kura yangu kwa watu wanafanya wananchi ni wajinga kama chadema. Watawashika masikio hao hao wasiotaka shule wala kazi kutwa kuandamana kama manyumbu na uvivu wao kusubiri wanasiasa ambao ni wafanya biashara kuwaletea maendeleo.
Unaumizwa na constitutional rights??! Hao mashabiki wa Magufuli hawakukeri? Kushabikia magaeuzi ni ujinga na kutokwenda shule?Umekula maharage ya wapi wewe?
 
"Mwnyekiti wa chama cha
CHADEMA Freeman Mbowe
amesema kuna vijana watatu
wametoka jeshini wataalamu
wa mambo ya Kompyuta
wamenda Tume ya Taifa
Uchaguzi kushughulika na
BVR na wakiwa pale
hawajitambulishi kama
wanajeshi".
Mbowe amesema ushahidi
upo na kama Mwamunyange
akibisha atamuekekeza kambi
wanaotoka, wameanza kazi
tarehe ngapi na majina yao
na wapo NEC kwa kazi ipi.
Amesema jaji Lubuva naye
ajitokeze asema vijana hao
wako ofisini kwake kwa
malengo yapi..
Mbowe aliyasema hayo
alipokuwa kwenye mkutano
wa kutambulisha mgombea
urais kwa tiketi ya CHADEMA
Edward Lowasa jana kwenye
uwanja wa furahisha
ulioudhuriwa na umati
mkubwa sana wa watu.
Chanzo: Tanzania Daima

Miaka saba yote alikua akiimba wimbo wa Lowasa Fisadi. Kama ana ushahidi apeleke mahakamani, aache kutudanganya watanzania wenye akili timamu. hayo maneno yake aendelee kuwaambia vibaka wenzie na wacheza disco wenzio.
 
Umeona wapi kitu kinachoitwa chadomo....kiwembe kazi yake kunyolea nywele zote uzijuazo na sio kukatia gogo.
Angalia na maneno yako hayo.

Katibu Mkuu wa chadomo babu daktari wa kanoni padri Dr.W.Slaa yuko wapi?
 
Jeshi la wananchi wa Tanzania ni lazima liwajibike kwa wananchi wenye jeshi lao.Serikali ya Tanzania ni lazima iwajibike kwa watanzania.Mbowe na watanzania wengine tunahitaji majibu kwa maswali yaliyoulizwa na sio vitisho.Lubinga na wenzio mnaitwa makanali kwa sababu mpo ndani ya chombo chetu kilichowaajiri.Kila mkivaa hizo kofia zenu kumbukeni hao bibi na bwana ndani ya hiyo ngao ya taifa ndio waajiri wenu.Wacheni vitisho,tunahitaji majibu.
 
Nimesoma maelezo yote hapo ya huyo msemaji wa jeshi, hakuna mahali popote amejibu hoja ya msingi ya CHADEMA kuhusu mchezo mchafu unaoendelea katika kambi za majeshi kwa askari wote kuamriwa kupeleka taarifa za vitambulisho vyao vya kupiga kura.

Huyo msemaji ametoa vitisho vitupu badala ya kujibu hoja. Jeshi sio vitisho bali jeshi ni kanuni, sheria na Utaratibu. Ni ujinga na ushamba mkubwa kwa karne hii na dunia ya sasa kuwa na jeshi linaloamini kutishia watu badala ya kujenga urafiki na mahusiano mema na raia na taasisi.

Kwa namna IGP na huyu msemaji wa Jeshi la JWTZ walivyoshindwa kutoa majibu ya msingi katika hoja nzito zilizotolewa kwao, inaashiria kabisa wamepanic sana hususani baada ya hicho kichafu walichokuwa wanakificha sasa kimeanza kuwa hadharani.

Hivi wewe una uhakika kuwa Jwtz inahakiki vitambulisho vya kupigia kura kwa askari wake?
 
walioko jeshini ndo wanalaumu mnawafosi kuchukua vitambulisho vyao...na ukwel mfano wanadai hata wenyewe wameichoka ccm...wanadai muwaachie uhuru...muwaachie wananchi uhuru pia wafanye yao

Hao walioko jeshini walikuambia? wewe uliwahi kuona wanajeshi wanazungumza siasa?
 
Truth pains but must be told.

Ni kweli majeshi yetu pamoja na polisi walichukua vitambulisho vya kupigia kura vya mapolisi na wanajeshi wote na kwenda kuvinakili namba kwa sababu zinazojulikana.
Acheni demokrasia ichukue mkondo wake kihalali.

Mkuu peleka ushahidi au chama kilichosema kimeambiwa kitoe ushahidi, magazeti yapo, mitandao na vitu kama hivyo dunia ya leo na siasa hizi havitaki "ramli" tena!!!!!

Aliyetoa shutuma kaambiwa atoe ushahidi hilo tu baas!!
Masaa mangapi yamepita??!!!
 
25 October mbivu na mbichi ndo zitajulikana hizo zote ni sarakasi tu kati ya mlinda na mlindwa.
 
Lazima jeshi liambiwe ukweli,lisijihushe na siasa wasubili tuwachagulie boss wao,wakome vitisho wanaishi kwa mishahara ya Kodi zetu
 
Iko wazi kuwa taasisi zote za ulinzi na usalama wameamriwa kupeleka number za vitambulisho vyao vya kupigia kura, huyu anaekanusha anashiriki tu ktk kufunga bao la mkono!

Tanzania ikiingia kwny machafuko ya kisiasa mi wazi CCM ndio watakuwa wamesababisha!

Hakuna machafuko yoyote japo mnapenda iwe hivyo ndorooobo nyie
 
Bado tunataka majibu toka kwa CDF kama alivyouliza Mbowe, wale maafisa wa IT wamjeshi wameenda kufanya kazi gani ya siri Tume ya Uchaguzi? Hakuna mamlaka isiyohojiwa katika nchi inayoendeshwa kidemokrasia hivyo lazima tupate majibu na sio vitisho.
Mbowe kauliza kwa uthabiti mkubwa kabisa na uwazi. Kwa nini kuwe na siri kati ya Tume na Jeshi? Kwa nini vyombo vya dola vichukue namba za askari za shahada zao?

CDF hayupo kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazoelekezwa ndani ya jeshi, ndio maana kuna kitengo cha habari ambacho kimewajibu wakina mbowe kuwa wapeleke ushahidi wa tuhuma zao.
 
Back
Top Bottom