Waache waendelee kuropoka dawa yao ipo jikoni... kwa style hii hata wafanyeje hawatakaa wainufaishe nchi ni wapuuzi sana hawa jamaa kila kukicha heshima yangu kwao inashuka kwasababu ya ujinga kama huu. Sijui lowassa kawapa nini walahi siwezi toa kura yangu kwa watu wanafanya wananchi ni wajinga kama chadema. Watawashika masikio hao hao wasiotaka shule wala kazi kutwa kuandamana kama manyumbu na uvivu wao kusubiri wanasiasa ambao ni wafanya biashara kuwaletea maendeleo.
Huyu jamaa alipaswa kujibu habari za kukusanya kadi za wapiga kura wanajehsi.
Kazi ya jeshi ni ulinzi wa mipaka ya nchi. Ina taratibu zake na mara zote hatuingilii masuala ya usalama wa nchi .
Suala la uchaguzi wa viongozi wa nchi ni la kiraia wala si la kijeshi. Linapaswa kufanyika kwa taratibu na sheria zilizopo na wala halina matinki yoyote ya ujeshi.
Kama wanajeshi waliona hawawezi kufanya siasa, kuchagua viongozi wa nchi na Watanzanai wenzao, wangeweka miiko ya kazi ili watu wao wasijiandikishe na wakakae huko huko maporini wakisubiri vita.
Habari ya viongozi wao kuleta ubabe kwenye siasa hata wanapotuhumiwa kuvunja taratibu kwa kisingizio kwamba wao wana uwezo wa kuua watanzania wote, haiwajengi wao wala chama chao. Mtu mweye ufahamu na uelewa wa siasa, suala la kiraia alipaswa kutambua haki za kiraia za wanajenshi walionyang'anywa kadi, na mipaka ya jehsi katika masuala ya kiraia, na hivyo kuwapa uhuru wa kupiga kura kama raia wengine bila vitisho.
Msemaji wa jeshi alipaswa kutoa hoja aidha kukanusha tuhuma ama ku justify na si kutishia. Na ninasikitika kuona viongozi wa jeshi wanaonyesha kuiuinga mkono ccm ambayo ilikataliwa na wanajeshi wengi sana mwaka 2010. Hii tarayi inaashirika mgawanyiko ndani ya jeshi ambao kama busara haitatumika, likitokea la kutokea, jeshi linagawanyika mara moja na wenye akli wanaeewa nini ninasema.
Jeshi kama limeamua kuhusika na siasa za nchi, lisiingize ujeshi wake kwenye siasa. Lifuate taratibu na sheria za nchi a hivyo kuacha kukusanya kadi za wapiga kura kwa vitisho amri na kadhalika. Linapokiuka sheria za nchi, na kuhojiwa vitendo vyake hivyo, liache ubabe, badala yake, likanushe ama kutoa ufafanuzi na si vitisho. Huku kwenye kura siyo jehsini na hatuhitaji karinye karinye zao.
Vinginevyo, ninachokiona ni ule ule mwendelezo wa tabia za wanajeshi wanaofahamika kwa matumizi mengi ya nguvu, kuliko mbegu za juu.
Majibu haya yamenikumbusha amuri kwa kruter waazimane appetite, ili wote wapate chakula. . Ninakumbuka namna tu tunavyoweza kutoa " C" yaani mapumziko kwa kuruta anayesema ana uongonjwa unaoitwa " Chronic Chlorophyll of the Mitochondria ".
Au tunavyoweza kumpa mtu kibali cha special diet kwa kuwa ana "Vascular Bundles" kwenye mikono na tena akae mbali na wenzake maana huo ni ungojwa hatari sana wa kuambukiza.
Narudia tene kusema, nilitegemea afande ajibu hoja badala ya vitisho. Asisahau hao aliowachukulia kadi zao ndio wapiganaji na wana uhuru na utashi wako wa kumchagua kiongozi wanayemtaka. Jeshi halimiliki nafsi za hao wapiganaji.
Akumbuke pia sababu za jeshi kugawanyika na madhara yake ndipo aamue kusema na kufanay anchotaka. Asisahau wanajeshi wanandugu zao wengi abao huwa hawako "BARAKIS" ambao wanahitaji kuwalinda na kuwatetea.
Ni vema aktumia maarifa kuliko ubabe maana sasa athari zake, wenye akili wanaziona ziko dhahiri.