CHADEMA yaonywa na JWTZ 'Leave us alone" - Army

CHADEMA yaonywa na JWTZ 'Leave us alone" - Army

Nimeangalia taarifa ya habari ya itv ,wewe mtoa mada labda umepotosha mada yako kwa makusudi au kwa bahati mbaya kutokana na uelewa wako.
yule muheshimiwa wa jwtz ameelezea vizuri kabisa tena kwa umakini kuwa waandishi wa habari wawe makini wasiandike habari ambayo ni ya uongo kwani itapotosha jamii,kama habari ni za kweli jwtz wapelekewe taarifa wazifanyie kazi.
akaendelea kusema jeshi ni la watoto wa wakulima,wafanyakazi na wafanyabiashara kwahivyo ni jeshi la watanzania wote.
munaoleta habari hapa muwe makini musilete taarifa kwa nia ya uchochezi miongoni mwa watanzania na taasisi nyeti kama jwtz.
demokrasia idaiwe kwa misingi ya ukweli na amani sio kinyume chake,sio vizuri kuhusisha habari za kisiasa na jeshi,tuwapige vita waandishi wa habari wote wenye dhamira mbaya ya uchochezi kwani hawa ni sawa na ugonjwa wa ukoma na ikiwezekana wachukuliwe hatua kali bila kusubiri muda.
waandishi wa habari wa aina hii naweza kusema ni mamluki waliotumwa na watu wenye nia mbaya na tanzania,tuliona rwanda na kenya jinsi waandishi wenye nia mbaya walivyoleta uchochezi na madhara yake.
 
Maneno meeeengi!...
Kulikuwa na shida gani kama tu wangesema hawajaorodhesha hivyo vitambulisho na wakaishia hapo!
 
Truth pains but must be told.


Ni kweli majeshi yetu pamoja na polisi walichukua vitambulisho vya kupigia kura vya mapolisi na wanajeshi wote na kwenda kuvinakili namba kwa sababu zinazojulikana.

Acheni demokrasia ichukue mkondo wake kihalali.
 
Huyu jamaa alipaswa kujibu habari za kukusanya kadi za wapiga kura wanajehsi.

Kazi ya jeshi ni ulinzi wa mipaka ya nchi. Ina taratibu zake na mara zote hatuingilii masuala ya usalama wa nchi .

Suala la uchaguzi wa viongozi wa nchi ni la kiraia wala si la kijeshi. Linapaswa kufanyika kwa taratibu na sheria zilizopo na wala halina matinki yoyote ya ujeshi.

Kama wanajeshi waliona hawawezi kufanya siasa, kuchagua viongozi wa nchi na Watanzanai wenzao, wangeweka miiko ya kazi ili watu wao wasijiandikishe na wakakae huko huko maporini wakisubiri vita.

Habari ya viongozi wao kuleta ubabe kwenye siasa hata wanapotuhumiwa kuvunja taratibu kwa kisingizio kwamba wao wana uwezo wa kuua watanzania wote, haiwajengi wao wala chama chao. Mtu mweye ufahamu na uelewa wa siasa, suala la kiraia alipaswa kutambua haki za kiraia za wanajenshi walionyang'anywa kadi, na mipaka ya jehsi katika masuala ya kiraia, na hivyo kuwapa uhuru wa kupiga kura kama raia wengine bila vitisho.

Msemaji wa jeshi alipaswa kutoa hoja aidha kukanusha tuhuma ama ku justify na si kutishia. Na ninasikitika kuona viongozi wa jeshi wanaonyesha kuiuinga mkono ccm ambayo ilikataliwa na wanajeshi wengi sana mwaka 2010. Hii tarayi inaashirika mgawanyiko ndani ya jeshi ambao kama busara haitatumika, likitokea la kutokea, jeshi linagawanyika mara moja na wenye akli wanaeewa nini ninasema.

Jeshi kama limeamua kuhusika na siasa za nchi, lisiingize ujeshi wake kwenye siasa. Lifuate taratibu na sheria za nchi a hivyo kuacha kukusanya kadi za wapiga kura kwa vitisho amri na kadhalika. Linapokiuka sheria za nchi, na kuhojiwa vitendo vyake hivyo, liache ubabe, badala yake, likanushe ama kutoa ufafanuzi na si vitisho. Huku kwenye kura siyo jehsini na hatuhitaji karinye karinye zao.

Vinginevyo, ninachokiona ni ule ule mwendelezo wa tabia za wanajeshi wanaofahamika kwa matumizi mengi ya nguvu, kuliko mbegu za juu.


Majibu haya yamenikumbusha amuri kwa kruter waazimane appetite, ili wote wapate chakula. . Ninakumbuka namna tu tunavyoweza kutoa " C" yaani mapumziko kwa kuruta anayesema ana uongonjwa unaoitwa " Chronic Chlorophyll of the Mitochondria ".

Au tunavyoweza kumpa mtu kibali cha special diet kwa kuwa ana "Vascular Bundles" kwenye mikono na tena akae mbali na wenzake maana huo ni ungojwa hatari sana wa kuambukiza.

Narudia tene kusema, nilitegemea afande ajibu hoja badala ya vitisho. Asisahau hao aliowachukulia kadi zao ndio wapiganaji na wana uhuru na utashi wako wa kumchagua kiongozi wanayemtaka. Jeshi halimiliki nafsi za hao wapiganaji.

Akumbuke pia sababu za jeshi kugawanyika na madhara yake ndipo aamue kusema na kufanay anchotaka. Asisahau wanajeshi wanandugu zao wengi abao huwa hawako "BARAKIS" ambao wanahitaji kuwalinda na kuwatetea.

Ni vema aktumia maarifa kuliko ubabe maana sasa athari zake, wenye akili wanaziona ziko dhahiri.

Kaka umegusa mulemule yani kukosa busara ni tatizo kubwa sana hasa kwa hawa vijungu jiko seniors... Juzi tu nilikua naongea na mkuu flani wa ngere ngere akadai ni tatizo mpaka sasa kuna 2 antagonistic part ndani ya jeshi yani tatizo.
 
Ulitarajia tangazo liwe na sifagan?

Hata magari na zana zao zinasura mbaya.

Au ulitaka iandikwe kwa risasi?

Lile bandiko limefojiwa ili kukujazeni ujinga watu kama wewe usiechambua mambo.
 
tatizo lao chadema walopokaji wengi

Unafikiri tatizo lao ni kusema ovyo na matusi tu,vile vile wana element ya ukosefu wa UTU wanafikia hatua ya kutaka kufanya mandamano ya kisiasa kwenye MISIBA!!

Kisaikolojia wahusika wakuu wanaonekana wazi wazi reasoning capacities zao zimechukua likizo wasipo kemewa mapema wanaweza kuwa chanzo cha kutulete majanga katika Taifa letu,hawana strategy yoyote ya kushinda chama tawala wamebaki wanatopeza muda wao mwingi wakijaribu ku-instigate waajiliwa kwenye vyombo vya usalama specifically Polisi,JWTZ nk wakati wakijua fika kwamba vyombo hivyo haviruhusiwi kujishugulisha na masuala ya siasa!
 
Nimeangalia taarifa ya habari ya itv ,wewe mtoa mada labda umepotosha mada yako kwa makusudi au kwa bahati mbaya kutokana na uelewa wako.
yule muheshimiwa wa jwtz ameelezea vizuri kabisa tena kwa umakini kuwa waandishi wa habari wawe makini wasiandike habari ambayo ni ya uongo kwani itapotosha jamii,kama habari ni za kweli jwtz wapelekewe taarifa wazifanyie kazi.
akaendelea kusema jeshi ni la watoto wa wakulima,wafanyakazi na wafanyabiashara kwahivyo ni jeshi la watanzania wote.
munaoleta habari hapa muwe makini musilete taarifa kwa nia ya uchochezi miongoni mwa watanzania na taasisi nyeti kama jwtz.
demokrasia idaiwe kwa misingi ya ukweli na amani sio kinyume chake,sio vizuri kuhusisha habari za kisiasa na jeshi,tuwapige vita waandishi wa habari wote wenye dhamira mbaya ya uchochezi kwani hawa ni sawa na ugonjwa wa ukoma na ikiwezekana wachukuliwe hatua kali bila kusubiri muda.
waandishi wa habari wa aina hii naweza kusema ni mamluki waliotumwa na watu wenye nia mbaya na tanzania,tuliona rwanda na kenya jinsi waandishi wenye nia mbaya walivyoleta uchochezi na madhara yake.


Mkuu wakuu wa majeshi yetu wamepotoka mara kadha. Historia hujirudia na ukweli haufichiki

1. A. Shimbo alitumika vibaya

2. Chagonga mara kadhaa katumika vibaya - Alifikia hatua kusema chadema imeuwa D. Mwangosi, picha zikamuumbuwa

3. Omar Mahita alitumika vibaya

4. Kamuhanda alitumika vibaya

Mifano nimingi na huwezi kuukanusha kizembezembe namna hiyo.
 
Hii ina ushahidi gani kama imetoka FFU, mbona limeandikwa kama tangazo la kuuza viwanja huko mbande na sio amri,tuache kupanda chuki tuweke ukweli hapa.Nimekaa JKT miaka miwili, sijawahi kuona hawa jamaa wakitumia neno tangazo, labda mtu binafsi anauza kitu chake ndiyo huweka tangazo

Tayari jibu tumepata. Umekaa miaka miwili JKT maana yake wewe ulienda kama wale wakujitolea (Volunteers) ambao kazi yao kubwa ni kwenda kulima mashamba ya jeshi hayo mengine utayajulia wapi? Kama kitu hukielewi ni bora ukakaa kimya.
BTW ulipomaliza hiyo miaka yako miwili ulipata ajira au uko kwenye kampuni za ulinzi? Usije kuwa wewe ndio mlinzi wetu (ambaye katoka kwenye kampuni ya ulinzi) maana kila saa unachati na simu kumbe uko JF unaandika haya.
 
Maneno meeeengi!...
Kulikuwa na shida gani kama tu wangesema hawajaorodhesha hivyo vitambulisho na wakaishia hapo!

Unajuwa hawa jamaa bado wanadhani Tanzania bado ni ile ya miaka ileee, dunia ya kutishana haipo siku hizi. Wewe tumia nguvu zako za kijeshi kwa muda lakini dunia nzima itakushukia na utamu wa dunia utauona mchungu maisha yako yote yaliyo baki. Na sii wewe pekee uliyeanzisha jambo hilo bali hata mkeo,watoto na jamaa yako itauona uchungu wa ulichokianzisha.
Hawajifunzi kutoka hata hapo Burundi tuu? Kwanza ndani ya jeshi lenyewe wapo pro Watawala na pro Wananchi.
 
Waache waendelee kuropoka dawa yao ipo jikoni... kwa style hii hata wafanyeje hawatakaa wainufaishe nchi ni wapuuzi sana hawa jamaa kila kukicha heshima yangu kwao inashuka kwasababu ya ujinga kama huu. Sijui lowassa kawapa nini walahi siwezi toa kura yangu kwa watu wanafanya wananchi ni wajinga kama chadema. Watawashika masikio hao hao wasiotaka shule wala kazi kutwa kuandamana kama manyumbu na uvivu wao kusubiri wanasiasa ambao ni wafanya biashara kuwaletea maendeleo.

Na mabadiliko ya hii nchi yataletwa na hao hao ambao unawaita manyumbu!!! Subiri october
 
Unafikiri tatizo lao ni kusema ovyo na matusi tu,vile vile wana element ya ukosefu wa UTU wanafikia hatua ya kutaka kufanya mandamano ya kisiasa kwenye MISIBA!!

Kisaikolojia wahusika wakuu wanaonekana wazi wazi reasoning capacities zao zimechukua likizo wasipo kemewa mapema wanaweza kuwa chanzo cha kutulete majanga katika Taifa letu,hawana strategy yoyote ya kushinda chama tawala wamebaki wanatopeza muda wao mwingi wakijaribu ku-instigate waajiliwa kwenye vyombo vya usalama specifically Polisi,JWTZ nk wakati wakijua fika kwamba vyombo hivyo haviruhusiwi kujishugulisha na masuala ya siasa!

Unaelewà unachokijadili?

Katibu mkuu ccm cap Yusuf Makamba

Katibu mkuu ccm Gen A. Kinana

Mwenyekiti wa ccm ....Kikwete

Balozi A. Shimbo Gen

Mgombea urais ccm, Jaji mkuu A. Ramadhan

Sasa nakupa home work utafute function ya jeshi na mahakama ni relation ipi inatumika

Inversily related

Directly related

Majesh na mahakama ni integral part ya ccm

Usijione unafaham ilhali mbabaishaji mkuu wangu.
 
Viongozi wa juu tu lkn maprivate hawaungi mkono hujuma

Nani kakudanganya jeshi la Tz linaishi kwa hujuma? yawezekana haujafatilia marekebisho aliyoyafanya JK kwa jeshi letu sahivi na wanavyofurahia maisha tofauti na zamani ..wana heshima zao bwana
 
Tayari jibu tumepata. Umekaa miaka miwili JKT maana yake wewe ulienda kama wale wakujitolea (Volunteers) ambao kazi yao kubwa ni kwenda kulima mashamba ya jeshi hayo mengine utayajulia wapi? Kama kitu hukielewi ni bora ukakaa kimya.
BTW ulipomaliza hiyo miaka yako miwili ulipata ajira au uko kwenye kampuni za ulinzi? Usije kuwa wewe ndio mlinzi wetu (ambaye katoka kwenye kampuni ya ulinzi) maana kila saa unachati na simu kumbe uko JF unaandika haya.

hapa ndo umejibu hoja,njoo hapa kariakoo utaona nafanya nini kwa sasa, ila najivunia kupitia JKT, na kamwe sitoliangamiza Taifa langu kwa kusapoti hoja za kichochezi. mazee nikualike kwenye shuguri zangu kariakoo wenda ukawa mteja wangu karibu.
 
Kiwembe kingine hiki tumekivunja:
View attachment 276852

RCO wa pwan hii ni kweli tangazo hilo ni la kwenu?
Mm naona cybercrime ianze kufanya kaz juu ya uzushi huu. Ninavyojua mambo hayo kama ni kweli yapo hakuna raia anayeweza kuyaona zaidi ya askar wako.

Kuna ulazma wa kuwa karibu sana na hii ili ukweli ujulikane,
 
Nimesoma maelezo yote hapo ya huyo msemaji wa jeshi, hakuna mahali popote amejibu hoja ya msingi ya CHADEMA kuhusu mchezo mchafu unaoendelea katika kambi za majeshi kwa askari wote kuamriwa kupeleka taarifa za vitambulisho vyao vya kupiga kura.

Huyo msemaji ametoa vitisho vitupu badala ya kujibu hoja. Jeshi sio vitisho bali jeshi ni kanuni, sheria na Utaratibu. Ni ujinga na ushamba mkubwa kwa karne hii na dunia ya sasa kuwa na jeshi linaloamini kutishia watu badala ya kujenga urafiki na mahusiano mema na raia na taasisi.

Kwa namna IGP na huyu msemaji wa Jeshi la JWTZ walivyoshindwa kutoa majibu ya msingi katika hoja nzito zilizotolewa kwao, inaashiria kabisa wamepanic sana hususani baada ya hicho kichafu walichokuwa wanakificha sasa kimeanza kuwa hadharani.

Unachokosea wewe ni kufikiri kuwa majeshi yetu yameshitakiwa na yanatakiwa kujibu!
Hapo hakuna tuhuma za kujibu kwa kuwa habari husika haikupelekwa na chadema katika channels zinazoyafanya majeshi yajibu!
Ukitoa kauli za kiusalama ambazo zinaharibu heshima ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ktk vijiwe ni lazima uonywe! Kama chadema wakiwa na ushahidi wanatakiwa kuupeleka ktk vyombo husika na sio just rumours ambazo hamna ushahidi uliowasilishwa!
Hatupaswi kulilazimisha jeshi lichague upande ktk uchaguzi Mkuu! Wana uwezo mkubwa wa kuharibu matokeo!
 
Lile bandiko limefojiwa ili kukujazeni ujinga watu kama wewe usiechambua mambo.


Ulichokiongea nikinyume chake

1. A) katibu ccm Y. Makamba Capt-Jeshi
B) katibu ccm A. Kinana Gen-jeshi
C) Mwekiti ccm J. Kikwete mjeshi
D) Balozi uchina A. Shimbo mjeshi

Swali hawa woote wanajeshi kunauhusianogan kati ya ccm na jeshi?

2. Chagonja aliibuka mbele ya vyombo vya habari kulitangazia Taifa wafuasi wa cdm wamemuuwa D. MWANGOSI.

a) Tangazo lake uliliamin kwa vigezogan ilhal alidanganya?

3. Omar Mahita alikiuwa CUF kwa uzushi akitumia nafasi yake ya ukuu wa polisi

kwanini tusiamini bandiko hilo iwapo wakuu wa majeshi kila uchaguzi hutumika kuzusha uwongo, kupotosha umma nakukibeba waziwazi ccm?

Mfano IGP Mahita, Chagonja na Gen A. Shimbo.
 
Huyu jamaa alipaswa kujibu habari za kukusanya kadi za wapiga kura wanajehsi.

Kazi ya jeshi ni ulinzi wa mipaka ya nchi. Ina taratibu zake na mara zote hatuingilii masuala ya usalama wa nchi .

Suala la uchaguzi wa viongozi wa nchi ni la kiraia wala si la kijeshi. Linapaswa kufanyika kwa taratibu na sheria zilizopo na wala halina matinki yoyote ya ujeshi.

Kama wanajeshi waliona hawawezi kufanya siasa, kuchagua viongozi wa nchi na Watanzanai wenzao, wangeweka miiko ya kazi ili watu wao wasijiandikishe na wakakae huko huko maporini wakisubiri vita.

Habari ya viongozi wao kuleta ubabe kwenye siasa hata wanapotuhumiwa kuvunja taratibu kwa kisingizio kwamba wao wana uwezo wa kuua watanzania wote, haiwajengi wao wala chama chao. Mtu mweye ufahamu na uelewa wa siasa, suala la kiraia alipaswa kutambua haki za kiraia za wanajenshi walionyang'anywa kadi, na mipaka ya jehsi katika masuala ya kiraia, na hivyo kuwapa uhuru wa kupiga kura kama raia wengine bila vitisho.

Msemaji wa jeshi alipaswa kutoa hoja aidha kukanusha tuhuma ama ku justify na si kutishia. Na ninasikitika kuona viongozi wa jeshi wanaonyesha kuiuinga mkono ccm ambayo ilikataliwa na wanajeshi wengi sana mwaka 2010. Hii tarayi inaashirika mgawanyiko ndani ya jeshi ambao kama busara haitatumika, likitokea la kutokea, jeshi linagawanyika mara moja na wenye akli wanaeewa nini ninasema.

Jeshi kama limeamua kuhusika na siasa za nchi, lisiingize ujeshi wake kwenye siasa. Lifuate taratibu na sheria za nchi a hivyo kuacha kukusanya kadi za wapiga kura kwa vitisho amri na kadhalika. Linapokiuka sheria za nchi, na kuhojiwa vitendo vyake hivyo, liache ubabe, badala yake, likanushe ama kutoa ufafanuzi na si vitisho. Huku kwenye kura siyo jehsini na hatuhitaji karinye karinye zao.

Vinginevyo, ninachokiona ni ule ule mwendelezo wa tabia za wanajeshi wanaofahamika kwa matumizi mengi ya nguvu, kuliko mbegu za juu.


Majibu haya yamenikumbusha amuri kwa kruter waazimane appetite, ili wote wapate chakula. . Ninakumbuka namna tu tunavyoweza kutoa " C" yaani mapumziko kwa kuruta anayesema ana uongonjwa unaoitwa " Chronic Chlorophyll of the Mitochondria ".

Au tunavyoweza kumpa mtu kibali cha special diet kwa kuwa ana "Vascular Bundles" kwenye mikono na tena akae mbali na wenzake maana huo ni ungojwa hatari sana wa kuambukiza.

Narudia tene kusema, nilitegemea afande ajibu hoja badala ya vitisho. Asisahau hao aliowachukulia kadi zao ndio wapiganaji na wana uhuru na utashi wako wa kumchagua kiongozi wanayemtaka. Jeshi halimiliki nafsi za hao wapiganaji.

Akumbuke pia sababu za jeshi kugawanyika na madhara yake ndipo aamue kusema na kufanay anchotaka. Asisahau wanajeshi wanandugu zao wengi abao huwa hawako "BARAKIS" ambao wanahitaji kuwalinda na kuwatetea.

Ni vema aktumia maarifa kuliko ubabe maana sasa athari zake, wenye akili wanaziona ziko dhahiri.

shukrani sana mkuu.
 
RCO wa pwan hii ni kweli tangazo hilo ni la kwenu?
Mm naona cybercrime ianze kufanya kaz juu ya uzushi huu. Ninavyojua mambo hayo kama ni kweli yapo hakuna raia anayeweza kuyaona zaidi ya askar wako.

Kuna ulazma wa kuwa karibu sana na hii ili ukweli ujulikane,

haa haa mkuu unaanzaje kuhukumu wakati bado hujajiridhisha?
 
Ulielewa akiposema oviously Kura za wanajeshi zitaenda kwa kwa potential people ?
Jamani kama kitu kinaenda ndivyo sivyo, watu wasiseme au to raise their concern kwa vile ni jeshi? Tunajua mna mizinga ,bunduki and all weapons of mass destruction, lakini bado ni watumishi wa wananchi unless mkiuke kiapo cha utumishi sawa kwa wananchi! Uungwana ni kujibu tuhuma na si kutoa vitisho.
 
Back
Top Bottom