PreGE2025 CHADEMA yakamata mtandao, CCM yangu hoi

PreGE2025 CHADEMA yakamata mtandao, CCM yangu hoi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Mitandao haipigi kura
Kamuulize Ruto kilichomkuta kutoka kwa Gen z kilianzia wapi. Akikujibu, uwqnong'oneze ccm kuwa mitandao hupiga kura! Na Kama haipigi kura, ni kwani Magufuli aliifungia kabla ya uchaguzi wa 2020? Au ulikuwq hujazaliwa?
 
Mitandao ya bongo hakuna mambo ya maana yanayojadiliwa.sana sana ni umbea, na ubishi wa simba na yanga.Ata hizo mada za chadema nyingi ni malalamiko porojo na malumbano ambayo hayawezi kusaidia sana kwenye harakati zaidi ya umaarufu ambao haukusadii kwenye meza ya mabadiliko.Mitandao ingekua na uzito kama kungekua mijadala na mada nzito zinazokuza uelewa.Ata hapa JF zile mada nkonki siku hizi hazipo.
 
Mitandao ya bongo hakuna mambo ya maana yanayojadiliwa.sana sana ni umbea, na ubishi wa simba na yanga.Ata hizo mada za chadema nyingi ni malalamiko porojo na malumbano ambayo hayawezi kusaidia sana kwenye harakati zaidi ya umaarufu ambao haukusadii kwenye meza ya mabadiliko.Mitandao ingekua na uzito kama kungekua mijadala na mada nzito zinazokuza uelewa.Ata hapa JF zile mada nkonki siku hizi hazipo.
People are changing
 
Na Veronica France 🇹🇿 🇹🇿

Well, Dunia imebadilika sana, Dunia ya Leo Ktk Siasa lazima uwe na nguvu ya kudhibiti na kuendesha mitandao ya kijamii...huu Ni Wakati ambao tunaishihudia CCM ikiwa hoi bin taaban mitandaoni na Chadema ikishika Mitandao Yote, Nini Kimetokea? turejee Nyuma kidogo

Katika Vuguvugu la Siasa mwanzoni Mwa Mwaka 2010 Mwenyekiti wa Zamani wa Chadema Freeman Mbowe Pamoja na Katibu wake Dr Slaa walikuwa akizunguka Katika Vyuo Vikuu na kushawishi Vijana wenye Maarifa Mengi Top Class (Intelligent) ili wajiunge na Chadema, Vijana Makini ambao wanaweza kuhoji na Hata Kujenga Hoja Katika kuisemea Chadema, Mfano Kama Juliana Shonza, Zitto Kabwe, John Mnyika,Halima Mdee n.k na ndio Wakati huo huo ambao CCM ilikuwa imezubaa na ikiwekeza Nguvu Nyingi Kwa Vijana "Viazi" ambao hawana Maarifa yoyote ya Ujenzi wa Hoja na kukitetea Chama Dhidi ya Hoja nzito za Upinzani, Vijana Wengi Hawa walipewa majukumu hayo kupitia Historia za aidha Wazazi au Wakubwa Katika Familia zao ndani ya CCM..na Hapa ndipo Nguvu ya Mtandao ikahodhiwa na Chadema.

Wakati Hayati Rais Magufuli anakaribia Kuingia Madarakani Kiliibuka kikundi Cha Vijana ndani ya CCM, Hawa vijana hawakuwa na Historia ya Ndugu zao Ktk Chama, Back up au kubebwa, Hawa walijitolea kukijibia Chama Kila Hoja, na Kujenga Hoja, Hoja za "Akili" zikajibiwa Kwa "Akili"..hatimaye CCM ikauchukua Mtandao, Zama za Ukivaa Sare ya CCM Mtaani unazomewa Zikafa Rasmi,mind you Ku post picha ya waziri katua Vietnam au picha ya rais akitua uwanja wa ndege wa Angola Hiyo ni taarifa ya kawaida ambayo hata Ikulu Mawasiliano wanaifanya lakini kuelezea how ziara ya rais Angola itamsaidia mtanzania wa msoga kupata maendeleo inahitaji akili iliyotulia na yenye upeo wa juu,Juzi tumemskia MNEC ASAS alitaka vijana wajibu hoja,tena hizi za Lissu na heche?? Utaona gap aliyoiona MNEC ASAS inahitaji kuzibwa hasa kuelekea uchaguzi mkuu 2025...

Humphrey Polepole akiwa Mwenezi akatambua Kuwa huwezi kufanya "Uenezi" Kwa kueneza Taarifa, Propaganda na Hoja Kwa kuzunguka na Mabasi kilometa mamia Kwa mamia Wakati Mtandao unaweza kueneza Jambo au Hoja au kuzima Hoja Kwa Sekunde tu!, ikaandikwa Proposal ya kuundwa Kwa "Team Mtandao " ndani ya CCM na wana-CCM hao waiojitolewa Watambuliwe na Team Mtandao ya CCM irasimishwe, na Mchakato Ukaendelea Walaji wakawa wanachukua Mpunga Kwa ajili ya Facilities na Wanatafuna! wakajichomeka Kuwa Wasemaji wa Chama Mitandaoni huku Vile Vichwa Makini Vilivyoisimamisha CCM mitandaoni vikiwekwa kando na Chawa wakichukua Nafasi!, Chawa ambao wameshindwa Kumjibia Mwenyekiti wa CCM Hoja!, Chawa ambao Wameshindwa Kukitetea Chama!, hasa Katika Nyakati hizi.Mnauhakika Steve Nyerere au mwijaku wataelezea uma wa watanzania kwanini deni la taifa limepanda na himilivu??? Are u serious?? Dhidi ya Profesa Issa Shivji? Heche? Mwamakula? Ngoja Kwanza....

Ieleweke kuwa Chama kama CCM kinatakiwa kuwa na Taasisi inayojitegemea ya mitandaoni peke yake kwaajili ya Ku update na kuandika na kueneza na kutengeneza matukio...ni kweli Kura hazipo mitandaoni lakini mitandao ndio inaweza ikafanya wanasiasa wakademuka na mitandao ya kijamii,ina nguvu ya kipeleka habari Kwa Haraka kuliko Toyota V8 iliyobeba Chawa kumpeleka Mtwara akaogelee Kwenye Matope Akisema "CCM Oyeeee!"

My question je?? Katika Wakati huu ambao CCM imelowa Mitandaoni Nani atajibu Hoja za Lissu?, nani atamjibu Heche?, Makala Pamoja na Kuteleza Kwenye Hoja ya Ebola ana Kazi ya Kufanya!....Team za Mtandao zimejaa Chawa na Watu wasio na Hoja, je Makala nae anasubiri mpaka mwezi October?? Science na technology is inevitable in politics na spinning and propaganda all rebuild the muscles of political functionality....

Listen "KIGOGO" Ni Kama Taasisi, KIGOGO alijulikana mpaka vijijini,kuna mawaziri walijaa upepo wakajibu litaasisi ambalo alitangaza mpaka kifo cha Magufuli wakati serikali ilisema hajafa imagine...

Kama kuna sehem serikali inatakiwa kuwekeza pamoja na Chama basi ni hapa kwenye mitandao ya kijamii...sio kila IT atakupa content nzuri ya kupost,au atapeleka kwenye magroup lazima iwe Taasisi ijumuishe watu wenye experience mbalimbali watakaoweza Ku operate mitandao ya kijamii...

#Fact Arab movements zilianzia Facebook tu wakafanya Mapinduzi ya serikali zao,GenZ hapo Kenya walitumia mitandao ya kijamii Ku initiates maandamano kila siku,CCM inaweza kuwa advance kwa kuanzia Taasisi imara itakayojitegemea na kufanya Kazi za kuzima na kuanzisha mashambulizi kupitia mitandao ya kijamii sio kutumia machawa kuanzisha kampeni flani then zikizima ndo zimekufa...

Mimi sijui kama wapo,kama wapo basi kunasehem hamna nguvu na kama hamna anzisheni chap...mind you Chadema were very smart in 2009-2015 waliishia mitandao ya kijamii kiasi kwamba hata wasomi wengi na vijana walikuwa updated easily,kabla ya mabadiliko na kugeuza ule upepo and still they are...we need to work smart enough to win the majority.....

Credit: Veronica France FB

View attachment 3296898
CCM imekamata ushindi
 
Kwa hiyo ni kweli CCM kukaa kote madarakani bado wananchi wamekwa miaka 40 ya CCM madrakani
Mikwamo ya kiuchumi kubadilika badilika na kwa kulitambua hilo ndiyo maana CCM dhana yake kupindua mikwamo hii, kuwa furusa ya kuwakwamua wananchi, kimekuwa kikija na njia za kimapinduzi kukabili mikwamo hii. Njia hizo uanishwa ndani ya Ilani za uchaguzi za Chama hicho, sera, mikakati, na taratibu kupitia serikali inayoongozwa na Chama hicho. Mifano ipo mingi nitataja mmoja.

Mfano huo ni huu, Kutokana na changamoto za kiuchumi zikizolikabili Taifa Chama kiliagiza serikali kuwepo na Kodi ya kichwa kwa Kila mtu Mzima pamoja na Kodi ya baiskeli. Kodi hizi zilisaidia lakini zilikumbana na changamoto, CCM ikatumia mbinu ya kisasa na kuondoka Kodi hizo za kichwa na baiskeli na kuleta VAT, Kodi ambayo ilikuwa Haina adha kw mtu...na kwa umuhimu wa VAT bado mbinu hii ipo na inazidi kuboreshwa.

Sasa kama Kuna Chama kingine kina mbinu mbadala kukabili mikwamo tajwa kiiweke wazi mbinu hizo tuzikague kwanza kabla ya kukiamini. Hatuwezi kukubali kuuziwa "mbuzi akiwa ndani ya gunia".

Upo? Au umekimbia? Ha ha 😂 😂 😂
 
Back
Top Bottom