Abdul Said Naumanga
JF-Expert Member
- Jan 28, 2024
- 745
- 1,470
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewasilisha malalamiko rasmi kwa FIFA Ethics Committee dhidi ya Klabu ya Young Africans SC (Yanga). Malalamiko hayo yanahusu mchango wa TZS milioni 100 uliotolewa na Yanga kwa chama cha siasa (CCM) katika hafla ya Gala Dinner iliyofanyika Mlimani City, Dar es Salaam, tarehe 12 Agosti 2025. Katika malalamiko hayo, CHADEMA inadai kuwa kitendo hicho kilichofanywa na Yanga ni uvunjaji wa moja kwa moja wa kanuni za FIFA zinazolinda misingi ya political neutrality na uhuru wa vyama vya michezo dhidi ya ushawishi wa kisiasa.
Kwa mujibu wa barua hiyo, kitendo cha Rais wa Yanga, Eng. Hersi Said, kutangaza mchango huo mbele ya viongozi wa kitaifa wa chama tawala wakati wa kampeni za uchaguzi, ni tendo linalotafsiriwa kama explicit political alignment. Kwa maneno mengine, klabu imejipambanua hadharani kisiasa. FIFA Statutes, hasa Articles 4, 14, 19 na 20, pamoja na FIFA Code of Ethics (Articles 15 na 20), zinaweka wazi kwamba klabu na viongozi wake wanapaswa kubaki huru dhidi ya ushawishi wa kisiasa, na marufuku hii inalenga kulinda hadhi ya michezo kama jukwaa la umoja wa kijamii bila kujali imani au itikadi.
Tatizo kubwa siyo tu uvunjaji wa kanuni, bali athari za kijamii na kitaasisi zinazoweza kutokea. Yanga ni taasisi ya kijamii yenye mashabiki na wanachama wanaotoka pande zote za kisiasa. Mara klabu inapojitokeza wazi kuunga mkono chama fulani, inawa alienate mashabiki na wanachama wanaotoka nje ya mstari huo. Hii inavunja msingi wa michezo kama chombo cha umoja, inahatarisha taswira ya klabu katika soko la wadhamini, na inaweza kuibua mfarakano wa ndani. Zaidi ya hapo, inaleta mfano hatari unaoweza kufuatiwa na vilabu vingine, na hatimaye kugeuza sekta ya michezo kuwa uwanja wa siasa za vyama.
Kwa mantiki hiyo, hoja ya CHADEMA mbele ya FIFA si hoja nyepesi ya siasa za ndani, bali ni hoja ya kulinda misingi ya utawala bora wa michezo duniani. FIFA mara nyingi imeonyesha msimamo mkali dhidi ya ushawishi wa kisiasa, ikiwahi hata kuzuia mashirikisho ya kitaifa kushiriki michuano pale ambapo serikali au vyama vya siasa vimeonekana kuingilia maamuzi ya michezo. Ikiwa FIFA itaona uzito wa malalamiko haya, hatua dhidi ya Yanga au viongozi wake zinaweza kuwa fundisho kubwa kwa vilabu vyote Afrika na kwingineko, kwamba siasa na michezo lazima zibaki na mipaka yao.
Kwa mtazamo wangu, hili si jambo la kupuuzwa. Hata kama ndani ya Tanzania linaweza kuonekana kama jambo la kawaida la kisiasa, kwenye mizani ya sheria za michezo za kimataifa ni suala linaloweza kupelekea adhabu kali, kuanzia onyo, faini, kufungiwa viongozi husika, au hata kuathiri ushiriki wa klabu kimataifa endapo TFF itabainika kushindwa kudhibiti wanachama wake. Hivyo basi, hatua ya CHADEMA imefungua ukurasa mpya wa mjadala; Je, Tanzania tupo tayari kulinda michezo yetu dhidi ya ushawishi wa kisiasa, au tutaendelea kuziacha klabu zetu zibebeshwe ajenda za vyama?
Kwa mujibu wa barua hiyo, kitendo cha Rais wa Yanga, Eng. Hersi Said, kutangaza mchango huo mbele ya viongozi wa kitaifa wa chama tawala wakati wa kampeni za uchaguzi, ni tendo linalotafsiriwa kama explicit political alignment. Kwa maneno mengine, klabu imejipambanua hadharani kisiasa. FIFA Statutes, hasa Articles 4, 14, 19 na 20, pamoja na FIFA Code of Ethics (Articles 15 na 20), zinaweka wazi kwamba klabu na viongozi wake wanapaswa kubaki huru dhidi ya ushawishi wa kisiasa, na marufuku hii inalenga kulinda hadhi ya michezo kama jukwaa la umoja wa kijamii bila kujali imani au itikadi.
Tatizo kubwa siyo tu uvunjaji wa kanuni, bali athari za kijamii na kitaasisi zinazoweza kutokea. Yanga ni taasisi ya kijamii yenye mashabiki na wanachama wanaotoka pande zote za kisiasa. Mara klabu inapojitokeza wazi kuunga mkono chama fulani, inawa alienate mashabiki na wanachama wanaotoka nje ya mstari huo. Hii inavunja msingi wa michezo kama chombo cha umoja, inahatarisha taswira ya klabu katika soko la wadhamini, na inaweza kuibua mfarakano wa ndani. Zaidi ya hapo, inaleta mfano hatari unaoweza kufuatiwa na vilabu vingine, na hatimaye kugeuza sekta ya michezo kuwa uwanja wa siasa za vyama.
Kwa mantiki hiyo, hoja ya CHADEMA mbele ya FIFA si hoja nyepesi ya siasa za ndani, bali ni hoja ya kulinda misingi ya utawala bora wa michezo duniani. FIFA mara nyingi imeonyesha msimamo mkali dhidi ya ushawishi wa kisiasa, ikiwahi hata kuzuia mashirikisho ya kitaifa kushiriki michuano pale ambapo serikali au vyama vya siasa vimeonekana kuingilia maamuzi ya michezo. Ikiwa FIFA itaona uzito wa malalamiko haya, hatua dhidi ya Yanga au viongozi wake zinaweza kuwa fundisho kubwa kwa vilabu vyote Afrika na kwingineko, kwamba siasa na michezo lazima zibaki na mipaka yao.
Kwa mtazamo wangu, hili si jambo la kupuuzwa. Hata kama ndani ya Tanzania linaweza kuonekana kama jambo la kawaida la kisiasa, kwenye mizani ya sheria za michezo za kimataifa ni suala linaloweza kupelekea adhabu kali, kuanzia onyo, faini, kufungiwa viongozi husika, au hata kuathiri ushiriki wa klabu kimataifa endapo TFF itabainika kushindwa kudhibiti wanachama wake. Hivyo basi, hatua ya CHADEMA imefungua ukurasa mpya wa mjadala; Je, Tanzania tupo tayari kulinda michezo yetu dhidi ya ushawishi wa kisiasa, au tutaendelea kuziacha klabu zetu zibebeshwe ajenda za vyama?
==========================