Chama cha Demokrasia na maendeleo-CHADEMA kimeibomoa vibaya ngome ya waziri wa Uchukuzi Harisson Mwakyembe jimboni kwake Kyela.
Hali hiyo imetokea baada ya mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mbeya Juma Mwalunga kujiunga na CHADEMA na kulaani CCM kwamba ni chama kilichochoka na kinapaswa kuondolewa madarakani mara moja.
Kiongozi huyo alikuwa ni nguzo kuu ya CCM jimboni Kyela na ndiye aliongoza kampeni za CCM jimboni humo.
Wanachama kadhaa wa CCM waliohojiwa kuhusu uamuzi huo wameshtushwa na kusema ni wazi CCM itazikwa Kyela.
Source:Tanzania Daima.
Hali hiyo imetokea baada ya mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mbeya Juma Mwalunga kujiunga na CHADEMA na kulaani CCM kwamba ni chama kilichochoka na kinapaswa kuondolewa madarakani mara moja.
Kiongozi huyo alikuwa ni nguzo kuu ya CCM jimboni Kyela na ndiye aliongoza kampeni za CCM jimboni humo.
Wanachama kadhaa wa CCM waliohojiwa kuhusu uamuzi huo wameshtushwa na kusema ni wazi CCM itazikwa Kyela.
Source:Tanzania Daima.