Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,722
- 218,282
Pamoja na Ukweli kwamba Jimbo la Kyela ni sehemu ya ngome imara za Chadema kwenye Mkoa wa Mbeya ikiwemo pia Kanda ya Nyasa , lakini mara zote Jimbo hili husahauliwa kwenye ziara muhimu za Viongozi wa Kitaifa , naandika haya nikiwa Mkazi wa Kyela , kijiji cha Kajunjumele , njia kuu kuelekea Itungi Port , kwahiyo naandika nikiwa na ushahidi wa kutosha .
Kyela ni mwisho wa nchi , hakuna barabara kuu ya viongozi kupita kuelekea kwingine , kwamba labda na sisi wanaKyela tuwazuie njiani na kuwalazimisha watuhutubie kama wafanyavyo majimbo mengine , Kiongozi anayekuja KYELA ni lazima apange safari ya Kuja Kyela moja kwa moja , ni lazima viongozi wa Kanda ya Nyasa wamwelekeze kwamba , TUKIFIKA UYOLE HEBU KATA KUSHOTO UENDE UKAHUTUBIE WANANCHI WA KYELA .
Viongozi wa Kanda ya Nyasa ni lazima safari hii Tundu Lissi akanyage Kyela , Afike Katumbasongwe , Ngonga , Ikolo , afike mpaka Ikato lya Nyerere , Bujonde , kajunjumele , Ipyana na Kwingineko , Tunataka Lissu afike Boda , ambako Bendera 5 za mwanzo unazoziona zinapepea ukitokea Malawi , zote ni Bendera za Chadema , sisi Kyela tulishaiua ccm kitambo sana , sasa hivi ni kama tunapambana na Polisi tu .
Labda kwa Taarifa tu ni kwamba CHADEMA KYELA ndio imemstaafisha siasa Mwakyembe , huyu hatukumpa muda wa kufurukuta , tuliziba njia zake zote , ilifika wakati Mwakyembe aliogopa hata kuitisha mikutano ya hadhara kwa hofu ya kuzomewa , yale mambo yao ya " ALILE KAKO " Ilikuwa nyongeza tu , ni lazima sasa viongozi wa Kitaifa wafahamu kazi kubwa tuliyoifanya ya kuua ccm Kyela kwa KUITAMBUA .
Mungu ibariki Chadema
Naomba kuwasilisha .
NAKALA : Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula , Sugu , China , Peter Msgwa , Tundu Lissu , Gwamaka Mbughi , John Mwambigija