issenye
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 3,781
- 5,205
Wana JF tulijadili na hili kwa manufaa ya Taifa letu
Serikali yawapindua wananchi katika mchakato
na Edward Kinabo na Lucy Ngowi
KAMA vile imeshindwa kusoma alama za nyakati, serikali imeamua kuchakachua mchakato wa marekebisho ya katiba mpya kwa kuandaa muswada ambao unapinga yote yanayopendekezwa na wananchi.
Badala yake, serikali inarejesha yote yanayokataliwa na wadau, hali ambayo inaweza kuhatarisha amani ya nchi na hatimaye kusababisha mchakato mzima kurudiwa huko mbele.
Mabadiliko ya katiba ni madai ya msingi na matakwa ya lazima kama nchi hii inataka kujenga na kudumisha amani ya kweli na kuleta maendeleo kwa watu wake.
Katika mazingira ambamo wananchi wamekuwa wanalalamikia mamlaka yaliyopitiliza ya rais, kama kikwazo cha maendeleo na badiliko la msingi katika katiba, muswada wa sasa unaoletwa na serikali, unalenga kuendelea kusimika mamlaka hayo.
Uchambuzi uliofanywa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), ambaye awali ndiye alidhamiria kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu mchakato wa katiba mpya, unaonyesha kuwa muswada huo uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11, Machi 2011, unataka kumpa rais mamlaka ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi.
Wakati wanaharakati na wananchi kwa ujumla wamekuwa wanasisitiza wananchi wawe na mamlaka ya mwisho katika kuamua hatima ya katiba yao, muswada huu wa serikali unarejesha mamlaka hayo kwa rais.
Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011 unatarajiwa kuwasilishwa bungeni hivi karibuni, na CCM kwa kutumia wingi wa wabunge wao, wanaoiunga mkono serikali hata kwa masuala wasiyokubaliana nayo, wanatarajiwa kuunga mkono muswada huo, kuhujumu mabadiliko makubwa ambayo taifa lingefanya baada ya miaka 50 ya uhuru.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, ambayo gazeti hili lina nakala yake, mbunge huyo wa Ubungo anasema:
Maudhui ya muswada huu yamedhihirisha tahadhari niliyotoa mara kadhaa kwamba serikali haina dhamira ya kweli ya kuhakikisha panakuwepo na mchakato mzuri wa kuwa na katiba mpya.
Muswada huo umelenga kuhalalisha yote ambayo yalitangazwa kufanywa na rais kuhusu mchakato wa katiba mpya na kupingwa na wadau mbalimbali; sasa yanataka kupewa uhalali kwa sheria inayotaka kutungwa na Bunge kupitia muswada huo.
Muswada huo unataka kumpa mamlaka rais ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi. Muswada huo pia utaka kumpa rais mamlaka ya kuteua wajumbe wa tume husika bila kushauriana na mtu yeyote isipokuwa Rais wa Zanzibar.
Muswada huo unaelekeza kuwa katika kuteua wajumbe, rais atazingatia uwakilishi wa makundi ya kijamii, lakini makundi husika hayatajwi hata kwa ujumla wake, hivyo kuacha mamlaka yote ya kuamua uwakilishi kubaki kwa rais.
Muswada huo unataka kumpa rais mamlaka ya kutengeneza hadidu rejea za tume, jambo ambalo lilipaswa kufanywa na Bunge kwa kuwa sehemu ya sheria husika ama kufanywa na mkutano mkuu wa kikatiba. Kwa kutoa mamlaka ya kuunda hadidu rejea kwa rais, mwanya umetolewa kwa mtu mmoja kuweka mipaka ya nini kinastahili kufanywa na tume wakati wa mchakato wa katiba mpya, hivyo kuminya wigo wa mabadiliko.
Muswada huo unataka tume iwasilishe ripoti yake kwa rais ambaye atampa nakala Rais wa Zanzibar na baadaye kumwelekeza waziri mwenye dhamana kupeleka yale atakayoamua rais bungeni. Muswada huu kwa kuwa na kifungu hiki utaendeleza yaliyofanywa na marais waliopita kuhusu ripoti na mapendekezo ya tume nyingine, hivyo kukwamisha mabadiliko ya kweli.
Muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa tume itakayoundwa kuitisha jukwaa (fora) ambalo litaundwa kwa ajili ya kupata maoni pekee (ad hoc) badala ya kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa Katiba (National Conference/congress) kama wadau walivyohitaji.
Aidha, uwakilishi katika jukwaa hilo umetajwa tu kuwa ni wa kijiografia na kimakundi bila kuweka bayana mnyumbuliko wa uwakilishi. Muswada huo unataka kutoa mamlaka finyu kwa jukwaa hilo kuwa ni kutoa ushauri kuhusiana na muswada; tofauti na mkutano mkuu wa kikatiba ambao ungekuwa na mamlaka zaidi katika mchakato husika.
Muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa rais kuitisha Bunge la katiba (constituent assembly) ikiwemo kuteua wajumbe wa Bunge husika. Muswada huo unataka kutoa mamlaka makubwa kwa rais kuteua wawakilishi wa chombo kikuu zaidi katika mchakato wa katiba bila kushauriana na kundi lolote ama wananchi kuhusika katika uteuzi ama kuwa na wawakilishi walioteuliwa na makundi yenyewe, mathalani vyama vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama vya wakulima, vyama vya wanafunzi, vyama wa wafanyakazi nk.
Muswada huo unataka rais ashauriane na Rais wa Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pekee. Muswada huo unatoa mamlaka makubwa zaidi ya rais kuamua hata kufanya Bunge la kawaida kuwa ndilo Bunge la Katiba, jambo ambalo linaweza kurejesha udhaifu uliofanywa katika mchakato wa katiba inayotumika sasa ambapo umma uliporwa wajibu na mamlaka yake ya kushiriki moja kwa moja katika kupitisha katiba.
Muswada huo kwa ujumla haujaeleza muda wa mchakato wa katiba na vipindi vitakavyotumiwa na vyombo mbalimbali katika hatua mbalimbali za mchakato wa katiba; ama kutoa mamlaka ya kuwekwa kwa muda huo kwa chombo chenye uwakilishi mpana wa umma kama mkutano wa katiba au Bunge, hivyo kutoa mwanya kwa mchakato mzima kucheleweshwa.
Haya ni baadhi ya maudhui ndani ya muswada husika ambayo yamenishtusha na kunifanya nitoe tamko hili la awali wakati nikiendelea kufanya uchambuzi wa kina ambao nitautolea kauli katika hatua za baadaye.
Mnyika alitoa wito kwa vyama vya siasa, asasi za kiraia, vyombo vya habari, taasisi za dini na Watanzania kwa ujumla kufuatilia na kupata nakala ya muswada huo ama maudhui yake kwa ajili ya kuujadili kwa dharura na kutoa matamko.
Sanjari na hilo, alitoa wito kwa serikali itoe taarifa kwa umma namna ambavyo wananchi wanaweza kupata nakala za muswada huo nyeti na sababu za serikali kupuuza maoni mengi ya wadau yaliyotolewa kabla ya kuandaliwa kwa muswada huo kuhusu mchakato unaofaa kuongoza mabadiliko ya katiba katika taifa letu.
Mara kwa mara mbunge huyo amekuwa akisisitiza kuwa ipo haja kwa mchakato wa katiba mpya kupata uhalali wa umma kwa kurejea ibara 8 ambayo inatamka kwamba, madaraka na mamlaka ni umma na serikali inafanya kazi kwa niaba na Bunge ndicho chombo kikuu cha kusimamia wajibu huo kwa kutokana na mamlaka ya kikatiba yaliyopo kwenye ibara ya 63(2) na (3) na ibara ya 98 inayohusika na mabadiliko ya katiba.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika hotuba yake bungeni Februari 8 mwaka huu, pamoja na mambo mengine, alieleza kwamba muswada kuhusu mchakato wa katiba utawasilishwa kwenye mkutano wa tatu wa Bunge mwezi Aprili mwaka huu na kwamba utahusu kuundwa kwa tume.
Makongamano, mikutano na midahalo imekuwa ikifanyika kujadili suala la mabadiliko ya katiba na wanazuoni wamesisitiza mara kadhaa kuwa katiba isiyotokana na matakwa ya wananchi, na isiyopitishwa na wananchi, si ya wananchi.
Iwapo serikali itapuuza wito huu, itakuwa inalielekeza taifa katika machafuko ya kisiasa, na italazimika kufanya mchakato mpya ili kukidhi matakwa haya ya kisheria katika uundwaji wa katiba mpya.
Hatua hii ya serikali kuchakachua mchakato wa katiba imedhihirisha pia kwamba Rais Jakaya Kikwete alidandia hoja asiyoijua mapana na marefu yake alipokiri kwamba nchi inahitaji katiba mpya, baada ya wimbo na joto la kisiasa lililoibuliwa na aliyekuwa mgombea urais kupitia CHADEMA, Dk. Willibrord Slaa.
Dk. Slaa aliahidi kuwa angeanzisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku 100 za utawala wake. Rais Kikwete hakuwahi kuahidi wakati wa kampeni kwamba angerekebisha katiba.
Hata hivyo, baada ya wananchi kudai katiba, huku Mnyika akiahidi kupeleka hoja binafsi bungeni kwa ajili hiyo, ghafla Rais Kikwete alitekeleza ahadi hiyo ndani ya siku 100 za utawala wake hatua ambayo wachambuzi walisema ililenga kuwanyamazisha wananchi na kuipokonya CHADEMA ajenda.
Hata hivyo, wananchi wanaendelea na mijadala kuhusu katiba mpya; na sasa linaandaliwa kongamano la pili lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), lenye lengo la kuwapa wananchi uelewa wa kutosha ili waweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa katiba mpya.
Mwenyekiti wa UDASA, Dk. Mushumbusi Kibogoya, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, alisema mada kuu katika kongamano hilo ni Maudhui na Misingi ya Katiba Mpya.
Safari hii tunataka watu waweze kujua zaidi kuhusu katiba, wawe tayari kutoa mawazo ili tume au kamati itakapowatembelea wawe na kitu cha kusema, watakapoachwa hivi hivi hawatakuwa na cha kuzungumza, alisema Dk. Mushumbusi.
Watoa mada katika kongamano hilo litakalofanyika keshokutwa ni Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samatta na Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Francis Kiwanga.
Serikali yawapindua wananchi katika mchakato
na Edward Kinabo na Lucy Ngowi
Badala yake, serikali inarejesha yote yanayokataliwa na wadau, hali ambayo inaweza kuhatarisha amani ya nchi na hatimaye kusababisha mchakato mzima kurudiwa huko mbele.
Mabadiliko ya katiba ni madai ya msingi na matakwa ya lazima kama nchi hii inataka kujenga na kudumisha amani ya kweli na kuleta maendeleo kwa watu wake.
Katika mazingira ambamo wananchi wamekuwa wanalalamikia mamlaka yaliyopitiliza ya rais, kama kikwazo cha maendeleo na badiliko la msingi katika katiba, muswada wa sasa unaoletwa na serikali, unalenga kuendelea kusimika mamlaka hayo.
Uchambuzi uliofanywa na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), ambaye awali ndiye alidhamiria kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu mchakato wa katiba mpya, unaonyesha kuwa muswada huo uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11, Machi 2011, unataka kumpa rais mamlaka ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi.
Wakati wanaharakati na wananchi kwa ujumla wamekuwa wanasisitiza wananchi wawe na mamlaka ya mwisho katika kuamua hatima ya katiba yao, muswada huu wa serikali unarejesha mamlaka hayo kwa rais.
Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011 unatarajiwa kuwasilishwa bungeni hivi karibuni, na CCM kwa kutumia wingi wa wabunge wao, wanaoiunga mkono serikali hata kwa masuala wasiyokubaliana nayo, wanatarajiwa kuunga mkono muswada huo, kuhujumu mabadiliko makubwa ambayo taifa lingefanya baada ya miaka 50 ya uhuru.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, ambayo gazeti hili lina nakala yake, mbunge huyo wa Ubungo anasema:
Maudhui ya muswada huu yamedhihirisha tahadhari niliyotoa mara kadhaa kwamba serikali haina dhamira ya kweli ya kuhakikisha panakuwepo na mchakato mzuri wa kuwa na katiba mpya.
Muswada huo umelenga kuhalalisha yote ambayo yalitangazwa kufanywa na rais kuhusu mchakato wa katiba mpya na kupingwa na wadau mbalimbali; sasa yanataka kupewa uhalali kwa sheria inayotaka kutungwa na Bunge kupitia muswada huo.
Muswada huo unataka kumpa mamlaka rais ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi. Muswada huo pia utaka kumpa rais mamlaka ya kuteua wajumbe wa tume husika bila kushauriana na mtu yeyote isipokuwa Rais wa Zanzibar.
Muswada huo unaelekeza kuwa katika kuteua wajumbe, rais atazingatia uwakilishi wa makundi ya kijamii, lakini makundi husika hayatajwi hata kwa ujumla wake, hivyo kuacha mamlaka yote ya kuamua uwakilishi kubaki kwa rais.
Muswada huo unataka kumpa rais mamlaka ya kutengeneza hadidu rejea za tume, jambo ambalo lilipaswa kufanywa na Bunge kwa kuwa sehemu ya sheria husika ama kufanywa na mkutano mkuu wa kikatiba. Kwa kutoa mamlaka ya kuunda hadidu rejea kwa rais, mwanya umetolewa kwa mtu mmoja kuweka mipaka ya nini kinastahili kufanywa na tume wakati wa mchakato wa katiba mpya, hivyo kuminya wigo wa mabadiliko.
Muswada huo unataka tume iwasilishe ripoti yake kwa rais ambaye atampa nakala Rais wa Zanzibar na baadaye kumwelekeza waziri mwenye dhamana kupeleka yale atakayoamua rais bungeni. Muswada huu kwa kuwa na kifungu hiki utaendeleza yaliyofanywa na marais waliopita kuhusu ripoti na mapendekezo ya tume nyingine, hivyo kukwamisha mabadiliko ya kweli.
Muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa tume itakayoundwa kuitisha jukwaa (fora) ambalo litaundwa kwa ajili ya kupata maoni pekee (ad hoc) badala ya kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa Katiba (National Conference/congress) kama wadau walivyohitaji.
Aidha, uwakilishi katika jukwaa hilo umetajwa tu kuwa ni wa kijiografia na kimakundi bila kuweka bayana mnyumbuliko wa uwakilishi. Muswada huo unataka kutoa mamlaka finyu kwa jukwaa hilo kuwa ni kutoa ushauri kuhusiana na muswada; tofauti na mkutano mkuu wa kikatiba ambao ungekuwa na mamlaka zaidi katika mchakato husika.
Muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa rais kuitisha Bunge la katiba (constituent assembly) ikiwemo kuteua wajumbe wa Bunge husika. Muswada huo unataka kutoa mamlaka makubwa kwa rais kuteua wawakilishi wa chombo kikuu zaidi katika mchakato wa katiba bila kushauriana na kundi lolote ama wananchi kuhusika katika uteuzi ama kuwa na wawakilishi walioteuliwa na makundi yenyewe, mathalani vyama vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama vya wakulima, vyama vya wanafunzi, vyama wa wafanyakazi nk.
Muswada huo unataka rais ashauriane na Rais wa Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pekee. Muswada huo unatoa mamlaka makubwa zaidi ya rais kuamua hata kufanya Bunge la kawaida kuwa ndilo Bunge la Katiba, jambo ambalo linaweza kurejesha udhaifu uliofanywa katika mchakato wa katiba inayotumika sasa ambapo umma uliporwa wajibu na mamlaka yake ya kushiriki moja kwa moja katika kupitisha katiba.
Muswada huo kwa ujumla haujaeleza muda wa mchakato wa katiba na vipindi vitakavyotumiwa na vyombo mbalimbali katika hatua mbalimbali za mchakato wa katiba; ama kutoa mamlaka ya kuwekwa kwa muda huo kwa chombo chenye uwakilishi mpana wa umma kama mkutano wa katiba au Bunge, hivyo kutoa mwanya kwa mchakato mzima kucheleweshwa.
Haya ni baadhi ya maudhui ndani ya muswada husika ambayo yamenishtusha na kunifanya nitoe tamko hili la awali wakati nikiendelea kufanya uchambuzi wa kina ambao nitautolea kauli katika hatua za baadaye.
Mnyika alitoa wito kwa vyama vya siasa, asasi za kiraia, vyombo vya habari, taasisi za dini na Watanzania kwa ujumla kufuatilia na kupata nakala ya muswada huo ama maudhui yake kwa ajili ya kuujadili kwa dharura na kutoa matamko.
Sanjari na hilo, alitoa wito kwa serikali itoe taarifa kwa umma namna ambavyo wananchi wanaweza kupata nakala za muswada huo nyeti na sababu za serikali kupuuza maoni mengi ya wadau yaliyotolewa kabla ya kuandaliwa kwa muswada huo kuhusu mchakato unaofaa kuongoza mabadiliko ya katiba katika taifa letu.
Mara kwa mara mbunge huyo amekuwa akisisitiza kuwa ipo haja kwa mchakato wa katiba mpya kupata uhalali wa umma kwa kurejea ibara 8 ambayo inatamka kwamba, madaraka na mamlaka ni umma na serikali inafanya kazi kwa niaba na Bunge ndicho chombo kikuu cha kusimamia wajibu huo kwa kutokana na mamlaka ya kikatiba yaliyopo kwenye ibara ya 63(2) na (3) na ibara ya 98 inayohusika na mabadiliko ya katiba.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika hotuba yake bungeni Februari 8 mwaka huu, pamoja na mambo mengine, alieleza kwamba muswada kuhusu mchakato wa katiba utawasilishwa kwenye mkutano wa tatu wa Bunge mwezi Aprili mwaka huu na kwamba utahusu kuundwa kwa tume.
Makongamano, mikutano na midahalo imekuwa ikifanyika kujadili suala la mabadiliko ya katiba na wanazuoni wamesisitiza mara kadhaa kuwa katiba isiyotokana na matakwa ya wananchi, na isiyopitishwa na wananchi, si ya wananchi.
Iwapo serikali itapuuza wito huu, itakuwa inalielekeza taifa katika machafuko ya kisiasa, na italazimika kufanya mchakato mpya ili kukidhi matakwa haya ya kisheria katika uundwaji wa katiba mpya.
Hatua hii ya serikali kuchakachua mchakato wa katiba imedhihirisha pia kwamba Rais Jakaya Kikwete alidandia hoja asiyoijua mapana na marefu yake alipokiri kwamba nchi inahitaji katiba mpya, baada ya wimbo na joto la kisiasa lililoibuliwa na aliyekuwa mgombea urais kupitia CHADEMA, Dk. Willibrord Slaa.
Dk. Slaa aliahidi kuwa angeanzisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku 100 za utawala wake. Rais Kikwete hakuwahi kuahidi wakati wa kampeni kwamba angerekebisha katiba.
Hata hivyo, baada ya wananchi kudai katiba, huku Mnyika akiahidi kupeleka hoja binafsi bungeni kwa ajili hiyo, ghafla Rais Kikwete alitekeleza ahadi hiyo ndani ya siku 100 za utawala wake hatua ambayo wachambuzi walisema ililenga kuwanyamazisha wananchi na kuipokonya CHADEMA ajenda.
Hata hivyo, wananchi wanaendelea na mijadala kuhusu katiba mpya; na sasa linaandaliwa kongamano la pili lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), lenye lengo la kuwapa wananchi uelewa wa kutosha ili waweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa katiba mpya.
Mwenyekiti wa UDASA, Dk. Mushumbusi Kibogoya, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, alisema mada kuu katika kongamano hilo ni Maudhui na Misingi ya Katiba Mpya.
Safari hii tunataka watu waweze kujua zaidi kuhusu katiba, wawe tayari kutoa mawazo ili tume au kamati itakapowatembelea wawe na kitu cha kusema, watakapoachwa hivi hivi hawatakuwa na cha kuzungumza, alisema Dk. Mushumbusi.
Watoa mada katika kongamano hilo litakalofanyika keshokutwa ni Jaji Mkuu mstaafu Barnabas Samatta na Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Francis Kiwanga.