dhah! kama chadema ndo wameongea hivi yani wajue hata kula yangu hawaipati tena na kadi yao narudisha, kwaiyo walitaka wawaache hao wahuni waendelee na hizo vurugu bila kuchukuliwa hatua sio???? mmeniboa chadema from 2 day i hate all of you.
Halina mvuto!
Wamepima wakaona mbali sana.kura za zanzibar zinaamua nani anakua rais wa Tanzania.kwa chadema kupata hata asiliamia 30 za kura zao inawapeleka karibu na ndoto zao za kukamata dola.ukichukulia kua wameshakubalika kwa jamii wakristo.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimekutana na waandisihi wa
habari makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam leo, ambapo wajumbe wa Kamati Kuu, Profesa Abdallah Safari na Mabere Marando, wameweka waziwazi msimamo wa chama hicho kuhusiana na mgogoro kati ya waislamu na serikali na kukamatwa kwa Sheikh Farid huko Zanzibar.
Wanasheria hao wa CHADEMA wamesema kuwa kitendo cha serikali kumnyima dhamana Sheikh Ponda ni kinyume cha katiba na kwamba Chadema kama chama kinachojiandaa kuchukua dola, hakiwezi kuvumilia kuona haki za raia zikivunjwa.
Tunaweza kuwa miongoni mwetu, wapo watu wanaomchukia Sheikh Ponda, lakini hatuwezi kuficha ukweli kwamba Sheikh Ponda kama raia wa Jamhuri ya Muungano au mkazi wa Jamhuri hii, anayo haki ya kusikilizwa na kupewa dhamana. Makosa ambayo Sheikh Ponda ameshitakiwa yanadhaminika kwa mujibu wea sheria, hivyo ni makosa kwa serikali kufanya hila kumnyima dhamana kiongozi huyu wa kidini, ameeleza Marando katika mkutano huo.
Marando alifika mbali zaidi kwa kusema tatizo lililopo sasa kati ya serikali na waislamu, limetokana na hatua ya serikali kuwalazimisha waislamu wote kuwa waumini wa Bakwata, chombo ambacho wengi wanakiona kinatumika kuwakandamiza.
Naye Profesa Safari alionya matumizi ya nguvu za kijeshi yanayotumiwa na serikali kwa kisingizio cha kulinda amani, huku akieleza kuwa matumizi ya kijeshi siyo suluhu ya kutatua matatizo yaliopo.
Kuhusu kukamatwa kwa Sheikh Faridi na kumzuia kwa siku tatu, wanasheria hao wamesisitiza kuwa kitendo hicho hakikubaliki.
Kitendo cha kumkamata na kumshikiria Sheikh Faridi, huku serikali na vyombo vyake vikisema havihusiki, wakati ukweli ni kuwa alikuwa anashikiliwa na watu wa USALAMA wa TAIFA, ni uharamia mkubwa unaopaswa kulaaniwa na wote wanaolitakia mema taifa hili, ameeleza Marando.
Kuhusu uvunjwaji wa makanisa, Profesa Safari amesema CHADEMA kimelaani hatua hiyo iliyotokana na wananchi kujichukulia sheria mkononi. Amewataka waislamu kuvuta subira.
Hata hivyo, Profesa Safari amesena matatizo yanayotokea sasa, yameletwa na CCM kutokana na hatua yao ya kuwatumia baadhi ya waislamu kupandikiza mbegu ya udini nchini.
Jamani hawa jamaa wamesema wamesema mengi, lakini kwa sasa yanatosha kueeleza hayo.
Wafuasi wengi wa chadema wana weledi wenye kutaka maendeleo. Mambo ya dini na ukabila singles hizo zilisha expire....
Leta nyingine.
Mie chadema damu ila ponda anatakiwa anyongwe!!
sasa nimekuelewa ila kama chama cha siasa duniani kote walichofanya ni sahihi kama chama cha siasa japo sio sahihi kusema wameisapoti serekali, na mimi nimezunguza kitaalamu hapo awali (Kisheria)Hukunielewa kumbe
mimi nawazungumzia CHADEMA...
sijasema Ponda asipewe dhamana
wala sijasema ni sahihi kukamatwa..
my point was deep down Chadema wana sapoti serikali
but hawawezi sema hadharani,since kisiasa hawataeleweka
so wameongea kujikosha
Kwa hili am not supporting chadema wale majaaa hawafai chadema tulieni mtajiaibisha hakuna atae enda mtaaani tena
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Nimependa sana tamko hili la CHADEMA maana lingekuwa ni la kuzidi kumkandamiza yule hayawani Ponda basi wale wote wanaoichukia CHADEMA wangepata nafasi ya kuchonga zaidi....``Unawaona hawa CHADEMA hakuna siku wanaweza kusimama kumtetea Muislamu nchi hii, wanawachukia sana Waislamu angekuwa ni Padri kakamatwa kauli ya CHADEMA isingemkandamiza Mkristo mwenzao``...Hongereni sana CHADEMA....
Sifagilii hata kidogo yaliyofanywa na Ponda kama sheria zinaruhusu apewe dhamana basi Serikali impe dhamana na masharti makali yakiambatana na dhamana hiyo, akivunja masharti hayo basi arudishwe lupango mara moja.
dhah! yani kama chadema ndo wameongea haya maneno kuanzia leo siwataki tena na kura yangu hawataiona, na hili likadi lao narudisha yani wanawatetea hawa wahuni, kwaiyo walitaka waendelee kufanya maandamano na kudumisha vurugu sio??? kumbe ni bora hata hiyo ccm, eti ponda awekewe dhamana kwaiyo ndo mnaingia lasmi kum defend huyo gaidi????? yani chadema mmeniboa mbaya and from 2 day i hate all of you.
Ngoja kwanza niwe msomaji wa huu uzi kabla sijachangia chochote.
Chadema haiwezi kuongoza Tanzania na huu ni ushahidi tosha....wanamuunga mkono gaidi ponda kipindi hiki tunateseka.....mbwa kabisa