CHADEMA wamkana Zitto

CHADEMA wamkana Zitto

Zitto anasoma alama za nyakati,vijana wenye hoja zaidi yake ndani ya CDM wapo wengi tu, na wanaoitaka nafasi yake ndani ya chama wapo tu,alikuwa wapi kufata sheria toka amekua mwenyekiti wa hiyo kamati,kama anayoyasema ni kweli na anahulumia fedha ya watanzania basi kwa huluma yake awajibike ndani ya chama na kwenye kamati yake,miaka minne hajafatilia hivyo vyama ni zaidi ya uzembe wanaoufanyaga ccm.
 
Hapa kuna jambo linafuata siku si nyingi!
Khaa!! umeona eeeh.
Mkiti Wilbrod Slaa
KM Freeman Mbowe
NKM Zitto Zuberi Kabwe
huyu naye Ni Anthony Komu.
Hebu wabadilike kidogo ndiyo maana yale majamaa ya lumumba yanawadungua kirahisi kisha mnabaki mnalialia tu 😎
 
Hivi ni nani asiejua kama Zitto ni kiongozi ndani ya CDM, kwa hivyo kama anajua mahesabu ya ndani hayajui hiyo siyo interest ya bunge. Na hata kama anayajua kunataratibu za kuwasilisha matumizi ya vyama vya siasa bungeni, hawezi jibebea mafaili ya CDM bila ya kuombwa.

Halikadhalika Zitto pia ni chair wakamati ya bunge kwenye ukaguzi wa matumizi ya hela zinatolewa na serikali, yeye/wao kuomba kuona auditors report ya matumizi ya hela vyama ndio kazi yao. Sasa hatakama anajua CDM wako sawa au vipi wacha na wabunge wenzake wajue ndio kazi yao, pengine CDM wako sawa wengine je?

Sioni kosa la kiongozi kufanya kazi yake, kesho pia wanaweza mwita waziri wa kilimo wakauliza pesa ya pembejeo imetumika vipi, wao kazi yao ni kuangalia matumizi ya hela iliyotolewa na walipa kodi, sasa kama vyama vya siasa ni moja wa beneficiaries where is the problem.

Nani anajukumu la kukagua that is not their intrest kama kamati nyie lumbaneni mwisho wa siku jamaa wameomba auditors report ya matumizi ya mpunga wa serikali. Hata sheria inasema vyanzo vingine viandikiwe ripoti yake kwengine mpunga wa serikali ufanyiwe audit kivyake na jamaa wanataka kujua umetumika vipi huko bungeni si chamani kwenu. Sasa kama zitto anajua au hajui ni vipi kinachotakiwa ni ripoti bungeni na kamati husika ifanye kazi yake.

Mbona waafrika tunapenda kuaribu taratibu za kisheria na kuanza kuzunguka mmbuyu wakati wajibu huko wazi, kila mtu afanye kazi yake tutafika.
 
Zitto anasoma alama za nyakati,vijana wenye hoja zaidi yake ndani ya CDM wapo wengi tu, na wanaoitaka nafasi yake ndani ya chama wapo tu,alikuwa wapi kufata sheria toka amekua mwenyekiti wa hiyo kamati,kama anayoyasema ni kweli na anahulumia fedha ya watanzania basi kwa huluma yake awajibike ndani ya chama na kwenye kamati yake,miaka minne hajafatilia hivyo vyama ni zaidi ya uzembe wanaoufanyaga ccm.

Yaani katika page zoote 11 nilizozisoma tokea jana mpaka muda huu sijaliona KOSA la Mh Zitto, Sijalionaaa....!

Mnamuita Mh Zitto majina mengi sana ya kumdhalilisha lakini ndio ninyi ninyi mnampongeza kufichua Mabilioni ya Uswis ! Hivi mtaacha lini Unafiki?

Kwanini hamtaki Mh Zitto kama Mwenyekiti wa PAC asifanye kazi yake? Mwenye jukumu la kusema kuwa Hesabu hizo zimekaguliwa na kapelekewa Msajili wa Vyama ni CAG na sio vyama vya Siasa.... Jamani acheni Unafiki!

UFISADI HUU UTALIANGAMIZA TAIFA !
 
Hapa kuna jambo linafuata siku si nyingi!

uhakika ni kwamba cdm haina matatizo na mahesabu yake wala haigopi kukaguliwa hata kwa kuwavizia , wamejipanga siku nyingi ! Majanga yako ccm , hata kinana hajui kinachoendelea !
 
jipu hili likiiva litapasuka tu likipasuka itajulikana nani aliyekuwa anatafutwa kwenye hili sakata.
 
Khaa!! umeona eeeh.
Mkiti Wilbrod Slaa
KM Freeman Mbowe
NKM Zitto Zuberi Kabwe
huyu naye Ni Anthony Komu.
Hebu wabadilike kidogo ndiyo maana yale majamaa ya lumumba yanawadungua kirahisi kisha mnabaki mnalialia tu 😎

mkuu , unamaanisha nini hapo ? hebu fafanua .
 
Ukiangalia kwa makini utaona upotoshaji mkubwa wa gazeti la Tanzania Daima badala ya kujadili maagizo ya (PAC) wanapambana na Zitto.

Tanzania Daima ni gazeti chovu kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Mi nanavyofahamu Zitto ni mwanasiasa pili anatoka Chadema tatu ndani ya Chadema yeye ni Naibu Katibu mkuu! Kwahiyo yeye ni mjube wa kamati kuu anapaswa na yeye kuwajibika moja kwa moja! Nataarifa aliyo itoa Anthony Komu kabla haijapelekwa kwa msajili baada ya kukaguliwa na mkaguzi wa hesabu za Serikali lazima zipite kwenye ofisi Naibu Katibu Mkuu nakwenda kwa Katibu Mkuu! Sasa Zitto anakwepaje msalaba huu? Nafikiri kuna kitu hapa!

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Waufuasi wa CHADEMA msiwe vichwa maji kiasi hicho! Actually, tamko la Zitto ni la kuungwa mkono na CHADEMA kwa vile Zitto aliyasema aliyoyasema akijua kabisa kuwa CDM wana record nzuri na zilizokaguliwa.

Anachotaka kufanya Zitto ni kuipa umaarufu CDM pale itakapobainika kuwa, out of all political parties, ni CDM pekee kilichokuwa na hesabu nzuri. Nyie vipi? Mpaka mshikwe mkono? Zitto anajua anakula na kipofu hawezi kufanya hivyo.

CDM bana! mteteweje?

Waliotakiwa kumuona Zitto kama mnafiki ni vile vyama vyenye mahesabu mabovu.

Au mnawasi wasi na segregation of duties ndani ya chama chenu?

Msiwe na wasi wasi, ile issue ya mkopo wa DR Slaa ilifuata taratibu zote!
 
Kama hii taarifa ya Bw. Anthony Komu ni sahihi basi Zitto Kabwe atakuwa ana matatizo makubwa sana kwenye ubongo wake. Kwamba haelewei haya ndani ya chama chake hadi kukiingiza kwenye kapu la kutaka kikatiwe ruzuku? Vipi kwa NCCR Mageuzi ambao nao taarifa za ukaguzi wake zinaonekana kufika kwa CAG na msajili wa vyama? Right, inawezekana analenga kile anachokiita maslahi ya taifa lakini hata kutaka kujiridhisha kwa taarifa anashindwa?

Si haki kumlaumu Zitto kuwa na matatizo baada ya kutuhumu vyama kutopeleka mahesabu kama sheria inavyotaka.

Tatizo litakuwa pande mbili tu, ama Ofisi ya CAG au Msajili wa Vyama vya Siasa, maana Zitto amepata taarifa kupitia Ofisi hizo mbili.
 
jamàa ni felyaa,kama ÿ si mnafiki mbona amenyamaza kuhusu vijisent vya uswis? cdm wanabahati mbaya kumfuga kenge badani pamoja na kuku!!
 
hili ndio tatizo la mashetani wa chadema, nakumbuka kauli ya kamati ya ulinzi na usalama(ambayo msemaji wake ni mnadhimu mkuu wa jeshi) ilipogeuzwa na kuwa kauli ABDULRAHMAN SHIMBO!!!
grow up mbururas, ZZK anaongea kama mwenyekiti wa POAC na sio mbunge wala kiongozi wa chama, huu upumbavu wa kushambulia watu badala ya taasisi ni ushetani ulioletwa na chadomooooo
 
Kuna wakati huwa nina mashaka hata na MBA ya Zitto!!

Kwangu binafsi bado haiingi akilini...otherwise Bw. komu atakuwa ameleta habari za kizushi na kizandiki!!!

ZZK anaingia kwenye mtego na mazoea ya Serikali yetu, maana Serikali ya TZ na vyombo vyote vinavyohusiana nayo, havijawahi kufanya kazi kuonyesha vi ndani ya serikali moja yenye rais mmoja!!

Any ways....ni maudhi tu kila kona.
 
Huyu zito ni lazima achunguzwe kwa umakini mkubwa. Kila anapoibuka na hoja unakuta kuna swala zito wananchi wanasubiria ili kupata muafaka. Wakati huu wakati taifa zima tumeweka mawazo yetu kwenye swala la katiba mpya tunaona Zito anakuja na hoja zake mbalimbali.
  1. Mshahara wa waziri mkuu, Ikafell
  2. Mshahara wa rais, nayo ikefall
  3. Sasa ameamua kuja na hoja ya kutaka vyama vya siasa viwakilishe hesabu za matumizi yao kwenye ofisi ya CAG. Na jambo la kuuzunisha vyombo vya hapari vimekuwa washabiki bila kuchunguza kwa undani nini kinaendelea.
Hapa cha kujiuliza ni kwanini hii hoja yake ailete kipindi hiki na wakati kwa jinsi anavyodai hesabu hizo haijakaguliwa leo mwaka wa 4. Hapa kuna jambo linaendelea nyuma ya pazia na kwabahati nzuri Watanzania walio wengi wameligundua.
 
Kama ni kweli chama chake hakijakaguliwa mahesabu kwa miaka minne basi mimi nasema kuwa ZITTO naye ni mtuhumiwa kwa sababu hizi

1. Mh, Zitto ni naibu katibu mkuu,ni mbunge wa CDM,ni makamu mwenyekiti wa kambi ya upinzani bungeni,ni waziri kivuri wa fedha na mwisho ni mjumbe wa kamati kuu CDM, sasa inakuweje chama chake ni kituhumiwa wakati naye ni mtendaji mkuu?

2.Ni kwa nini hakuchukua hatua mapema kukinusuru chama chake na tuhuma nzito kama hii wakati yeye ni mwenyekiti wa PAC na alikuwa anajua kuwa chama chake ni mtuhumiwa no 1.

3.Yeye kama kiongozi wa chama huwa anajua kila kitu kinachoendelea ndani yake hata kama ni ubadhirifu yeye anajua je?ni kwa nini hakuweza kukitahadharisha chama chake huku akituhumu kuwa CAG alikuwa anaogopa kumbe alijua hili siku nyingi.

4.Kwa mujibu wa Zitto hivi vyama havijapeleka mahesabu yao kwa miaka minne sasa na mda wote wamekuwa wakipewa Ruzuku nyingine na kwa kipindi chote Zitto ni mwenyekiti wa kamati ya PAC sasa ni kwa nini alikuwa kimya mda wote huo na kuja sasa? Au alikuwa anategeshea upepo wa siasa ili aweze kujibeba naye?
 
Back
Top Bottom