CHADEMA wamkana Zitto

CHADEMA wamkana Zitto

Pamoja na umaarufu alionao Zito, mi bado naamini pamoja na mabo mengine anataka kuonekana maarufu zaidi ndo maana anakuja na hoja za aina hii. Kama kiongozi ndani ya Chadema, yeye binafsi amefanya nini kuhakikisha chama chake kinafuata sheria ikiwa ni pamoja na kukaguliwa kwa kipindi chote anachokisema?,ina maana hata yeye hana lolote kama hawezi hata kusimamia chama chake ambacho anatuaminisha kushika dola miaka michache ijayo.

Siamini kama kweli hajui chama chake kimekaguliwa au la?, ila binafsi basi hafai kama hajasimamia sheria ndani ya chama chake kabla hata ya watanzania hatujampa majukumu ya kutawala nchi. Ni sawa na mtu anashindwa kusimamia familia yake harafu anakuwa mstari wa kwanza kulaumu familia nyingine. Tenda ninayosema badala ya matendo yangu ni msemo uliopitwa na wakati,watu watuoneshe kwa mfano. Amefanya mengi mazuri lakini pia atuheshimu na watz wengine kwa uelewa wetu na atuambie mambo ya tija zaidi
 
Zitto uwa anakurupuka kuongea mambo. Na hii inamponza mara nyingi hata kwenye CDM
 
Hivi zile za USWISS zimeshakaguliwa? Hvi ameshawaita wahusika wakajieleza mbele ya kamati yake? Mbona aliahidi kutupatia majina yahao walioficha hzo hela huko lkn mpaka sasa kimya? Je nikwamba Zitto kashapewa10% akatulia? Je zitto anayoyaongelea ataweza kuyasimamia na kuyatekeleza?

Watu wa Kilimanjaro wana historia nzuri tu ya kua na uwezo wa kufikiri na kuchambua mambo. Ni bahati mbaya sana wewe uwezo huo hauna pengine kwa makusudi tu au umetumwa.
Kwa kukusaidia ingawa hautakua tayari kuelewa maana najua umetokea Buku 7FC ni kwamba Fedha za Uswis anapaswa kuhojiwa serikali (werema) in specific maana ndiye aliepewa jukumu bungeni la kufatilia na kurejesha ripoti ndani ya bunge. Kama taarifa hiyo inakuwa na walakini, bunge litaunda tume ya uchunguzi inayomjumuisha Zitto pia.
Werema hadi leo hajafikisha taarifa bungeni, Leo hii unamhoji Zitto!!!????
Poor you!
 
Zito ni naibu katibu mkuu wa chadema,hyo tarehe ya makatibu kuitwa kama docta slaa hayupo atakaewakilisha chadema badala ya docta ni yeye mwenyew sa sijui atatoaje ushahidi
 
Zitto kachemka sana.mtuhumiwa hapo ni Msajiri na ndiyo kamati ya zitto inapoishia kiutendaji, Kinachofanywa na PAC kwa sasa ni sawa na CEO wa shirika aulize utendaji kazi wa mhudumu wa ofisi wakati MAJIBU ANAPASWA APATE KUTOKA KWA dIRECTOR of HR.This is too low kwa PAC. Anyways!!!au kwa sababu kamati yenyewe imekusanya takataka hadi kina ADEN RAGE.Poleni wana PAC kuna siku mtakwenda na TANAPA kuuliza akina nani wame-supply goods and services
Msajiri asipotimiza wajibu wake; Je sheria inairuhusu PAC kumburuza mahakamani? if yes basi zitto angeishughulika hiyo office ya msajiri kama ana ubavu huo.

Nimependa mfano wako mzuri, hata sisi watu wa viti virefu ni sawa na Owner wa Bar kuanza kupanga zamu za usafi kwa wahudumu wakati Manager wa Bar huyo - au kwa sisi wababa kuanza kuajiri / kufukuza wafanyakazi wa ndani wakati mama yupo. Mgawanyo wa Madaraka.
 
Siajwahi kuwa na wasiwasi na kauli/hoja za Zitto hata siku moja,ninaamini kuna jambo zuri litakuja baada ya taarifa ya Komu.Huyu kamanda huwa akurupuki wapiga deal Chadema kaeni mkao wa kuendesha.
 
Zitto kachemka sana.mtuhumiwa hapo ni Msajiri na ndiyo kamati ya zitto inapoishia kiutendaji, Kinachofanywa na PAC kwa sasa ni sawa na CEO wa shirika aulize utendaji kazi wa mhudumu wa ofisi wakati MAJIBU ANAPASWA APATE KUTOKA KWA dIRECTOR of HR.This is too low kwa PAC. Anyways!!!au kwa sababu kamati yenyewe imekusanya takataka hadi kina ADEN RAGE.Poleni wana PAC kuna siku mtakwenda na TANAPA kuuliza akina nani wame-supply goods and services

Yaani mimi nilivyomuona Rage tu jana eti ndio makamu mwenyekiti niliindoa maana kamati nzima kwa sababu nilikuwa nadhani makamu mwenyekiti ni Deo Fulikunjombe.

Hivi huyu Rage bingwa wa mazabe eti naye leo hii umuweke makamu mwenyekiti wa PAC!!

Tusubili tu bunge la 2015 hatuna Bunge kwa sasa limesheheni wahuni na waadirifu wachache wanamezwamo.
 
Yaani mimi nilivyomuona Rage tu jana eti ndio makamu mwenyekiti niliindoa maana kamati nzima kwa sababu nilikuwa nadhani makamu mwenyekiti ni Deo Fulikunjombe.

Hivi huyu Rage bingwa wa mazabe eti naye leo hii umuweke makamu mwenyekiti wa PAC!!

Tusubili tu bunge la 2015 hatuna Bunge kwa sasa limesheheni wahuni na waadirifu wachache wanamezwamo.

Nilicheka sana kumuona mhalifu kama Rage naye anaongea kwa niaba ya Kamati.

Nikakumbuka siku ile alivyopanda na bastola Jukwaani Igunga halafu akaingia mitaani kutangazia watu mgombea wa Chadema amejitoa.
 
Siajwahi kuwa na wasiwasi na kauli/hoja za Zitto hata siku moja,ninaamini kuna jambo zuri litakuja baada ya taarifa ya Komu.Huyu kamanda huwa akurupuki wapiga deal Chadema kaeni mkao wa kuendesha.

Hivi wewe ndio mama Mingoi yule aliyekuwa anakata mauno Twanga pepeta miaka ya 2000? Maana nimelikumbuka lile shuzi.
 
CAG anatakiwa kwnd kukagua kikatiba,Zito aseme kama CAG alinyimwa hesabu hizo,chini ya kifungu cha 14 kifungu kidogo cha 2 cha sheria ya vyama vya siasa,chama kipeleke audited accounts kwa msajili.hii inapotoshwa makusudi

Kama vyama vinakaguliwa na CAG na Zitto anajua, basi kuna jambo Zitto analitafuta, ama anatafuta umaarufu ambao unataka kupotea. Hapa kuna ka harufu ya mgombea binafsi inanukia kwa Zitto
 
Last edited by a moderator:
Inashangaza Zitto anahoji matumizi ya ruzuku ya pesa kwa vyama vya siasa kama moja ya mjukumu ya kamati yake ya PAC,lakini wanaojiita wazalendo na wenye uchungu na nchi hii wanadiriki kumuita mnafiki? watanzania tupunguze mahaba ya kisiasa hawa wenye dhamana ya uongozi katika vyama vya siasa ni binadamu na wanamapungufu kama binadamu wengine sio malaika hawa.
 
bado sijajua kama nitapiga kura mwaka 2015 naona kuchanganyikiwa tu ,, najutia muda niliopoteza juani mwaka 2010,, nilisimama juani jua likanibanika,, sikujua kama nimechagua maumivu,,, nilichagua baniko la moyo wangu!!!
 
Zitto ni mnafki. Period.

Yeye ni sehemu ya uongozi Chadema licha ya kwamba anaongea kwa niaba ya kamati ya PAC lakini ana uwezo wa kuwasiliana na viongozi wenzake internal. Huyu jamaa bichwa lilishamvimbaga kwa kutafuta sifa za kijinga ila kwa hili amejikaanga mwenyewe na kila mwenye akili timamu sasa anafahamu fika Zitto ameamuwa kupigana vita ya makundi ndani ya Chadema kwa kuitumia kamati ya PAC.

Vita hii haiwezi kwani atakuwa defeated tu, anajaribu kudivert akili za wajinga kutoka kwenye hoja kuu ya katiba mpya.

Nb: Eti kamati yenyewe ya PAC makamu mwenyekiti ni Aden Rage Al shabaab mwizi aliyewahi kufungwa jela kwa wizi wa pesa za FAT.

Nimeshangaa sana huyu kwanza akakamilishe ukaguzi wa hesabu za Simba pale Msimbazi na akabidhi pesa za Okwi.

Hebu rudia kusoma ulichoandika juu hapo!!....×3

Umeona Kaka unachomaanisha?? Yaani Zitto angetoa kwa umma taarifa ya ukaguzi wa fedha wa chama chake kwanza,alafu ndiyo aite vyama vingine kuwasilisha hesabu zao!!
Umenishangaza sana Matola,sikuwahi kufikiria kama you have cheap mind in such a way. Punguzeeni chuki kwa Zitto,it is misleading you.
 
Last edited by a moderator:
Hivi wewe ndio mama Mingoi yule aliyekuwa anakata mauno Twanga pepeta miaka ya 2000? Maana nimelikumbuka lile shuzi.
Mimi ni yule aliekuwa anamsalandia dada yako alipovunja ungo
 
Mtu akikosea ni vizuri kukubali kosa lake.

Kwa hili Zitto Kachemka na akubali kuchemka kwake.

Labda aseme ukaguzi uliofanyika ndani ya chama chake una mapungufu. Atoe mapungufu hayo. Au aseme ni ukaguzi maalumu baada ya kugundua kuwa kilichofanyika hakikuwa sahihi. Otherwise Msajili wa vyama yupo na CAG yupo waseme tatizo liko wapi.
 
Alieleza kuwa ni vema vyama hivyo vikapeleka ripoti kwa msajili na kuachana na malumbano yasiyo na tija, huku akiwashukia waliokuwa wakidai kuwa anatafuta umaarufu kwa maelezo kuwa tayari ni maarufu.

Source: Tanzania Daima Ijumaa
hapo Zitto umenena
 
There are currently 299 users browsing this thread. (49 members and 250 guests)
 
Zito anatimiza wajibu wake kama m/kiti wa PAC, kwa sasa hawezi kuvaa kofia ya unaibu katibu mkuu CHADEMA. Anajua kinachoendelea ndani ya CDM ila ndio hawezi kusemea kwa sasa, mambo ya itifaki tuu. Hapo ametegwa mtu subirini ngoma bado mbichi kabisa. CCM lazima ashikwe tuu..vuteni subira
 
Back
Top Bottom