CHADEMA wamfungulia kesi Nape

CHADEMA wamfungulia kesi Nape

Kutokana na vyanzo vyangu vilivyopo Mahakama kuu ya Tanzania Leo Nape amefunguliwa kesi ya madai na imepewa namba 186 ya mwaka 2012.

Kesi hii ni kuhusiana na madai ya nnape kuwa CDM wana pokea pesa kutoka nje ya nchi.

Tuendelee kufuatilia


Updates.

Inaitwa civil case no.186 of 2012 ,board of registered trustees of chadema ... Plaintiff versus nnape nnauye defendant .

Kesho utasikia Nape/CCM wafungua kesi zidi ya Dr. Slaa/cdm
 
Hivi ile kesi ya Uchaguzi mdogo wa Igunga ilisimamiwa na Mahakama gani vile? Wewe inaonekana hujui hata ulisemalo! Maneno ya Tundu Lissu kuhusu Mahakama zetu na Majaji wake haiwezi kuzuia Haki za msingi za chama au Mwana-CDM yeyote.Hatuwezi kuwekewa Majaji kwenye Mahakama zetu ambao hawawezi kuamua kesi yoyote au kama wakitoa uamuzi ni kwa maelekezo ya Kiongozi fulani wa CCM au Serikali yake. Tunataka utawala wa sheria na siyo sharia!

Tundu Lissu alizungumza ukweli na ushahidi uko kwenye maandishi ukiwa umeandikwa na Majaji hao hao ambao hawakubalini na uteuzi wa kijinga unaoangalia udini,ukoo,ukabila na urafiki! Uteuzi wa aina hii unaofanywa na rais wako Kiwete unaenda kwa mfumo huo na kwa maana hiyo uteuzi huo hauna tija kwa Taifa sana sana unazidi migogoro na migongano ya kiutawala.

Kautipe na utumbo wa kuku ,Mbutolwe mwana wa uma hayo mtaenda kusemea mahakamani ,hivi hamkujua maana ile ya msemo wa kiswahili usemao ...! Usimtukane mkunga na uzazi ungalipo.." yaani hapa mahakimu ndio wanatupilia mbali likesi lenu ! Afu tuwone mtakimbilia wapi ,mnasikitisha na kutupa huruma sana !
 
Prof. Safari, Lissu na Marando ni kikosi kamili cha ushindi dhidi ya Katibu Mwenezi wa NYINYIEM.
hapo kwenye red ndio tatizo sio nyinyiem ila ni wao em, Gosbertgoodluck ukisema nyinyiem unamaanisha sisi wasomaji wakati mimi sipo huko naomba utumie wao em
 
nape alidhani Dr slaa anapotoa shutuma vs ccm na serikali huwa anakurupuka.
Kimsingi Dr Slaa hutoa shutuma huku akiwa na ushahidi lukuki!
Sasa nape kazi unayo....tupe ushahidi wa hizo nchi zilizomwaga fedha tuzijue.
Hii kesi ni mbaya na majaji hawawezi kuichakachua kwa sababu wakifanya hivyo nchi husika zitakuja juu ile mbaya!
 
tusubiri tuone majingambo ya kilazi Nape maana nilimuona amevaa miwani utazani sio Mtanzania kumbe ni kichaa mmoja asiyejua nini anafanya
 
A lie may take care of the present, but it has no future : kazi kwako nape na uropokaji wako!
 
Alilikoroga, acha alinywe na alimeze mwenyewe kisha askilizie utamu au uchungu wake. Ukijifanya mjanja kupita kiasi, mwisho unaweze kujikuta ukila kinyesi ukidhani ni chapati. Juzi juzi aliropoka kuwa anaushahidi wa alichokisema, sasa kumekucha ajiandae kusimama mbele ya pilato kujibu mashtaka ya uropokaji.
 
Anasimama na Lissu Mahakamani pembeni kuna Prof.Safari au kuna kitu gani kwa upande wa Chadema ? Na hii ndiyo watanzania watajua kwamba Chadema wako serious sasa .Komesha kuropoka bila ushahidi .Marando am sure hatakosa hapa kuongoza kuutafuta ukweli .

Hivi mwanasheria wa CCM ni nani au wanaweza kumtumia nani katika hili? Nimrudi Mkono, Masumbuko Lwamai,Mizengo Pinda?
 
Kusema uongo sio kazi, kazi ni kuulinda huo uongo ili usijulikane. Sasa ropoka ropoka ya Nape imemfikisha hapa. Nape unalo.
 
Matumizi mabaya ya rasilimali, hakukuwa na haja ya kumfungulia kesi labda kama watu wanatengeneza mazingira ya kupiga hela ya chama. Kama umahili wa wanasheria si bora wangewasaidia wananchi wanaosota na kesi na hawana hata msaada wa kisheria, hii itakuwa kesi kama ya mengi na manji wanaodaiana sh. 1 na wakifika mahakamani kesi zote zinasimama kuwapa nafasi wauza nyago watokee katika media na wasio na hatia wanarudi tena lupango.

Pole. Mzuieni Nape kuropoka.
 
Jamaa wanamkana Davida cameroon hivi hivi.nape mwaga mboga sasa.
 
wataumbuka vibaya sana mahakamani na ndo mwisho wa chadema
 
heshima ya Nape imeshuka, amekuwa akiongea maneno ya ovyo kama ya watu ambao wasiostaarabika.
 
Back
Top Bottom