Ndugu
Mahesabu with all due Respect sidhani kama hao Wanasheria wa Pro CCM uliowaorodhesha kama unawafahamu vyema.
1. Said Elmaamry - Huyu yuko bize sasa hivi kuhakikisha Mzee mwenzake Idd Simba haendi jela kwa kesi ya kutolewa sadaka na CCM wenzake. hapa usitegemee msaada wa Elmaamry.
2. Nimrod Mkono - huyu kila mtu anamfahamu vyema hana muda wa kujihusisha na kuharibu credibility yake kwenda kumtetea mtu ambaye inajulikana wazi huwa anaanza kuongea halafu ndio anafikiri. Mkono yeye anadeal na wezi wakubwa kabla hawajaiba yeye anawapa ushauri wa kisheria namna ya kujidefend kama kikinuka, mfano hai Rostam Aziz na Dowans yeye kila sehemu eti ana Power of Attorney lakini si mmiliki!!
3. Masumbuko Lamwai - Huyu ni sawa anaweza kwenda kusimama Mahakamani maana zama za kitabu chake zilishapita na mtu ukimuuliza kama kuna Wakili anaitwa Lamwai sidhani kama atakujibu, kwa kifupi Lamwai sasa hivi ni mahiri na gwiji la kunywa pombe na siyo sheria.