Ofisi ya Msajili "IMEMPROVOKE" HECHE bila kujua,hatamaye ameweza kufhnguka kwamba wao ndio walifanya Oct 29 iwe Oct 29 kupitia No Reforms No Election.
nakubariana na wewe kabisa kwa sehemu.lakini hii slogan ilianza kama nakumbuka chadema ilipobadili uogozi since february 2025.na mpaka TL anakamatwa chanza ilikuwa slogan hii.ndani yake tuliona kuna uhaini.
sisi kama viongozi tulifanya ni kuhakikisha ya 29 hayatokei? tulijifanya viziwi na vipofu kana kwamba tuko dunia ya 1977. Genz Z ni kizazi chenye akili.siyo kile kizazi mtoto wa miaka miaka 10 anakuuliza eti mama huyu mtoto mchanga umempata wapi unamjibu eti nimetoka sokoni kumnunua naye kwa akilizake anakubari
🙂🙂🙂🙂.kwa nyakati hizi mtoto wa miaka 3 anajua mtoto anapatikaneje.
isipokuwa kama kweli ni chadema ilihamasisha vulugu zile ( maana ile ilikuwa siyo maandamano ya kuzuia uchaguzi bali vurugu kwa sababu unapoandamana sharti ubebe bango na utuambia mnaelekea wapi na mnaenda kumuona nani kueleza kero zenu ) waliwafanyia watanzania ubaya sana.huwezi kiuzuia uchaguzi siku ya uchaguzi .
Agalia hapa chini taratibu za kuandamana kwa amani.
MAMBO 10 YA KUZINGATIA WAKATI WA MAANDAMANO.
Leo ni siku ya mwisho ya maandalizi ya maandamano ya amani jijini Dar es Salaam.
1.Andaa viatu vyako vyepesi kwa mfano raba na epuka aina ya viatu vya mchuchumio au moka.
2.Hakikisha nguo zako ni nyepesi kwa mfano Suruali na T shirt epuka kuvaa vazi zito au nguo nyingi mwilini.
3.Jitahidi uwe japo na chupa ya maji mikononi yatakusaidia Juani
au beba soda aina ya fanta au mirinda kukuongezea nguvu
4.Andaa bango lako lenye Ujumbe maalum wa kufikisha kwa Watawala au beba Kipeperushi au bendera inayoendana na maandamano
5.kwa sababu ya matembezi ya umbali mrefu epuka kubeba mzigo wa aina yoyote kama vile pochi na vitu vinginevyo.
6.kwa sababu ya msongamano mkubwa wa watu,epuka kuvaa vitu vya thamani kama cheni,hereni na kutembea na kiasi kikubwa cha pesa mfukoni.
(simu yako usiache nyumbani ni muhimu sana)
7.Epuka kutumia nguvu kubwa wakati wa maandamano kama vile kukimbia au kurukaruka wakati wa maandamano.
8.Muda wote wa maandamano sikiliza maelekezo ya Viongozi au waratibu wa maandamano kuepuka ajali au kulinda usalama wa watumiaji wengine wa barabara.
Ukiona mtu anatenda uhalifu wakati wa maandamano,mripoti kwa Viongozi haraka sana.(katika msafara wa Mamba kenge hawakosekani)
9.Ukichoka Kutembea au ukihisi dalili ya kuishiwa nguvu usikae kimya waambie Viongozi au waratibu wa maandamano watakupa njia mbadala wa kupumzika katika magari maalum yanayotufuata nyuma ya maandamano.
10.Baada ya Kufika mwisho wa maandamano usiondoke kimya kimya,
wataarifu Viongozi au watu uliokuwa nao kuwa umefika salama na unarudi nyumbani kwako (kuhakikisha wote tunamliza salama)
Imeandaliwa Na
Boniface Jacob
Mwandamanaji mzoefu
Sasa angalia namba 4 na namba nane.kumbe ili iwe maandamano ya amani inatakiwa kuwe na kiongozi wa maandamano na waandamanaji wawe na bango la ujumbe maalum au malalamiko maalum.
maandamano ya vurugu hayana bango,hayana kiongozi ,ni kufanya uharifu na hakuna atayewajibika.ndicho kilichotokea oktoba 29.nani awezaye kujitokeza hadharani aseme kuwa ndiye alikuwa kiongozi wa maandamano ya kuzuia uchaguzi?waandamanaji walipata kibari wapi cha kuandamani?
kwa leo niishie hapa