CHADEMA 'walishinda' uchaguzi katika kata zote 27!

CHADEMA 'walishinda' uchaguzi katika kata zote 27!

Ujinga mwongine mbaya sana.... endelee hivyohivyo et chama pendwa umati wa watu kwenye mikutano sio ndo wapiga kuru.... ccm kata 23 chadema 3 ndo kimeshinda acha ujinga wewe

ok hamna tabu. lakini hebu nipe mwanzo yako kidogo KIBE, unadhani kwa jinsi hali ya nchi ilivyo kwa sasa; ccm wanastahili kuendelea kushinda chaguzi?
 
Yaani hawa waganga njaa wanachekesha sana na hadithi zao,

mtu alikuwa na watoto 27 wakafa 4 utaendelea kusherehekea ati wamepona 23. Hujiulizi kwa nini hao 4 wamekufa ?!

WHO is more loser btn the 2 CCM or CDM
 
Hii ni moja wapo ya thread za kijinga kuliko ujinga wenyewe!


"Serikali ya CCM inajenga bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Ulaya"-Dr Slaa
 
mtu alikuwa na watoto 27 wakafa 4 utaendelea kusherehekea ati wamepona 23. Hujiulizi kwa nini hao 4 wamekufa ?!

WHO is more loser btn the 2 CCM or CDM

Mfano wa mtu mwenye madhara ya kutumia bangi au gongo mda mrefu!



"Serikali ya CCM inajenga bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Ulaya"-Dr Slaa
 
hii inanikumbusha miaka ya tisini enzi hizo watu waliamini tyson ndiye mbabe wa masumbwi hakuna mwingine..alipopigwa na Evanda pambano la kwanza wakasema kawekew dawa kwenye maji...wajuvi tunaomjua tyson tulijua akishavusha round ya 5 hajashinda ujue nitokee kama alivyofanywa na Douglass...ukipenda sana chongo utaona kengeza tu
 
attachment.php
 
Hapa nimeongelea takribani masuala manne lakini badala ya watu kujibu hoja kwa hoja, baadhi yao wanaanza kuniporomoshea matusi. Nimegusia hoja zifuatazo ambazo ndizo zinapaswa kuwa nguzo ya mjadala wetu:

1. Nguvu ya CHADEMA ambayo inazidi kukua siku hadi siku kwa kuungwa mkono na makundi ya vijana na wazee ukilinganisha na chaguzi zilizotangulia-kuna baadhi ya maeneo, hasa Morogoro, Iringa, Singida, Dodoma, Tabora, nk ambako CHADEMA ilikuwa haisikiki kabisa. Lakini kufuatia mikutano ya M4C iliyofanyika takribani nchi nzima, wananchi wameanza kuipa support CHADEMA. Katika suala hili hatupaswi kuelekeza macho yetu katika uchaguzi ulioisha hivi karibuni bali tuangalie mwelekeo wa CHADEMA kwa ujumla tangu mwaka 2000 hadi leo.

2. Idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura ni ndogo sana (<25% ya wapiga kura waliojiandikisha). Hili tatizo limeathiri vyama vyote lakini CHADEMA ndio wameathirika zaidi kwa kuwa vijana wake wengi hawakujitokeza kupiga kura. Hili ni suala ambalo linapaswa kufanyiwa utafiti zaidi ili kujua ni kwani vijana hawapendi kupiga kura.

3. Mwamko wa kisiasa miongoni mwa wananchi (hasa yale makundi nyanyaswa-walimu, polisi, magereza, wakulima, etc) bado upo chini sana. Watu wengi hawajapata kutambua uhusiano uliopo kati ya umasikini na maisha duni wanayoishi na udhaifu wa serikali iliyoko madarakani.

4. Ushauri wa jumla kwa serikali, tume ya uchaguzi na vyama vya siasa kuhusu namna ya kufanya wananchi wapende kushiriki siasa kwa maendeleo yao. Umuhimu wa kupiga kura na thamani ya kura kwa kila mpiga kura inapaswa kuelezwa kwa umma ili kuwafanya raia wapende kushiriki katika chaguzi mbalimbali.

Haya ndiyo mambo ninayotaka tuyaongelee hapa badala ya kuleta kejeli za &#8216;chopa 3 kata 3' na upuuzi mwingine kama huo. Tatizo ni kwamba kuna baadhi ya watu wanadhani kwamba CCM kuendelea kukaa madarakani (for no reasons) ni muhimu kuliko kuzingatia usatwi wa watanzania walio wengi wanaotaabika na ufisadi, udhalimu na utapanyaji mali unaofanywa na CCM na serikali yake huku maisha ya watanzania walio wengi yakizidi kudidimia.

Turudi kwenye mjadala.:israel:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom