Ni wangapi hatujapiga kura tangu 2015,

Ni wangapi hatujapiga kura tangu 2015,

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
2,739
Reaction score
8,328
Bila kujali nilikuwa upande wa chama tawala au chama cha upinzani, uamuzi wa kutopiga kura nilifanya kwa sababu, kimantiki, mazingira ya uchaguzi yalishatabiri mshindi.

Katika chaguzi za 2020 na 2025, matokeo yalionekana kutabirika kirahisi sana. Hivyo, kwangu, kwenda kupiga kura kulionekana kama kushiriki mchakato ambao tayari niliona mwelekeo wake. Si kwamba sipendi kupiga kura. Niliona tu kwamba kura yangu haikuwa na nafasi ya kubadili mwelekeo wa matokeo.

Kama niko upande wa chama tawala, kura yangu ilikuwa kama kuongeza tone moja kwenye bahari, isingeweza kubadili matokeo yanayobandikwa yenye ushindi mpana sawa na bahari. Na kama niko upande wa upinzani, kura yangu ingekuwa na thamani gani ikiwa mazingira yenyewe yalishatabiri mshindi?

Huo ndio ulikuwa mtazamo wangu. Sio suala la chama nilichokuwa nacho, bali ni imani yangu kwamba kura yangu, katika mazingira hayo, isingekuwa na uwezo wa kubadili matokeo.
 
Bila kujali nilikuwa upande wa chama tawala au chama cha upinzani, uamuzi wa kutopiga kura nilifanya kwa sababu, kimantiki, mazingira ya uchaguzi yalishatabiri mshindi.

Katika chaguzi za 2020 na 2025, matokeo yalionekana kutabirika kirahisi sana. Hivyo, kwangu, kwenda kupiga kura kulionekana kama kushiriki mchakato ambao tayari niliona mwelekeo wake. Si kwamba sipendi kupiga kura. Niliona tu kwamba kura yangu haikuwa na nafasi ya kubadili mwelekeo wa matokeo.

Kama niko upande wa chama tawala, kura yangu ilikuwa kama kuongeza tone moja kwenye bahari, isingeweza kubadili matokeo yanayobandikwa yenye ushindi mpana sawa na bahari. Na kama niko upande wa upinzani, kura yangu ingekuwa na thamani gani ikiwa mazingira yenyewe yalishatabiri mshindi?

Huo ndio ulikuwa mtazamo wangu. Sio suala la chama nilichokuwa nacho, bali ni imani yangu kwamba kura yangu, katika mazingira hayo, isingekuwa na uwezo wa kubadili matokeo.
Bahati nzuri matokeo ya uchaguzi hayaangalii idadi ya wapiga kura.
 
Bila kujali nilikuwa upande wa chama tawala au chama cha upinzani, uamuzi wa kutopiga kura nilifanya kwa sababu, kimantiki, mazingira ya uchaguzi yalishatabiri mshindi.

Katika chaguzi za 2020 na 2025, matokeo yalionekana kutabirika kirahisi sana. Hivyo, kwangu, kwenda kupiga kura kulionekana kama kushiriki mchakato ambao tayari niliona mwelekeo wake. Si kwamba sipendi kupiga kura. Niliona tu kwamba kura yangu haikuwa na nafasi ya kubadili mwelekeo wa matokeo.

Kama niko upande wa chama tawala, kura yangu ilikuwa kama kuongeza tone moja kwenye bahari, isingeweza kubadili matokeo yanayobandikwa yenye ushindi mpana sawa na bahari. Na kama niko upande wa upinzani, kura yangu ingekuwa na thamani gani ikiwa mazingira yenyewe yalishatabiri mshindi?

Huo ndio ulikuwa mtazamo wangu. Sio suala la chama nilichokuwa nacho, bali ni imani yangu kwamba kura yangu, katika mazingira hayo, isingekuwa na uwezo wa kubadili matokeo.
Gentleman,
wewe upige kura au usipige kura , mamilioni ya waTanzania watapiga kura kwa niaba yako, mshindi atapatikana na Taifa letu litasonga mbele bila kisirani au mbambamba za mtu awaye yote anaejifanya special zaidi ya mtakatifu 🐒
 
Uchaguzi wa 2025 Bakwata waliomba hadi malaika na majini kupiga kura, nadhani hao viumbe walishiriki kwa kina katika huo uchaguzi.
 
Back
Top Bottom