CHADEMA wako tayari kumpokea Lowassa

CHADEMA wako tayari kumpokea Lowassa

Sidhani Lowasa kama ni mchafu sana kiasi hicho kama tunavyotaka kuaminishwa, kwangu mimi kosa kubwa la Lowasa ambalo namhukumu nalo, ni kwakuwa alishiriki kwa kiasi kikubwa katika mipango ya kumweka Kikwete madarakani na huku akichafua wengine kupitia mtandao wao walioubuni enzi hizo, na Sitta akiwemo. Kuhusu suala la Richmond, jamani ifike mahali sasa na EL naye aseme hadharani Richmond alihusika vipi. M/kiti wa kikao cha baraza la Mawaziri ni Rais, sasa kuendelea kukaa kimya kwa EL ndiyo ataendelea kujichimbia kaburi. Ok ametubu kama Mwigamba alivyosema na viongozi wakapima akaja CDM na akawa mwanachama wa kawaida, je akataliwe? na wote mnaomhukumu kiasi hicho kila mtu ajitazame ni msafi kiasi gani. Kwetu sisi wakristo Biblia inatuambia kuwa hata yule mwana mpotevu baada ya kutapanya mali za baba yake, akagundua kosa, akajuta, akarudi kwa baba yake, je baba yake si alimpokea?
 
jaman ikumbukwe chadema 2nakaribsha viongozi vijana a2taki wazee koz nafasi zao zpo ful so lowasa pambana uko uko ccm
 
Lowassa akitubu madhambi yake tumkaribishe chadema, kwani binadamu hasamehewi?
 
To be honest, wazee wangu wa chama kama mtapata kuisoma hii thread, au kama kuna mtu humu anaweza kuilink na mtandao wanaouingia afanye hivyo ili tu wapate kuisoma, na kama kwa bahati mbaya hawataelewa kwa muda huu, hakuna tatizo nitajitahidi kuirudisha humu kila wakati, na ikiwezekana nitatafuta muda niwatokee wazee wangu wa chama. Langu ni hili Chonde chonde, msimpokee EL, ni fisadi, yuko kwenye list of shame, alisababisha kubakwa demokrasia Arusha, aliingiza nchi kwenye dimbwi la hasara. Wazee wangu ninawaheshimu sana tena sana, sasa mkijipaka matope shauri yenu na hamtanilazimisha niwaheshimu tena.
 
Siamini ninachokisoma hapa..kweli EL ana mkono mrefu. Nini alichonacho EL ambacho hakipatikani ndani ya CDM?. Huyu jamaa akiingia huko haya ni baadhi ya mambo ambayo hayatakwepeka
1. Dhambi ya makundi kushamiri ndani ua chama
2. Kutoweka kwa tofauti kati ya CDM na CCM katika kupiga vita rushwa na ufisadi
3. Watanzania kuaminishwa kirahisi kwamba CDM ni chama cha kifisadi kwa kurejea matamko ya awali ya CDM dhidi ya EL, RA, CHENGE n.k
4. CDM kukimbiwa na wanachama na viongozi wengi..na labda kushihudia kuibuka kwa chama mbadala wa CDM haraka sana!


Umeona mbali mkuu! Pokea LIKE!! Ila viongozi watupe msimamo wao juu ya hili, watwambie tukimkosa Lowasa tutakosa nini na akijiunga tutapata nini.
 
Feedback, mda huu tupo kikazi zaidi,kuliondoa GAMBA CCM, na sio KULIVUA, maana lote ni GAMBA! sidhani kama tuna mda kweli wa kulijadili ni jinsi GANI lilikuwa GAMBA KAKA? ila kama walipenda GAMBA nisikukatishe tamaa, endelea nalo
 
Mzee Mtei, Mzee Makani, Dr. Slaa na Kamanda Mbowe kamwe hawataweza kuiangusha CDM kwa kumkaribisha Lowassa hata kama kasha alizonazo si za kweli kwa sababu kisiasa ni kifo kwa CDM. Hatuwezi kuua CDM kwa mtu mmoja kama Lowassa ukizingatia CDM imetambulika na kukubalika na watanzania bila msaada wa Lowassa. Lowassa aende TLP, UDP,DP, TADEA, NCCR-Mageuzi na kwingineko.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA mkoani Arusha, Samson Mwigamba, amesema kuwa yeye yuko tayari kumpokea hata Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, endapo ataamua kufanya uamuzi wa kubadilika na kujiunga na CHADEMA.

“Lowassa akiamua kuondoka CCM ni lazima atakuwa na sababu za kufanya hivyo, lakini na sisi ni lazima atatueleza juu ya tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazoelekezwa kwake, tutamsikiliza, tukimwelewa hatutakuwa na sababu ya kumnyima uanachama,” alisema.

Source: Tanzania Daima

My take: Nimeanza kuamini kuwa inawezekana kabisa Lowassa anaandaliwa mazingira ya kusafishwa.

Chama Makini kama Chadema. Hakuna kitu kama hicho........, Hakuna kitu chochote Lowassa anaweza kuwaongezea Chadema. Isitoshe Lowassa anaifanyia kazi vyema Chadema akiwa ndani ya CCM.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA mkoani Arusha, Samson Mwigamba, amesema kuwa yeye yuko tayari kumpokea hata Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, endapo ataamua kufanya uamuzi wa kubadilika na kujiunga na CHADEMA.

“Lowassa akiamua kuondoka CCM ni lazima atakuwa na sababu za kufanya hivyo, lakini na sisi ni lazima atatueleza juu ya tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazoelekezwa kwake, tutamsikiliza, tukimwelewa hatutakuwa na sababu ya kumnyima uanachama,” alisema.

Source: Tanzania Daima

My take: Nimeanza kuamini kuwa inawezekana kabisa Lowassa anaandaliwa mazingira ya kusafishwa.

Ofcourse it will be a great deal. Watanzania tumekuwa na tabia kufuata mkumbo, siamini kwamba tumewahi tafakari vyakutosha juu ya tihuma tunazo mpatia huyo mzee by the way ni nini kibaya ametufanyia kama taifa?Je ni Richmond, mbona majibu yake ameshayatoa bungeni na mchango wa JK unajulikana katika hilo na Mzee hana shida yeyeto au ni uzalendo wake? Kweli mzee anamiliki baadhi ya mali lkn tujiulize ni bora yupi anayewekeza ndani ya nchi au hawa wanaoiba nakupeleka nje ya nchi Chenge, Mkapa, Jk and others?
Kiukweli tatizo linalomkabili huyu mzee si ufisadi kama unavyo semekana ni ia yake hiyo ya kuwa Raisi! Wote hao kina SIta, Mwakyembe, Nape, Jk and Others wanapambana na Uraisi na siyo Lowasa as Lowasa.

I hope kama taifa tumejifunza mengi mpaka hivi sasa Hivi? ule uzalendo wa Sita Umeishia wapi leo, Uzalendo wa Mwakyembe, Sendeka, Kilango and others uko wapi si tunawasikia Bungeni jamani?

Wewe kama wewe unamtuhumu Lowasa kwa lipi just Be fair nad Square?

Kwachadema kuwa na uhakika wa Kuchukua urais 2015, tunahitajika kufanya zaidi, Tanzania ni kubwa our coverage todate is minimal hardly 30% so the coming of Lowasa is our Victory 2015 this is the hard Trueth.

All the Best Peopleeeeeeeeeeeeeeeeeeeees Poweeeeeeeeeeeeeeers
 
Mbowe na Dr Slaa wakimpokea Lowassa tutaanza kuwapopotoa mawe wenyewe kabla ya Lowassa wasije wakatuchelewesha kwenye mabadiriko,bwana LOWASSA hafai kwa namna yeyote ile
 
Mwenyekiti wa CHADEMA mkoani Arusha, Samson Mwigamba, amesema kuwa yeye yuko tayari kumpokea hata Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, endapo ataamua kufanya uamuzi wa kubadilika na kujiunga na CHADEMA.

“Lowassa akiamua kuondoka CCM ni lazima atakuwa na sababu za kufanya hivyo, lakini na sisi ni lazima atatueleza juu ya tuhuma mbalimbali za ufisadi zinazoelekezwa kwake, tutamsikiliza, tukimwelewa hatutakuwa na sababu ya kumnyima uanachama,” alisema.

Source: Tanzania Daima

My take: Nimeanza kuamini kuwa inawezekana kabisa Lowassa anaandaliwa mazingira ya kusafishwa.

Sitaki kabisa kusikia habari za Lowassa kuwa mwanachama wa CCM!
Sitaki kuanza kufikiri kwa habari ya rangi na taswira nyingine tofauti na ninavyoijua chama changu.
Nitajutia sana
 
Feedback mkuu wangu, hapo ulipo bold utapatenganishaje na Lowasa ikiwa aliyeshindwa Arusha ni mtu wake(Batilida)

Ukisema CCM wanaunda propaganda kumchafua mtu, usisahau kwamba hata Lowasa pia ni mmoja wao. Alafu pia Millya ishu yake ni tofauti na Lowasa, Millya hatotughalim kumsafisha, hana madhara ki-propaganda kutoka CCM lakini huyu mwizi Lowasa tukimkubali tu, tumekwisha!! Ataongea nini kwa wananchi ambao wanajua ndie aliewafikisha hapa walipo?

"HAKIKA VIONGOZI WOTE WA CDM WATAZOMEWA NA KUPIGWA MAWE KILA MAHALI KWASABABU YA HUYU MWIZI!!"
STIDE najua EL amechafuka lakini kumbuka politics is a dead game anaweza kuja na gea ya kumshambulia Kikwete, am sure wananchi wataanza kumkubali waki-refer matatizo waliyonayo na rais wao. Na nikuambie my friend, wananchi wengi vijiji hawajui makosa ya Lowassa wala hawajui Richmond ni mdudu gani ni mimi na wewe tu wenye uelewa kidogo the rest EL kwao ni hero si tunaona anavyopokewa akienda makanisani? Mimi nakwambia Lowassa akipata mpiga kinubi mzuri na Lowassa mwenyewe kuanza kumrushia madongo ya waziwazi Kikwete atarudi upya kwenye political arena. Mwisho hata mimi na wewe hatuna uhakika kama Richmond ni yake au kambebea mtu.
 
Tuseme ukweli, kashfa ya Lowassa ambayo watu wanampigia kelele ni Richmond/Dowans, kama kuna nyingine watu waseme. Sasa hii ya Richmond ladokeza kule Dom kwenye halmashauri ya magamba, kuwa mwenyewe hasa ni JK. Laiti kama atapata nafasi ya kueleza zaidi huenda tukafahamu kuwa actually Ricmond ni JK mwenyewe na yeye alitumiwa tu. Sasa kama hilo atalithibitisha na kuungama kwa watanzania kwa kukaa kimya na ukweli kwa muda mrefu kwa nini asikubaliwe CDM?
 
Ngoja ninunue hilo gazeti kwanza maana siamini kuwa ni Mwigamba ninayemfahamu. Huyu akiingia cdm siku hiyohiyo naachana nacho na kadi yao nawarudishia pale ngome

kaka tusaidie kutoorodheshea kashfa za Lowassa! Na haya mabilioni yaliyoliwa kwenye Halmashauri zetu nazo kala Lowassa. Acheni kufuata siasa za mkumbo! Serikali nzima na CCM ndio vimeoza!
 
Ngoja ninunue hilo gazeti kwanza maana siamini kuwa ni Mwigamba ninayemfahamu. Huyu akiingia cdm siku hiyohiyo naachana nacho na kadi yao nawarudishia pale ngome

siku el akihama ccm utakuwa ndo mwisho wa jk. Cdm wamesema watahitaji ajibu tuhuma zote zinazomkabili ndo wamkubali. Hapo ndipo atakapovumbua siri za uozo kati ya uchumi wetu na magamba. Siri zikianikwa hadharani ndipo wananchi wataingia barabarani, polisi watagoma,madereva wa daladala,bodaboda,taxi nao watagoma. Huu utakuwa ndo ukombozi wa nchi yetu. Lakini akija kavu kavu bila kuungama mbele ya watanzania wanaohangaika na kuendelea kunyanyasika hata mimi narudisha kadi na kuacha ushabiki wa vyama.
 
Lowassa akitubu madhambi yake tumkaribishe chadema, kwani binadamu hasamehewi?

Sio kutubu tu bali pia atatakiwa kurudisha vyote alivyojipatia kwa njia ya haramu ndipo sasa tufikirie kumpatia uanachama.

Hata hivyo sisfikirii na sitegemei hata kidogo kumuona Lowasa akijiondoa ccm. Hawezi ku survive nje ya ccm na yeye hilo analitambua sana, hawezi kufanya kosa la ku cross borders.
 
Back
Top Bottom