CHADEMA waita wanachama nchi nzima tarehe 6 Desemba, 2018

CHADEMA waita wanachama nchi nzima tarehe 6 Desemba, 2018

Mkuu Mathias Raymond Nyakapala, kwanza asante kwa taarifa hii, pili, kwa ruhusa yako, naomba niitumie sehemu ya bandiko hili kama mbegu kupandishia bandiko langu fulani.

Japo siungi mkono kitendo cha Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mbowe na Mbunge Esta Matiko kufutiwa dhamana, kwa sababu lengo la mtu kushikiliwa mahabusu no ili asitoroke kujibu mashitaka yanayomkabili, the common sense logical inaelekeza mtu kuwa Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani Tanzania, hiyo pekee tuu ni dhamana tosha, na Mbowe sio Mwenyekiti tuu wa Chadema bali pia ni Mbunge wa Bunge la JMT, hii pia ni dhamana tosha, sasa kwa kesi hii ambayo haina kichwa wala miguu, Mwenyekiti wa chama na Mbunge akimbie wapi, akimbie nini?!

Ipo haja ya kufanya mapitio ya sheria zetu kuhusu haki ya dhamana na sifa za mtu kujidhamini mwenyewe na masherti ya dhamana.

P
umenena sawia[emoji123]
 
Chadema wamechanganyikiwa
Niache shughuli zangu mbeya nije dar kusikiliza wapuuzi waliovunja sheria makusudi?
Hata kama ningeishi Tandale kwa mkunduge siwezi kuhribu nauli yangu
we[emoji126] bakia huko na NIANGUSAGE TU[emoji160] [emoji196] na usije kabisaa
wanaume tutaenda[emoji123]
 
Esther Bulaya wa CHADEMA ndio aliyeanika UOZO wa CCM kupora pesa za wastaafu

CCM nyie mna nini?

FAO LA KUJITOA

Kingu Mbunge anasema eti mifuko ya Jamii inaleta maendeleo kama Viwanda

Sasa kwa nini Wabunge, Viongozi wakuu na Maofisa wa ngazi za juu - Hawachangii?????
 
Ni jambo jema tukaungana na Mwenyekiti wetu na wengineo kufuatilia kesi inayowakabili,Ruzuku ale mwenyekiti na wengine wachache nauli ya kusikiliza hatma yake nitoe mfukoni mwangu,nikipata nitakuja.
 
Ni upumbavu wa hali ya juu,kuna muda hata huoni hauoni faida ya upinzani,wana mambo ya hovyo hovyo tu. Dawa yao ni kuwapiga pin tu miezi kadhaa lupango hao viongozi akili zirudi,mbona Lema na Sugu akili zipo zipo sasa.
Upinzani ulikuwa na Nguvu kipindi kile uTawala ulikuwa legevu
 
MGONJWA MAHUTUTI HATA KWA AKILI YAKO....
YUKO VILE?
It doesn't matter Mami !!. Watu hupata dharura, na mdhamini au wakili anakuripitia, hasira hizi za mami mwenzio kulingana na jina lake za nini ?!. Huyu mnaeonekana kumpigania sana, anailinda hiyo katiba ?!
 
It doesn't matter Mami !!. Watu hupata dharura, na mdhamini au wakili anakuripitia, hasira hizi za mami mwenzio kulingana na jina lake za nini ?!. Huyu mnaeonekana kumpigania sana, anailinda hiyo katiba ?!
kumbuka kuidanganya mahakama ni kosa.Wadhamini wameshiriki kosa hilo.Ningekuwa mimi nihakim ningefunga na wadhamini wake
 
Hapo mnajitakia shida tu,bora mtulize tu mtafute options zingine za kufikisha ujumbe
 
Haki gani ya kumtetea Mbowe aliyedanganya Mahakama kuwa yuko mahututi SA mara akaibukia Ubelgiji anapiga self na mgonjwa Lissu huku wakikenua meno kama mazuzu?!! Mahakama siyo ya kuchezea pia naamini watz hawawezi kuchezewa kiasi hicho eti waje Kisutu kwa gharama ya nani na wakikamatwa na kuwekwa lupango utawatetea wakati wapo waliondamana kwenye uchaguzi mdogo Kinondoni wanasota na kesi hata ruzuku hawapati ili ziwasaidie bali group la Mbowe ndiyo linapiga ruzuku pekee yao. Hata Kubenea anajua hivyo!
Mjinga kama wewe hastahili kujibiwa.
 
Hakuna aliyedhani kama Tanzania itafikia hatua hii; kwa sasa hatuwacheki Kongo Rwanda wala Burundi; tumo kwenye boti moja.
Aliyetenda kosa yupo huru aliyetendewa yupo kwa pirato!! Hii ndiyo Tanzania Mpya!! ambapo kudai haki yako ni kosa tena la jinai.
 
Back
Top Bottom