Mr. Django
JF-Expert Member
- Jul 25, 2014
- 1,830
- 2,434
Hivi huyu KM kiazi mlimtoa wapi huko Ufipa? Anaorganize vitu vya kijinga kabisa! Huwezi amini anatoa wito kama huu!
Kwani akiwa mahututi ubelgiji akipata nafuu arudi hapohapo bila kusubiria au picha ilikua inatoa sautiKwa hiyo Mashinji anataka kusema Mbowe alikuwa mahututi ndio maana hakufika mahakamani? Ile picha ya Ubeligiji ndio alikuwa Mahututi?
Mkuu Mathias Raymond Nyakapala, kwanza asante kwa taarifa hii, pili, kwa ruhusa yako, naomba niitumie sehemu ya bandiko hili kama mbegu kupandishia bandiko langu fulani.#BREAKING_NEWS
Chadema yaita Wanachama wake wote Nchi nzima kufika Kisutu Dar Es Salaam Desemba 6, 2018.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimewataka wanachama wake wote Nchi nzima kufika Mahakamani wakati kesi inayowakabili Viongozi wake watano itakapounguruma ili wajionee uendeshwaji wa kesi na kuamua kwa pamoja nini cha kufanya.
Wito huo wa CHADEMA umekuja Saa chache baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu kuamua kufuta dhamana ya Viongozi wawili wa Chama hicho, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Ester Matiko kutokana na kukiuka masharti ya dhamana.
Akizungumza na wanahabari, Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni Jijini Dar ES Salaam, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dkt. Vicent Mashinji amesema, "Wanachama wa CHADEMA nchi nzima, suala hili ni zito, ni nyeti na linahusu mustakabali wa nchi yetu, usisubiri kusimuliwa njoo uone mwenyewe kinachoendelea Mahakamani kwa sababu kumekuwa na upotoshaji mkubwa".
"Tunaomba tuje tusikilize wenyewe Mahakamani na baada ya hapo tuamue ni hatua gani tutachukua sisi kama Watetea haki wa Watu wote katika Taifa hili," ameongeza.
Aidha katika hatua nyingine, Chama hicho kimeazimia kukata Rufaa katika Mahakama Kuu kwa kile ilichokidai kuwa; ni kupinga juu ya hatua ya kufuta Dhamana ya Viongozi wake iliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
"Tumeamua kukata Rufaa kwenda Mahakama Kuu na tumeshawasilisha Barua yetu, bado tunasubiria watupe namna. Na katika Barua yetu tumeeleza haya mashaka yetu yote juu ya mwenendo wa hii kesi".
Chanzo; East Africa Television (EATV)
Only in Tz , especially awamu ya 5. Unataka amani, huwezi kuwasumbua wapinzani wako kwa kesi za kishenzi namna hii. Mwanzo wa hii kesi unaujua , na sababu zake unazijua . Yuko wapi mkurugenzi wa kinondoni kama unataka kutenda haki ?! Akili za waTz za hovyo sana.Nondo ameshinda kwa maelekezo ya nani? Muache uzwazwa!!! Kakiuka masharti ya dhamana ni kawaida kukumbushwa hilo.
Haki ipiTujaribu kujitambua na kuzidai haki zetu.tatizo là watanzania ni waoga kuthubutu.
Kwa ghalama ya naniTutakuja!
Ni mtazamo wakoOnly in Tz , especially awamu ya 5. Unataka amani, huwezi kuwasumbua wapinzani wako kwa kesi za kishenzi namna hii. Mwanzo wa hii kesi unaujua , na sababu zake unazijua . Yuko wapi mkurugenzi wa kinondoni kama unataka kutenda haki ?! Akili za waTz za hovyo sana.
Haki ipi
Kama bunge limeitaarifu court, kwamba mbunge ni sehemu kamati na amewakilisha taifa, bado hakimu haridhiki mpaka atimize kiu yake, utasemaje dhana yangu ?!Kwani matiku na mbowe kufutiwa dhamana wameonewa? Je walifuata masharti ya dhamana au waliyavunja makusudi
Sababu waliotoa ni kwamba ni mgonjwa yupo South Africa.. Mara tunamuona mitandaoni yupo kwa lisu UbelgijiKama bunge limeitaarifu court, kwamba mbunge ni sehemu kamati na amewakilisha taifa, bado hakimu haridhiki mpaka atimize kiu yake, utasemaje dhana yangu ?!
Furahini wakoloni weusi
iweke tuioneKwa hiyo Mashinji anataka kusema Mbowe alikuwa mahututi ndio maana hakufika mahakamani? Ile picha ya Ubeligiji ndio alikuwa Mahututi?
acha ungese we zwazwa.. wa lumumbaAcheni ujinga Ufipa, suala ni Mbowe hakufuata sheria, nakwambia hiyo mnayosema ya kukutana Kisutu CHADEMA wote, je ni kwamba mna wanachama wachache hivo?
Au ni kwamba eneo la mahakama limepanuliwa ili muenee?
Au unadhani atakayethubutu kusema anaorganize watu kufika atajuta sana anaweza kuswekwa ndani kwa kosa la kuitisha mkusanyiko
ruxuku ya fisiem anakula naniHaki gani ya kumtetea Mbowe aliyedanganya Mahakama kuwa yuko mahututi SA mara akaibukia Ubelgiji anapiga self na mgonjwa Lissu huku wakikenua meno kama mazuzu?!! Mahakama siyo ya kuchezea pia naamini watz hawawezi kuchezewa kiasi hicho eti waje Kisutu kwa gharama ya nani na wakikamatwa na kuwekwa lupango utawatetea wakati wapo waliondamana kwenye uchaguzi mdogo Kinondoni wanasota na kesi hata ruzuku hawapati ili ziwasaidie bali group la Mbowe ndiyo linapiga ruzuku pekee yao. Hata Kubenea anajua hivyo!