CHADEMA waita wanachama nchi nzima tarehe 6 Desemba, 2018

CHADEMA waita wanachama nchi nzima tarehe 6 Desemba, 2018

#BREAKING_NEWS

Chadema yaita Wanachama wake wote Nchi nzima kufika Kisutu Dar Es Salaam Desemba 6, 2018.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimewataka wanachama wake wote Nchi nzima kufika Mahakamani wakati kesi inayowakabili Viongozi wake watano itakapounguruma ili wajionee uendeshwaji wa kesi na kuamua kwa pamoja nini cha kufanya.

Wito huo wa CHADEMA umekuja Saa chache baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu kuamua kufuta dhamana ya Viongozi wawili wa Chama hicho, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Ester Matiko kutokana na kukiuka masharti ya dhamana.

Akizungumza na wanahabari, Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni Jijini Dar ES Salaam, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dkt. Vicent Mashinji amesema, "Wanachama wa CHADEMA nchi nzima, suala hili ni zito, ni nyeti na linahusu mustakabali wa nchi yetu, usisubiri kusimuliwa njoo uone mwenyewe kinachoendelea Mahakamani kwa sababu kumekuwa na upotoshaji mkubwa".

"Tunaomba tuje tusikilize wenyewe Mahakamani na baada ya hapo tuamue ni hatua gani tutachukua sisi kama Watetea haki wa Watu wote katika Taifa hili," ameongeza.

Aidha katika hatua nyingine, Chama hicho kimeazimia kukata Rufaa katika Mahakama Kuu kwa kile ilichokidai kuwa; ni kupinga juu ya hatua ya kufuta Dhamana ya Viongozi wake iliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

"Tumeamua kukata Rufaa kwenda Mahakama Kuu na tumeshawasilisha Barua yetu, bado tunasubiria watupe namna. Na katika Barua yetu tumeeleza haya mashaka yetu yote juu ya mwenendo wa hii kesi".

Chanzo; East Africa Television (EATV)
Natamani angeita wafuasi wote kwa masuala kama ya katiba mpya, mafao ya kustaafu, kuzuia watoto wa kike wenye mimba wasiende shule, vitu vinavyomgusa mwananchi moja kwa moja siyo issue personal za kiongozi wa upinzani inawafanya kuonekana kama wanatumia wafuasi wao kwa maslahi yao binafsi tu. Ni bora hata basi wangeitisha maandamano pale Lissu alipopigwa risasi naamini watu wengi wangeitikia wito hata hivyo hebu tuone itakavyokuwa hiyo 6 Desemba kwasababu upinzani wa barabarani unahitajika kwasasa, Wafuasi jitokezeni .
 
Kwa taarifa yako:

Kuna misingi 211,298 ya Chadema nchi nzima ambayo kwa mujibu wa kanuni za chama wanachama wachache sana ni 30 kwa msingi.
Kuna ofisi za Vijiji 19,191 na Kata na takribani idadi ya wanachama waliohuisha kadi zao kupitia zoezi la chadema msingi na maandalizi yake mwaka 2017 na 2018 ni 6,717,898.

Endapo wanachama 3 tu Yaani kiongozi mmoja na wanachama wa kawaida 2 wataitikia wito wa Chama kuhudhuria mahakamani Kisutu tarehe 6 Disemba hii, kutakuwa na wanachama wa Chadema 633,874 mahakamani hapo. Hii haijumuishi wapenzi na washabiki wa semokrasia na marafiki zao. Na wale wasio na Vyama au WANA CCM huru
 
Wapinzani waoga kama kungulu hamangalii hata opportunities,biashara ngumu,wakulima hali mbaya,wafanyakazi ndio usiseme,polisi wanalia,sasa kwanini msitumie mwanya huuo kuitisha maandamano ya amani nnchi nzima???mioga tuu,sanasana vicent!!!
 
Mimi nawashauri wapinzani mjikite kwenye mada ya mafao,masuala ya mahakama iachiwe mahakama hakikisheni sheria ya mafao inabadilishwa na siyo kudanganya watu mamilioni wajikusanye kwenye chumba kimoja jambo ambalo haliwezekani.
 
#BREAKING_NEWS

Chadema yaita Wanachama wake wote Nchi nzima kufika Kisutu Dar Es Salaam Desemba 6, 2018.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimewataka wanachama wake wote Nchi nzima kufika Mahakamani wakati kesi inayowakabili Viongozi wake watano itakapounguruma ili wajionee uendeshwaji wa kesi na kuamua kwa pamoja nini cha kufanya.

Wito huo wa CHADEMA umekuja Saa chache baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu kuamua kufuta dhamana ya Viongozi wawili wa Chama hicho, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini, Ester Matiko kutokana na kukiuka masharti ya dhamana.

Akizungumza na wanahabari, Makao Makuu ya Chama hicho yaliyopo Mtaa wa Ufipa, Kinondoni Jijini Dar ES Salaam, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dkt. Vicent Mashinji amesema, "Wanachama wa CHADEMA nchi nzima, suala hili ni zito, ni nyeti na linahusu mustakabali wa nchi yetu, usisubiri kusimuliwa njoo uone mwenyewe kinachoendelea Mahakamani kwa sababu kumekuwa na upotoshaji mkubwa".

"Tunaomba tuje tusikilize wenyewe Mahakamani na baada ya hapo tuamue ni hatua gani tutachukua sisi kama Watetea haki wa Watu wote katika Taifa hili," ameongeza.

Aidha katika hatua nyingine, Chama hicho kimeazimia kukata Rufaa katika Mahakama Kuu kwa kile ilichokidai kuwa; ni kupinga juu ya hatua ya kufuta Dhamana ya Viongozi wake iliyofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

"Tumeamua kukata Rufaa kwenda Mahakama Kuu na tumeshawasilisha Barua yetu, bado tunasubiria watupe namna. Na katika Barua yetu tumeeleza haya mashaka yetu yote juu ya mwenendo wa hii kesi".

Chanzo; East Africa Television (EATV)
Uongozi wa sasa umefilisika ki_fikra. Mimi kama mwana CHADEMA naona ni wakati muafaka kubadili uongozi mzima wa chama kama bado tuna nia ya dhati kuhakikisha chama chetu kinasonga mbele.
 
Ni fursa nzuri ya kuionyesha dunia unyama wanaofanyiwa wapinzani Tz.
 
Kama bunge limeitaarifu court, kwamba mbunge ni sehemu kamati na amewakilisha taifa, bado hakimu haridhiki mpaka atimize kiu yake, utasemaje dhana yangu ?!

Furahini wakoloni weusi


Alafu mbona unajina la kikenya ...?

MBOWE ALIKWENDA WAPI KIKAZI ?
 
Kama bunge limeitaarifu court, kwamba mbunge ni sehemu kamati na amewakilisha taifa, bado hakimu haridhiki mpaka atimize kiu yake, utasemaje dhana yangu ?!

Furahini wakoloni weusi
Unaongea nini punguani wewe?
 
Sasa jina ndiyo point kweli ?! Wafuasi wa watawala mbona hamnazo hivi ?! Wewe ulivyojiita njiwa, tuseme we ni ndege pori ?!. Acha ujinga
Mwambie Rais kama hatojali wilaya za Tarime na Rorya azigawe kama hupendi kusikia majina hayo.

Kuhusu Mbowe yule ni KUB . Kwa nchi zinazoheshimu democracy asingekuwa anasumbuliwa, sema tunaongozwa na watu malimbukeni wa power na democracy. Yule kikatiba anaiwakilisha taifa mahali popote na inakuwa official.

Alafu mbona unajina la kikenya ...?

MBOWE ALIKWENDA WAPI KIKAZI ?
 
Alikuwa anajaribu kama anaweza kuipaka brichi mahakama.

Haki gani ya kumtetea Mbowe aliyedanganya Mahakama kuwa yuko mahututi SA mara akaibukia Ubelgiji anapiga self na mgonjwa Lissu huku wakikenua meno kama mazuzu?!! Mahakama siyo ya kuchezea pia naamini watz hawawezi kuchezewa kiasi hicho eti waje Kisutu kwa gharama ya nani na wakikamatwa na kuwekwa lupango utawatetea wakati wapo waliondamana kwenye uchaguzi mdogo Kinondoni wanasota na kesi hata ruzuku hawapati ili ziwasaidie bali group la Mbowe ndiyo linapiga ruzuku pekee yao. Hata Kubenea anajua hivyo!
 
Endeleeni kusema Yule ni KUB utazan katiba na sheria zimemfanya mtu spesho saana kana kwamba sheria ziwe mbali naye.


Sasa jina ndiyo point kweli ?! Wafuasi wa watawala mbona hamnazo hivi ?! Wewe ulivyojiita njiwa, tuseme we ni ndege pori ?!. Acha ujinga
Mwambie Rais kama hatojali wilaya za Tarime na Rorya azigawe kama hupendi kusikia majina hayo.

Kuhusu Mbowe yule ni KUB . Kwa nchi zinazoheshimu democracy asingekuwa anasumbuliwa, sema tunaongozwa na watu malimbukeni wa power na democracy. Yule kikatiba anaiwakilisha taifa mahali popote na inakuwa official.
 
Endeleeni kusema Yule ni KUB utazan katiba na sheria zimemfanya mtu spesho saana kana kwamba sheria ziwe mbali naye.
Hujui unalolisema si shangai !! Je unajuwa ni kwa nini KUB analipwa mshahara na kuhudumiwa na serikali ?! Wakati wa In kule US, marehemu Maccain pamoja na kuwa mpinzani wake kwenye uchaguzi, tumeona akiiwakilisha American kwenye mambo mbalimbali, na hata kutembelea majeshi ktk operations zake. Hapa KUB ni kudhalilishwa
 
Back
Top Bottom