Profesa
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 905
- 624
Nimepita jangwani na nikatulia kwenye Luninga yangu nikifuatilia hotuba kem kema nzuri zenye mvuto za viongozi wa CDM. Pamoja na kufurahishwa na mengi yaliyozungumwa, kuna mambo kadhaa ambayo ningependa njiyaseme:
1. Ule umati kwa kiasi kikubwa ni wa vijana ambao wengi wanashauku kubwa ya mabadiliko, tena ya haraka maana ndoto zao hazilingani na hali halisi ya mambo. hawahawa ndio wanaoweza kuigeuka CDM iwapo haitatimiza matarajio yao. Wakipata mwingine mwenye kuwa na mvutop na hamasa, hawasiti kuelekea kwake!
2. Nimekerwa na matumizi mabaya ya muda, ni vema waandaaji wakawa wanajua watu ambao hata kama sio wasemaji wakuu, wanapaswa kuandaliwa muda wa kutosha kutokana na hoja zao kuwa moto kama akina Mh Tundu Lisu. Kumlazimisha Mh Tundulisu kutumia dk 5 ukijua fika hoja zake zina mchango mzito tu na msukumo kwa yale mnayokusudia ni udhalilishaji kwani atakapotumia muda mwingi zaidi, mnaionekana poor kwenye time management. Ama sivyo muwe mna uhakika hahitaji muda mwingi kiasi hicho maana hawezi katisha hoja.
3. Hamkuweza kuleta hamasa hasa katika kuvua gamba na kuvaa gwanda, hilo zoezi lingekuwa la kwanza mapema na Wasemaji wakuuu ndio wakamalizia kutoa hotuba.
4. Nimefurahishwa sana na uhamasishaji wa kufungua matawi, ila, pamoja na kuwa hilo ni jambo muhimu kuliko yote, bado hamkulipa uzito wa kutosha na ufafanuzi unaoeleweka, kama mtizamaji ni rahisi kufikiri Matawi hayana utaratibu yanafunguliwa tu popote na kwa idadi ya watu wowote. Sawa si vema kuleta urasimu ila ni jambo ambalo mngelihamasisha vya kutosha na kutoa ufafanuzi wa jinsi matawi yanavyoweza kukipa nguvu chama, nadhani hilo hamlioni. Uhai wa Chama chochote ni matawi imara yanayochangia kwenye ngazi za juu, na si umati unao=hang out of structure. Mnahitaji huo mfumo kama mnakusudia kuendesha serikali pamoja na mambo mengine.
Kila la kheri mnaleta changamoto nzuri kwa chama chetu cha CCM.
1. Ule umati kwa kiasi kikubwa ni wa vijana ambao wengi wanashauku kubwa ya mabadiliko, tena ya haraka maana ndoto zao hazilingani na hali halisi ya mambo. hawahawa ndio wanaoweza kuigeuka CDM iwapo haitatimiza matarajio yao. Wakipata mwingine mwenye kuwa na mvutop na hamasa, hawasiti kuelekea kwake!
2. Nimekerwa na matumizi mabaya ya muda, ni vema waandaaji wakawa wanajua watu ambao hata kama sio wasemaji wakuu, wanapaswa kuandaliwa muda wa kutosha kutokana na hoja zao kuwa moto kama akina Mh Tundu Lisu. Kumlazimisha Mh Tundulisu kutumia dk 5 ukijua fika hoja zake zina mchango mzito tu na msukumo kwa yale mnayokusudia ni udhalilishaji kwani atakapotumia muda mwingi zaidi, mnaionekana poor kwenye time management. Ama sivyo muwe mna uhakika hahitaji muda mwingi kiasi hicho maana hawezi katisha hoja.
3. Hamkuweza kuleta hamasa hasa katika kuvua gamba na kuvaa gwanda, hilo zoezi lingekuwa la kwanza mapema na Wasemaji wakuuu ndio wakamalizia kutoa hotuba.
4. Nimefurahishwa sana na uhamasishaji wa kufungua matawi, ila, pamoja na kuwa hilo ni jambo muhimu kuliko yote, bado hamkulipa uzito wa kutosha na ufafanuzi unaoeleweka, kama mtizamaji ni rahisi kufikiri Matawi hayana utaratibu yanafunguliwa tu popote na kwa idadi ya watu wowote. Sawa si vema kuleta urasimu ila ni jambo ambalo mngelihamasisha vya kutosha na kutoa ufafanuzi wa jinsi matawi yanavyoweza kukipa nguvu chama, nadhani hilo hamlioni. Uhai wa Chama chochote ni matawi imara yanayochangia kwenye ngazi za juu, na si umati unao=hang out of structure. Mnahitaji huo mfumo kama mnakusudia kuendesha serikali pamoja na mambo mengine.
Kila la kheri mnaleta changamoto nzuri kwa chama chetu cha CCM.