Kilasara
JF-Expert Member
- Dec 21, 2008
- 577
- 116
Nafuatilia kwa karibu sana mahusiano ya CHADEMA na Taasisi za nje. Zitto Kabwe, Naibu Katibu Mkuu wa CDM amenufaika katika mafunzo ya uongozi aliyokuwa akichukua huko Ujermani. Mahusiano na Konrad Adenauer Stiftung yamekuwa baina yake na CHADEMA, Zitto akiwa kama mwakilishi wa CHADEMA wakati akiwa mwanafunzi huko. Hakuna usiri wowote katika hili.
Rais Mstaafu wa Ujermani, Dk. Horst Kohler, ambaye pia ni mkurugenzi wa KAS, alipotembelea Afrika Mashariki wiki iliyopita alihutubia mkutano wa wadau wa East African Community, akiwepo Katibu Mkuu mpya wa EAC anayetokea Rwanda na Mzee Edwin Mtei, aliekuwa Katibu Mkuu wa mwisho wa EAC iliyovunjika mwaka wa 1977. Mzee Mtei pia ni Muasisi wa CHADEMA na alipata fursa ya kuzungumza na Horst Kohler. Viongozi wa CHADEMA kitaifa walikutana na Dk. Kohler kabla ya yeye kukamilisha ziara yake, na niliona picha yao katika gazeti moja la hapa nchini; ikidhihirisha hakukuwepo na usiri wowote.
Huko kujuta kwa CHADEMA, au usiri wa kuwa na mahusiano na taasisi ya KAS unatoka wapi? Kama hii taasisi ya Ujermani itatoa mafunzo kwa vijana wanaCHADEMA hakuna sababu ya kiongozi yeyote kujuta. CDM itaimarika tu.
Rais Mstaafu wa Ujermani, Dk. Horst Kohler, ambaye pia ni mkurugenzi wa KAS, alipotembelea Afrika Mashariki wiki iliyopita alihutubia mkutano wa wadau wa East African Community, akiwepo Katibu Mkuu mpya wa EAC anayetokea Rwanda na Mzee Edwin Mtei, aliekuwa Katibu Mkuu wa mwisho wa EAC iliyovunjika mwaka wa 1977. Mzee Mtei pia ni Muasisi wa CHADEMA na alipata fursa ya kuzungumza na Horst Kohler. Viongozi wa CHADEMA kitaifa walikutana na Dk. Kohler kabla ya yeye kukamilisha ziara yake, na niliona picha yao katika gazeti moja la hapa nchini; ikidhihirisha hakukuwepo na usiri wowote.
Huko kujuta kwa CHADEMA, au usiri wa kuwa na mahusiano na taasisi ya KAS unatoka wapi? Kama hii taasisi ya Ujermani itatoa mafunzo kwa vijana wanaCHADEMA hakuna sababu ya kiongozi yeyote kujuta. CDM itaimarika tu.