CHADEMA ni chachu tu, haiwezi kuikomboa Tanzania

Bayana hana mada yenye mashiko. Ni wale wale wanaotumwa kukatisha watu tamaa ya abadiliko baada ya kuona Chadema wanachanja mbunga. Hana kitu cha kuwaeleza wa tz. Ukabila na ukanda uko wapi? Huko tumeshatoka tunasonga mbele haturudi nyuma kwa sababu za kizee. Kiwewe cha nini? Kama ni yeye na wajomba zake wakae chonjo kujibu mashtaka ya wizi na matumizi mabaya ya raslimali za taifa. Hakuna pa kujificha, hatuna haja ya chama mnachotaka nyie. Jibuni hoja na mkae mkao wa kushughulikiwa kila mtu kufuatana na makosa yake kwa jamii. hatudanganyiki sisi. pole sana kwa yanayowafika sasa hadi mnapanda majukwaani kulalamika badala ya kutatua kero
 
Nafikiri mleta mada hujafanya utafiti wa kutosha au hujafanya utafiti kabisa. madai yako yameegemea kwenye mambo ambayo ccm na TBC wanataka watu wayasadiki. unapo sema chama kitakacho kubalika na wengi ni kile kilichoanzishwa na wasomi, unauhakika?wasomi wengi wanatoka mikoa hihyihiyo na siyo muda mrefu hayahaya madai yatajitokeza. kwa sisi tulioko kwenye opposition hususan CHADEMA tunakiamini chama chetu na tunamatarajio makubwa nacho. wewe na nadharia zako kaa pembeni tuache sisi tufanye mabadiliko. hivi nini duniani kisicho na kasoro? HUKO CCM udini,ukabila, kujuana ndio mambo yaliyo kithiri, wanabahati vyombo vya dola vinawasaidia kwa kiasi kikubwa.2015 kitaeleweka tu.

Kwa kumbukumbu zako CDM ilianziashwa mwaka gani? Ni mwaka gani ulianza kuona CDM ikiwa maarufu? Ni kitu gani kilifanya CDM kiwe maarufu kwa wakati huo? Nyie mliofanya utafiti wa kutosha, hebu tupeni majibu ya hayo maswali.
 
Ukiona mtu au chama kinaingiza udini ili kujikubalisha ujue kimeishiwa sera chadema wangeishiwa sera wangeweza kukurupuka na kusema raisi wetu muislamu makamu wa rais muislam,igp muislam,makamanda sijui kina kova ok tuseme hawa tusiwahesabu rais wa zanzibar muislam,makamu wa kwanza wa rais zanzibar muislam,makamu wa pili wa rais zanzibar hali kadhalika ukija kwa majaji ndio hivyo hivyo lakini chadema hawawezi kuzungumzia hayo maana wanasera za kutosha itafika sehemu mtasema biashara zinafanyika kikanda kwa nini wachaga wengi ndio wanamaduka maana hata hapo mtaani kwako ukipita huku duka la mangi ukikata pale duka la mchaga tuwe na mawazo mwanga na sio giza
 
Ukiona mtu au chama kinaingiza udini ili kujikubalisha ujue kimeishiwa sera chadema wangeishiwa sera wangeweza kukurupuka na kusema raisi wetu muislamu makamu wa rais muislam,igp muislam,makamanda sijui kina kova ok tuseme hawa tusiwahesabu rais wa zanzibar muislam,makamu wa kwanza wa rais zanzibar muislam,makamu wa pili wa rais zanzibar hali kadhalika ukija kwa majaji ndio hivyo hivyo lakini chadema hawawezi kuzungumzia hayo maana wanasera za kutosha itafika sehemu mtasema biashara zinafanyika kikanda kwa nini wachaga wengi ndio wanamaduka maana hata hapo mtaani kwako ukipita huku duka la mangi ukikata pale duka la mchaga tuwe na mawazo mwanga na sio giza

Uko sahihi kabisa nakubaliana na wewe 100%. Ndio maana na mimi napinga mawazo ya aina hiyo. Hebu check hii halafu niambie mzee MTEI alikuwa sahihi na huu udini hapa?

http://1.bp.blogspot.com/-xTseBL2c_9...00/KATIBA2.png

Ya huko nyuma labda watu waliyasahau, lakini haya ya kutaka tume ya mabadiliko ya katiba iwe na uwiano wa wateuliwa kulingana na dini zao ni nini? Sio udini?

Shaka yangu ni kuwa nikikuunga mkono mwisho CDM itakuja ishia kuwa kama CCM! Muda wa kurekebisha ni sasa.
 
Kama kuna jambo ambalo ni dhahiri kwa sasa kwa Tanzania, ni hamu ya watanzania kupata mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi. Lakini pengo kubwa linaloonekana ni kukosekana kwa nguvu na sauti moja ambayo itaungwa mkono na watanzania kutoka makundi yote ya kijamii bila kujali makabila yao, dini zao, rangi zao, jinsia n.k.
Wakati ikionekana ni wazi kuwa CCM ni chama ambacho watanzania wangependa kikae chonjo ili kupisha mabadiliko na kujikarabati upya, hakuna chama cha upinzani ambacho kinawaunganisha watanzania kufikia malengo hayo kwa mujibu wa tofauti zao.
Hii ni kutokana na kasoro mbali mbali zikiwemo za kuzuwa na nyingine ni za kweli ambazo kwa kiasi kikubwa zimeweza kuaminiwa na baadhi ya wananchi walio wengi.
Vyama vingi viliibuka na kufifia mfano TLP na NCCR kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubinafsi wa viongozi waliovianzisha, migogoro ya kimaslahi na mapandikizi kutoka chama tawala.
Mfano wa udhaifu katika vyama vya upinzania hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:

1) CHADEMA
Kwa sasa ndicho chama ambacho kinaonekana kuwa na nguvu kubwa kama chama kikuu cha upinzani.

Hata hivyo kinakabiliwa na shutuma zifuatazo:
i)Ukabila na ukanda
ii)Ukosefu wa maadili kwa watendaji wake wakuu
iii)Kutokuaminiana kati ya viongozi wake wakuu ikidhaniwa kwamba baadhi ni mapandikizi kutoka chama tawala.
iv)Dhana ya CHADEMA kwamba vyama vyote vya upinzani ni mapandikizi ya CCM, hivyo kukataa ushirikiano na vyama vingine.
v)Udini

2)CUF
Ni chama ambacho ni cha pili cha upinzani baada ya CHADEMA. Hata hivyo kinashutumiwa kwa mambo yafuatayo:
i) Udini
ii) Usultani wa viongozi wakuu kuhodhi madaraka na kutokuwapisha wengine kukamata nafasi kubwa za uongozi
iii) Kuwa na nguvu upande mmoja wa muungano

3) NCCR: Huko mwanzo kilishawahi kuhusishwa na ukanda na ukabila. Hata hivyo kwa sasa madai haya hayasikiki kwa vile nguvu zake zimepungua kama ilivyo TLP.
4) Vyama vingine vilivyobaki vinachukuliwa kama NGOs za kujipatia mapato kwa waliovianzisha.
Hizi shutma iwe zina uhakika au ni za kukisia, tukubali kuwa ni pengo kwa ukombozi wa kweli wa Tanzania na ni ngumu kuziondoa kwa sasa kwa vile jamii imeshagawanywa kwa misingi hiyo.

HITIMISHO:

Ili kukata kiu ya mabadiliko ya watanzania, ni vyema wasomi mbalimbali maarufu wanaokubalika wasiohusika na kashfa hizo hapo juu kuungana na kuanzisha chama ambacho kitakubalika na watanzania walio wengi.
Vugu vugu hili la mabadiliko ya kweli litafaa zaidi kama litaanzia kwenye taasisi za elimu ya juu.
Tukifika hapo TZ in 2015 ni vifijo na nderemo! Kinyume chake, tusahau kuingóa CCM madarakani kutokana na advantage ya mgawanyiko kutokana na tofauti tajwa hapo juu.
Weka ushabiki wa chama pembeni unapochangia hii thread! Mihemko ikikuzidi, fanya kama vile hujaiona hii thread!

Hii singo hamchoki nayo tu?
 
Kama kuna jambo ambalo ni dhahiri kwa sasa kwa Tanzania, ni hamu ya watanzania kupata mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi. Lakini pengo kubwa linaloonekana ni kukosekana kwa nguvu na sauti moja ambayo itaungwa mkono na watanzania kutoka makundi yote ya kijamii bila kujali makabila yao, dini zao, rangi zao, jinsia n.k.
Wakati ikionekana ni wazi kuwa CCM ni chama ambacho watanzania wangependa kikae chonjo ili kupisha mabadiliko na kujikarabati upya, hakuna chama cha upinzani ambacho kinawaunganisha watanzania kufikia malengo hayo kwa mujibu wa tofauti zao.
Hii ni kutokana na kasoro mbali mbali zikiwemo za kuzuwa na nyingine ni za kweli ambazo kwa kiasi kikubwa zimeweza kuaminiwa na baadhi ya wananchi walio wengi.
Vyama vingi viliibuka na kufifia mfano TLP na NCCR kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubinafsi wa viongozi waliovianzisha, migogoro ya kimaslahi na mapandikizi kutoka chama tawala.
Mfano wa udhaifu katika vyama vya upinzania hapa Tanzania ni kama ifuatavyo:

1) CHADEMA
Kwa sasa ndicho chama ambacho kinaonekana kuwa na nguvu kubwa kama chama kikuu cha upinzani.

Hata hivyo kinakabiliwa na shutuma zifuatazo:
i)Ukabila na ukanda
ii)Ukosefu wa maadili kwa watendaji wake wakuu
iii)Kutokuaminiana kati ya viongozi wake wakuu ikidhaniwa kwamba baadhi ni mapandikizi kutoka chama tawala.
iv)Dhana ya CHADEMA kwamba vyama vyote vya upinzani ni mapandikizi ya CCM, hivyo kukataa ushirikiano na vyama vingine.
v)Udini

2)CUF
Ni chama ambacho ni cha pili cha upinzani baada ya CHADEMA. Hata hivyo kinashutumiwa kwa mambo yafuatayo:
i) Udini
ii) Usultani wa viongozi wakuu kuhodhi madaraka na kutokuwapisha wengine kukamata nafasi kubwa za uongozi
iii) Kuwa na nguvu upande mmoja wa muungano

3) NCCR: Huko mwanzo kilishawahi kuhusishwa na ukanda na ukabila. Hata hivyo kwa sasa madai haya hayasikiki kwa vile nguvu zake zimepungua kama ilivyo TLP.
4) Vyama vingine vilivyobaki vinachukuliwa kama NGOs za kujipatia mapato kwa waliovianzisha.
Hizi shutma iwe zina uhakika au ni za kukisia, tukubali kuwa ni pengo kwa ukombozi wa kweli wa Tanzania na ni ngumu kuziondoa kwa sasa kwa vile jamii imeshagawanywa kwa misingi hiyo.

HITIMISHO:

Ili kukata kiu ya mabadiliko ya watanzania, ni vyema wasomi mbalimbali maarufu wanaokubalika wasiohusika na kashfa hizo hapo juu kuungana na kuanzisha chama ambacho kitakubalika na watanzania walio wengi.
Vugu vugu hili la mabadiliko ya kweli litafaa zaidi kama litaanzia kwenye taasisi za elimu ya juu.
Tukifika hapo TZ in 2015 ni vifijo na nderemo! Kinyume chake, tusahau kuingóa CCM madarakani kutokana na advantage ya mgawanyiko kutokana na tofauti tajwa hapo juu.
Weka ushabiki wa chama pembeni unapochangia hii thread! Mihemko ikikuzidi, fanya kama vile hujaiona hii thread!
Hapo kwenye nyekundu. Kuzua/kuzusha dhidi ya upinzani ni kawaida ya chama cha wezi!!CCM. Hutaweza kuanzisha chochote kisipate namna ya kupakwa matope! Unakumbuka UDINI wa CUF ulivyopandishwa chati na magamba? Unakumbuka IGP mzima wa Jeshi la polisi ananunua majambia na kuyapaka rangi ya bendera ya CUF na kutangaza kwenye chombo cha habari "yameingizwa na CUF". Watanzania wangeng'amua hiyo janja ya serikali wakapuuza na kuiunga mkono CUF tungeiondoa CCM. Unakumbuka zama za TLP na mzee Lyatonga na kisa cha yule mwana dada aliyeenda kwenye geti la Mrema na kusaula nguo zote akidai kuzalishwa na Lyatonga! unajua kuwa alikuja kukiri kupewa hela na viongozi wa serikali kufanya ule umajununi kwa ajili ya kumchafua mzee wa Kiraracha. Unakumbuka yule jamaa aliyedai kuwa Dr Slaa amemnyang'anya mke ameshakiri kuwa alilipwa na Yusuf Makamba? Hata sasa vita dhidi ya CDM na Uzushi wote ni woga wa kuona tishio la kuondoka. Tuache uvivu wa kufikiri tuiunge mkono CDM tuondoe majambazi madarakani!! Jamani!
 


UKOMBOZI toka kwa NANI?
Kama kawaida ya Wasio jua DEMOKRASIA Unahusisha CHAMA cha CHADEMA na UDINI; UHAKIKA wako UKO WAPI wakati ina Wabunge; Madiwani wa DINI MBALIMBALI?

Dr. Slaa; Mbowe; Zitto - Hao wote watatu wako DINI tofauti na Dr. Slaa na Mbowe wako Madhehebu Mbalimbali
Sasa UDINI wako UNAUTOA WAPI?

Kwasababu inaonyesha UNAONGEA kama Rais KIKWETE alipokuwa anagombea URAIS 2010; Alihusisha CHADEMA na UDINI na UKABILA lakini hakuwa na UTHIBITISHO - Na Sasa yanamtokea ya UAMSHO na SHEIKH PONDA

Kama Unaweka HOJA ni bora UWE NA UTHIBITISHO wa Kauli zako Unazozitoa; TUSITAFUTE UMASHUHURI



Nadhani mtoa mada atakuwa amekusoma vizuri mkuuu,thats is it!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hapo kwenye nyekundu. Kuzua/kuzusha dhidi ya upinzani ni kawaida ya chama cha wezi!!CCM. Hutaweza kuanzisha chochote kisipate namna ya kupakwa matope! Unakumbuka UDINI wa CUF ulivyopandishwa chati na magamba? Unakumbuka IGP mzima wa Jeshi la polisi ananunua majambia na kuyapaka rangi ya bendera ya CUF na kutangaza kwenye chombo cha habari "yameingizwa na CUF". Watanzania wangeng'amua hiyo janja ya serikali wakapuuza na kuiunga mkono CUF tungeiondoa CCM. Unakumbuka zama za TLP na mzee Lyatonga na kisa cha yule mwana dada aliyeenda kwenye geti la Mrema na kusaula nguo zote akidai kuzalishwa na Lyatonga! unajua kuwa alikuja kukiri kupewa hela na viongozi wa serikali kufanya ule umajununi kwa ajili ya kumchafua mzee wa Kiraracha. Unakumbuka yule jamaa aliyedai kuwa Dr Slaa amemnyang'anya mke ameshakiri kuwa alilipwa na Yusuf Makamba? Hata sasa vita dhidi ya CDM na Uzushi wote ni woga wa kuona tishio la kuondoka. Tuache uvivu wa kufikiri tuiunge mkono CDM tuondoe majambazi madarakani!! Jamani!

Nimekukubali! Atleast unakuja na hoja badala ya kauli dhaifu. Ila naomba nijibu yafuatayo ili tuamini kwamba ni propaganda ziizokuwa za kweli. This came from the mouth of Edwin Mtei - Muasisi na mshauri wa karibu wa CDM. Huyu naye anaizulia CDM ili ife?

http://1.bp.blogspot.com/-xTseBL2c_9...00/KATIBA2.png

Ya huko nyuma labda watu waliyasahau, lakini haya ya kutaka tume ya mabadiliko ya katiba iwe na uwiano wa wateuliwa kulingana na dini zao ni nini? Sio udini?

Shaka yangu ni kuwa nikikuunga mkono mwisho CDM itakuja ishia kuwa kama CCM! Muda wa kurekebisha ni sasa.
 
Kwanza huyo jamaa mimi namuona yeye ndiyo mbaguzi kwa nini aseme kianzishwe chama cha wasomi ina maana wasio wasomi hawana nafasi ya kuchangia mabadiliko wakiwa wanachama??? Nadhani hata uelewa wake una kasoro na kama kapita shule basi alinunua mitihani kwa kutumia pesa ya ada ya shule au pocket money alopewa na wazazi wake shame on him/her

CHADEMA hakiwezi kukosa mapungufu,pengine aliyoyaandika siyo 100% lkn it may be true to some % km ilivyo kwa vyama vyote Kikiwemo Chama Cha Majangili.siyo muda sahihi kuanza kuunda vyama vipya leo,cha msingi tuendelee kufanyia kazi baadhi ya tuhuma zinazoweza kuwa za kweli,binafsi naamini CHADEMA kinashika dola kuanzia nov 2015
 
Nimekukubali! Atleast unakuja na hoja badala ya kauli dhaifu. Ila naomba nijibu yafuatayo ili tuamini kwamba ni propaganda ziizokuwa za kweli. This came from the mouth of Edwin Mtei - Muasisi na mshauri wa karibu wa CDM. Huyu naye anaizulia CDM ili ife?

http://1.bp.blogspot.com/-xTseBL2c_9...00/KATIBA2.png

Ya huko nyuma labda watu waliyasahau, lakini haya ya kutaka tume ya mabadiliko ya katiba iwe na uwiano wa wateuliwa kulingana na dini zao ni nini? Sio udini?

Shaka yangu ni kuwa nikikuunga mkono mwisho CDM itakuja ishia kuwa kama CCM! Muda wa kurekebisha ni sasa.
Ukisema kurekebisha nitakuelewa!! lakini ukija na hoja dhaifu kuwa tuanzishe sijui kikundi sijui chama hujatatua Uzushi wa = CCmajambazi.
Hayo ya mtei ni maoni yake binafsi na siyo uunganishe kila hoja na kila maneno ya wanachama wa CDM na CDM! Ni uonevu!!
 
Ukisema kurekebisha nitakuelewa!! lakini ukija na hoja dhaifu kuwa tuanzishe sijui kikundi sijui chama hujatatua Uzushi wa = CCmajambazi.
Hayo ya mtei ni maoni yake binafsi na siyo uunganishe kila hoja na kila maneno ya wanachama wa CDM na CDM! Ni uonevu!!

Hili ni pigo la kwanza kwa CDM. Ikiwa mlezi ana mawazo mabovu unahisi mtoto atakuzwa katika misingi ya tabia njema? In short mtoto huchukua tabia za mlezi wake! Unajitetea vipi hapo?
 
Mdau umeanza na kujikita kwenye Umoja wa Kitaifa lakini umehitimisha kwenye Utengano kuanzaisha chama kingine yaani kuongeza vyama zaidi i.e. Divide and Rule nadhani hiyo itaisaidia zaidi CCM! Bora Ungesema vyama hiavi viungane au Vishirikiane au vikemee mbegu hii ya UDINI, UKABILA na UKANDA maana kama mbegu ipo utakuwa umebadili jina au COVER lakini simu ileile!


HITIMISHO:

Ili kukata kiu ya mabadiliko ya watanzania, ni vyema wasomi mbalimbali maarufu wanaokubalika wasiohusika na kashfa hizo hapo juu kuungana na kuanzisha chama ambacho kitakubalika na watanzania walio wengi.
Vugu vugu hili la mabadiliko ya kweli litafaa zaidi kama litaanzia kwenye taasisi za elimu ya juu.
Tukifika hapo TZ in 2015 ni vifijo na nderemo! Kinyume chake, tusahau kuingóa CCM madarakani kutokana na advantage ya mgawanyiko kutokana na tofauti tajwa hapo juu.
Weka ushabiki wa chama pembeni unapochangia hii thread! Mihemko ikikuzidi, fanya kama vile hujaiona hii thread!
 
Hili ni pigo la kwanza kwa CDM. Ikiwa mlezi ana mawazo mabovu unahisi mtoto atakuzwa katika misingi ya tabia njema? In short mtoto huchukua tabia za mlezi wake! Unajitetea vipi hapo?
Acha mambo ya ajabu wewe Ulezi hauna maana ya kusaidiwa kufikiri!! au kuamua au kuchambua!! Ule ujinga wa zidumu fikra za--- hauko CDM pole ndugu. Upo kwa Chama cha wezi.
 
Mdau umeanza na kujikita kwenye Umoja wa Kitaifa lakini umehitimisha kwenye Utengano kuanzaisha chama kingine yaani kuongeza vyama zaidi i.e. Divide and Rule nadhani hiyo itaisaidia zaidi CCM! Bora Ungesema vyama hiavi viungane au Vishirikiane au vikemee mbegu hii ya UDINI, UKABILA na UKANDA maana kama mbegu ipo utakuwa umebadili jina au COVER lakini simu ileile!

You have a point. Lakini CDM haioni wa kuungana naye, kwa vile inaonekana haiwaamini wapinzani wengine. Halafu ikwa mlezi wa CDM ndiye mwenye mawazo ya udini, unafikiri utafanikiwa kirahisi? Watoto ni pro-baba, hawawezi kumtupa muasisi >> I mean Mzee Mtei.
 
Dhana ya kuhamasisha wasomi na makundi mengine ya jamii kuungana na kuunda chama kipya cha siasa kisicho na "udini', "ukabila" na ukibaraka wa ccm ni moja ya mbinu kubwa za ccm kuvuruga mwenendo wa upinzani wenye nguvu tanzania, tuhuma zote zinazosikika kwa wapinzani waliofanikiwa zimeasisiwa na ccm, ndio maana naona shaka na mtoa mada kama kweli amefanya utafiti au naye nisehemu ya mkakati wa kuvuruga upinzani wenye nguvu.
 
Acha mambo ya ajabu wewe Ulezi hauna maana ya kusaidiwa kufikiri!! au kuamua au kuchambua!! Ule ujinga wa zidumu fikra za--- hauko CDM pole ndugu. Upo kwa Chama cha wezi.

Sasa mbona kama chama hamkumkanya na kuupinga udini wa mzee Edwin MTEI ili sisi raia wengine tuone kuwa you are not supporting the same. Mashaka yangu ni kuwa mnafuata mtindo ule ule wa zidumu fikra za m/kiti! Mlezi siku zote ana influence na ku shape your way of thinking! Ulikuwa hujui? Waulize wazee watakwambia.
 
You have a point. Lakini CDM haioni wa kuungana naye, kwa vile inaonekana haiwaamini wapinzani wengine. Halafu ikwa mlezi wa CDM ndiye mwenye mawazo ya udini, unafikiri utafanikiwa kirahisi? Watoto ni pro-baba, hawawezi kumtupa muasisi >> I mean Mzee Mtei.
Kwa hiyo Bayana ni Gamba! nimepoteza muda kumjibu! vizuri anajitahidi kutafuta visingizio vya kitoto!!
 
Back
Top Bottom