CHADEMA ngoma mbichi Arusha

Sina tu katiba ya Chadema lakini nina hakika wakienda mahakamani kudai haki yao ya kuondolewa uanachama wao na sababu walizotoa CC ya Chadema nina imani watarudishwa kwa amri ya mahakama na kuendelea na udiwani wao.

lakini vile vile nina imani kama uchaguzi utafanyika katika kata zote hizo tano CCM watachukua kata zote kwani wananchi wamechoshwa na malumbano kila siku bali wanataka maendeleo. na hapo sasa kutakuwa hakuna haja ya muafaka baina ya CCM na Chadema.
Kama hata katiba ya Chadema huna hizo imani zinatoka wapi.........wewe endelea tu kuwa na imani zako.
 
Hongera CC Chadema kwa kuonyesha mfano wa kutoa maamuzi magumu, hakuna anayemiliki CDM bwana! Tatizo hapa siyo kurudisha seats ila kuondoa majambawazi ndani ya chama
 
Kwanza nitafurahi kama utanipa link ya kuweza kuipata hiyo katiba ya Chadema ili niipitie.

lakini naomba ujue kuwa Lema npamoja na kuwa Mbunge lakini ni sehemu ya baraza la madiwani wa hapo Arusha. Hivyo kwa namna yoyote ile taarifa za muafaka ule alikuwa nazo kwani pasi na shaka ulikuwa ni mchakato ulioitishwa kisheria na kwa barua na minutes ambazo hata kama hujaudhulia lakini minutes alizipata hivyo kujua mchakato mzima.

na kama kweli alikuwa hajui basi yeye atakuwa yupo mbali sana na madiwani wake kiutendaji ima anakuwa mbame au mjuvi. lakini ni lazima alikuwa na taarifa. Kitendo cha kuwakana kinaonyesha yeye ni kiongozi Mnafiki na asiyefaa kabisa kuiongoza jamii ile ya machalii wangu wa pale Arusha.

Nafikiri amepoteza umaarufu wake na wa chama chake hapo Arusha kwani siku zote wananchi wa Arusha hawataki malumbano bali wanataka maendeleo yaani barabara zao za kule kaloleni, mbauda, majengo na hata njia yetu ya kwenda shuleni kwetu Ilboru kupitia BINO road au ile ya Mianzini ziitiwe lami.

natabili mwisho wa Lema hapo Arusha. Bora arudi shemeji yetu


Nimekuwekea link ya katiba ya CHADEMA huko juu kama hukuiona hii hapa tena Gonga hapa

nainaonekana kama hujui kilichotokea kwenye sakata hili hebu msome Dr. Slaa hapa chini…

1) Msingi wa mgogoro wa Madiwani Arusha ni Uvunjifu wa Kanuni, Taratibu na Sheria zinazoongoza uchaguzi wa U meya katika Manispa ya Arusha. Kamati ya Marando imebaini kuwa "mchakato na utaratibu mzima wa uchaguzi wa Naibu Meya haikuzingatia Kanuni na Taratibu za Chama na Halmashauri" (Marando Kif.4.2). Hivyo, kama Chadema ilipinga ukiukwaji katika uchaguzi wa Meya, haiwezi kamwe kuidhinisha ukiukwaji ambao kwa bahati mbaya ni maradufu zaidi katika uchaguzi wa Naibu Meya.

2) Ni kweli mazungumzo husika yalijulikana kwa ngazi ya Taifa. Mara ya kwanza Makao Makuu yalifahamu document ya mwafaka ya 15/4/2011, kwa kuona document tarehe 29/4/2011 katika Mkutano baina ya viongozi wa Madiwani akiwemo Mwenyekiti wao Mhe. Mallah na Mnadhimu Mkuu wa Kamati ya Madiwani Mhe. John Bayo. Kikao kilifanyika New Safari Hotel, Arusha chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu. Miniti za Kikao hicho zinaonyesha mambo 5 ambayo Katibu Mkuu alibainisha kama msingi wa mazungumzo yeyote kama yatakuwepo. Nayo ni:-

i)Serikali ikiri kosa kuwa kanuni na mwongozo wa uchaguzi wa Meya Arusha mjini zilikiukwa.
ii)Uchaguzi wa Umeya urudiwe kwa vile haukufuata kanuni na Taratibu.
iii)Serikali itoe pole kwa wahangaa tukio la tarehe 5 Januari 2011
iv) Serikali ipitie madai ya msingi ya Chadema ikiwa ni ni kuwawajibisha Mkurugenzi wa Manispaa (kwa sababu ndiye alivunja kanuni) na OCD wa Arusha mjini
v) Kesi ya ya Viongozi wa chama na baadhi ya wananchi haina msingi hivyo ifutwe.

Kisha kikao kilijadili document ya 15/4 na kuona ina mapungufu makubwa. Iliazimiwa ifuatavyo:-
1) Miniti hii ina hila na ni ya unafiki na hivyo isitumike katika kufikia muafaka wa suala la Umeya hapa Arusha mjini.
2) Mwenyekiti wa Madiwani Estomih Mallah na Mnadhimu wa Madiwani Mhe. John Bayo wawajulishe madiwani na Mkuu wa Wilaya kuwa muafaka huu kwa mujibu wa chama una mapungufu ambayo chama hakitaweza kuyaafiki na hivyo usitumike kwa kufikia muafaka wowote.
3) Kwa kutambua kuwa CCM wapo tayari kwa mazungumzo, Mhe. Katibu Mkuu atayapeleka mapendekezo ya muafaka huu kwa wanasheria wa chama ili kuyafanyia marekebisho na mapendekezo hayo yatakuwa ni sehemu ya mazungumzo kati ya Mwenyekiti wa Chama Mhe. Freeman Mbowe (MB, KUB na Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda.

Kwa bahati mbaya, tarehe 20/6/2011 Madiwani waliridhia mwafaka wao kama ulivyokuwa kwenye Hati yao ya tarehe 15/4/2011, na kuendelea na uchaguzi, bila kujali mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea kati ya Mhe. Mbowe na Waziri Mkuu. Isitoshe utaratibu wa kisheria wa uchaguzi wa Naibu Meya nayo ilikiukwa (kwa mujibu wa Taarifa ya Marando kukiwa na kugushiwa kwa saini ya Katibu wa Wilaya wakati pia hakuna kikao chochote cha Kamati Tendaji kilichojadili na kuteua mgombea wa Chadema). Hiki ndicho kilichofikisha Kamati Kuu kuelekeza Madiwani waliochaguana kinyume na Kanuni wajiuzulu ndani ya siku 3.

Baada ya hapo Madiwani 6 wakiongozwa na Mallah walikata rufaa, kwa bahati mbaya kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chama rufaa zao hazikukidhi mahitaji ya Kikatiba na Kanuni. Maswala yote hayo sasa yanarudi mikononi mwa Kamati Kuu ambayo hivi Karibuni itatolea ufumbuzi swala la Madiwani kwa mujibu wa Katiba ya Chadema.
 
Yaani kwa kweli, ninaombea sana ishu ya madiwani Arusha isije kuvuruga CDM, wananchi waelewe tu kwamba chama hakiwalei watu wanaokiuka utaratibu na kufanya mambo kinyume na utaratibu tuliojiwekea!
 
Chadema walitenda haki kuwaondoa magamba yaendelee kutapatapa wataishia tum na magamba yao waende CCM sasa wakatetee ugamba wao.Chademe juu na chama tawala 2015.
 
Swala la wao kwenda mahakamani ni kupoteza muda ili angalau waendelee kula bata kidogo kwa tiketi ya cdm. Ukweli ni kwamba mahakama haiwezi kutengua maamuzi yaliyofanyika kwa mujibu wa katiba!
 
Kwa uchanga wa fikra, inaonekana kama ngoma mbichi, lakiini chama chochote kisichozingatia kanuni, hupoteza dira. Kumbuka maneno ya Kolimba. Hagereni sana CDM kutoa picha ya good ledership (Not good governance).
 
Shughuli ya Arusha ni nzito, CDM hawawezi kutetea viti vyote hivyo. Madiwani walichagliwa kw anguvu ya Umma, leo wanatolewa kwa nguvu ya CDM CC.

Hapa umegonga penyewe hasa. Viti 5 vya madiwani wameshavikosa maana vyote vitarudi CCM. Ile nguvu ya umma iliyowachagua mbunge Lema na hao madiwani si nguvu ya CHADEMA au Dr Slaa, ingekuwa hivyo CHADEMA kingeshinda nchi nzima. Ni nguvu ya watu wa Arusha, ambayo akina Slaa na Mbowe wameamua kuipuuza. Elimu ni ghali.
 
Hapa umegonga penyewe hasa. Viti 5 vya madiwani wameshavikosa maana vyote vitarudi CCM. Ile nguvu ya umma iliyowachagua mbunge Lema na hao madiwani si nguvu ya CHADEMA au Dr Slaa, ingekuwa hivyo CHADEMA kingeshinda nchi nzima. Ni nguvu ya watu wa Arusha, ambayo akina Slaa na Mbowe wameamua kuipuuza. Elimu ni ghali.
Karibu kesho kwenye mkutano wa CDM.
 
Nimesoma tena sakata zima nimegundua kuwa bado Kamati kuu ya CHADEMA iko sahihi katika uamuzi wake wa kuwafukuza madiwani hao uanachama kwa utovu wa nidhamu.

Madiwani hao 5 wamedhihirisha kuwa hawasimamii tena msingi ambao chama chao kiliweka kuhusu suala hili, kwa hiyo hawawezi tena kuendelea kuwa ndani ya chama hicho. Kwa bahati mbaya, bado itawagharimu CHADEMA kukosa viti hivyo.
 
Karibu kesho kwenye mkutano wa CDM.
Makamanda wameshaanza kuingia na leo watafanya mikutano kwenye kata zifatazo Elerai atakuwepo wenje na makamanda wengine, Kimandolu sijajua nani atakuwepo huko, Mjini kati atakuwepo Tundu Lisu na wabunge viti maalumu....ila kazini ni kesho hapo NMC
 
Swala la wao kwenda mahakamani ni kupoteza muda ili angalau waendelee kula bata kidogo kwa tiketi ya cdm. Ukweli ni kwamba mahakama haiwezi kutengua maamuzi yaliyofanyika kwa mujibu wa katiba!

hata wao vile vile watakwenda kudai kuwa wameondolewa uanachama wao na kuona kuwa katiba ilikiukwa.

Ndio maana kuna mahakama ambayo inatoa haki kwa pande zote kuleta hoja na kisha mahakama inatoa haki kwa upande mmoja.

wana kila haki ya kwenda mahakamani kudai haki yao walioporwa.
 
Kama hata katiba ya Chadema huna hizo imani zinatoka wapi.........wewe endelea tu kuwa na imani zako.

Kutokana na kusoma tamko lililotolewa la kuwavua uanachama madiwani hao. Kimsingi na Elimu yangu hafif ya Sheria naona kuna mengi sana yamekiukwa na wana nafasi kubwa sana kuwashinda kama watawapeleka mahakamani.

Kwenye katiba ya CHADEMA nilitaka kuona kipengele kimoja tu cha KUFUKUZWA UANACHAMA ili niweze kutoa comment zangu kwa uhakika ingawa kwa aina yoyote wana nafasi kubwa kuwashinda mahakamani kutokana na mazingira na hoja hafifu zilizotumiwa na CC ya Chadema kuwaengua.
 
Bwana Kithuku

Nimependa jinsi ulivyojifahamisha muda mfupi na kuweka tena mawazo mapya baada ya kusoma! Nahisi mara nyingi watu wengi tunakuja na judgements kabla ya kujiridhisha na kile tunacho-conclude.

Binafsi pamoja na kwamba si mwanachama wa chama chochote cha siasa ni mpenzi wa CDM. Hata hivyo nilifurahishwa na kipindi kilichotumika kwa CDM kufatilia mzozo huu kabla ya kuja na maamuzi haya. Sidhani kama CDM CC hawakufanya uchambuzi wa kutosha (kisheria na kimadhara kuhusu kata hizo) kabla ya kuja na maamuzi ya kuwafukuza. Yumkini kila aliyesoma yale ambayo Dr Slaa aliandika kuhusu chanzo cha mgogoro atajua CC ya CDM wanajua athari za maamuzi yao, na pengine inaweza kuwa ni spring-board to higher levels of political win.
Nimesoma tena sakata zima nimegundua kuwa bado Kamati kuu ya CHADEMA iko sahihi katika uamuzi wake wa kuwafukuza madiwani hao uanachama kwa utovu wa nidhamu. Madiwani hao 5 wamedhihirisha kuwa hawasimamii tena msingi ambao chama chao kiliweka kuhusu suala hili, kwa hiyo hawawezi tena kuendelea kuwa ndani ya chama hicho. Kwa bahati mbaya, bado itawagharimu CHADEMA kukosa viti hivyo.
 
Mtafaruku wa kisiasa ndani ya CDM halmashauri ya manispaa ya ARUSHA unazidi kuendelea. Madiwani waliofukuzwa na CDM wameandaa kikao jioni ya leo mjini Arusha kwa lengo la kuwapa wananchi hali halisi kuhusiana na sakata zima la CDM hapo A town. Tunaomba kwa mwenyezi mungu, sakata la CDM liishe salama ili chama kizidi kuchanja mbuga na kushiriki vizuri mchuano wa IGUNGA wasije kupata kisingizio watapopata kipigo cha mbwa mwizi jimboni IGUNGA wasije na kisinngizio cha mtafaruku wa A town.

Rudini CCM there is only where you are allowed to be stupid, msitupotezee muda!
 
Rudini CCM there is only where you are allowed to be stupid, msitupotezee muda!

ni chama kimoja tu chenye uerevu na kutetea wanyonge hawa waliionewa na CDM. Ni CCM please tunawaomba muwapokee hawa watumishi wema ili waende kwa kasi zaidi nguvu zaidi na zaidi.

Hivyo basi warudi CCM watarudisha diwanii zao na kujenga A town. kwa kweli kule wasihangaike hakuwafai kabisaa na kesi futeni watapoteza muda tu.
 
Back
Top Bottom