CHADEMA ngoma mbichi Arusha

CHADEMA ngoma mbichi Arusha

Shughuli ya Arusha ni nzito, CDM hawawezi kutetea viti vyote hivyo. Madiwani walichagliwa kw anguvu ya Umma, leo wanatolewa kwa nguvu ya CDM CC.
acha tusitete hata kata moja lakini heshima itakuwepo...wewe ni sawa na Mwanaume unamfuma mkeo analiwa na jamaa halafu unasita kutoa maamzi kisa utapata wapi mke mzuri kama yeye....
 
Wao wanaitisha kikao na kina nani?
Wanaitisha kikao kama nani?
TUNAWASUBIRI.
 
Maamuzi haya ndiyo tuliyasubiri kwa muda mrefu, ni maamuzi makini na yenye nia ya kujenga kitu ambacho kimekosekana hapa nchini, ni maamuzi yanayolenga kuipeleka nchi kwenye utawala wa kufuata sheria na uwajibikaji.

Kwa Maamuzi haya napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa CC ya Chadema, mmefanya kile ambacho wengi tulitaka kukisikia, na ieleweke hakuna mtu muhimu kuliko chama kwa maendeleo ya taifa hili, na pia ieleweke hata kama uchaguzi ukirudiwa na ukafanyika kwa haki na kufuata taratibu na sheria na ccm wakashinda kata zote itakuwa sawa kuliko kubakia na watu waliowarafi wa madaraka na kama ikitokea hivyo yatakuwa ni maamuzi ya wana wa A town. lakini ninaimani na wana A town na ngoja tusubiri uchaguzi na kata zote zitarudi Chadema.

na ikithibitika kwamba Meya aliyeingia office kwa kuvunja taratibu amehusika katika kuwa rubuni tuwajulishe magamba nao waone ukweli na wafanye maamuzi magumu kama wataweza.
 
Unajua watu hawajuhi Gharama wa walichokuwa wankifanya hawa madiwani, Mimi nawashahuri wote wanao pinga wakamuulize Prof. LIPUMBA ni nini gharama ya Ndoa ya CUF na CCM zanzibar kwa CUF Bara.
 
hayo ni maamuzi mepesi yalofanywa na CDM ambayo CCM mnaona ni mazito..............SHAME UPON U CCM
 
Madiwani watano wa CDM, waliovuliwa uanachama na Kamati kuu ya chama hicho mwishoni wa wiki iliyopita wanakwenda mahakamani kupinga uamuzi huo.
Diwani wa Kata ya Elerai, John Bayo, alieleza kwa njia ya simu akiwa njiani kutokea Dodoma walipokwenda kuhojiwa kabla uamuzi wa kutimuliwa kufikiwa.
Bayo alisema kabla ya kuchukua uamuzi wowote watazungumza na wapiga kura kwenye kata zao kuwaeleza yaliojiri na kuacha nafasi ya uamuzi wa hatua zinazostahili mikononi mwa umma uliwaamini na kuwapa dhamana yb uongozi.
"Binafsi sina kinyongo na chama changu nimepokea nimepokea uamuzi huo, lakini nakuhakikishia nitaendelea na nafasi ya udiwani hadi uchaguzi mkuu ujao, kuna njia nyingine ya kupinga uamuzi huo kupitia vikao au mahakama" alisema Bayo.

SOURCE: Gazeti la habari za kiswahili la kila siku Tanzania, linaongoza
8 August 2011

Hakika kwa namna yoyote ile kama suala la kufukuzwa Chama kwa sababu ambazo CC ya Chadema wamezitoa sidhani kama zitakidhi haja na kuweza kuwaengua. Kwa kuwa sina katiba ya Chadema ningeweza kuisasambua kuliangalia hilo. Lakini naamini wakienda mahakamani watashinda pasi na shaka kwani walifanya muafaka kwa nia njema ya kuleta amani na ustawi wa jamii ya watu wa Arusha.

Hakika Chadema walishindwa kusoma alama za nyakati kwa kushinda kufahamu kuwa wananchi Arusha wanataka maendeleo na sio malumbano.
 
Mimi namweshimu sana crashwise kwa jinsi anavyotuletea habari za AR lakini siku za hivi karibuni anaonekana kama kaumizwa na kitendo cha madiwani kufuzwa ila bado anajitahidi sana ku balance habari asionekane yuko upande gani.


Mkuu Feedback
,
Ni kweli nakiri kuwa jambo hili limeniumiza si lakini haiimanishi nimechakachuliwa. kwanini limeniumiza kama nilivyosema huko juu baadhi ya madiwani niliwapigania kuhakikisha wameshinda na kwa rekodi zao huko nyuma tangu walivyokuwa CCM, CUF/NCCR mpaka CHADEMA zilikuwa hazina mushikeli hivyo ziliniaminisha kuwa hawa ni wasimamia haki labda nikukumbushe kuwa siku chache kabla ya uchaguzi wa meya CHADEMA ilificha madiwani wake isipokuwa baadhi akiwemo Malla na Bayo, unajua kwanini? walikuwa wana waamini sana kuwa hawawezi kununuliwa na Magamba ukizingatia ndiyo waliokuwa wagombea.

2. huwa sipendi kumshambulia mtu kabla sijapata ukweli ndiyo maana siku za mwanzo za sakata hili pengine nilikuwa sieleweki lakini kwa mtu makini utajua niko wapi huhitaji Phd kulitambua hilo kwani kwangu

Kuwa-neutral mwiko naweza kuwa neutral wakati natafuta ukweli tu, madiwani waliofukuzwa ulikuwa ukiwauliza wanasema makao makuu wana taarifa zote za majadiliano mpaka muafaka na walikuwa wanasema hata kabla ya kukubaliana waliwajulisha makao makuu na kusema kinachoendelea na fitina za mbunge..nikafunga safari kwa diwani wa TLP akaniambia kuwa makao makuu wanajua kilichokuwa kinaendelea isipokuwa ni vita ya ubunge ya mwaka 2015 nikamuulizaVipi juu ya waliokufa na majeruhi ambao wengine wana hatari ya kukatwa miguu mpaka sasa, vipi swala la Mary Chitanda, vipi kuhusu kesi ya viongozi wa CHADEMA ambayo kimsingi chanzo ni hili swala mliloingia mwafaka na CCM alichonijibu ni kuwa tuyaache yapite kwani CCM kamwe hawako tayari kukaa meza moja na CHADEMA na wanachokifanya kwasasa madiwani wa CHADEMA yaani kususia kuhudhuria vikao ni kama kususia nyama dhidi ya fisi atakula tena atafurahi sana labda kama CHADEMA inamajeshi waingie vitani hapo ndipo wanaweza kutekelezewa matakwa yaolakini zaidi wananchi wataendelea kuumia na akasisitiza kuwa CHADEMA taifa walikuwa na taarifa juu ya yote yaliyokuwa yanaendelea swali kwangu likawa kwanini kama makao makuu walikuwa na taarifa waliwageuka, nikaongea na Nanyaro ambae tangu siku ya mwafaka yeye aliupiga bila kujingatangata na alinieleza walichokifanya Malla, Bayo na siku chache baadae Dr. Slaa alianzisha thread hapa (JF) na kuliweka vizuri swala hili hapo ndipo nilipojua akina Malla na Bayo ni wasaliti na maandamano waliyoyafanya jumamosi hapa napo nilizidi kupata ukweli kuwa kweli jaamaa wamedhamiria kukichafua chama na hawastahili kuendelea kubaki CHADEMA kwani wameonyesha uroho wa madaraka na upeo mdogo sana kwani nikuhakikishie aliyepanga maandamano ya watu wasiozidi 17 yaliofanyika Jumamosi na kwenda kwenye ofisi ya CHADEMA mkoa kutaka kuifunga ni mtu wa karibu sana na Bayo na anavijisenti na aliwachukua viongozi wa kata ya kaloleni na themi ambaye mmoja ni kinyozi na kuwalipa vijisenti ili kutekeleza adhma hiyoNilibahatika kumuona jioni yake huyu Emma(Kinyozi) alivyokuwa anafakamia bia ungeweza kuzani labda ni mkurungezi wa mashirika kama TANAPA
 
Maamuzi haya ndiyo tuliyasubiri kwa muda mrefu, ni maamuzi makini na yenye nia ya kujenga kitu ambacho kimekosekana hapa nchini, ni maamuzi yanayolenga kuipeleka nchi kwenye utawala wa kufuata sheria na uwajibikaji.

Kwa Maamuzi haya napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa CC ya Chadema, mmefanya kile ambacho wengi tulitaka kukisikia, na ieleweke hakuna mtu muhimu kuliko chama kwa maendeleo ya taifa hili, na pia ieleweke hata kama uchaguzi ukirudiwa na ukafanyika kwa haki na kufuata taratibu na sheria na ccm wakashinda kata zote itakuwa sawa kuliko kubakia na watu waliowarafi wa madaraka na kama ikitokea hivyo yatakuwa ni maamuzi ya wana wa A town. lakini ninaimani na wana A town na ngoja tusubiri uchaguzi na kata zote zitarudi Chadema.

na ikithibitika kwamba Meya aliyeingia office kwa kuvunja taratibu amehusika katika kuwa rubuni tuwajulishe magamba nao waone ukweli na wafanye maamuzi magumu kama wataweza.
kwa ujumla nimefurahia sana na maamuzi ya chadema! ilikuwa hakuna njia nyinggine
 
Si kweli kabisa, Habari ya Arusha ndo imeshaisha vizuri kabisa na pengine itaiongezea sifa Chadema kama ilivyoripotiwa leo na baadhi ya magazeti. Hivi hawa madiwani wakikodi magari na kutoa matangazo ya mkutano wao, watasemaje? Maana hawawezi tena kutumia jina la Chadema.

Ama watatumia majina yao?
Sikutegemea John Bayo niliyemfahamu japo kidogo angefanya uamuzi wa kitoto namna ile. Am very sorry for him.
 
Ni wewe wasema! Tuliwachagua kwa kudhani ni watu kumbe ni viatu! Subiri uchaguzi ufanyike ndo utaelewa maana yake!

Mkuu ni kweli uchaguzi utafanyika?!!!!!!!!! siasa bwana ukiijua poa! usipoijua wewe ni shabiki.

nisiulizwe kwa nini hautafanyika wait nd si!
 
naomba mwenye link ya thread aliyoweka dr Slaa kuelezea haya mambo aiweke ili tulioikosa tuipitie.
 
Si kweli kabisa, Habari ya Arusha ndo imeshaisha vizuri kabisa na pengine itaiongezea sifa Chadema kama ilivyoripotiwa leo na baadhi ya magazeti. Hivi hawa madiwani wakikodi magari na kutoa matangazo ya mkutano wao, watasemaje? Maana hawawezi tena kutumia jina la Chadema.
Ama watatumia majina yao?
Sikutegemea John Bayo niliyemfahamu japo kidogo angefanya uamuzi wa kitoto namna ile. Am very sorry for him.

Hakika hao madiwani ni majasiri sana na wanasiamamia yale waliokubaliana hivyo hawamo katika kundi la wanafiki kama alivyo Mbunge wao Lema na madiwani wengine waliokuwa vigeugeu.

Sina tu katiba ya Chadema lakini nina hakika wakienda mahakamani kudai haki yao ya kuondolewa uanachama wao na sababu walizotoa CC ya Chadema nina imani watarudishwa kwa amri ya mahakama na kuendelea na udiwani wao.

lakini vile vile nina imani kama uchaguzi utafanyika katika kata zote hizo tano CCM watachukua kata zote kwani wananchi wamechoshwa na malumbano kila siku bali wanataka maendeleo. na hapo sasa kutakuwa hakuna haja ya muafaka baina ya CCM na Chadema.

Lakini vile vile 2015 Godbless lema hawezi pewa Ubunge hapo Mjini Arusha. Kwani ameonyesha ni dhaifu sana na hana ushirikiano na madiwani wake hivyo hawezi kuwaletea maendeleo watu wa mjini Arusha,
 
hakuna ngoma mbichi arusha, mambo yapo sawa sawia, uzuri wenyewe chadema kwa sasa hakuna kiongozi maarufu kuliko chadema yenyewe, wale washaeleweka ni waganga njaa sasa wakaendelee kuganga njaa yao. big up cc.
 
Hakika hao madiwani ni majasiri sana na wanasiamamia yale waliokubaliana hivyo hawamo katika kundi la wanafiki kama alivyo Mbunge wao Lema na madiwani wengine waliokuwa vigeugeu.

Sina tu katiba ya Chadema lakini nina hakika wakienda mahakamani kudai haki yao ya kuondolewa uanachama wao na sababu walizotoa CC ya Chadema nina imani watarudishwa kwa amri ya mahakama na kuendelea na udiwani wao.

lakini vile vile nina imani kama uchaguzi utafanyika katika kata zote hizo tano CCM watachukua kata zote kwani wananchi wamechoshwa na malumbano kila siku bali wanataka maendeleo. na hapo sasa kutakuwa hakuna haja ya muafaka baina ya CCM na Chadema.

Lakini vile vile 2015 Godbless lema hawezi pewa Ubunge hapo Mjini Arusha. Kwani ameonyesha ni dhaifu sana na hana ushirikiano na madiwani wake hivyo hawezi kuwaletea maendeleo watu wa mjini Arusha,


  1. Kusimamia kituambacho si cha msingi ni wendawazimu…
  2. katiba ya chadema Hii hapa
  3. Hata tukibaki na diwani mmoja tutadai uchanguzi utakaofata kanuni na sheria..
  4. Mbunge ameonyesha hana ushirikiana kwa lipi kutokwenda kuchukua wagonjwa wa kata za madiwani wake na kuwapeleka kwa Babu Loliondo…haha
  5. Godbless Lema bado ananguvu kuliko unavyodhania na kama huamini njoo alhamisi makamanda watakapo kuwa Arusha…..
 
.

Sina tu katiba ya Chadema lakini nina hakika wakienda mahakamani kudai haki yao ya kuondolewa uanachama wao na sababu walizotoa CC ya Chadema nina imani watarudishwa kwa amri ya mahakama na kuendelea na udiwani wao.
,

Ukimtaliki mkeo mahakama ina haki ya kulazimisha awe mkeo?
 
Ukimtaliki mkeo mahakama ina haki ya kulazimisha awe mkeo?

Kama ulikiuka sheria za talaka, Sheria au mahakama inamrudisha mpaka utakapo timiza sheria za talaka. Kwa mujibu wa sheria hilo linawezekana pasi na shaka.

Mfano ni Mbunge wa CUF bi Naila Jidawi alipofukuzwa na CUF na alipopeleka shauri lake mahakamani alirejeshwa kwa nguvu ya mahakama na kuendelea na ubunge wake mpaka Bunge lilipovunjwa. Hivyo nao inawezekana.
 
  1. Kusimamia kituambacho si cha msingi ni wendawazimu…
  2. katiba ya chadema Hii hapa
  3. Hata tukibaki na diwani mmoja tutadai uchanguzi utakaofata kanuni na sheria..
  4. Mbunge ameonyesha hana ushirikiana kwa lipi kutokwenda kuchukua wagonjwa wa kata za madiwani wake na kuwapeleka kwa Babu Loliondo…haha
  5. Godbless Lema bado ananguvu kuliko unavyodhania na kama huamini njoo alhamisi makamanda watakapo kuwa Arusha…..

Kwanza nitafurahi kama utanipa link ya kuweza kuipata hiyo katiba ya Chadema ili niipitie.

lakini naomba ujue kuwa Lema npamoja na kuwa Mbunge lakini ni sehemu ya baraza la madiwani wa hapo Arusha. Hivyo kwa namna yoyote ile taarifa za muafaka ule alikuwa nazo kwani pasi na shaka ulikuwa ni mchakato ulioitishwa kisheria na kwa barua na minutes ambazo hata kama hujaudhulia lakini minutes alizipata hivyo kujua mchakato mzima.

na kama kweli alikuwa hajui basi yeye atakuwa yupo mbali sana na madiwani wake kiutendaji ima anakuwa mbame au mjuvi. lakini ni lazima alikuwa na taarifa. Kitendo cha kuwakana kinaonyesha yeye ni kiongozi Mnafiki na asiyefaa kabisa kuiongoza jamii ile ya machalii wangu wa pale Arusha.

Nafikiri amepoteza umaarufu wake na wa chama chake hapo Arusha kwani siku zote wananchi wa Arusha hawataki malumbano bali wanataka maendeleo yaani barabara zao za kule kaloleni, mbauda, majengo na hata njia yetu ya kwenda shuleni kwetu Ilboru kupitia BINO road au ile ya Mianzini ziitiwe lami.

natabili mwisho wa Lema hapo Arusha. Bora arudi shemeji yetu
 
Kaka Hope ni mweji Arusha,Mimi mgeni na nina siku kama Mbili mjini hapa na nimekuwa nikiongea na watu tofautitofauti, na kuna mtu kaniambia kuwa DIWANI wa KITI MAALUMU Kafungua DUKA la HARDWARE KUBWA HAPO TOWN kwa hizo hela za RUSHWA, Je wewe unasemaje kuhusu hilo?

Ni makosa kutoa ushuhuda pasipo utafiti. Je wajua historia ya diwani husika, huyo kadunduliza mapesa SACCOS, baadaye kakopa na kufungua duka.
 
Hao madiwani waliovuliwa uanachama huu ndio ulikwa wakati wao muafaka wa kuomba radhi katika kamati kuu ya CDM. Ili warudishiwe
uanachama wao, na sio kuishupalia CDM ( CC ) kwamba mtaipeleka kesi mahakamani eti kwa sababu mnataka mbakie kuwa madiwani
bila kuwa wanchama wa CDM. Kama mmekiuka katiba na kanuni za chama na amtaki kuomba radhi hapo inakuwa sheria ni msumeno.

uchaguzi mdogo unakuja gombeeni kupitia hao walioshika vichwa vyenu ccm muone kama wananchi watakuchagueni.

Kaeni chini mtafakari jambo la kufikiri na kutimiza mambo ya maendeleo yanakushindeni vipi.
 
CDM wanazidi kuumbuka, uchunguzi nilioufanya takribani mwaka, unaonyesha kwamba watu wengi walikiunga mkono CDM kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana!

Wameanza kujutia uamuzi wao huo, wakisema wazi kwamba CDM kingeshinda na kukamata dola nchi ingeingia kwenye machafuko makubwa ya umwagaji damu!

Baadhi ya wananchi waliokipigia kura CDM walisema chama hicho kama kingeshinda na kuunda serikali, utawala wake usingekuwa na tofauti na utawala zamani wa Ujerumani, chini ya Dikteta Adolf Hitler.
 
Back
Top Bottom