Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wadau,
Kama tunavyoona, moto waliouwasha Chadema baada ya kumteua Dr Slaa kugombea urais umeanza kuwa mkali kila kukicha. Inaonekana kama vile Watanzania wengi wanataka mabadiliko, lakini hiari yaho hii inapigwa vita na chama tawala ambacho kiko tayari kutumia mbinu, na nguvu zote, pamoja na zile za dola kuondoa uwezekano wa matakwa haya.
Kama vile walivyokifanyia CUF huko nyuma, sasa hivi inaletwa hoja ya udini -- kwamba Chadema ni chama cha Wakristo na kwamba Dr Slaa ni pendekezo la Kanisa (Katoliki). Hii inashangaza kwani hapo nyuma Kanisa hilo liliposema JK ni chaguo la Mungu, hakukuwa na rabsha yoyote -- hasa kutoka kwa Waisilamu.
Lakini yote hayo hayanipi tabu. Wasiwasi wangu mkubwa ni pale serikali ya CCM itakapoanza kukipaka Chadema label ya "Chama vurugu" -- kama vile walivyokuwa wanafanya kwa NCCR -Mageuzi mwaka 1995 under Mzee Ruksa, na CUF mwaka 2000 under Mkapa.
Tatizo kubwa la CCM ni kwamba wakikiona chama chochote cha upinzani kinaanza kuwa tishio kwake, basi hutumia jeshi la polisi kukisaidia, na hii ndiyo huwa silaha yao kubwa. Mwaka 2000 mara kadha jeshi la polisi under IGP Mahita lilikuwa linaingilia mikutano ya CUF na kuanza tu kulipua mabomu ya machozi, bila ya sababu yoyote, eti tu kuonyesha tu CUF ni chama cha vurugu tu.
Chadema waliangalie hilo na wajue namna ya kukabili nalo -- ingawa naamini JK siyo Mkapa, na Saidi Mwema siyo Omar Mahita. Lakini kama tujuavyo, paka ukimkabili sana hadi ukutani atakuparua tu. hana namna nyingine ya kujihami kwani siyo binadamu. Wasiwasi wangu ni huo tu.
Kama tunavyoona, moto waliouwasha Chadema baada ya kumteua Dr Slaa kugombea urais umeanza kuwa mkali kila kukicha. Inaonekana kama vile Watanzania wengi wanataka mabadiliko, lakini hiari yaho hii inapigwa vita na chama tawala ambacho kiko tayari kutumia mbinu, na nguvu zote, pamoja na zile za dola kuondoa uwezekano wa matakwa haya.
Kama vile walivyokifanyia CUF huko nyuma, sasa hivi inaletwa hoja ya udini -- kwamba Chadema ni chama cha Wakristo na kwamba Dr Slaa ni pendekezo la Kanisa (Katoliki). Hii inashangaza kwani hapo nyuma Kanisa hilo liliposema JK ni chaguo la Mungu, hakukuwa na rabsha yoyote -- hasa kutoka kwa Waisilamu.
Lakini yote hayo hayanipi tabu. Wasiwasi wangu mkubwa ni pale serikali ya CCM itakapoanza kukipaka Chadema label ya "Chama vurugu" -- kama vile walivyokuwa wanafanya kwa NCCR -Mageuzi mwaka 1995 under Mzee Ruksa, na CUF mwaka 2000 under Mkapa.
Tatizo kubwa la CCM ni kwamba wakikiona chama chochote cha upinzani kinaanza kuwa tishio kwake, basi hutumia jeshi la polisi kukisaidia, na hii ndiyo huwa silaha yao kubwa. Mwaka 2000 mara kadha jeshi la polisi under IGP Mahita lilikuwa linaingilia mikutano ya CUF na kuanza tu kulipua mabomu ya machozi, bila ya sababu yoyote, eti tu kuonyesha tu CUF ni chama cha vurugu tu.
Chadema waliangalie hilo na wajue namna ya kukabili nalo -- ingawa naamini JK siyo Mkapa, na Saidi Mwema siyo Omar Mahita. Lakini kama tujuavyo, paka ukimkabili sana hadi ukutani atakuparua tu. hana namna nyingine ya kujihami kwani siyo binadamu. Wasiwasi wangu ni huo tu.