CHADEMA na wapinzani wameshinda

CHADEMA na wapinzani wameshinda

Very poor and awkward analysis; Ili upime nguvu ya uungwaji mkono lazima ushiriki uchaguzi wala sio kususa. Swala la kususa linapelekea mambo mawili kutokea:
  • Kundi lisilokuunga mkono wewe uliyesusa kutokujitokeza kupiga kura maana wana uhakika yule wamtakaye ameshinda.
  • Kundi la wanao kuunga mkono kutokujitokeza kupiga kura kwa sababu wamtakaye kasusa.
Wote hawa, wataonekana kuwa hawakupiga kura; lakini kwa sababu tofauti. Hivyo ni swala la ajabu ukijisifu kuwa wale wote ambao hawajapiga kura wapo upande wao.

Tusubiri muendelezo pengine hoja yako ikawa sahihi. Miongoni mwa maagizo ya upinzani, pamoja na kuhimiza watu kutokujitokeza kupiga kura, wamehimizwa pia kutokushirikiana na viongozi watakaokuwa wamepatikana. Tunasubiri tuone kwawingi huohuo wakisusa viongozi, kwamaana hata mwananchi akihitaji barua ya utambulisho asuse kwenda kwa kiongozi; hapo tutaamini kuwa wamesusa.

Binafsi sikujitokeza kupiga kura kwa kuwa hapakuwa tena na ushindani.
Kwanza naomba nikueleze kwamba mihuri ni mali ya serikali si mali ya wenyeviti wa vijiji , ndio maana hata mwenyekiti akifa bado mihuri inaendelea kutumika , kuna wakati wenyeviti wa vijiji waliamriwa kukabidhi mihuri kwa watendaji wa vijiji , sijui kama umesahau hili.

Kwahiyo wananchi kutumia mihuri ama kupewa barua ya utambulisho haihusiani na kutomtambua Mwenyekiti aliyepachikwa uongozi , ndio maana hata baada ya wenyeviti kumaliza muda wao mihuri iliendelea kugongwa na barua za utambulisho ziliendelea kutolewa .
 
Hii ni baada ya kampeni yao ndogo sana na ya muda mfupi ya kuhamasisha wananchi kususia uchaguzi feki wa serikali za mitaa kuungwa mkono na wananchi kwa zaidi ya 90%, hii ni rekodi.

Kwa mfano, msimamizi mmoja wa kituo cha uchaguzi jijini Dar es salaam ametoa siri kwamba kati ya watu zaidi ya 500 waliojiandikisha, waliopiga kura hawakufika 50, hii ni pamoja na wale wanaojifanya wanaccm, maana ya jambo hili ni kwamba ccm imekataliwa hata na wanaojiita wanachama wake yenyewe, hii ni hatua kubwa sana na ya kujivunia kwa wapinzani, maana sasa ni wazi kwamba wamefanikiwa mipango yao ya kupenya kwenye ngome za ccm na hivyo kujitengenezea mtaji wa baadaye.

Hakika Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana!

======
Maoni ya wadau
Aibu kwa jiwe na wafuasi wake majiwe.
 
.
IMG-20191125-WA0029.jpeg
 
Katika hili la kujitokeza kupiga kura kwa uchache jibu lake ni rahisi sana.
Falsafa ya mwanadamu hupenda kushabikia kitu chenye ushindani ndani yake.
Kwa mfano , Kuna timu nne za mpira wa miguu zinajiandaa na mashindano.
Katika timu hizi nne, tatu zikakosa viwanja vya kufanyia mazoezi na kushindwa kujiandaa vyema.
Kwa hali yoyote timu hizi tatu hata kushindana zenyewe kwa zenyewe zitakuwa haziwavutii watazamaji.
Timu kama ya Yanga kama inamgogoro na imeshindwa kuandaa timu yake kucheza na Simba na pia inajua kuwa ikipeleka timu uwanjani itafungwa magoli mengi, haitapeleka timu uwanjani. Kama itapeleka timu na washabiki wa Simba wakajua kuwa hakuna ushindani, hawatajitokeza kwa wingi uwanjani na wale wa Yanga hawatakwenda kabisa.
Vyama vya upinzani vimeundwa na Chama Tawala cha CCM.
Rais wetu mchapakazi na anaeiletea Sifa kubwa Tanzania Kiuchumi ni TUNDA la vyama vya upinzani.
Kama si upinzani wenye nguvu, CCM wangeweza kuingiza mgombea dhaifu kwa maslahi binafsi.
Washauri wa Rais wetu mpendwa wawe na maono na watoe ushauri mzuri kuhusu vyama vya Siasa kama wanavyotoa ushauri mzuri kuhusu maswala ya uchumi, ulinzi, usalama, afya, elimu nk.
 
pamoja na kujitoa mnafuatilia uchaguzi kwa makini hivyo?

Jitoeni ubunge muone msukuma kama anajaribiwa...
Kwani ubunge ni nini ubunge unaweza kiachwa tukapigania tume huru
Na ninasema Mimi ni mwana ccm niliye kulia katika msingi ya utawala bora na kuheshimu wengine siku vurugu zikitokea wasababishaji watakuwa ni ccm wenyewe maana wengine tunaona kama hawafai kuwa katika taifa hili imefika kipindi kuwa mpinzani ni adui wa taifa
Uongozi utapita lakini Tanzania itabaki
Vizazi vyetu vitakuja kujivunia nini
Kama tunaona chama kinapendwa tuache ushindani uwe huru
Tanzania ni yetu sote .
 
ubongo wako uko one sided.
Hizo vurugu utagombana na mkeo sio za nchi
Kwani ubunge ni nini ubunge unaweza kiachwa tukapigania tume huru
Na ninasema Mimi ni mwana ccm niliye kulia katika msingi ya utawala bora na kuheshimu wengine siku vurugu zikitokea wasababishaji watakuwa ni ccm wenyewe maana wengine tunaona kama hawafai kuwa katika taifa hili imefika kipindi kuwa mpinzani ni adui wa taifa
Uongozi utapita lakini Tanzania itabaki
Vizazi vyetu vitakuja kujivunia nini
Kama tunaona chama kinapendwa tuache ushindani uwe huru
Tanzania ni yetu sote .
 
Mkuu hivi Akili yako inaona mbali kweli.. Unapoteza mitaa na vijiji harafu unasema Ni hatua nzuri kisiasa?
Hivi unapoambiwa Siasa Ni mchezo Mchafu huwa unaelewa Nini?

Kwa Hali hii CCM itaendelea kukaa Madarakani mpaka hiki kizazi kitakapotoweka.
FB_IMG_1570952637609.jpg

Kwenye hali kama hii unashiriki uchaguzi upi ?
 
Hapa hakuna mshindi bali one big looser ambaye ni Tanzania na Watanzania....
 
pamoja na kujitoa mnafuatilia uchaguzi kwa makini hivyo?

Jitoeni ubunge muone msukuma kama anajaribiwa...

Hatuhitaji kujua kabila la mtu hapa...!Unataka kutambika?
Tunataka Rais anayejali maslahi ya NchI na anayefuata sheria na Katiba ya nchi, full Stop!
Kabila lake is very immaterial!!!
 
Hatuhitaji kujua kabila la mtu hapa...!Unataka kutambika?
Tunataka Rais anayejali maslahi ya NchI na anayefuata sheria na Katiba ya nchi, full Stop!
Kabila lake is very immaterial!!!
Achana na huyo mshamba
 
Back
Top Bottom