CHADEMA na wapinzani wameshinda

CHADEMA na wapinzani wameshinda

Mngekuwa mnafanya mambo yenu kisayansi, hii ilikuwa ni fursa yenu nzuri sana ya kuanzia kampeni zenu, kuanzia sasa na kwenda mbele.

Mngekuwa mmejipanga vizuri kunasa namba sahihi ya:
- waTanzania waliojiandikisha kupiga kura
- waTanzania waliojitokeza kupiga kura
- sababu hasa zilizosababisha kuwepo upungufu, kama namba zenu hizo zitawaonyesha hivyo
- ni maeneo yapi hasa ya nchi yanayohitaji kulengwa kwa karibu na ufuatiliaji wa mara kwa mara
- ni viongozi (watu) gani hasa kwenye jamii mnaotakiwa kuwalenga ili kazi yenu ifane, n.k,. n.k.

Haya yote yangewasaidia kuelekeza nguvu zenu huko huko wananchi wanakoelekea ili kuwasaidia kujipanga vizuri kukabili yajayo.

Kwa bahati mbaya sana Erythro, mipango yenu bado mnaifanya kishaglabagara na kama kubahatisha tu, kama unavyotueleza katika mada yako hii.

Namba za hayo unayosema hapo zipo wapi na wapi?

Kazi ya kufanya siasa ni aina ya sayansi fulani. Inazo taratibu zake, sio kurukia tu mambo.

Kuna wakati, miaka michache iliyopita niliwaona kama mmeanza kuelekea huko, lakini hapa katikati, mmeonyesha kuvurugwa sana, na zile hatua za mwanzo mlizokuwa mmezianza zote zimepotea.

Ajabu ni kwamba, ruzuku yenu iliongezeka, na kila mtu angetegemea muitumie vizuri kuwafundisha vijana wenu wafanye kazi zao kisayansi, - matokeo yanaonyesha kinyume cha hapo!

Hata kuajiri ma-'consultant', nguli wa mambo haya kwa muda tu pia imewawia vigumu? Raslimali zenu mmezitawanya wakati ambapo mlitakiwa mzitumie kwa makini sana wakati huu ambao mabavu yanatumika kuwamaliza.
Haya maguvu mngeweza kuyapiku kwa kutumia sayansi, huku mkitumia akili zaidi.

Ona sasa mnavyoendeshwa!



KNCU
Waliojiandikisha 166
waliopiga kura
CCM 21
TLP 6
 
ukiruhusiwa unafanya fujo kwanini usikatazwe

1574681195213.png

1574681679635.png


Hizi ndiyo Sera za Hapa Kazi tu....!!
Ukiwa mpinzani, media au Mwanaharakati kisago ni kama inavoonekana hapo juu!
Ni hatari...!
 
unanipangia cha kuwaza na bado mnajiita chama cha demokrasia?
nchi imejaa mapimbi kama nyinyi.
Hatuhitaji kujua kabila la mtu hapa...!Unataka kutambika?
Tunataka Rais anayejali maslahi ya NchI na anayefuata sheria na Katiba ya nchi, full Stop!
Kabila lake is very immaterial!!!
 
Mngekuwa mnafanya mambo yenu kisayansi, hii ilikuwa ni fursa yenu nzuri sana ya kuanzia kampeni zenu, kuanzia sasa na kwenda mbele.

Mngekuwa mmejipanga vizuri kunasa namba sahihi ya:
- waTanzania waliojiandikisha kupiga kura
- waTanzania waliojitokeza kupiga kura
- sababu hasa zilizosababisha kuwepo upungufu, kama namba zenu hizo zitawaonyesha hivyo
- ni maeneo yapi hasa ya nchi yanayohitaji kulengwa kwa karibu na ufuatiliaji wa mara kwa mara
- ni viongozi (watu) gani hasa kwenye jamii mnaotakiwa kuwalenga ili kazi yenu ifane, n.k,. n.k.

Haya yote yangewasaidia kuelekeza nguvu zenu huko huko wananchi wanakoelekea ili kuwasaidia kujipanga vizuri kukabili yajayo.

Kwa bahati mbaya sana Erythro, mipango yenu bado mnaifanya kishaglabagara na kama kubahatisha tu, kama unavyotueleza katika mada yako hii.

Namba za hayo unayosema hapo zipo wapi na wapi?

Kazi ya kufanya siasa ni aina ya sayansi fulani. Inazo taratibu zake, sio kurukia tu mambo.

Kuna wakati, miaka michache iliyopita niliwaona kama mmeanza kuelekea huko, lakini hapa katikati, mmeonyesha kuvurugwa sana, na zile hatua za mwanzo mlizokuwa mmezianza zote zimepotea.

Ajabu ni kwamba, ruzuku yenu iliongezeka, na kila mtu angetegemea muitumie vizuri kuwafundisha vijana wenu wafanye kazi zao kisayansi, - matokeo yanaonyesha kinyume cha hapo!

Hata kuajiri ma-'consultant', nguli wa mambo haya kwa muda tu pia imewawia vigumu? Raslimali zenu mmezitawanya wakati ambapo mlitakiwa mzitumie kwa makini sana wakati huu ambao mabavu yanatumika kuwamaliza.
Haya maguvu mngeweza kuyapiku kwa kutumia sayansi, huku mkitumia akili zaidi.

Ona sasa mnavyoendeshwa!
Mkuu sijui kama utaeleweka, mimi niligusia kidogo baadhi ya haya uliyo shauri siku chache zilizo pita.
Naweza kukuambia hali hii ya kubahatisha mambo na kutoajiri watu sahihi imeongezeka kidogo baada ya kuondoka watu flani ktk nafasi flani za juu kwenye chama, mmojawapo ni Dr. Slaa.

Kuna wengine wapo chamani lakini wamekaa kimya wananogopa kuonekana wasaliti kwa kukosoa hali ya sasa.
Usipoitwa msaliti basi utaambulia matusi.
 
unanipangia cha kuwaza na bado mnajiita chama cha demokrasia?
nchi imejaa mapimbi kama nyinyi.

Pimbi kasoro mkia ni weye usejua hata maana pana ya Demokrasia…!
Demokrasia ni pamoja na uhuru wa kujenga na kupinga hoja so kama mnavofanya maficcm wa Lumumba na babu yenu JPM…!
 
Hii ni baada ya kampeni yao ndogo sana na ya muda mfupi ya kuhamasisha wananchi kususia uchaguzi feki wa serikali za mitaa kuungwa mkono na wananchi kwa zaidi ya 90%, hii ni rekodi.

Kwa mfano, msimamizi mmoja wa kituo cha uchaguzi jijini Dar es salaam ametoa siri kwamba kati ya watu zaidi ya 500 waliojiandikisha, waliopiga kura hawakufika 50, hii ni pamoja na wale wanaojifanya wanaccm, maana ya jambo hili ni kwamba ccm imekataliwa hata na wanaojiita wanachama wake yenyewe, hii ni hatua kubwa sana na ya kujivunia kwa wapinzani, maana sasa ni wazi kwamba wamefanikiwa mipango yao ya kupenya kwenye ngome za ccm na hivyo kujitengenezea mtaji wa baadaye.

Hakika Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana!

======
Maoni ya wadau


MBOWE BABA LAO!! ✌ 😎
 
Kalamu1,
Unaandika kama vile unaota, Wote wanashinda mahakamani, siasa imepigwa pini,
Watu msiotaka kushughulisha vichwa vyenu kama wewe ndio mtakaozidi kulididimiza taifa hili. Visababu na visingizio visivyo na mwisho havitawapeleka popote.
Kwani unadhani mimi sijui kwamba wanashinda mahakamani? Wafunge osisi zote basi wahamie wote huko huko mahakamani kabisa.
Kila mara visingizio na visababu visivyo na mwisho. Acheni siasa moja kwa moja basi ya nini kuendelea kuwapa watu matumaini kama kazi hamuiwezi!
 
Sikubaliani na wewe kwamba mipango yetu tunaifanya kishaghalabhagala , labda kama unataka tulete VITA ( hili jambo bado Chadema haijaamua kulifanya ) , hakuna usichokijua kuhusu yanayoendelea nchini Tanzania , Chadema imeamua kushawishi nguvu ya umma kwa njia ya amani na imefanikiwa , itoshe tu kusema mazuri uliyoandika hapa tutachukua mabaya na kejeli tutaacha
Erythro, umeamua maksudi kabisa kutoelewa nilichoandika, au unapotosha kwa faida unayoijua wewe.

Hakuna sehemu yoyote niliyoandika "nguvu ya umma" itumike. Nisome tena kwa utulivu.

In fact, hali inavyozidi kwenda, mkitumia maarifa katika kazi zenu na wananchi, hakuna lazima yoyote ya vurugu kuleta mabadiliko. Wananchi wataamua tu kwa utulivu kuyaleta mabadiliko hayo. Lakini wanahitaji uongozi wa kuwaunganisha pamoja kufikia adhma hiyo. Hapa ndipo mnapopwaya.
 
KNCU
Waliojiandikisha 166
waliopiga kura
CCM 21
TLP 6
Safi kabisa. Sijui kama Erythrocyte takwimu kama hizi hawezi kuzikusanya na kutafuta njia ya kuzitumia kwa manufaa ya chama.!
CHADEMA na ACT-Wazalendo wana viongozi wao na wananchama nchi nzima, watashindwa kweli kukusanya takwimu kama hizi na mambo ziada yanayoweza kuwasaidia kujua wananchi wanasema nini, na ni kipi kinahitajika kifanyike kuwaunga mkono?
 
you are just stupid...
Demokrasia ni kuheshimu mawazo ya kila mtu...
Pimbi kasoro mkia ni weye usejua hata maana pana ya Demokrasia…!
Demokrasia ni pamoja na uhuru wa kujenga na kupinga hoja so kama mnavofanya maficcm wa Lumumba na babu yenu JPM…!
 
Hata mm Siamini katika Ujamaa. Siwezi fanya kazi kwa nguvu halafu nikagawane na mvivu NO. Na si kwamba nakubaliana na ccm kwenye kila jambo NO, ni vile ccm hakina mbadala kwa sasa na Ni kwamba upinzani nao ni wanaccm, na wanapenda kuwa ccm maana ni chama baba Lao kwa sasa hizi nyingine ni porojo.
Watu msiotaka kushughulisha vichwa vyenu kama wewe ndio mtakaozidi kulididimiza taifa hili. Visababu na visingizio visivyo na mwisho havitawapeleka popote.
Kwani unadhani mimi sijui kwamba wanashinda mahakamani? Wafunge osisi zote basi wahamie wote huko huko mahakamani kabisa.
Kila mara visingizio na visababu visivyo na mwisho. Acheni siasa moja kwa moja basi ya nini kuendelea kuwapa watu matumaini kama kazi hamuiwezi!
Kama hasira ulizonazo ungezielekeza kwa ccm ningekuona una akili
 
Watanzania wameonyesha ccm na Jiwe kuwa hawataki ujinga huu unaoendelea nchini.
 
Kichwa cha habari yako kimenikumbusha matukio ya rafiki yangu Frank, bwana huyu alikua akipenda ugomvi haswaa, na pale alipokua akiukosa Basi alikua akiutafuta kwa hila.

Hila yenyewe alikua akienda kwenye viwanja vya mpira na kuuchukua mpira uwanjani na kukimbia nao, hivyo kujikuta akidondokea kichapo cha mashabiki na wachezaji pia.

Frank alipitiliza ugomvi wake na siku katika masiku akaenda Bar, na kupindua meza kibabe, walevi wale waliamua kutumia busara na kumnunulia bia, Kisha wakamwambia matendo yako yamevuma sana hivyo kwa ulichokifanya tukajua huyu ndiye.

MORAL OF THE STORY
Vyama vya upinzania wameipa CCM ilichokia ikikihitaji, hivyo tathmini mujarabu katika uchaguzi wa Jana CCM wamepata walichokua wanakihitaji.

Hivyo wao ni washindi, isivyokua bahati, Vyama vya upinzani wanadhani kwamba wameikomesha CCM.
 
Back
Top Bottom