kijana wa leo
JF-Expert Member
- Nov 28, 2011
- 2,856
- 7,003
Kupitia hili suala la Mbunge wa Nkasi pamoja na wabunge wa viti maalumu, CHADEMA wamejitanabaisha ni kiasi gani wamekua wanafiki kwa watanzania na wapenda Haki na amani wote.
Uchaguzi wa mwaka 2015 CHADEMA walikiri wazi kuwa ni uchaguzi ambao haukua huru na Haki hadi kupelekea kususia hotuba ya Rais Bungeni lakini ajabu walikubali kuapa na majina ya viti maalumu yakapelekwa bila hata kuchelewa.
Ajabu na unafiki ni mwaka huu, hoja ileile ya uchaguzi kutokua huru na Haki lakini ajabu ni kwamba kwa sababu viongozi wakuu wamekosa basi safari hii hawataki hata yule aliyepata au nafasi za viti maalumu walivyopata kuzitumia, wanataka wakose wote, wakati uchaguzi uliopita viongozi walipata na wagombea wengine wa CHADEMA walidhurumiwa ushindi wao, hakuna aliyewajali zaidi ya kuacha machozi yao yaende na maji.
CHADEMA waache kuwa wanafiki.
Uchaguzi wa mwaka 2015 CHADEMA walikiri wazi kuwa ni uchaguzi ambao haukua huru na Haki hadi kupelekea kususia hotuba ya Rais Bungeni lakini ajabu walikubali kuapa na majina ya viti maalumu yakapelekwa bila hata kuchelewa.
Ajabu na unafiki ni mwaka huu, hoja ileile ya uchaguzi kutokua huru na Haki lakini ajabu ni kwamba kwa sababu viongozi wakuu wamekosa basi safari hii hawataki hata yule aliyepata au nafasi za viti maalumu walivyopata kuzitumia, wanataka wakose wote, wakati uchaguzi uliopita viongozi walipata na wagombea wengine wa CHADEMA walidhurumiwa ushindi wao, hakuna aliyewajali zaidi ya kuacha machozi yao yaende na maji.
CHADEMA waache kuwa wanafiki.