CHADEMA na unafiki uliotukuka

CHADEMA na unafiki uliotukuka

Hoja mufilisi kabisa, kwa kususa kunasaidia nini? Chaguzi karibia zote za marudio walikua wanasusa kutokana na mazingira mabaya ya hizo chaguzi, kipi kiliwafanya washiriki huu uchaguzi kama sio unafiki...
Sikubaliani na wewe, guy ulikuwa uwanja moana wakupambana na kujua mbivu na mbichi,ila kwasababu refa aliamua kutoa ushindi mezani Bila kuchezesha mechi,hivyo ushindi ukawa upande wa refa. Kwa ukatili wa kiwango kilicho shuhudiwa.
 
Kupitia hili suala la Mbunge wa Nkasi pamoja na wabunge wa viti maalumu, CHADEMA wamejitanabaisha ni kiasi gani wamekua wanafiki kwa watanzania na wapenda Haki na amani wote.

Uchaguzi wa mwaka 2015 CHADEMA walikiri wazi kuwa ni uchaguzi ambao haukua huru na Haki hadi kupelekea kususia hotuba ya Rais Bungeni lakini ajabu walikubali kuapa na majina ya viti maalumu yakapelekwa bila hata kuchelewa.

Ajabu na unafiki ni mwaka huu, hoja ileile ya uchaguzi kutokua huru na Haki lakini ajabu ni kwamba kwa sababu viongozi wakuu wamekosa basi safari hii hawataki hata yule aliyepata au nafasi za viti maalumu walivyopata kuzitumia, wanataka wakose wote, wakati uchaguzi uliopita viongozi walipata na wagombea wengine wa CHADEMA walidhurumiwa ushindi wao, hakuna aliyewajali zaidi ya kuacha machozi yao yaende na maji.

CHADEMA waache kuwa wanafiki.
"Kwa sababu viongozi wakuu wamekosa.....wanataka wakose wote" hivi waliokosa ni viongozi wakuu tu??? Woteeeee wamekosa I mean wamenyimwa ubunge. Hadi wagombea wasio viongozi, acha kupotosha.
 
Wewe nini kinakuuma yeye akiongelea hiyo issue? ni lini wana JF tumeanza kupangiana vitu vya kuandika? Kwahiyo mtu akiongelea issue za team ya Barcelona naye ataambiwa nini kinakuuma kuongelea mabaya ya Barcelona? kama ni hivyo basi JF itabidi wote tuwe Mabubu!
Lakini kumbuka uchaguzi huu ni tofauti kabisa na chaguzi zote zilizopita. Na pia kumbuka mwaka jana tumeona kioja kingine: Uchaguzi wa serikali za mitaa, ambapo nchi nzima ccm wamebeba. Tulishuhudia maafisa wahusika wakifunga ofisi hata wiki nzima ili tu wagombea wa upinzani wasipate fomu, au kurejesha fomu kwa wakati.

Miaka ya nyuma kulikuwa na uporaji for sure, lakini mwaka huu, hii ni kitu ingine kabisa. Inashangaza waleta mada kama hii, wala hawayaoni haya. Pengine ni makusudi?

Maana katika serikali ya Magufuli , kuwa mpinzani tu ni kosa la jinai.

Lakini ukiangalia vizuri, hao waliotangazwa kushinda, sio hasa wapinzani wenye misimamo mikali. Ni kama Magufuli "kagawa" ushindi wake kuwapa ambao hawatamsumbua Bungeni. Kule ambako unashangaa ccm wamepitapitaje, mfano Tunduma na Mbeya mjini, ndio unaambiwa ccm imeshinda.

CHADEMA bado wana muda wa kutosha kufanya maamuzi. Ni hekima kutoa muda kwanza, maana sheria inatoa muda wa vikao 3 vya Bunge. Ni mapema mno kuwahukumu
 
Mnatusumbua kwa kujifanya wapenda Democracy kumbe wahuni na wezi kama wale wengine tu.
Kwa hiyo mwizi ni CHADEMA ? Unachekesha sana. Lakini wakati watu kama wewe mnasherehekea "ushindi wa kishindo" katika mazingira ambayo mnajua kabisa bila polisi na Tume ya Uchaguzi inayopendelea ccm, wala msingetoboa, hamuangalii athari za ujambazi huu kwa taifa letu.

Kama alivyosema rais mstaafu Obama, matendo ya rais Trump na Republican wake yanaharibu taasisi nzima ya Demokrasia katika taifa hilo, na akasema kwamba hiyo ni "dangerous" path.

Nafikiria hivyo kwa nchi yetu pia. Akina Mwinyi, Mkapa na Kikwete walifikiria mbali zaidi ya ccm. Lakini Magufuli wala si kwamba anaifikiria ccm, bali yeye mwenyewe . Na hiyo ni habari mbaya kwa taifa la Tanzania
 
Mengi tuu...
Kuna clip ya jiwe anasema kwny mkutano wa hadhara kuwa Bunda hakuna taa za barabarani sabb tu wana mbunge wa upinzani!!!
Kwa hiyo kwa elimu yako mataa ya barabarani Bunda ni maendeleo? Mikoa au wilaya ngapi zenye wabunge wa CCM hazina hizo taa za barabarani?
 
Kupitia hili suala la Mbunge wa Nkasi pamoja na wabunge wa viti maalumu, CHADEMA wamejitanabaisha ni kiasi gani wamekua wanafiki kwa watanzania na wapenda Haki na amani wote.

Uchaguzi wa mwaka 2015 CHADEMA walikiri wazi kuwa ni uchaguzi ambao haukua huru na Haki hadi kupelekea kususia hotuba ya Rais Bungeni lakini ajabu walikubali kuapa na majina ya viti maalumu yakapelekwa bila hata kuchelewa.

Ajabu na unafiki ni mwaka huu, hoja ileile ya uchaguzi kutokua huru na Haki lakini ajabu ni kwamba kwa sababu viongozi wakuu wamekosa basi safari hii hawataki hata yule aliyepata au nafasi za viti maalumu walivyopata kuzitumia, wanataka wakose wote, wakati uchaguzi uliopita viongozi walipata na wagombea wengine wa CHADEMA walidhurumiwa ushindi wao, hakuna aliyewajali zaidi ya kuacha machozi yao yaende na maji.

CHADEMA waache kuwa wanafiki.
We kijana wa zamani acha kuwa mjinga kwa kushabikia chama zee.
 
Hoja mufilisi kabisa, kwa kususa kunasaidia nini? Chaguzi karibia zote za marudio walikua wanasusa kutokana na mazingira mabaya ya hizo chaguzi, kipi kiliwafanya washiriki huu uchaguzi kama sio unafiki...
Kwa hiyo wewe kwa maono yako na uwezo wako woote bado hujaiona faida ya wao kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu??? Haya baki masikini hivoivo! Lakini usilazmishe na wengine wafikiri kwa kimo kidogo kama chako!
 
Kwa hiyo wewe kwa maono yako na uwezo wako woote bado hujaiona faida ya wao kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu??? Haya baki masikini hivoivo! Lakini usilazmishe na wengine wafikiri kwa kimo kidogo kama chako!
Sasa kama kulikua na faida unafiki wa kususa unatoka wapi?
 
Hivi nani alitengeneza ile orodha ya viti Maalum Chadema..bila ya Mnyika kuikana ilikuwa inapita...Chadema kuna Vichwa sana na yule mbunge wa Nkasi hafukuzwi uwanachama ila anakuwa labelled kibaraka
 
Kwani **** amekamatwa ? Au wenge la kukosa ubunge
Kwa hiyo Kama mwizi alikamatwa mwaka juzi akapigwa mawe, miaka yote wakamataji watumie adhabu ile ile?!

Mwaka huu adhabu kwa mwizi yule yule ni tofauti. Tulia tulii
 
Back
Top Bottom