Ni mara nyingi sana Chadema wamekuwa wanapewa ushauri wa kuimarisha majimbo ya uchaguzi kama vile kuwa na ofisi za maana kwenye kata, tarafa, wilaya na mikoa, hata na makao makuu yenyewe.
Kukiwa na ofisi za maana na zikasimamiwa na watu makini inakuwa ni rahisi kazi za chama kuendelea kufanyika hata kama siyo vipindi vya uchaguzi, na ni katika harakati za namna hii unaweza ukaspoti potentials kwenye nafasi kama wenyeviti wa vijiji, madiwani na wabunge. Siyo kusubiria kina Bulaya, Lembeli na CCM washindwe ndo wahamie kugombea kupitia CDM.
Na hili likifanyika ki-ufasaha ni rahisi kuongeza idadi kubwa ya wabunge ambao wanaweza kuleta impact hata kwenye kuzipitisha hizo sheria.
Mpaka tutakapokuwa na idadi ya wabunge pinzani yenye kumiliki kura bungeni ndipo tutaweza kuufikiria Urais, maana kwa hii katiba ambayo refa ni wa CCM, kamisaa na vibendera ni CCM, uwanja ni wa CCM hatuwezi kushinda mechi ya fainali.