CHADEMA na ubunge 2020

CHADEMA na ubunge 2020

Mi navyoona mambo yanavyokwenda, hakuna wa kuitoa CCM madarakani... labda CCM ipasuke vipande viwili.

Wamemiliki kila kitu kinachoweza kuwapa ushindi wa haki au wa wizi.

Kwa mfumo huu, CDM na ndugu zao wote, watasubiri sana kuwatoa hawa wezi madarakani.

Lakini unajua nini Komredi...?

Vipi kuhusu kitu kama ile 'Arab spring'?

Mbona ilimng'oa yule Hosni Mubarak wa Misri na yule Ben Ali wa Tunisia...

Tatizo ninaloliona kuhusu hapa kwetu ni uoga.

Tulio wengi hatupo tayari kupoteza damu zetu, maisha yetu, au hata kutandikwa mijeredi na kupigwa virungu vya polisi katika kudai haki zetu.

Mimi naamini kabisa kuwa mwisho wa siku sisi wananchi tuna nguvu kuliko polisi, jeshi, Magufuli, na CCM.

Tukiamua kuwatoa watatoka tu ingawa pia watu watalipa gharama kubwa sana.

Hebu ona kwa mfano kule Zimbabwe...yaani kile kibabu kinawapeleka puta hadi watu wanaishia kukamata panya ili wamfanye kitoweo lakini cha kushangaza eti bado kipo madarakani!

Hivi kweli unadhani Wazimbabwe wakiamua na kusema sasa basi imetosha...kile kibabu unadhani kitaendelea kuwepo madarakani?

Tatizo letu sisi Waafrika wa huku kusini mwa Sahara wengi wetu tuko waoga sana.

Waarabu huwezi ukawafanyia huo ujinga ujinga aisee....watajilipua wenyewe na kukulipua wewe.

Unakumbuka jinsi UKUTA ulivyochimbiwa biti na hatimaye ukaishia kuporomoka wenyewe?

Kwa kweli saa ingine hata sisi wananchi ni wa kulaumiwa kwa kuwaendekeza hawa viongozi.

Sisi wananchi tupo wengi mno kushinda hayo majeshi yao, tupo wengi kushinda usalama wa taifa, tupo wengi kushinda CCM.....lakini tunavyopelekeshwa sasa....

Hata sisi kwa kiasi chetu tunastahili lawama....
 
Sijui hawa jamaa wana mkakati gani na uchaguzi mkuu wa 2020 hususan kwenye upande wa wabunge.

Kulialia kuhusu sheria mbaya hakutobadilisha sheria mbaya kuwa sheria nzuri.

CHADEMA kama kweli wapo serious basi wangeanza sasa kuwaandaa watu wa kugombea ubunge kwenye majimbo yote ya Tanzania.

Mambo ya kuwaachia wagombea wa CCM wapite bila kupingwa halafu mnakuja kulialia baadaye kuwa eti sheria ni mbaya na mnamwomba Magufuli abadili sheria [wakati Magufuli hatungi hizo sheria] ni utoto wa kisiasa.

Anzeni sasa kuwa groom wagombea ubunge na muweke wagombea wenye sifa kwenye kila jimbo.

Msipoweka wagombea mnakosa kabisa hata nafasi ya kushinda. Uchaguzi ulopita kuna majimbo hamkuwa na wagombea ubunge. Aibu.

Msiwaze urais tu. Bunge nalo ni la msingi.
Hata wakiweka mikakati mizuri naamini 2020 wataivuruga tena kwa tamaa za wachache. (gia ya angani)Tunakuwa nao pamoja kwenye kujenga lkn wakioneshwa pesa ni wepesi kututenga wajengaji na kuwakaribisha wabomoaji.
 
Hata chaguzi zilizopita walipata viti mahali na mahali ila walinyang'anywa ushindi the issue is watazuiaje Cruelness ya CCM kuiba kura na pia wajipange kuweka watu sahihi sio waliokatwa uko ndo waje uku au watu wasiojua hata wanapogombea ni wapi
 
Lakini unajua nini Komredi...?

Vipi kuhusu kitu kama ile 'Arab spring'?

Mbona ilimng'oa yule Hosni Mubarak wa Misri na yule Ben Ali wa Tunisia...

Tatizo ninaloliona kuhusu hapa kwetu ni uoga.

Tulio wengi hatupo tayari kupoteza damu zetu, maisha yetu, au hata kutandikwa mijeredi na kupigwa virungu vya polisi katika kudai haki zetu.

Mimi naamini kabisa kuwa mwisho wa siku sisi wananchi tuna nguvu kuliko polisi, jeshi, Magufuli, na CCM.

Tukiamua kuwatoa watatoka tu ingawa pia watu watalipa gharama kubwa sana.

Hebu ona kwa mfano kule Zimbabwe...yaani kile kibabu kinawapeleka puta hadi watu wanaishia kukamata panya ili wamfanye kitoweo lakini cha kushangaza eti bado kipo madarakani!

Hivi kweli unadhani Wazimbabwe wakiamua na kusema sasa basi imetosha...kile kibabu unadhani kitaendelea kuwepo madarakani?

Tatizo letu sisi Waafrika wa huku kusini mwa Sahara wengi wetu tuko waoga sana.

Waarabu huwezi ukawafanyia huo ujinga ujinga aisee....watajilipua wenyewe na kukulipua wewe.

Unakumbuka jinsi UKUTA ulivyochimbiwa biti na hatimaye ukaishia kuporomoka wenyewe?

Kwa kweli saa ingine hata sisi wananchi ni wa kulaumiwa kwa kuwaendekeza hawa viongozi.

Sisi wananchi tupo wengi mno kushinda hayo majeshi yao, tupo wengi kushinda usalama wa taifa, tupo wengi kushinda CCM.....lakini tunavyopelekeshwa sasa....

Hata sisi kwa kiasi chetu tunastahili lawama....
Ewaaa... hapo umesema vema komredi.

Ila mwenzangu uko ughaibuni hii comment haiwezi kukuweka matatani.

Nachelea kusema naiunga mkono kwa maana kesho sichelewi kupelekwa ununio kule wakani-Roma Mkatoliki.

Ulichosema ndio ukweli mtupu. Bila njia hiyo, tutaendelea kubaki na sera zetu za zidumu fikra za mwenyekiti.

Miafrika Ndivyo Tulivyo: Source Usa Baby
 
Kuwa kweli na nafsi yako, unaona dalili au mkakati wowote wa CDM kuongeza majimbo 2020 ?
Ni wazi 2020 CDM wanaenda kupoteza majimbo mengi, na Dsm ndio watakaongoza kwa kupokonywa majimbo, visingizio vitakuwa lukuki ila ukweli ushajulikana.
Kuota ndoto ni haki yako ila usipoteze muda kulazimisha iaminiwe.
Wenzio wanaoogopa hata mikusanyiko yoyote ya upinzani, wanajua vizuri zaidi wanachokiogopa kuliko wewe. Ukienda kuwaeleza haya utanyimwa posho na kufukuzwa uanachama.
 
NN, utaambiwa yote haya ni matatizo ya Magufuli. Kama wakati wa JK hawakuweza kusimamisha wagombea kwenye majimbo yote na wenye kukubalika kivile, wanafikiri wataweza vipi wakati huu wa Magufuli? Na zaidi ya yote, hata wale wabunge wa sasa wenyewe sasa hivi watapata shida sana kuelekea 2020 kwa sababu wameamua kufanya siasa za mapambano na mtu. Angalau kuelekea 2015 tulikuwa tunaonekana tunapambana na fikra fulani na mwelekeo fulani hivi. Sasa hivi kila mpinzani anakotaka kutokea ni "I'm against Magufuli". Hawajui ni sawasawa na kupewa kisu kikali wakaanza kung'ang'ania kila mmoja avute kwa kushika makali!

Mkuu ulivyobadilika inashangaza sana. Sijui kama yale uliyokuwa ukiyapigania miaka yote utayapata kwa utawala huu wa Magufuli hata kwa 10%. Nategemea utarudi tu kuwa mlalamikaji. Muda utaamua.
 
Mzee Mwanakijiji hawa watu hawasaidiki tena kwa sasa, Majimbo mengi walishinda kutokana na kura za chuki dhidi ya CCM na si ubora wa wagombea wao, ila upepo umeshabadilika, EL alikuwa na pesa ndefu ya kufanya hamasa na amsha amsha, kwa 2020 hakuna mfanyabiashara atakayeweka pesa yake kwa EL au CDM sababu ni wazi hawana uwezo tena wa kumtoa Magu.
Ni matokeo ya utafiti au porojo za kutafutia posho? Weka hadharani BASI huo utafiti wako.
 
Boss Nyani Ngabu Pale Mwana CCM anaposhauri CHADEMA. Hii ina maana gani? Unaitakia mema Chadema? Umeichoka CCM? Unataka CCM wawe Wapinzani 2020. Bado sijakuelewa Boss.

Ungetaka kuwashauri, anza na Msingi mwenyewe. Washauri Upinzani wote Waungane. Den wasimamishe Mgombea mmoja kwa kila Kijiji, Kata, Mtaa, Wilaya, Mkoa. Kila Mahali ni Mgombea Mmoja tu Vs CCM.

Ukimaliza hapo pia washauri wawe na Mgombea mmoja tu wa Urais. Anayekubalika na kuuzika. Awe damu changa, anayeweza Mziki wa Ngosha. Anayeweza kupiga Push Up. Otherwise 2020 mambo ni yale yale.

Sijui hawa jamaa wana mkakati gani na uchaguzi mkuu wa 2020 hususan kwenye upande wa wabunge.

Kulialia kuhusu sheria mbaya hakutobadilisha sheria mbaya kuwa sheria nzuri.

CHADEMA kama kweli wapo serious basi wangeanza sasa kuwaandaa watu wa kugombea ubunge kwenye majimbo yote ya Tanzania.

Mambo ya kuwaachia wagombea wa CCM wapite bila kupingwa halafu mnakuja kulialia baadaye kuwa eti sheria ni mbaya na mnamwomba Magufuli abadili sheria [wakati Magufuli hatungi hizo sheria] ni utoto wa kisiasa.

Anzeni sasa kuwa groom wagombea ubunge na muweke wagombea wenye sifa kwenye kila jimbo.

Msipoweka wagombea mnakosa kabisa hata nafasi ya kushinda. Uchaguzi ulopita kuna majimbo hamkuwa na wagombea ubunge. Aibu.

Msiwaze urais tu. Bunge nalo ni la msingi.
 
sahihi sana inatakiwa chama kiangalie hili,kingine si kuokoteza ama kutegemea viongozi waliohama chama au kutoka chama tawala kuja kwao kwamba ndo wawe wagombea wakati CDM ina vijana wengi wanaweza kujenga hoja.so ni jukumu lao kwa pamoja kuliangalia na kutafuta viongozi wa ndani katika kila jimbo.
 
Boss Nyani Ngabu Pale Mwana CCM anaposhauri CHADEMA. Hii ina maana gani? Unaitakia mema Chadema? Umeichoka CCM? Unataka CCM wawe Wapinzani 2020. Bado sijakuelewa Boss.

Ungetaka kuwashauri, anza na Msingi mwenyewe. Washauri Upinzani wote Waungane. Den wasimamishe Mgombea mmoja kwa kila Kijiji, Kata, Mtaa, Wilaya, Mkoa. Kila Mahali ni Mgombea Mmoja tu Vs CCM.

Ukimaliza hapo pia washauri wawe na Mgombea mmoja tu wa Urais. Anayekubalika na kuuzika. Awe damu changa, anayeweza Mziki wa Ngosha. Anayeweza kupiga Push Up. Otherwise 2020 mambo ni yale yale.

Mimi ni mwana CCM?

Unaumwa wewe!
 
Je,Tume huru ipo?
Yani mteule wa rais DED ndo anatangaza matokeo ya mwisho ya ubunge!!!


Tume huru idaiwe mapema ccm itoke vinginevyo watanzania mtapata tabu sana.
 
Sijui hawa jamaa wana mkakati gani na uchaguzi mkuu wa 2020 hususan kwenye upande wa wabunge.

Kulialia kuhusu sheria mbaya hakutobadilisha sheria mbaya kuwa sheria nzuri.

CHADEMA kama kweli wapo serious basi wangeanza sasa kuwaandaa watu wa kugombea ubunge kwenye majimbo yote ya Tanzania.

Mambo ya kuwaachia wagombea wa CCM wapite bila kupingwa halafu mnakuja kulialia baadaye kuwa eti sheria ni mbaya na mnamwomba Magufuli abadili sheria [wakati Magufuli hatungi hizo sheria] ni utoto wa kisiasa.

Anzeni sasa kuwa groom wagombea ubunge na muweke wagombea wenye sifa kwenye kila jimbo.

Msipoweka wagombea mnakosa kabisa hata nafasi ya kushinda. Uchaguzi ulopita kuna majimbo hamkuwa na wagombea ubunge. Aibu.

Msiwaze urais tu. Bunge nalo ni la msingi.

Hayo yote uliyosema cdm wanayajua vizur sana. Je unadhan ccm ni wajinga wayakuli hayo unayosema. Ivi unadhan kama Mungu angesimamia uchaguzi uliopita ccm wangekua madarakani leo?
 
Mambo kama haya CDM hawapendi kuambiwa, hauna ofisi za kueleweka na resources zinatumika ovyo kununuliwa Tshirt za 120,000/Tsh unategemea nini?
Unataka kuingia Ikulu huku ukiwa na wabunge 40, ni wazi hata ikitokea miujiza ukaingia Ikulu, waziri mkuu na Spika bado watatoka CCM sababu ndio watakuwa na wabunge wengi bungeni, na wao ndio wataamua wamuondoe lini Rais sababu uwezo na nguvu hizo wanazo.
Hiyo bidii yako ya ushawishi uitumie zaidi huko kwenu. Wingi wenu hauna faida kwa maendeleo ya taifa, mmekalia KUUTUMIA kutuletea sheria na mikataba mbofumbofu halafu kuunda kamati magumashi kuchunguza madhara mloleta wenyewe.
 
""Tulimpokea Lowasa si kwa sababu siyo fisadi bali tunaamnini ataipasua CCM vipande vipande na kutufikisha sehemu ambapo sisi hatuna wagombea""Adui yetu ni CCM siyo ufisadi """

Hizo eti ni sababu zilizowafanya wampokee Mh Lowasa na kumpa heshima ya kugombea urais!!

Sasa sijui Lowasa kawasaidia kweli kuipasua CCM?

Siasa za kilaghai hizi zinairusha nyuma Africa yetu!!

Chadema wanamini MTU siyo chama Chao!!

Sasa wajiandae kwa kipigo kama cha mbwa aliyeiba kipande cha nyama
Hivi mshafukuza wangapi vile? Uchambuzi bado waendelea.
 
Hivi kwa nini kila siku hapa tunaongelea CHADEMA na jinsi itakavyoshindwa uchaguzi lakini hatuongelei sera za CCM na nini wanafanya kumkomboa Mtanzania. Kuna mtu hapa anaweza kunieleza sera za utawala wa Magufuli kwenye kilimo? Je ana mpango gani na hii sekta inayotoa ajira kwa zaidi ya 80 percent ya Watanzania? Kilimo sehemu nyingi duniani kinakuwa subdize na serikali...
 
Back
Top Bottom