CHADEMA na TBC kunani?

CHADEMA na TBC kunani?

twende kazi

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
1,520
Reaction score
461
Nasikitishwa sana kuona wabunge wa CHADEMA hawashiriki katika mijadala inayoendeshwa na television ya taifa (TBC) hususani vile vipindi vya asubuhi.

Sifurahishwi kwa sababu kuna watanzania wengi wana access na station hii na wanahitaji sana michango murua kutoka kwa wabunge machachari wa CHADEMA.

Niwaulize enyi viongozi wa CHADEMA,je mna mgogoro na TBC na nyinyi TBC je mna mgogoro na CHADEMA?Na kama jibu ni ndiyo kwanini msikae mkayamaliza?Hamuwatendei haki watanzania kwa kweli.

Jirekebisheni.
 
Nasikitishwa sana kuona wabunge wa Chadema hawashiriki katika mijadala inayoendeshwa na television ya taifa(TBC) hususani vile vipindi vya asubuhi.Sifurahishwi kwa sababu kuna watanzania wengi wana access na station hii na wanahitaji sana michango murua kutoka kwa wabunge machachari wa Chadema.Niwaulize enyi viongozi wa Chadema,je mna mgogoro na TBC na nyinyi TBC je mna mgogoro na Chadema?Na kama jibu ni ndiyo kwanini msikae mkayamaliza?Hamuwatendei haki watanzania kwa kweli.Jirekebisheni.
TBC ni vilaza, husikute hata ccm ndo inawapa maagizo ya ni kipi kifanyike na ni yupi akifanye.
 
kuna kipindi flani hapo nyuma TBC ilifanya kazi nzuri, walikua objective na walionyesha professionalism angalau kwa kiwango kizuri., lakini lately mimi pia nadhani TBC kwa sasa iko compromised,

na hii haionekani kwa hayo tu lakini hata habari zake mara nyingi hazionyeshi ukweli wote zinatoa half truths mara nyingi na kuonyesha kuegemea upande mmoja., this is never healthy, ni muhimu kwa serikali kujifunza kuzikabili changamoto zote kama zinavyo kuja badala ya kupambana kuiziba midomo inayo kosoa utendaji wake.,
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.
 
Nasikitishwa sana kuona wabunge wa Chadema hawashiriki katika mijadala inayoendeshwa na television ya taifa(TBC) hususani vile vipindi vya asubuhi.Sifurahishwi kwa sababu kuna watanzania wengi wana access na station hii na wanahitaji sana michango murua kutoka kwa wabunge machachari wa Chadema.Niwaulize enyi viongozi wa Chadema,je mna mgogoro na TBC na nyinyi TBC je mna mgogoro na Chadema?Na kama jibu ni ndiyo kwanini msikae mkayamaliza?Hamuwatendei haki watanzania kwa kweli.Jirekebisheni.

TBS ni ccm. Chadema na ccm hatuwez kukaa pamoja.
 
Baada ya Tido kuondolewa TBC na Mshana kada wa CCM kuingia pale akaona si vyema kuwapa CHADEMA forum wakapata umaarufu dhidi ya chama chake ndipo uhusiano ulipovunjika
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.
Nani anaiangalia siku hizi? Na wakubwa wote wa TBC watashtakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka na mali ya umma we subiri tu
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.

Mjinga kama wewe utasema haya na uwezo wa Lema ila wenye mbwa hawalali kwa uwezo mkubwa alionao Lema wa kujenga hoja na ujasiri unawatisha MaCCM .Sasa wenye mbwa wanajua ila sijui wewe uko Dunia gani .
 
TBC siyo chombo cha taifa ni cha CCM, na hata watendaji wake nasikitika sana watu na weledi zao wanashindwa kusimamia wanaendeshwa na siasa nafikiri ni mambo ya vyeo na njaa zao
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.

Inaheshimika kwa kuwalinda mafisadi na wa uza pembe za ndovu.Mshana 2015 jiandae kwenda segerea kwa matumizi mabaya ya chombo cha uma.Tbc ni mali ya uma na siyo ya ccm.Peopleeeeeeeeeee''''''' paka kieleweka hakuna kulala wezee wa mogogoni.
 
kuna kipindi flani hapo nyuma TBC ilifanya kazi nzuri, walikua objective na walionyesha professionalism angalau kwa kiwango kizuri., lakini lately mimi pia nadhani TBC kwa sasa iko compromised,

na hii haionekani kwa hayo tu lakini hata habari zake mara nyingi hazionyeshi ukweli wote zinatoa half truths mara nyingi na kuonyesha kuegemea upande mmoja., this is never healthy, ni muhimu kwa serikali kujifunza kuzikabili changamoto zote kama zinavyo kuja badala ya kupambana kuiziba midomo inayo kosoa utendaji wake.,

Tido ndiye aliyeitengeneza TBC, ameiweka vizuri wanasiasa wakaanza kuingilia utendaji na kumfukuza kazi, sasa hivi TBC kwishnei imebakia TBCCM!
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.


heshima yake iliongezeka maradufu pale walipopiga taarabu bandika bandua wakati meli ilipozama zanzibar. kitendo hicho kiilikuwa cha kishujaa sana na kiliiongezea nchi hii heshima kubwa kimataifa
 
Freeman Mbowe; TBC ni kipeperushi cha ccm.
Mkuu kama sikosei wewe ni kiongozi wa Chadema.Je ni sahihi kwa nyinyi kuendelea kuisusia TBC?Mmeshapima athari zake mpaka saivi?Please,kaeni nao kitako mzungumze yaishe kwa maslahi ya taifa letu.
 
Si TBC na Radio zake zote tu, pia na STARTV na Radio zake nao wamo katika orodha ya vyombo vya habari ambavyo kwa kipindi kirefu sasa vinafanya kazi kimkakati na kipropaganda zaidi na si kwa kuzingatia weledi wa taaluma ya habari/utangazaji. Kuna wakati vituo hivi vinatangaza habari ambazo ni uongo wa wazi na wa mchana kweupe na hasa habari za kisiasa!!Na katika vipindi vyao vya majadiliano ya kisiasa au kiuchumi wanafanya hivihivi,kimkakati zaidi....THIS IS NOT HEALTHY AT ALL.....Na mimi binafsi niseme kwa ukali kabisa kuwa,huu ni ujinga na upambavu mwingine unaopaswa kukemewa na kulaaniwa na wapenda haki wote!. Na je, huu unaweza kuwa ni mkakati wa serikali ya CCM kuhakikisha hivi vituo vya Tv(TBC na STARTV) ndo vinakuwa accessible kwa watu wote zaidi kuliko vingine ili wavitumie kufanikisha mikakati yao ya kisiasa??.......Swali hili ni muhimu tujiulize kwa sababu kabla ya kuhamia digitali serikali ilituhakikishia kuwa vituo vyote vya Tv vya kitaifa kwa maana ya TBC,STARTV,ITV,CHANNEL TEN,EATV,(CLOUD Tv?) vingeonakana bure kama free on air channels ili kila mwananchi aweze kupata taarifa muda wote pasipo kulazimika kulipia ile monthly subscription fee ya king'amuzi katika ving'amuzi vyote!!....Lakini hii sidhani kama ilikuwa ni kweli kwa sababu mimi binafsi nina king'amuzi cha DSTV lakini kati ya channels hizo zinazoonekana katika king'amuzi hiki ni mbili tu TBC na STARTV !!
 
Back
Top Bottom