Phillemon Mikael
Platinum Member
- Nov 5, 2006
- 10,590
- 8,718
nasikitishwa sana kuona wabunge wa chadema hawashiriki katika mijadala inayoendeshwa na television ya taifa (tbc) hususani vile vipindi vya asubuhi.
Sifurahishwi kwa sababu kuna watanzania wengi wana access na station hii na wanahitaji sana michango murua kutoka kwa wabunge machachari wa chadema.
Niwaulize enyi viongozi wa chadema,je mna mgogoro na tbc na nyinyi tbc je mna mgogoro na chadema?na kama jibu ni ndiyo kwanini msikae mkayamaliza?hamuwatendei haki watanzania kwa kweli.
Jirekebisheni.
tbc ni aibu ta taifa....
Sijawahi kuona wakosefu wa weledi kama hawa...
Huwezi kila siku unaandaa vipindi vya mijadala na kuwatenga wabunge wa chama kikuu cha upinzani....sio kosa kuwaalika wengine lakini unapobagua hadi kipofu anaona hiyo ni aibu kabisa ....na ushahidi wa wazi wa uwepo wa mkakati ovu juu ya chama kikuu cha upinzani....
Tbc inaendeshwa kwa kodi za wananchi ....ingekuwa ccm wanatumia televisheni yao sawa....lakini kitendo cha kutumia kodi zetu vibaya hakikubaliki....
Juzi mkutano wa moro wa ccm umehudhuriwa na watu kama elfu moja.....kwenye taarifa ya habari wakasema maelfu ya watu ..hadi yule kaka msomaji wa habari akaona aibu......hapo hapo habari za mikutano ya kisiasa iliyofanywa na chama kingine siku hiyo haikuoneshwa...aibu...
Ziara ya kinana ilikuwa na coverage kwa siku zote kwa kodi zetu!!!
Huyo ndio clement mshana .....zoba..au boya la tbc...ni wazi tido mhando au suzane mongy asingekubali haya!!