Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 18,081
- 12,235
Ndugu zangu Watanzania,
Chama kikuu cha upinzani hapa Nchini CHADEMA kinapokea Ruzuku kutoka serikalini ya takribani Millioni 107 kwa Mwezi ambayo ni sawa na Billion 1 na Millioni 284 kwa mwaka. Yaani:
107,000,000 x 12= 1,284,000,000/=.
Ambapo hata hivyo CHADEMA inasema kiasi hicho ni kidogo sana ukilinganisha na mahitaji na matumizi ya chama. Hiyo ni kwa mujibu wa John Mrema ambaye anasema pesa hiyo haitoshi na haiwatoshi.
Anasema ni ndogo kwa sababu chama kina ofisi ya makao makuu Dar es salaam, makao makuu ndogo Zanzibar pamoja na ofisi 10 za kanda ambazo zina waajiriwa rasmi wanaolipwa mishahara.
Swali linalokuja kwangu na ambalo ningependa kuwauliza CHADEMA ni kuwa kama Million 107 kwa mwezi ni ndogo. Je, CHADEMA walitaka walipwe shilingi ngapi ambazo ndio wataona ni nyingi? Mbona wakati wanapokea nyingi hususani 2015-2020 walipokuwa na wabunge wengi napo hawakuwahi kusema kuwa wanapokea nyingi na badala yake tuliona ofisi za chama huku mikoani zikiwa zimechoka sana na hali mbaya sana.
Hali ambayo ilionyesha na kutoa ishara ya kuwa ofisi hizi zilikuwa hazipati pesa au pesa zilikuwa hazifiki katika ofisi hizi. Lakini ikumbukwe kuwa pamoja na kupokea kwake Ruzuku kubwa bado wabunge wake nao walikuwa wakikatwa pesa kila Mwezi kuchangia chama. na ajabu zaidi ikifika wakati wa uchaguzi wagombea wake wa ubunge wamekuwa wakikabiliwa na ukata mkubwa sana wa kifedha na kupelekea kusuasua kwa kampeni.
Lakini pia kama CHADEMA inaona pesa hizo ni ndogo jambo ambalo linaweza kuwa kweli katika kujiendesha kitaasisi. Je, imefanya mikakati gani na mipango gani kuwekeza katika miradi ya chama itakayokiingizia na kukiongezea chama kipato? Miradi ya chama ipo wapi? Kwanini chama hakina miradi wakati kimepokea pesa nyingi sana kwa miaka kadhaa iliyopita?
Ikumbukwe ya kuwa pamoja na kupokea pesa kwa wingi lakini chama hakina hata tu kituo cha Tv au hata redio .yaani CHADEMA nzima inazidiwa maarifa na uthubutu na wasanii kama Diamond aliye na kituo cha Tv pamoja na Redio. Inazidiwa hadi na Millard Ayo.
Unaweza kuona udogo wa mawazo kiliyo nayo chama hiki. Maana jambo kubwa linaanza kujengwa katika fikira kwanza yaani kichwani. Lakini chama hiki cha CHADEMA hakina fikira kubwa kichwani mwake za kujiongezea kipato kupitia miradi na vitega uchumi vyake na badala yake kinategemea kikinge mikono kutoka kwa serikali hii hii ya Jemedari wetu shupavu na imara Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
Ili sasa wakalipane mishahara na posho nene nene halafu wanarudi wanasema pesa ni kidogo na wakati mwingine wanaitukana na serikali inayowapa shibe na jeuri. CHADEMA hata wapewe kuongoza nchi kwa wiki moja kazi wanayoweza kuifanya ni kukomba na kukausha pesa zote hazina kama nyasi zilizopigwa dawa ya glamakisoni.
CHADEMA ni chama kisicho na ubunifu wala mikakati wala mbinu, wala njia ya kukiongezea na kutunisha mfuko wa pesa. Na lazima ifahamike ya kuwa siasa inahitaji uchumi ,chama kinahitaji kiwe na misuli ya kiuchumi na kifedha kwasababu huwezi kueneza chama kama huna pesa.
Kama huna pesa utashindwa hata kulipia ofisi wilayani na kwenye kata huko, kama ambavyo tumeshuhudia CHADEMA ikikosa ofisi ngazi hizo na pale ambapo zipo unakuta zimefungwa na kubaki maandishi nje tu, kwa sababu ya kukosa kodi ya nyumba ambayo unakuta ni ndogo tu lakini chama kimeshindwa kulipia, mpaka wenye nyumba wanaamua kuweka makufuri juu ya makufuri.
Naweka kalamu yangu chini.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Chama kikuu cha upinzani hapa Nchini CHADEMA kinapokea Ruzuku kutoka serikalini ya takribani Millioni 107 kwa Mwezi ambayo ni sawa na Billion 1 na Millioni 284 kwa mwaka. Yaani:
107,000,000 x 12= 1,284,000,000/=.
Ambapo hata hivyo CHADEMA inasema kiasi hicho ni kidogo sana ukilinganisha na mahitaji na matumizi ya chama. Hiyo ni kwa mujibu wa John Mrema ambaye anasema pesa hiyo haitoshi na haiwatoshi.
Anasema ni ndogo kwa sababu chama kina ofisi ya makao makuu Dar es salaam, makao makuu ndogo Zanzibar pamoja na ofisi 10 za kanda ambazo zina waajiriwa rasmi wanaolipwa mishahara.
Swali linalokuja kwangu na ambalo ningependa kuwauliza CHADEMA ni kuwa kama Million 107 kwa mwezi ni ndogo. Je, CHADEMA walitaka walipwe shilingi ngapi ambazo ndio wataona ni nyingi? Mbona wakati wanapokea nyingi hususani 2015-2020 walipokuwa na wabunge wengi napo hawakuwahi kusema kuwa wanapokea nyingi na badala yake tuliona ofisi za chama huku mikoani zikiwa zimechoka sana na hali mbaya sana.
Hali ambayo ilionyesha na kutoa ishara ya kuwa ofisi hizi zilikuwa hazipati pesa au pesa zilikuwa hazifiki katika ofisi hizi. Lakini ikumbukwe kuwa pamoja na kupokea kwake Ruzuku kubwa bado wabunge wake nao walikuwa wakikatwa pesa kila Mwezi kuchangia chama. na ajabu zaidi ikifika wakati wa uchaguzi wagombea wake wa ubunge wamekuwa wakikabiliwa na ukata mkubwa sana wa kifedha na kupelekea kusuasua kwa kampeni.
Lakini pia kama CHADEMA inaona pesa hizo ni ndogo jambo ambalo linaweza kuwa kweli katika kujiendesha kitaasisi. Je, imefanya mikakati gani na mipango gani kuwekeza katika miradi ya chama itakayokiingizia na kukiongezea chama kipato? Miradi ya chama ipo wapi? Kwanini chama hakina miradi wakati kimepokea pesa nyingi sana kwa miaka kadhaa iliyopita?
Ikumbukwe ya kuwa pamoja na kupokea pesa kwa wingi lakini chama hakina hata tu kituo cha Tv au hata redio .yaani CHADEMA nzima inazidiwa maarifa na uthubutu na wasanii kama Diamond aliye na kituo cha Tv pamoja na Redio. Inazidiwa hadi na Millard Ayo.
Unaweza kuona udogo wa mawazo kiliyo nayo chama hiki. Maana jambo kubwa linaanza kujengwa katika fikira kwanza yaani kichwani. Lakini chama hiki cha CHADEMA hakina fikira kubwa kichwani mwake za kujiongezea kipato kupitia miradi na vitega uchumi vyake na badala yake kinategemea kikinge mikono kutoka kwa serikali hii hii ya Jemedari wetu shupavu na imara Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
Ili sasa wakalipane mishahara na posho nene nene halafu wanarudi wanasema pesa ni kidogo na wakati mwingine wanaitukana na serikali inayowapa shibe na jeuri. CHADEMA hata wapewe kuongoza nchi kwa wiki moja kazi wanayoweza kuifanya ni kukomba na kukausha pesa zote hazina kama nyasi zilizopigwa dawa ya glamakisoni.
CHADEMA ni chama kisicho na ubunifu wala mikakati wala mbinu, wala njia ya kukiongezea na kutunisha mfuko wa pesa. Na lazima ifahamike ya kuwa siasa inahitaji uchumi ,chama kinahitaji kiwe na misuli ya kiuchumi na kifedha kwasababu huwezi kueneza chama kama huna pesa.
Kama huna pesa utashindwa hata kulipia ofisi wilayani na kwenye kata huko, kama ambavyo tumeshuhudia CHADEMA ikikosa ofisi ngazi hizo na pale ambapo zipo unakuta zimefungwa na kubaki maandishi nje tu, kwa sababu ya kukosa kodi ya nyumba ambayo unakuta ni ndogo tu lakini chama kimeshindwa kulipia, mpaka wenye nyumba wanaamua kuweka makufuri juu ya makufuri.
Naweka kalamu yangu chini.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.