CHADEMA na TBC kunani?

CHADEMA na TBC kunani?

TBC haina viwango vya kuitwa tv station na wala haina viwango vya kutazamwa na watu timamu, ile labda watoto na wale wanaochek tamthilia tu, kwanza ni ya chama halafu watangazaji hamna kitu na hata rang na habari zao ungese mtupu, mi huwa napta tu au kutazama komedi na tena nitaifuta kabisa.
 
Chadema ni wendawazimu hawana maadili.
Hawana UKWELI wala UHAKIKA wa wanayoyafanya.
Wataishia itv na gazeti la nipashe.
 
TBC haina viwango vya kuitwa tv station na wala haina viwango vya kutazamwa na watu timamu, ile labda watoto na wale wanaochek tamthilia tu, kwanza ni ya chama halafu watangazaji hamna kitu na hata rang na habari zao ungese mtupu, mi huwa napta tu au kutazama komedi na tena nitaifuta kabisa.
Mkuu kuna maeneo mengine nchi hii wanakamata TBC tu.Vipi ungetamani waendelee kusikiliza huo ungese tu?Nafikiri tunahitaji kufanya mabadiliko tukiacha hali hii kuendelea athari zake ni kubwa sana.
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.

Mbona unawatukana watu wote wa Arusha pamoja na majaji walioona kuwa Lema ni mbunge halali wa Arusha. Mbunge halali maana yake akili yake imetokana na makuzi mazuri ndio maana watu wakamkubali. Wewe vipi, nahisi wewe ndio una matatizo. Vyama vyote vya siasa vina nafasi sawa mbele ya Katiba ya nchi. Vina stahili sawa katika matumizi ya vyombo vya umma maana wanachama wote kwa ujumla wao ndio walipa kodi inayowezesha huduma zote za umma kufanya kazi. Hili la TBC kufanya ubaguzi wa wazi kwa kuwatenga Chadema, ni kitendo cha ukosefu wa hekima na busara ya kiuongozi ambayo mwisho wake inaweza kuwageukia wenyewe bila kutarajiwa. "Kipimo umpimiacho mwenzako ni kilekile utakachopimiwa wewe wakati ukifika." TBC tafakari hili.
 
tbc ni kama gazeti la uhuru au mtanzania.inafanya kazi kwa maslahi ya nyinyiem.
 
Tbc ni branch ya lumumba wanatuhujumu hasa baada ya kuondoka mh.tiddo muhando.wacha waendelee kuwahoji kina juma nkamia.
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.

wewe acha wehu km lema ana uwezo mdogo wa kufikiri mbona wananch wa arusha walimchagua akawawakilishe? by then km uwezo wake wakufiki ni mdogo mbona report yake aliyoitoa kwa spika km ushahidi wa jinsi waziri mkuu alivosema uongo bungeni haijasomwa? acha dharau.
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.

Ni kweli mkuu,mfano alisema Rais MDINI na ni kinara,alijibiwa vizuri na prf.Mwandosa kuwa jikoni kwa serikali ni Ikulu na Mawaziri wote ni wakristo yani KOMBANI, MKUCHIKA, CHIKAWE ,WASIRA na yeye MWANDOSA,pia Makatibu wote IKULU ni wakristo na kurugezi karibu zote 98% ni wakristo.Sasa Mjinga kama LEMA akaribishwe aseme nini ? na mpumbavu mwenzake NASARI ukimkaribisha anaweza kuendelea na msimamo wake wa kutaka kanda ya kaskazini ijitenge,na MSIGWA anasema Serekali ya wapumbavu,WENJE anasema Serikari ni ya Kikhanisi,Kwa mtazamo wangu ahafadhali MBOE au ZITO,pengine ugeni wa bungeni ni tatizo.
 
TBC inaheshimika sana duniani, haipo tayari kumualika mtu kama Mh. Lema ambaye anaonekana wazi kabisa kwamba uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na malezi yake ya utotoni hayakuwa mazuri.
SUMU---Hauna akili kabisa,wewe ni ------ no.2 after TBC,UNAMLINGANISHA LEMA NA TBC?kwa taarifa yako LEMA NI ZAIDI YA TBC.Hauna ADABU KABISA.
 
uwezo wa muuliza maswali ni mdogo kuliko wabunge wa cdm. 2. wabunge wa ccm uwa wana jazba wakipambanishwa na wa cdm, mfano wasira na mbowe. pia tbc wamepoteza mvuto kwa wananchi, siku hizi kipindi cha asubuhi ni cha chanel ten.
 
Kama utakumbuka vizuri wakati wa maandalizi ya kampeni 2010 kulikuwa na kipindi cha "Harakati Majimboni" kiliendeshwa na Shaban Kissu, kipindi kile ndicho kilichovumbua vipaji vya Watanzania. Tuliwafahamu vizuri sana wagombea. Upande wa pili wa "shilingi" Tido Mhando akaonekana kuwa aliendesha kipindi cha kuimaliza CCM akatemwa.

Leo hii Mwaandaaji wa kipindi hicho cha TBC bila shaka kila kukicha anaomba Mungu asije akatembelewa na Chadema maana ajira yake inaweza kuwa hatarini. Mfano halisi ni hii mikutano ya Chadema huko mikoani hawa wanaoitwa ma-RPC hawapendi kuisikia Chadema mikoani mwao kwani uwepo wao bila kusukwa sukwa itaashiria ma-RPC hao wanaiunga mkono Chadema rejea Daudi Mwangosi kule Nyololo Iringa aliyeuawa mbele ya RPC Michael Kamuhanda.
 
Nilikua sijui kama kuna mtu makini kabisa hua anaangaliaga TBC, anyway labda vipindi vya Bunge lakini otherwise kwangu mimi hua tunangaliga Ze Komedy na chereko basi, vipindi vingine hata sijui hua vikoje na vinarushwa saa ngapi!
 
Kama utakumbuka vizuri wakati wa maandalizi ya kampeni 2010 kulikuwa na kipindi cha "Harakati Majimboni" kiliendeshwa na Shaban Kissu, kipindi kile ndicho kilichovumbua vipaji vya Watanzania. Tuliwafahamu vizuri sana wagombea. Upande wa pili wa "shilingi" Tido Mhando akaonekana kuwa aliendesha kipindi cha kuimaliza CCM akatemwa.

Leo hii Mwaandaaji wa kipindi hicho cha TBC bila shaka kila kukicha anaomba Mungu asije akatembelewa na Chadema maana ajira yake inaweza kuwa hatarini. Mfano halisi ni hii mikutano ya Chadema huko mikoani hawa wanaoitwa ma-RPC hawapendi kuisikia Chadema mikoani mwao kwani uwepo wao bila kusukwa sukwa itaashiria ma-RPC hao wanaiunga mkono Chadema rejea Daudi Mwangosi kule Nyololo Iringa aliyeuawa mbele ya RPC Michael Kamuhanda.
Mmmmmmh
 
kuna kipindi flani hapo nyuma TBC ilifanya kazi nzuri, walikua objective na walionyesha professionalism angalau kwa kiwango kizuri., lakini lately mimi pia nadhani TBC kwa sasa iko compromised,

na hii haionekani kwa hayo tu lakini hata habari zake mara nyingi hazionyeshi ukweli wote zinatoa half truths mara nyingi na kuonyesha kuegemea upande mmoja., this is never healthy, ni muhimu kwa serikali kujifunza kuzikabili changamoto zote kama zinavyo kuja badala ya kupambana kuiziba midomo inayo kosoa utendaji wake.,

na ndicho kilichomponza thido muhando
 
Mkuu kama sikosei wewe ni kiongozi wa Chadema.Je ni sahihi kwa nyinyi kuendelea kuisusia TBC?Mmeshapima athari zake mpaka saivi?Please,kaeni nao kitako mzungumze yaishe kwa maslahi ya taifa letu.

Haina athari kwa kuwa wananchi wengi wanaoiunga mkono CHADEMA ni hohe hahe (wasio na hela ya king'amuzi) na baadhi ya watu ambao hawana hata umeme....wanategemea zaidi magazeti...
Wanaoangalia TBC wengi ni wale wazee wa dar es salaam.
 
Nilikua sijui kama kuna mtu makini kabisa hua anaangaliaga TBC, anyway labda vipindi vya Bunge lakini otherwise kwangu mimi hua tunangaliga Ze Komedy na chereko basi, vipindi vingine hata sijui hua vikoje na vinarushwa saa ngapi!
Mkuu mtu makini ni mtu wa namna gani?Je mtanzania ambaye ana uwezo wa kununua antena ndogo maarufu kama chadema na kukamata TBC tu naye unamweka kundi lipi?Tunahitaji kulizungumzia hili jambo katika uhalisia.Watu wananyimwa haki ya kuwasikiliza wawakilishi wao kwa mapana zaidi.Hili ni tatizo.
 
Back
Top Bottom