Huenda ulikuwa safarini na pia unakaa mbali na vyombo vinginevyo vya habari isipokuwa TBC na washirika wake. Hii ni kwa sababu CHADEMA walipofanya mkutano wao wa uongozi baada ya rabsha zilizotokana na kuzuiwa kwa mkutano wao na kuuwawa kwa Mwangosi, waliitangaza TBC kama janga la taifa na kutangaza kuisusia rasmi ikiwa ni pamoja na kuwataka wapenzi wake na wananchi kwa ujumla kuisusia. Taarifa hizi zilitolewa na vyombo mbalimbali vya habari, ila sina hakika kama TBC na washirika wake walizitoa. Kwa bahati mbaya, kwa kuwa wewe ni mshirika mzuri wa TBC ndio sababu huenda hukupata nafasi ya kufahamu lililokuwa nje ya box. Kwa msingi huo basi, sitegemei kiongozi yeyote wa CDM kushiriki katika jambo lolote lifanywalo na TBC hadi pale chombo hicho kitakapojirekebisha na kuwa cha kitaifa na sio kipeperushi cha CCM (maneno ya Mbowe).
Bahati mbaya, binafsi nilikuwa sinaga mpango kabisa na TBC kama nisivyojua kama RTD bado ipo hewani (Niliachana navyo tokea maigizo ya Mzee Jongo na Jangala).