CHADEMA na mikakati ya kujiimarisha kanda ya Pwani na Zanzibar

Kwa hali ya kisiasa inavyoenda sasa ni wazi kuwa CDM wanazidi kupata umaarufu bara na wanatishia ustawi wa vyama vya CCM na CUF(achilia mbali NCCR,TLP ...). Kutokana na kuwa nguvu iliyonayo CDM ni kubwa mno na inaonesha kuwa wameshindwa kudhibitiwa huku bara, CUF wanaona kuna hatari kubwa ya CDM kuvuka bahari na kuwa na nguvu huko pia, hivyo wanacho kifanya sasa ni kuwajaza maneno ya chuki Wazanzibari kuwa CDM inawachukia, na kuwa kutokana na idadi kubwa ya Wazanzibari kuwa waislam sitoshangaa kama CUF wataanza kusema CDM kina udini. Hii yote ni kulinda maslahi ya CUF visiwanai maana huku bara wameona hawana cha kwao.

Kutokana na kuwepo kwa umoja wa CCM na CUF katika serikali ya Znz kumefanya kutokuwepo demokrasia ya kweli,hakuna mpinzani atakaye ishinikiza serikali kutimiza wajibu wake. Naamini kuwa wapo wengi tu ambao hawakubaliani na vyama hivi viwili. Hivyo basi CDM yaweza kujipanga vizuri ikafanya utafiti na kujua jinsi gani ya kujiimarisha Zanz.
 
ktk marekebisho mapya rais wa jamhuri lazima apate zaidi ya 40% ya kura kwa kila upande wa muungano(tanganyika na zanzibar). hilo limo kwemye dai letu na kwa hapo chadema kamwe hawawi marais nchi hii

Kura walizopata CUF Zanzibar nzima ni sawa na kura za mbunge mmoja wa tu wa CHADEMA pale jimbo la Ubungo Kamanda John Mnyika. sisi Watanganyika zanzibar tunaconsider ni kama jimbo la uchaguzi tu, au kama mtaona tunawaonea tuwe na serikali tatu na kila nchi iwe na vyama vyake, kwa sababu ninavyojuwa mimi CCM sio chama kimoja bali ni muungano wa vyama vya TANU ASP, na HATA cuf sio chama kimoja vilevile bali ni muungano wa vyama vya KAMAHURU cha Maalim Seif na CHAMA CHA WANANCHI cha James Mapalala ndio ikazaliwa CIVIC UNITED FRONT, ila kwa kuwa James Mapalala ni mkristo akafanyiwa njama na mujahidina ambao walishajipenyeza CUF kwa kupitia misikitini na huo ndio ukawa mwisho wa James Mapalala pale CUF. lakini CHADEMA ni chama kimoja ambacho hakina ubia na chama kingine kinasimama chenyewe kwa miguu yake.
Ushauri badala ya kukimbilia kuja hapa JF kupost rubbish topics, ningeshauri tufunguwe websit nyingine tujifunze kupitia internet mambo ya political sience then tutakuwa ma analyst wazuri, kuliko kuja kuongea shombo hapa jamvini.
 
Hivi vyama vyote vina unafiki na uzandizi,not good for Tanzania.While their constitution and leaders won't admit,it's obvious there's some religious affiliation when it comes to CDM and CUF.
We've heard about local churches siding with chadema and always heard "Takbirr!!" wheneva lipumba passes by!.May be CCM is playing games with yall but so far these two parties stink!!
The union sux big time and when Tanganyika is back,we will start a whole new party that represents most Tanganyikans ideas!!!...not CDMor CUF.
Mkuu....unahakika na unachokisema dhidi ya Chadema?.....Labda ungeniambia CUF maana wao iko wazi kabisa. Hivi wewe unazijua propaganda za CCM au unazisikia tu? Sasa anzisha chama chako cha siasa alafu kiwe na mvuto na jamii alafu utajua CCM ni mnyama au binadamu. Tafakari....
 
Mimi ninavyoona CDM iendelee na mwendo wake wa ukombozi kwa nguvu zote, Hii itasaidia kupoteza sumu ya CUF, isisahaulike kuwa CUF huku bara wameshaona hawana chao tena ndio maana wanatumie hadi nguvu haramu kuhakikisha CDM haiwachukulii wapenzi wake km ilivyowafanyia huku bara, Pia natoa angalizo kwa nyie wazenji msitegemee CDM itajikomba kwa CUF ili iwaridhishe nyie wanachama wa CUF kwa kuwa hata ikifanya hivyo mtaendelea kuwa wana-CUF tu.
 
Kura walizopata CUF Zanzibar nzima ni sawa na kura za mbunge mmoja wa tu wa CHADEMA pale jimbo la Ubungo Kamanda John Mnyika. sisi Watanganyika zanzibar tunaconsider ni kama jimbo la uchaguzi tu, au kama mtaona tunawaonea tuwe na serikali tatu na kila nchi iwe na vyama vyake, kwa sababu ninavyojuwa mimi CCM sio chama kimoja bali ni muungano wa vyama vya TANU ASP, na HATA cuf sio chama kimoja vilevile bali ni muungano wa vyama vya KAMAHURU cha Maalim Seif na CHAMA CHA WANANCHI cha James Mapalala ndio ikazaliwa CIVIC UNITED FRONT, ila kwa kuwa James Mapalala ni mkristo akafanyiwa njama na mujahidina ambao walishajipenyeza CUF kwa kupitia misikitini na huo ndio ukawa mwisho wa James Mapalala pale CUF. lakini CHADEMA ni chama kimoja ambacho hakina ubia na chama kingine kinasimama chenyewe kwa miguu yake.
Ushauri badala ya kukimbilia kuja hapa JF kupost rubbish topics, ningeshauri tufunguwe websit nyingine tujifunze kupitia internet mambo ya political sience then tutakuwa ma analyst wazuri, kuliko kuja kuongea shombo hapa jamvini.
Mkuu Saigon......Hivi ulimsikia Hamadi Rashidi alipokuwa anamwaga sumu jana mkoani Tanga?.....yaani hata aibu hawana! Baada ya kuikosoa serikali ya CCM badala yake wanaishambulia Chadema. Sasa kama huku bara tu'wanamwaga sumu namna hii, Je, huko visiwani?
 
Mkuu....unahakika na unachokisema dhidi ya Chadema?.....Labda ungeniambia CUF maana wao iko wazi kabisa. Hivi wewe unazijua propaganda za CCM au unazisikia tu? Sasa anzisha chama chako cha siasa alafu kiwe na mvuto na jamii alafu utajua CCM ni mnyama au binadamu. Tafakari....
OF COURSE!!...kuhusu unafiki wa CDM tunaweza kuanzisha a whole new thread!! tukadiscuss their flipflopping throughot all these years!....we know CUF has no interest in the mainland so is CDM in the isles!...stop circumlocuting!!
 
ukweli u karibu, CDM ndo chama pinzani kinachojitegemea na sera zake. Na kwa msimamo wake ndo maana ni chama cha umma wa wa tz waliowengi (hata kma zanziba si wengi)!!!
 
OF COURSE!!...kuhusu unafiki wa CDM tunaweza kuanzisha a whole new thread!! tukadiscuss their flipflopping throughot all these years!....we know CUF has no interest in the mainland so is CDM in the isles!...stop circumlocuting!!
Nitajie unafiki mmoja tu wa CDM, kisha niwekee na ushahidi wa huo unafiki.....na isiwe propaganda.
 
Siyo lazima ikubarike huko! Chadema waeza kushinda uchaguzi na kuongoza nchi bila ya kukubarika Zenj!
Mkuu.
Chadema wanaweza kufanya hivyo. lakini wataongoza nchi ipi?
Kuna wanaosema Tanzania ni nchi moja. Kuna wanaosema tanzania ni nchi mbili.
Wewe umekusudia nchi ipi?
 
Wanamtambua kiwete kama rais?
Sasa hii ndiyo nini?....mbona unaleta utoto mkuu? Isitoshe wewe ulibezi sana kwenye udini kwa kusema Chadema ni wadini na wanasapotiwa na wakristo. So mie nilitegemea utaweka ushahidi hapa jamvini unaoonesha kuwa kweli hiki chama ni cha kidini. By the way CDM wanamtambua Kikwete kama Rais aliyewekwa hapo kwa nguvu za NEC na siyo kwa matakwa ya wananchi waliowengi kwa kutumia sanduku la kura.
 
CDM ina wabunge watatu wa viti maalum Zanzibar na ruzuku imeelekezwa kwenye majimbo yote ya visiwani hadi Pemba so wanachama wataongezeka tu,baaa ya kuelimika sio wote ni wajinga
 
CDM ina wabunge watatu wa viti maalum Zanzibar na ruzuku imeelekezwa kwenye majimbo yote ya visiwani hadi Pemba so wanachama wataongezeka tu,baaa ya kuelimika sio wote ni wajinga
Mkuu....hao wabunge wa viti maalum wametokea unguja au pemba? Na je wewe unaona kunadalili za CDM kukubalika Zanzibar?
 
Sasa hii ndiyo nini?....mbona unaleta utoto mkuu? Isitoshe wewe ulibezi sana kwenye udini kwa kusema Chadema ni wadini na wanasapotiwa na wakristo. So mie nilitegemea utaweka ushahidi hapa jamvini unaoonesha kuwa kweli hiki chama ni cha kidini. By the way CDM wanamtambua Kikwete kama Rais aliyewekwa hapo kwa nguvu za NEC na siyo kwa matakwa ya wananchi waliowengi kwa kutumia sanduku la kura.
Utoto?.....kwa hiyo wanamtambua rais,sasa kwa nini waliwalk out? au wamebadilisha mawazo?...huu ni upuuzi na unafiki wa kisiasa you either recognize or you dont!!
 
Kama u-mfatiliaji wa mambo ya siasa si ajabu unaelewa mambo yote yanayoendelea baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Mengi ya mambo hayo ni pale vyama vya CUF,NCCR MAGEUZI,TLP na UDP wanapoungana na chama tawala CCM kuishambulia Chadema kupitia Media na mikutano mbali mbali ya kisiasa ndani ya nchi yetu. Lakini kwenye maneno 10 ya viongozi wa CUF popote wahutubiapo,basi maneno 7 huwa wanaiongelea CDM tu dhidi ya serikali ya Zanzibar na watu wake.

Kama utafatilia kauli za Hamadi Rashidi,Prof Lipumba,Julius Mtatiro nk. basi utagundua hawa watu wanawalisha sumu wanzazibari kwamba Chadema haithamini Zanzibar na watu wake.....maana kila wakiongea utasikia ooooh CDM wanapinga muungano wa hizi nchi mbili,mara CDM wanapinga ccm na cuf kuungana,mara CDM ni wadini, mara CDM ni wahahini,mara CDM ni madictator kama Iddi Amini wa Uganda nk. hawana hata chembe moja ya ushahidi.

Ki ukweli hawa jamaa wanawalisha sumu kali sana wananchi wa Zanzibar juu ya hizi kauli zao za uzushi uzushi dhidi ya Chadema. Swali langu ni -: Hivi Chadema inaweza kukubarika Zanzibar? Kweli CDM inaweza fanya mkutano ZNZ bila kurushiwa mawe na mamluki wa CUF na CCM?


Mkuu.
Sahihi ni kusema vyama vyote Tanzania vinashambuliana na vinamwaga sumu kwa wananchi. CCM ndio kinara, na hivyo ulivyovitaja vimo katika mchezo huu mbaya lakini CHADEMA pia kimo. Wanatupiana madongo kama machizi.

Hili la kukubalika kwa Chadema Zanzibar kwa maoni yangu kama Chadema watakuwa na agenda ambazo ninagusa maslahi ya wazanzibari basi kitakubalika tu..la muhimu ni kujitangaza huko. Niliona video ya Dr. Slaa akiwa kavaa kibaragashia kama Mrema alipohutubia mkutano wa kampeni kule Zanzibar. Alipata wasikilizaji wengi kwa wingi wa watu wa Zanzibar. That was a smart move. Kama Chadema ingeekeza nguvu sawa na wanavyofanya huku bara basi ingekubalika.
Chadema itafute agenda ambazo zina-pin point specifically issues za wazanzibar halafu wazinadi. Kitakubalika. In fact watakuwa wameua hiyo sumu kuwa ni chama cha upande mmoja tu wa nchi au kuwa ni chama cha kidini.

Watu wa Zanzibar wana shida kubwa na maisha magumu kama wakazi wa sehemu yoyote ya Tanzania. Ujumbe wa Chadema wa ugumu wa maisha unagusa watu wote. wanahitaji kufanya hii operasheni "sangara", mtaa kwa mtaa, rafiki kwa rafiki, udugu kwa udugu pia huko zanzibar.
watafanya la maana sana kama watatoa kauli zisizogongana juu ya Zanzibar, muungano na muundo wake na uendeshaji wa muungano. hapo Chadema itawafurahisha wazanzibari na watapata kuungwa mkono. Wako wazanzibari wengi tu ambao wanaona CUF imekuwa goi goi na ambao hawaipendi kabisa CCM. Chadema inaweza kuwa mbadala.
 
CCM haijawahi kukubalika Pemba lakini imeongoza Zanzibar muda wote, vivyo hivyo hata kama CHADEMA haitakubalika Zanzibar, bado uwezekano wa kuongoza Tanzania upo 99.99%.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom