CHADEMA na kichaka cha "vikao halali vya chama"

CHADEMA na kichaka cha "vikao halali vya chama"

Mkuu, haya yanayoendelea yanatokea ndani ya CHADEMA. Ni makosa makubwa kwa CHADEMA kudhani kuwa kila baya linalotokea ndani ya chama chao linatokana na ushawishi au mkono wa ccm

Mkuu bora umeliona hili. Hapa kuna uwezekano mkubwa viongozi wakuu wa CHADEMA wanatumia falsafa ya kusema "kuna mkono wa CCM" ili kuweza kuficha maovu yao na kuwafunga mdomo wale ambao hawapendi mienendo yao.
 
nyie ccm & b7 co ltd...... achaneni na hilo li chadema linawanyonya damu ....hangaikeni na matatizo yetu wananchi achaneni na uzinduzi wa vibanda na barabara km 1.....hatuna maji runing water......wala dawa kuna watu wanakufa kila siku kwa kukosa dawa wakati wanalipa kodi
 
Ni lini ulishawahi kuwa na nia njema na CHADEMA hadi maoni yako yachukuliwe serious kiasi hicho wakati siku zote umeonyesha chuki ya hali ya juu dhidi ya CHADEMA?Acha hila

Ben hivi kwa nini unadhani mimi naichukia CHADEMA????!!Sio mara ya kwanza kusema haya hapa!!!

Kwa kumbukumbu tu mimi sijawahi,sio na wala siwezi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa ili niwe neutral na objective kuwakosoa,kushauri na kuwapongeza wote pale inastahili!!!!

Wewe umesoma na unajua criticisms huwa zinaenda kwa theory yenye mashiko ili kuiboresha, no body bothers to criticize a weak theory!!!! Kwa mtazamo huo jua kuwa we lie down critiques sababu nyie ndio second giant nchini!!!


Hebu jaribu siku moja kuwa msomaji tu humu jukwaan meanwhile umwambie afisa habari afanye yeye.hii kazi unayoifanya for that single day!!!!

Kama utajiridhisha yote yanayoandikwa humu ni hila,ujinga,upumbavu na uzandiki juu ya Chadema zibeni masikio na pamba muendelee na shughuli zenu!!!
 
Karibu vyama vyote vya siasa nchini hususani vile vikubwa vimekuwa vikitumia hoja ya VIKAO HALALI VYA CHAMA kama njia ya kubana wanachama wake kutoa maoni; au labda kwa usahihi, kuwazuia kueleza maovu ya chama. Katika hili, CHADEMA ndo sio wastahimilivu hata kidogo; heri ya CCM wanavumulia wanachama wao katika kile kinachoitwa kutoa habari za chama bila kupitia viako halali vya chama. Kwa bahati mbaya kabisa, wana-CHADEMA wa kawaida nao wameingia kwenye mtego huu, kwamba inapotokea mwana-CHADEMA ameeleza mambo yanayowachukiza viongozi nje ya utaratibu wa kawaida; wana-CHADEMA hawa wa kawaida watakuja juu na kumtuhumu mwenzao kwa kumuita majina mbalimbali ya hovyo hovyo!

Wapenzi, wanachama na mashabiki wa kawaida wa vyama vya kisiasa nadhani wanatakiwa kuamka na kugundua kwamba hiki kinachoitwa kwamba ni VIKAO HALALI VYA CHAMA ni ghiriba tu za viongozi wa vyama hivi ya kutaka yale mabaya ya vyama yasisemwe! Hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA kwa hakika kina jina la kuvutia na ndio maana hata wale wapenzi na wanachama wa kawaida nao wamekuwa wakiimba nyimbo hizi za VIKAO HALALI VYA CHAMA! Hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA ni kama kile kingine kinachoitwa UTAWALA BORA ambao Watanzania wengi tumekuwa tukiupigia upatu bila kufahamu kwamba UTAWALA BORA ni kichaka cha maovu ya viongozi na watendaji mbalimbali! Utawala Bora hauwezi kuwa na manufaaa kwa wananchi ikiwa unakuwa practiced kwenye jamii isiyo na maadili kama ya kwetu!

Sasa turudi kwenye hiki kinachoitwa kwamba VIKAO HALALI VYA CHAMA!! Hivi leo hii tuseme kuna mwanachama ana uhakika kabisa kwamba (say) Dr. Slaa au Freeman Mbowe amefanya ABC; tena jambo la fedheha kabisa! Hivi kweli mwanachama huyo anaweza kuwa na Ujasiri wa kusimama mbele ya VIKAO HALALI VYA CHAMA na kutamka waziwazi maovu hayo? Kama atakuwa na huo ujasiri, ni wanachama wangapi wanaweza kuwa na huo ujasiri wa kumchana LIVE mwenyekiti au katibu wa chama ambao tayari wamesha-prove kwamba hawana uvumilivu dhidi ya maoni hasi!

Kwa upande wangu, sina tatizo na hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA lakini nadhani ni busara watu tukaangalia ni nani wanapaswa kuachiwa kuimba nyimbo hizo! Mwacheni Mbowe, mwacheni Dr. Slaa au watu wengine kama hao waimbe hizo nyimbo za VIKAO HALALI VYA CHAMA kwani kutofanya hivyo ni kuhatarisha nafasi zao kwenye chama! Sitaki kuamini kwamba kutahatarisha uhai wa chama unless kama tunataka kusema CHADEMA ni MBOWE au SLAA! Wakati sioni tatizo kwa akina Mbowe kuimba nyimbo za VIKAO HALALI VYA CHAMA lakini kwa mpenzi, shabiki na mwanachama wa kawaida ambae wala hajui hata viatu anavyovaa Dr. Slaa ni rangi gani au vile vya Mbowe; basi kuimba nyimbo za VIKAO HALALI VYA CHAMA ni uzuzu! Ni uzuzu kwa sababu whether you like it or not; kamwe hutaweza kufahamu ukweli mchungu unaokihusu chama chako kupitia hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA unless if you’re prepared whether for bad or worse, wewe na chama chako tu kama ilivyo kwa Waislamu au Wakristo na dini zao!!

Hawa watu na wanachama wa kawaida nadhani ingekuwa ni busara zaidi kujadili contents za tuhuma kuliko kung’ang’ana na VIKAO HALALI VYA CHAMA ambavyo hata wao wenyewe hawahudhurii! Hili ambalo kwa wana-CHADEMA wanajidanganya kwamba eti ni kutowafumbia macho wasaliti ni ujinga mtupu, sana sana lina-prove ni jinsi gani UONGOZI WA CHADEMA unavyoandamwa na vivuli vya uoga! Swali la VIKAO HALALI VYA CHAMA linatumika kama njia ya kuwaziba watu midomo! Ni ajabu CCM iliyojaa ma-conservatives angalau inavumilia maoni makali ya wananchama wao yanayotolewa dhidi ya chama chao na wakati mwingine dhidi ya viongozi! Hivi ni nani asiyejua kwamba Nape na Samuel Sitta walikuwa on transit kuelekea CCJ? Hata hivyo waliwavumulia…. itakuwa ni ujinga kudhani kwamba uongozi wa juu wa chama na serikali hawakufahamu harakati hizo za akina Sitta!

Kuna Columnist mmoja kwenye gazeti la Raia Mwema anajiita MSOMAJI RAIA! Huyu jamaa huwa anaiponda wazi wazi serikali ya Kikwette! Na kwenye baadhi ya makala zake; huwa anamponda hata JK mwenyewe! Lakini what’s so interesting, MSOMAJI RAIA ni wa ndani katika serikali ya Kikwete; namfahamu! Sasa ikiwa mtu wa kawaida kama mimi nafahamu who’s MSOMAJI RAIA, itakuja kuwa KIkwette mwenyewe ambae amezungukwa na wana-intelejensia kadhaa kila Idara?! Hata hivyo, Kikwete anamvumilia MSOMAJI RAIA!

Huku Uswahilini kuna tabia Fulani imezoeleka kabisa! Unakuta mzazi analetewa mashitaka kwamba kijana wake amedokowa/ameiba mahali, au labda nyumba ya mtaa wa pili. Ni kawaida kukuta wazazi wanakuja juu, mithili ya moto wa kifuu kwamba mtoto wao anasingiziwa; KATU HAWEZI KUWA MWIZI. Wapo wanaofikia kusema hizo ni chuki tu utafikiri mzazi husika huwa anatembea na mwanae kila mahali! Siku wanakuja kutanabahi, anakuja kusikia kwamba Mwanao yupo Jela au kapigwa moto! Wazazi wa aina hii ndo mashabiki wengi wa CHADEMA walivyo! Wakati si Dr. Slaa wala Mbowe wana sifa za kuwa Malaika lakini wapenzi na mashabiki wa CHADEMA wanataka kufanya kama hawa watu ni MALAIKA ambao tunaambiwa huwa hawafanyi makosa!

Lililo wazi ni kwamba, mwanadamu pekee asiyefanya makosa ni MAITI! You’ll never be free of mistakes unless if you’re dead!

Mkuu naona hoja yako ni ya kinadhalia zaidi, ingekuwa vizuri ungeweka na ka_substance kidogo,,, mfano ungetuweka bayana kuwa kwa mtazamo wako hili sakata la Mwigamba halikustahili kufuata VIKAO HALALI YA CHAMA kwa kuwa alichosema kwa mtazamo wako ni halali. Hapa namaanisha kuwa uhalali wa hoja yako utakuwepo tu kama alichosema Mwigamba ni cha kweli.

Maoni yangu ni kuwa kama mtu ana ushahidi wa kitu anachotaka kusema ni bora aseme hadharani bila kufuata vikao halali vya chama kwa kuwa ukweli huweka kila mtu huru. Siungi mkono mtu uko kikaoni na wenzako ambako ndio fursa ya kuwananga hapo hapo lakini unatumia jina bandia kutoa tuhuma unazodhani ni halali kwako. Utawala bora unakiukwa kama anayetekeleza utawala bora hafuati misingi ya uwazi.
 
Mkuu naona hoja yako ni ya kinadhalia zaidi, ingekuwa vizuri ungeweka na ka_substance kidogo,,, mfano ungetuweka bayana kuwa kwa mtazamo wako hili sakata la Mwigamba halikustahili kufuata VIKAO HALALI YA CHAMA kwa kuwa alichosema kwa mtazamo wako ni halali. Hapa namaanisha kuwa uhalali wa hoja yako utakuwepo tu kama alichosema Mwigamba ni cha kweli.

Maoni yangu ni kuwa kama mtu ana ushahidi wa kitu anachotaka kusema ni bora aseme hadharani bila kufuata vikao halali vya chama kwa kuwa ukweli huweka kila mtu huru. Siungi mkono mtu uko kikaoni na wenzako ambako ndio fursa ya kuwananga hapo hapo lakini unatumia jina bandia kutoa tuhuma unazodhani ni halali kwako. Utawala bora unakiukwa kama anayetekeleza utawala bora hafuati misingi ya uwazi.
Kwa wanaojua hulka za akina Slaa na Mbowe hawezi kujiuliza maswali mengi kuhusu alichosema Mwigamba.
 
Na ndivyo inavyostahili kipindi hiki kuliko wakati wowote.Marafiki wa maadui zetu na mifumo yao hawatapata nafasi.

Majenerali wakuu hawabadilishwi katikati ya vita

Kama CCM mna uchungu sana wachukueni mnaowataka wakagombee huko kwenu.Msitupangie aina ya silaha za kuwapiga nazo ninyi.

Mtaishia kulalama tu na kupoteza muda.Hampati kitu.So, go home

Mkuu watu hawaelewi kuwa Demokrasia ya CHAMA inafanyika kwa mujibu wa taratibu za chama na hakuna kitu kibaya kwenye chama kama kiongozi msaliti anaye toa siri za mikakati ya cham kinyume na taratibu kwa kuficha utambulisho wake...kama mtu anaona hawezi kuwa ndani ya CHAMA aondoke kwani uanachama ni hiyari...nakuhakikishia hawawezi kuondoka hata wakitandikwa viboko maana wameajiriwa wafanye hilo wanalolifanya vinginevyo sioni haja ya mtu anayekituhumu chama kuendelea kung`ang`ania kuwa ndani ya Chama hicho hicho anacho kituhumu.
 
Hivi ni kiko gani halali cha chama kilichompa Ben Saanane kazi ua uspy wa chama?

Chadema haiendeshwi kwa vikao wala katiba. Inaendeshwa kwa utashi wa wale walioianzisha.
 
Ben hivi kwa nini unadhani mimi naichukia CHADEMA????!!Sio mara ya kwanza kusema haya hapa!!!

Kwa kumbukumbu tu mimi sijawahi,sio na wala siwezi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa ili niwe neutral na objective kuwakosoa,kushauri na kuwapongeza wote pale inastahili!!!!

Wewe umesoma na unajua criticisms huwa zinaenda kwa theory yenye mashiko ili kuiboresha, no body bothers to criticize a weak theory!!!! Kwa mtazamo huo jua kuwa we lie down critiques sababu nyie ndio second giant nchini!!!


Hebu jaribu siku moja kuwa msomaji tu humu jukwaan meanwhile umwambie afisa habari afanye yeye.hii kazi unayoifanya for that single day!!!!

Kama utajiridhisha yote yanayoandikwa humu ni hila,ujinga,upumbavu na uzandiki juu ya Chadema zibeni masikio na pamba muendelee na shughuli zenu!!!

Critics hukosoa kwa hoja.Tumekua humu JF siku nyingi na kukosoana kwa hoja.Wewe unaweka mipasho na hatred attitude.Unachoandika humu mara nyingi ni hate speech!
 
Hivi ni kiko gani halali cha chama kilichompa Ben Saanane kazi ua uspy wa chama?

Chadema haiendeshwi kwa vikao wala katiba. Inaendeshwa kwa utashi wa wale walioianzisha.

U-spy unatoka wapi?Kwa taarifa yako Kama ni spy basi kila mwanachama wa CHADEMA ni Spy.Haihitaji kikao
 
Critics hukosoa kwa hoja.Tumekua humu JF siku nyingi na kukosoana kwa hoja.Wewe unaweka mipasho na hatred attitude.Unachoandika humu mara nyingi ni hate speech!


Ha ha haaaa nilikuambia attitude yako inakuongoza vibaya!!!!!!!

Kwenye siasa zenu hoja huwa ni ile tu inayoendana na interest zenu sio????!!!! Kinyume cha hapo ni hatred speech na mipasho???!!!!! Uko sahihi sana!!!!

Nimekushauri hii mipasho na hatred speech za humu Jf achaneni nazo!!!!!!

All the best
 
Mkuu naona hoja yako ni ya kinadhalia zaidi, ingekuwa vizuri ungeweka na ka_substance kidogo,,, mfano ungetuweka bayana kuwa kwa mtazamo wako hili sakata la Mwigamba halikustahili kufuata VIKAO HALALI YA CHAMA kwa kuwa alichosema kwa mtazamo wako ni halali. Hapa namaanisha kuwa uhalali wa hoja yako utakuwepo tu kama alichosema Mwigamba ni cha kweli.

Maoni yangu ni kuwa kama mtu ana ushahidi wa kitu anachotaka kusema ni bora aseme hadharani bila kufuata vikao halali vya chama kwa kuwa ukweli huweka kila mtu huru. Siungi mkono mtu uko kikaoni na wenzako ambako ndio fursa ya kuwananga hapo hapo lakini unatumia jina bandia kutoa tuhuma unazodhani ni halali kwako. Utawala bora unakiukwa kama anayetekeleza utawala bora hafuati misingi ya uwazi.
Mkuu wangu kama ungenisoma vizuri ugegundua kwamba mimi siku-base suala la Samson Mwigamba bali nilichoangalia sana ni hii tabia ya viongozi wetu kutumia visingizio kama Katiba, Vikao Halali vya Chama and the like kama DEFENSIVE MECHANISM! HIZI ni ghiriba tu ambazo zimeenezwa kwenye Nyanja mbambali za jamii tangu enzi na enzi lakini lengo kuu likiwa ni kuwaziba midomo wana-jamii. Ni ghiriba ambazo zipo karne kwa karne, hazipo kwenye siasa pekee! Ghiliba za aina hii zipo kwenye masuala ya dini hadi kimila! Muislamu akihoji sana mambo ya dini yake ataambiwa anakufuru, Mkristo akihoji sana ataambiwa amepandwa na mapepo; na kama ni Mlokole ataambiwa "Ashindwe kwa Jina la Yesu!" Full ujanja ujanja kila mahali. Na hakuna shaka kabisa kwamba ni jamii yenye kuzing'amua ghiriba kama hizi tu ndizo pekee zinakuwa zenye ustawi bora! Akheri ya dini, tumeyakuta, tumeghiribiwa na tumeufyata! Sote hivi sasa tunaogopa kukufuru tusije kuchomwa moto wa milele! Enzi za utoto wetu ilikuwa tunaambiwa kwamba ukitaka kufahamu jinsi moto wa Jahanamu unavyovuma, basi ziba masikio yako kwa kutumia viganja vya mkono; INATISHA AISEE! Halafu ndo uambiwe utatupwa humo milele!

Haya basi, hayo ya dini tushayakubali, kwani ni nani asiyeogopa moto? Mimi naogopa, wewe je? Sasa hata na haya ya Wanadamu wenzetu bado tuendelee kughiribiwa kwa stahili ile ile; VIKAO HALALI VYA CHAMA, KATIBA na vitu kedekede!! Kwanini kuwe na double standard linapokuja suala la kuheshimu katiba? Sawa, sidhani kama kuna mtu anapinga suala la kuheshimu katiba au matumizi ya vikao halali vya chama! Lakini kama watu wanashindwa kutoa yale wanayoyaamini kupitia vikao halali vya chama; basi hapo kuna tatizo! Wengi wetu tumeishi na baba zetu wakati tukiwa wadogo! Baba mkali na asiye rafiki kwa watoto wake huogopwa na watoto kiasi kwamba mama huwa ndo anatumika kama conduit kati ya watoto na baba!

Lakini kwa upande mwingine, mimi sina tatizo kabisa na uongozi unapojibanza kwenye hoja za katiba na vikao halali vya chama! Kwa lugha ya kiungwana naweza kusema kwamba wana haki ya kujikita kwenye hayo kwa ajili ya maslahi ya chama! Lakini kama utaamua kutojitia upofu utagundua kimsingi si kwa ajili ya maslahi ya chama bali maslahi binafsi! Hata hivyo, wakati sioni tatizo kwa viongozi kujikita kwenye hoja za "vikao halali vya chama" au "kuzingatia katiba," kwa upande mwingine nina matatizo na sisi watu wa kawaida tunaotaka kuimba nyimbo zile zile za viongozi ambazo kimsingi zinalenga tu kuwanasua wao kutoka kwenye shutuma ama tuhuma mbalimbali.

Hapo kwenye RED naungana na wewe mia kwa mia! Lakini kwa upande mwingine tusijitie upofu! Kumtuhumu mtu kama Mbowe au Dr. Slaa si sawa na kumtuhumu mtu kama John Mnyika! Tukubali tu kwamba kuna baadhi ya watu ni untouchable; si tu ndani ya CHADEMA bali kwenye taasisi mbalimbali! Hapa Jamii Forums ku-encourage watu watumie Fake ID si kwamba wanaona Watanzania ni waoga bali walifahamu in advance kwamba huko mitaani na kwenye viti vya kuzunguka/maofisini kuna watu ni untouchable ambao huwezi kuwagusa mchana kweupe! It sounds like cowardly lakini ukweli wenyewe ndo huko hivyo! Wapo wenye ujasiri wa aina hiyo lakini ni wachache; na si ajabu miongoni mwa wale ambao waliwahi kupata ujasiri kama huo si ajabu mwisho wake uligeuka kuwa mbaya! Unless if you're prepared for any worse otherwise u better keep yourself Invisible ikiwa unafahamu kwamba unataka kugusa visivyogusika!!!!!!!!!!!
Jambo la kuzingatia ni kutotumia hiyo invisibility kuleta majungu au tuhuma ambazo hazipo!!
 
Mkuu bora umeliona hili. Hapa kuna uwezekano mkubwa viongozi wakuu wa CHADEMA wanatumia falsafa ya kusema "kuna mkono wa CCM" ili kuweza kuficha maovu yao na kuwafunga mdomo wale ambao hawapendi mienendo yao.
Hapo kwenye RED ni moja ya hoja ambazo huwa zinaniacha hoi sana; "kuna mkono wa CCM!" Kila linalotokea, ni lazima waihusishe CCM as if wanachama na viongozi wa CHADEMA can easily be manipulated or placed a price on top of their integrity!! Kama ulivyosema, hiyo nayo ni aina nyingine ya kuziba watu midomo coz' mtu ukifunguka lazima uonekane umenunuliwa na CCM hata kama hakuna kitu kama hicho!

Lakini kwa upande mwingine hii tabia ya kusukumizia matatizo sehemu nyingine inadhihirisha udhaifu katika uongozi. Kiongozi ni lazima apigane kufahamu chanzo cha matatizo na kuyatafutia ufumbuzi badala ya kukimbilia kutoa majibu mepesi kwamba "hawa wamenunuliwa na CCM!"
 
mkuu tumeona unawamudu vyema ndo maana tunakuacha upambane nao hao buku 7 FC, kiongozi wao Ritz sijui kakimbilia wapi.

Nasema hivi kiongozi aliemaliza muda wa uongozi anahaki ya kugombea na kuchaguliwa tena mradi awe anatimiza mashariti katika cheo kimoja hii iko kwenye ibara moja ya toleo la 2004 mwaka 2006 tulifanya renovation mwaka huo huo tulikubaliana kubadilisha baadhi ya vipengele mimi nilikuwa katibu wa wilaya na hiki kipengele hatukiozungumzia juzi wakati napitia katiba nikitaka kujua kwanini mbowe na zitto wanagombana nikaona hiki kipengelee hakipo, nikasema kwanini hatukuambiwa wajumbe wakati kinaondolewa...MBOWE, ARFI - bara, MOHAMEDI ISSA - zanzibar, DR SLAA, Naibu katibu mkuu MOHAMEDI YUSUF- zanzibar, ZITTO –Bar hawa mimi ndiyo nawapinga kuendelea kugombea.....
 
Ni kifungu Kipi nilichokiuka kikatiba?Mbona tangu nimekua JF hujawahi kuuliza kama mimi ni msemaji wa CHADEMA?Acheni woga.I'm here to stay.Siendi popote na nitaendeleza mapambano hata kama hamtaki

we sio mzima
 
Chadema ni chama makini sana hivo mamuluki mjipange upya
 
NasDaz sidhani kama wanakuelewa

Hitler alianza hivi hivi.....
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, nimetafuta kitufe cha Like sijakiona. Hakina unastahili like yangu na umeongea jambo la maana sana. Yaani siku hizi Ben Saanane ndo amekuwa msemaji wa CHADEMA! Na haya anayojibu yamepitia vikao halali vya chama? Je haya ayasemayo Ben Saanane hayapingani na katiba ya chama?
Ulitaka aisemee CCM chama cha ufisadi na rushwa?
 
masuala ya freedom of speech hayapaswi kujadiliana

watu wanapaswa wawe free kusema anytime,anywhere.....

ukiona chama mtu anadundwa kwa kuongea ujue hakuna siasa hapo
wana run a night club labda
 
Ukitaka kuona umhimu wa ------ basi kalia kichwa uone
 
Back
Top Bottom