CHADEMA na kichaka cha "vikao halali vya chama"

CHADEMA na kichaka cha "vikao halali vya chama"

Ningependa proponents wa hii kitu ya "kubadili uongozi wa juu ubadilishwe" kwa hoja hafifu ya uchaguzi NOW labda wangeweka hoja zao kwenye uzi mmoja mathubuti ili tuzisome, tupime na kufanya maamuzi.

So far nimekuwa nikiona/nikisoma tuhuma zilizosambaa ovyo ovyo tena baaadhi ni za ajabu ajabu tu. Nimeona mara kadhaa hawa "mashabiki wa uchaguzi NOW" wakichukua kipande kimoja hapa na kingine kule kisha kuvipa tafsiri waitakayo!

Nimeshuhudia namna ambayo hoja hizo huwa hazimami wala kufika mbali kwani hazina miguu wala uhai mbele ya ukweli. na
 
Samson Mwigamba ni ama amehongwa au ni mchanga kisiasa!
Yapo mengi ya kuiangusha chadema lakini hayasemwi kwa sasa kwani kiu ya watanzania kwa sasa ni kuiondoa ccm madarakani na sio uongozi wa chadema.Watu aina ya Mwigamba hata kama wana hoja haziwezi kusikilzwa kwa sasa iwe ndani au nje ya chadema.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Nilidhani CDM ni chama makini kumbe ni dhaifu kuliko hata chama cha SAU.....wanaogopana wao kwa wao tena hata kiongozi wa mkoa anawatoa Jasho kwa hoja nzito hadi mnaanda umafia kama wa gaidi mkuu Lwakatare?
Watanzania wameshatambua janja ya cdm kufanya fujo kwani sasa ni dhahiri laana ya kuua watu inafumuka kwa kasi,ndiyo maana wanaogopa kufanya uchaguzi kwani wakiuana Watanzania hawatakionea huruma hata kikifutwa kwa uchochezi na uvunjifu wa amani.
Mbowe hana tofauti na Lipumba au Seif ambao hawana ndoto ya kustaafu au kugombea Urais...

Wasomi makini wapo CCM kuanda sera za kisayansi ili uchaguzi ujao CCM itashinda kwa 90%


ni mtazamo wangu......
Your next Presidaa
 
Na ndivyo inavyostahili kipindi hiki kuliko wakati wowote.Marafiki wa maadui zetu na mifumo yao hawatapata nafasi.

Majenerali wakuu hawabadilishwi katikati ya vita

Kama CCM mna uchungu sana wachukueni mnaowataka wakagombee huko kwenu.Msitupangie aina ya silaha za kuwapiga nazo ninyi.

Mtaishia kulalama tu na kupoteza muda.Hampati kitu.So, go home

Chanaga united usipotetea wakula wapi utakula wewe....ukiwa mnafiki ujanani uzeeni utakuwa mchawi kabisa...sio wewe uliyemchafua ZZK hapa jamvini?? Waislam wanamssemo mmoja katika moja ya aya za Quran Isemayo SEMA UKWELI HATA KAMA UNAUMA
 
Ben, pamoja na kujitahidi kujibu maswali na hoja za wadau humu ndani huku hoja nyingi ukizipinga but they have a point, kuna watu wanaongea ukweli humu but wanashindwa kuuprove ukweli wao kwa kuwa hawana ushahidi mkononi lakini wanaongea kitu ambacho kipo na ambacho jamii inakiona, pamoja na kujitahidi kukitetea chama chako humu, jitahidi pia na kuyafikisha mawazo haya kwa uongozi wako wa juu ya myafanyie kazi.
kumbuka Beni, migogoro ikitumika vizuri itawajenga lakini pia ikitumika vibaya itawabomoa!
kazi kwenu!

Dijovisonjn,

Siku zote nimekua nikifanya haya haya uliyopendekeza.Asante sana kwa kuendelea kunikumbusha
 
Chanaga united usipotetea wakula wapi utakula wewe....ukiwa mnafiki ujanani uzeeni utakuwa mchawi kabisa...sio wewe uliyemchafua ZZK hapa jamvini?? Waislam wanamssemo mmoja katika moja ya aya za Quran Isemayo SEMA UKWELI HATA KAMA UNAUMA

Mnafiki ni wewe unayeleta majungu bila ushahidi
 
Wewe hupiganii taifa lako kwa namna yoyote ile bali upo humu kulinda mkate wako hasa baada ya kuchukua nafasi ya Ludovick. Pia hupiganii chama chako bali unapigania kakikundi kadogo ka viongozi wa juu ambao kwa namna moja au nyingine una nasaba nao au unanufaika kutokana na wao kuwa viongozi

Na mkuu huyu mlinda mkate wake baada ya Ludovick kutemwa wee muache tu werevu wameshamgundua wale bendera fuata mkumbo muda sii mrefu watamgundua na ndio itakuwa mwisho wake time will tell mkuu
 
Karibu vyama vyote vya siasa nchini hususani vile vikubwa vimekuwa vikitumia hoja ya VIKAO HALALI VYA CHAMA kama njia ya kubana wanachama wake kutoa maoni; au labda kwa usahihi, kuwazuia kueleza maovu ya chama. Katika hili, CHADEMA ndo sio wastahimilivu hata kidogo; heri ya CCM wanavumulia wanachama wao katika kile kinachoitwa kutoa habari za chama bila kupitia viako halali vya chama. Kwa bahati mbaya kabisa, wana-CHADEMA wa kawaida nao wameingia kwenye mtego huu, kwamba inapotokea mwana-CHADEMA ameeleza mambo yanayowachukiza viongozi nje ya utaratibu wa kawaida; wana-CHADEMA hawa wa kawaida watakuja juu na kumtuhumu mwenzao kwa kumuita majina mbalimbali ya hovyo hovyo!

Wapenzi, wanachama na mashabiki wa kawaida wa vyama vya kisiasa nadhani wanatakiwa kuamka na kugundua kwamba hiki kinachoitwa kwamba ni VIKAO HALALI VYA CHAMA ni ghiriba tu za viongozi wa vyama hivi ya kutaka yale mabaya ya vyama yasisemwe! Hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA kwa hakika kina jina la kuvutia na ndio maana hata wale wapenzi na wanachama wa kawaida nao wamekuwa wakiimba nyimbo hizi za VIKAO HALALI VYA CHAMA! Hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA ni kama kile kingine kinachoitwa UTAWALA BORA ambao Watanzania wengi tumekuwa tukiupigia upatu bila kufahamu kwamba UTAWALA BORA ni kichaka cha maovu ya viongozi na watendaji mbalimbali! Utawala Bora hauwezi kuwa na manufaaa kwa wananchi ikiwa unakuwa practiced kwenye jamii isiyo na maadili kama ya kwetu!

Sasa turudi kwenye hiki kinachoitwa kwamba VIKAO HALALI VYA CHAMA!! Hivi leo hii tuseme kuna mwanachama ana uhakika kabisa kwamba (say) Dr. Slaa au Freeman Mbowe amefanya ABC; tena jambo la fedheha kabisa! Hivi kweli mwanachama huyo anaweza kuwa na Ujasiri wa kusimama mbele ya VIKAO HALALI VYA CHAMA na kutamka waziwazi maovu hayo? Kama atakuwa na huo ujasiri, ni wanachama wangapi wanaweza kuwa na huo ujasiri wa kumchana LIVE mwenyekiti au katibu wa chama ambao tayari wamesha-prove kwamba hawana uvumilivu dhidi ya maoni hasi!

Kwa upande wangu, sina tatizo na hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA lakini nadhani ni busara watu tukaangalia ni nani wanapaswa kuachiwa kuimba nyimbo hizo! Mwacheni Mbowe, mwacheni Dr. Slaa au watu wengine kama hao waimbe hizo nyimbo za VIKAO HALALI VYA CHAMA kwani kutofanya hivyo ni kuhatarisha nafasi zao kwenye chama! Sitaki kuamini kwamba kutahatarisha uhai wa chama unless kama tunataka kusema CHADEMA ni MBOWE au SLAA! Wakati sioni tatizo kwa akina Mbowe kuimba nyimbo za VIKAO HALALI VYA CHAMA lakini kwa mpenzi, shabiki na mwanachama wa kawaida ambae wala hajui hata viatu anavyovaa Dr. Slaa ni rangi gani au vile vya Mbowe; basi kuimba nyimbo za VIKAO HALALI VYA CHAMA ni uzuzu! Ni uzuzu kwa sababu whether you like it or not; kamwe hutaweza kufahamu ukweli mchungu unaokihusu chama chako kupitia hiki kinachoitwa VIKAO HALALI VYA CHAMA unless if you're prepared whether for bad or worse, wewe na chama chako tu kama ilivyo kwa Waislamu au Wakristo na dini zao!!

Hawa watu na wanachama wa kawaida nadhani ingekuwa ni busara zaidi kujadili contents za tuhuma kuliko kung'ang'ana na VIKAO HALALI VYA CHAMA ambavyo hata wao wenyewe hawahudhurii! Hili ambalo kwa wana-CHADEMA wanajidanganya kwamba eti ni kutowafumbia macho wasaliti ni ujinga mtupu, sana sana lina-prove ni jinsi gani UONGOZI WA CHADEMA unavyoandamwa na vivuli vya uoga! Swali la VIKAO HALALI VYA CHAMA linatumika kama njia ya kuwaziba watu midomo! Ni ajabu CCM iliyojaa ma-conservatives angalau inavumilia maoni makali ya wananchama wao yanayotolewa dhidi ya chama chao na wakati mwingine dhidi ya viongozi! Hivi ni nani asiyejua kwamba Nape na Samuel Sitta walikuwa on transit kuelekea CCJ? Hata hivyo waliwavumulia…. itakuwa ni ujinga kudhani kwamba uongozi wa juu wa chama na serikali hawakufahamu harakati hizo za akina Sitta!

Kuna Columnist mmoja kwenye gazeti la Raia Mwema anajiita MSOMAJI RAIA! Huyu jamaa huwa anaiponda wazi wazi serikali ya Kikwette! Na kwenye baadhi ya makala zake; huwa anamponda hata JK mwenyewe! Lakini what's so interesting, MSOMAJI RAIA ni wa ndani katika serikali ya Kikwete; namfahamu! Sasa ikiwa mtu wa kawaida kama mimi nafahamu who's MSOMAJI RAIA, itakuja kuwa KIkwette mwenyewe ambae amezungukwa na wana-intelejensia kadhaa kila Idara?! Hata hivyo, Kikwete anamvumilia MSOMAJI RAIA!

Huku Uswahilini kuna tabia Fulani imezoeleka kabisa! Unakuta mzazi analetewa mashitaka kwamba kijana wake amedokowa/ameiba mahali, au labda nyumba ya mtaa wa pili. Ni kawaida kukuta wazazi wanakuja juu, mithili ya moto wa kifuu kwamba mtoto wao anasingiziwa; KATU HAWEZI KUWA MWIZI. Wapo wanaofikia kusema hizo ni chuki tu utafikiri mzazi husika huwa anatembea na mwanae kila mahali! Siku wanakuja kutanabahi, anakuja kusikia kwamba Mwanao yupo Jela au kapigwa moto! Wazazi wa aina hii ndo mashabiki wengi wa CHADEMA walivyo! Wakati si Dr. Slaa wala Mbowe wana sifa za kuwa Malaika lakini wapenzi na mashabiki wa CHADEMA wanataka kufanya kama hawa watu ni MALAIKA ambao tunaambiwa huwa hawafanyi makosa!

Lililo wazi ni kwamba, mwanadamu pekee asiyefanya makosa ni MAITI! You'll never be free of mistakes unless if you're dead!


Kila nyumba na utawala wake.Hebu,nieleze katika jamii yetu nani alimvumilia Mfanyakazi wa nyumbani/Housegirl ambaye anatoa siri za nyumbani kwake kwa majirani zake,wafanyakazi wenzake,wakristo wenzake,waislam wenzake,wanasimba wenzake au wanayanga wenzake???
 
magamba mtahangaika sana,hakika cdm ni kiboko yenu taka msitake!pipoz power
 
VIKAO HALALI/HARAMU sehemu pekee ya kujadili mswaada wa katiba ilikuwa bungeni lakini JeiKei kwa busara kabisa aliamua kukaaa meza moja na viongozi wa vyama vya upinzani, pamoja na mapungufu yako ila kwa hilo hongera JeiKei viongozi wengine wa vyama vya siasa igeni yale mazuri ya JeiKei
 
Hoja kuu ya post yangu ni kuwa Ben hayuko jukwaani kuwajibiwa viongozi wake wakuu wa chama hoja zinazoelekezwa kwao..yeye anatoa maoni yake binafsi.

Suala la kusema Ritz na wenzake kuwa si wanachama wakawaida ndani ya chama chao...haihalalishi hoja wanazojibu hapa jukwaani zikiwalenga viongozi wa chama chao kuwa kauli za viongozi wa chama tawala.

Vinginevyo uueleze ulimwengu kupitia JF kuwa Ritz na wenzake ndiyo viongozi wakuu wa Chama cha CCM....



Can we agree to disagree sir???!!!!

So that we save energy for other better uses than to minimize this discussion into a grapivine???!!!!
 
Chama ni chama,na viongozi wake ni binadamu wana mapungufu kwa hiyo kukosolewa sio kitu cha ajabu,kama chadema haitafanya uchaguzi hadi uchaguzi mkuu upite 2015 je endapo ikipewa inchi na watanzania wakati haijajipanga hapo ndio mwanzo wa mgogoro mkubwa zaidi.hivi sasa tu hali iko hivyo je baadae? Kama sasa mwanachama akitoa maoni mambo yanakua hivyo baadae ikipewa ikulu mwanachama akitoa maoni nadhani atakuja wekwa ndani kwa muda usiojulikana kabisa.
 
Kila nyumba na utawala wake.Hebu,nieleze katika jamii yetu nani alimvumilia Mfanyakazi wa nyumbani/Housegirl ambaye anatoa siri za nyumbani kwake kwa majirani zake,wafanyakazi wenzake,wakristo wenzake,waislam wenzake,wanasimba wenzake au wanayanga wenzake???
Kwamba kila nyumba na utawala wake ni jambo lisilo na shaka hata punje, na labda kwa nyongeza tu, hata kwamba kila utawala una sheria na taratibu zake si jambo linalohitaji mjadala; kwavile hivyo ndivyo hasa ilivyo! Kwa bahati mbaya mkuu wangu, naona nawe ni kama umejikita kwenye suala la Mwigamba; anyway, wengi akili zao wameelekeza huko ingawaje nilichosema mimi ni ghiriba ya viongozi wetu kutumia kile kinachoitwa vikao halali vya chama kama njia ya kuwafunga watu midomo! Lakini kwa upande mwingine, sina shida sana na hao viongozi wanaojificha kwenye kichaka cha Vikao Halali Vya Chama pamoja na Katiba; shida niliyonayo mimi ni hawa watu wa kawaida kushabikia nyimbo hizi bila kufahamu nini hasa malengo yake! Wengine ni vijana wadogo lakini huku wakikazana kujifunika gubi gubi kwa koti la Conservative Thinking!

Leo hii Jakaya Kikwete ni Rais wangu! Akitokea mtu ndani ya system akaja JF na Fake ID akasema Mr. President amefanya hili na lile na linaleta sense! Hakika nitakuwa zuzu nikimshutumu huyo mtu na kumwambia ni kwanini hakutumia Vikao Halali! Hayo ya Vikao Halali nitwaachia wahusika! Kama tuhuma zenyewe ni dhidi ya CCM nitawaachia akina Nape au ma-conservatives wengine kama akina Kingunge. Lau kama ni tuhuma ndani ya serikali pia nitawaachia wahusika, ikiwa ni akina Salva au yeyote Yule! Hao wana wajibu wa kufanya hivyo, kwa sababu pamoja na mambo mengine, tuache unafiki, pia watakuwa wanatetea mkate wao wa kila siku! Hakika kama tuhuma zinaleta sense, nitamshukuru huyu Fake ID Users kwa kunisaidia kufahamu ambayo ima faima; nisingeyafahamu! Sasa ikiwa JK angeendelea kugombea, basi uamuzi ungekuwa wangu; kwamba pamoja na yote hayo bado anafaa au vinginevyo!

Lakini kwa upande mwingine ni kwamba, ingawaje I don't abuse the use of Vikao Halali vya Chama na kuheshimu Katiba, lakini ninachosema ni kwamba wanasiasa wamekuwa wakitumia hoja hizo kama DEFENSE MECHANISM! Kama Defense Mechanism coz' wanafahamu ni watu wachache sana au hakuna kabisa watakaokuwa na ujasiri wa kutoa tuhuma mzito mzito mbele ya vikao halali vya chama hata kama kweli tuhuma hizo zipo! Tutake tusitake; kila sekta kuna BIG FISHES; THE UNTOUCHABLE! Na kitu kibaya zaidi ni kwamba, at any possible COURAGEOUS PERSON there's at least ONE BIG FISH behind or around him/her! Kwa mfano, mtu kama Ben Saanane, mie naamini kabisa kwamba he's so Courageous! Lakini hata hivyo; asikudanganye mtu, unaweza kuta Ben huyo huyo akikutana na baadhi ya watu/mtu mwenyewe anaufyata! Anaweza kuwa na ujasiri wa ajabu wa kueleza maovu ya Mr. X lakini asiwe na uthubutu wa kufanya hivyo against Mr. Y! That's to say, TO EVERY COURAGEOUS PERSON, THERE'S AT LEAST ONE BIG FISH AROUND/BEHIND HIM/HER!!!

Sasa yanapotokea mazingira kama hayo, kwamba tuseme mtu ana tuhuma dhidi ya BIG FISHE(S), na ana uhakika kabisa kwamba tuhuma alizonazo ni sahihi lakini hana ujasiri wa kutoa hadharani tuhuma hizo kutokana na uzito wa watuhumiwa! Sasa, ni ama mtu huyu azinyamazie tuhuma au atafute alternative means yak u-expose! Most likely, ikiwa mtu ataamua ku-expose basi wengi wao kama sio wote (pamoja na hawa ambao hapa wanaongelea Vikao Halali) wata-opt kutumia Nick Names kwenye mitandao ya kijamii kama JF! Lakini kwa vile akili yetu inaonekana kuthamini Chama Kwanza, si ajabu wengi wao wakaamua kukaa kimya unless kama tuhuma hizo zinawahusu wapinzani/wahasimu wao!!

Lakini kwa upande mwingine, kumekuwa na matumizi ya double standard linapokuja suala la umuhimu wa vikao halali na kuheshimu katiba! Kwa mfano, hata maoni ya wana-CHADEMA kwenye uzi huu; unakuta ni kama wengi wanaunga mkono suala la akina Mbowe na Dr. Slaa kuendelea kuwa madarakani! To be honest, it's none of my business! Lakini katiba si inasema hawawezi kugombea tena? Maana yake ni kwamba, wakigombea tena itakuwa katiba imebanangwa vibaya mno! Labda jibu jepesi katika hilo supportes watuzungumzia suala la kubadili katiba ili kuwapa extra time!! Watatumia maneno mazuri mazuri na tena yenye busara na hekima tele ili mradi tu kuhalalisha hilo! Wapo watakaosema it'll take a time for the new administration to take off wakati uchaguzi upo njiani; wapo watakaosema makamanda hawabadilishi in the middle of war; lakini yote hayo katu hayatafunika ukweli kwamba hatua kama hiyo itathibitisha mambo makuu mawili, ung'ang'anizi wa madaraka (a form of dictatorship) na ubanangaji wa kutisha wa katiba ile ile ambayo hapa hao hao supportes wanasema inabidi iheshimiwe!
 
Mkuu hapo kwenye number nne wala hawataki kupaongelea....shida ya ccm kwa sasa ni chadema .. Hawashughuliki na chama chao...na ukiangalia kelele nyingi zisizo na maana kuhusu uendeshwaji wa chadema ni za wana ccm au washabiki wa ccm.... Cuf wala hakuna anayewaongelea wakati lipumba.na seif sijui mwaka wa ngapi huu wako kwenye hizo nafasi za kudumu
na ndicho nafikiri alichomaanisha bwana ben saanane , tukiendelea tukisikiliza hizi porojo za humu hawa watu wanalo jambo, nalo ni kutusambaratisha kwa mambo madogo madogo , tujipange na tusonge mbele. bwana ben saanane ni kweli usiopingika kuwa huwezi ukabadili makomandoo katikati ya uwanja wa mapigano , mtashindwa tu na mtarudishwa nyuma kwa hili tutawajua chadema wa kweli na fake , mungu saidia chadema , saidia ukombozi huu tunaoutafuta katika kuikomboa tanzania
 
Chama ni chama,na viongozi wake ni binadamu wana mapungufu kwa hiyo kukosolewa sio kitu cha ajabu,kama chadema haitafanya uchaguzi hadi uchaguzi mkuu upite 2015 je endapo ikipewa inchi na watanzania wakati haijajipanga hapo ndio mwanzo wa mgogoro mkubwa zaidi.hivi sasa tu hali iko hivyo je baadae? Kama sasa mwanachama akitoa maoni mambo yanakua hivyo baadae ikipewa ikulu mwanachama akitoa maoni nadhani atakuja wekwa ndani kwa muda usiojulikana kabisa.
Hapa kuna jambo la ajabu kidogo kutoka kwa miongoni mwa wana-CHADEMA! Inaelekea wengi wao wanaishabikia hali hiyo, kwamba uchaguzi wa ndani usifanyike hadi general election ipite! Kama kawaida yao, wanaipaka mafutaka kauli yao ili mradi tu kuihalalisha; kwamba eti makamanda hawabadilishwi wakati wa vita! Lakini cha kushangaza, hao ni wale wale ambao walimtaka Mwigamba atumie vikao halali vya chama; bila shaka vikao halali kwa mujibu wa katiba huku wakisahau kwamba kutofanya uchaguzi 2014 itakuwa ni kuibananga katiba hiyo hiyo ambayo wanamtuhumu Mwigamba kuivunja! VERY CONTRADICTING!

Anyway, kwa ajili ya maslahi ya chama wanaweza kufanya mabadiliko na kuupa uongozi miaka miwili zaidi! Well and good especially kama wanaamini kwamba hakuna mwana-CHADEMA yeyote mwenye uwezo wa kukivusha chama 2015 but only Mbowe na Slaa! Lakini hili likifanyika, si tu kwamba litaleta mgongano miongoni mwao hususani kwa wale waliokuwa wanataka kugombea( including wafuasi wao) bali pia itachafua image ya uongozi wa juu kwamba ving'ang'anizi wa madaraka!
 
Back
Top Bottom