Nimesoma thread yako kwa umakini sana. Nimepata tafakari ya mambo ma-nne;
1. Vyama vyetu vya siasa vimejaa ubabaishaji, wachache walio na nyadhifa za juu wanaamua kwa makusudi kuhodhi madaraka na kufanya wapendavyo. Hii si tofauti kwa CCM,CDM,CUF au Vyama vingine.
2. Kutokana na taratibu za vyama kuvunjwa na viongozi hawa ambao jambo pekee wanalolijua kwenye katiba zao ni ''Vikao halali'' na ''adhabu kwa wasema ovyo'' wasiotumia vikao halali vya chama, vyama vingi vya kisiasa vimejaa manung'uniko na malumbano ya chini kwa chini
3. Kwa mfumo wa vyama vya siasa vya Tanzania inaonekana wazi kuwa kuna waanzilishi wa vyama ambao pia ni kama wamiliki hawa wana sauti na maamuzi ya mwisho hata kama hiyo itamaanisha kuvunja katiba ya Chama.
4. Wanasiasa wengi kama si wote wamejaa ubinafsi na wakandamizaji wakubwa wa DEMOKRASIANA NI WATU kujitazama wenyewe huku wakijivika tafswira ya kutetea wanyonge. Kwa mfano, kwa nini mtu mmoja abaki kuwa Mwenyekiti wa Chama kadiri apendavyo? Angalia pale CUF - Prof.Lipumba yeye yupo tu siku zote na mwenzake Maalim Seif. Hivi ni kweli kuwa hizi nafasi zinawatosha wao tu?!
Hii ndio sababu itakayochelewesha mabadiliko ya kisiasa kwenye hii nchi yetu.