TEKNOLOJIA
JF-Expert Member
- Jan 6, 2014
- 4,305
- 2,564
Ni muda mfupi tu tangu Madiwani wawili CHADEMA wa Shinyanga mjini watangaze kujiuzulu na kuhamia CCM,Dr Slaa ameibuka na madai mazito kwamba Chama Cha Mapinduzi wamehusika na mchezo mchafu wa kuwanunua Madiwani wake ili kukidhohofisha CHADEMA.
Dr. Slaa alitoa madai hayo wakati akiwa katika za kumnadi Mgombea Ubunge wa Chadema Bi Tendega.Madai ya Dr Slaa yanashangaza kwakweli na inaonyesha ni jinsi gani Viongozi wa juu wa Chama wanavyopenda kutoa kauli nyepesi kuhusiana na matatizo yanayoikabili CHADEMA.
Bahati mbaya sana tatizo hili la Viongozi wa CHADEMA kupenda kuiingiza CCM kila wanapokabiliwa na matatizo ya ndani limeonekana kuwaambukiza Wafuasi wake pia.
Hivi ni nani asiyejua kuwa CHADEMA wamegawanyika japo Viongozi wanatumia nguvu kubwa kuionyesha Dunia kuwa hakuna mgawanyiko wowote?Pamoja na Dr. Slaa kujaribu kuficha hali halisi iliyoko ndani ya Chama lakini mwisho wa siku akaonekana kukiri kiaina kuwepo kwa mgawanyiko pale alipodai milango iko wazi kwa yeyote anayetaka kuhama CHADEMA.
Dr. Slaa unaua CHADEMA.
Dr. Slaa alitoa madai hayo wakati akiwa katika za kumnadi Mgombea Ubunge wa Chadema Bi Tendega.Madai ya Dr Slaa yanashangaza kwakweli na inaonyesha ni jinsi gani Viongozi wa juu wa Chama wanavyopenda kutoa kauli nyepesi kuhusiana na matatizo yanayoikabili CHADEMA.
Bahati mbaya sana tatizo hili la Viongozi wa CHADEMA kupenda kuiingiza CCM kila wanapokabiliwa na matatizo ya ndani limeonekana kuwaambukiza Wafuasi wake pia.
Hivi ni nani asiyejua kuwa CHADEMA wamegawanyika japo Viongozi wanatumia nguvu kubwa kuionyesha Dunia kuwa hakuna mgawanyiko wowote?Pamoja na Dr. Slaa kujaribu kuficha hali halisi iliyoko ndani ya Chama lakini mwisho wa siku akaonekana kukiri kiaina kuwepo kwa mgawanyiko pale alipodai milango iko wazi kwa yeyote anayetaka kuhama CHADEMA.
Dr. Slaa unaua CHADEMA.