CHADEMA, Mshaurini Dr. Slaa abadilike, anakiua Chama!

CHADEMA, Mshaurini Dr. Slaa abadilike, anakiua Chama!

acha ife tu hiyo CHADOMO ya kazi gani..icho nacho chama cha siasa au kampuni binafsi ianyomilikiwa na watu fulani fulani
 
Ni muda mfupi tu tangu Madiwani wawili CHADEMA wa Shinyanga mjini watangaze kujiuzulu na kuhamia CCM,Dr Slaa ameibuka na madai mazito kwamba Chama Cha Mapinduzi wamehusika na mchezo mchafu wa kuwanunua Madiwani wake ili kukidhohofisha CHADEMA.

Dr. Slaa alitoa madai hayo wakati akiwa katika za kumnadi Mgombea Ubunge wa Chadema Bi Tendega.Madai ya Dr Slaa yanashangaza kwakweli na inaonyesha ni jinsi gani Viongozi wa juu wa Chama wanavyopenda kutoa kauli nyepesi kuhusiana na matatizo yanayoikabili CHADEMA.

Bahati mbaya sana tatizo hili la Viongozi wa CHADEMA kupenda kuiingiza CCM kila wanapokabiliwa na matatizo ya ndani limeonekana kuwaambukiza Wafuasi wake pia.

Hivi ni nani asiyejua kuwa CHADEMA wamegawanyika japo Viongozi wanatumia nguvu kubwa kuionyesha Dunia kuwa hakuna mgawanyiko wowote?Pamoja na Dr. Slaa kujaribu kuficha hali halisi iliyoko ndani ya Chama lakini mwisho wa siku akaonekana kukiri kiaina kuwepo kwa mgawanyiko pale alipodai milango iko wazi kwa yeyote anayetaka kuhama CHADEMA.

Dr. Slaa unaua CHADEMA.

We gamba tulia mche ukuingie vizuri. Utazaa tu vitoto vya panya.
 
Ben Saanane. CCM hawaishi vituko, eti adui yao wanaona ni mgonjwa ila wao wako busy kushauri dawa ya kunywa ili apone. Na wanaonyesha hudhuni kubwa usoni eti mgonjwa atakufa tumieni dawa hii. Sasa dawa wanayompatia adui chupa imeandikwa Maji ya Uzima ila ndani iko Dawa ya kumaliza maisha.
Hii ni kama wakati wa maamuzi ya KK juu ya MM watatu ushauri wa huruma ulikuja mwingi tuu na leo kiko wapi?

..... Nalikuwa vitani nikimkabili adui yangu. Nikiwa napanga vikosi, askari wanne watovu wa nidhamu nikawafukuza!. .. Mara adui akataharuki na kusema kwa sauti kuu HAO ULIOWAFUKUZA NDIO ASKARI HODARI KULIKO WOOOTE WALIOBAKI. WARUDISHE KIKOSINI KISHA UJE KUNIKABILI KWA SHAMBULIO KUU!. ... Nalicheka na kumwambia kwa kebehi....FURAHI EE ADUI YANGU KWAKUWA UTANIPIGA NA KUNIANGAMIZA HARAKA SANA PASI NA KUWA NA HAO WASALITI WANNE.
Adui yangu alikasirika na kurarua mavazi yake kwa hasira huku akisema ...UNAUA KIKOSI CHAKOOOO!


Itaendelea.........
 
Last edited by a moderator:
Unahusiana tu


hoja ni ile ile

je Slaa hachoki? hazeeki? hakosei?

kwanini yeye tu? hakuna wengine wanaoweza shika post yake?

wewe kama mtoto wa KIONGOZI WA CCM ( HII NI KUTOKANA NA UTAFITI KWAMBA WATETEZI WA CCM HAPA JF NI WATOTO AU WAKE WA VIONGOZI ) KWANINI USIMUACHE SLAA AIUE CDM BADALA YA KUMTONYA ? ILI NYINYI MUENDELEE KURITHI VYEO VYA BABA ZENU KAMA MTOTO WA MGIMWA !
 
Haya maneno mnayozungumza dhid ya chadema n ya kwenye kanga cdm n nan tangu uhuru cha maana hakuna .. cha msingi chadema washike hatam 2015 chin ya jemedar Dr. Slaa. halafu mambo yakianza kuwa mazur wewe na cdm yako lazima utafute pakujificha.
 
Kwani chadema ikifa si ndo furaha yenu sasa unalalamika nini? Mnawanunua kwa hela halafua mnalalamika eti Dr. Slaa anawalaumu CCM kwa kuwanunua madiwani wake.. Kwani ni uongo?

Hawa wa Shinyanga ------------ na Masele, sasa jamaa sijui wanabisha nini?
 
wachumia tumbo huwa wananunulika wapambanaji huwa wanapambana kufikia malengo hao madiwani ni wachumia matumbo na ni wabinafsi tu
 
Ni muda mfupi tu tangu Madiwani wawili CHADEMA wa Shinyanga mjini watangaze kujiuzulu na kuhamia CCM,Dr Slaa ameibuka na madai mazito kwamba Chama Cha Mapinduzi wamehusika na mchezo mchafu wa kuwanunua Madiwani wake ili kukidhohofisha CHADEMA.

Dr. Slaa alitoa madai hayo wakati akiwa katika za kumnadi Mgombea Ubunge wa Chadema Bi Tendega.Madai ya Dr Slaa yanashangaza kwakweli na inaonyesha ni jinsi gani Viongozi wa juu wa Chama wanavyopenda kutoa kauli nyepesi kuhusiana na matatizo yanayoikabili CHADEMA.

Bahati mbaya sana tatizo hili la Viongozi wa CHADEMA kupenda kuiingiza CCM kila wanapokabiliwa na matatizo ya ndani limeonekana kuwaambukiza Wafuasi wake pia.

Hivi ni nani asiyejua kuwa CHADEMA wamegawanyika japo Viongozi wanatumia nguvu kubwa kuionyesha Dunia kuwa hakuna mgawanyiko wowote?Pamoja na Dr. Slaa kujaribu kuficha hali halisi iliyoko ndani ya Chama lakini mwisho wa siku akaonekana kukiri kiaina kuwepo kwa mgawanyiko pale alipodai milango iko wazi kwa yeyote anayetaka kuhama CHADEMA.

Dr. Slaa unaua CHADEMA.

Kawaambia ambaye hataki aondoke!!, aende kwa maccm or ACT sasa unalialia nini?

Kama anaiua CHADEAMA sie tunaona anaijenga, unatokwa na povu la nini?

na bado mpaka mtakubali tu...
 
Unaona unavyozidi kulithibitishia jamvi kuwa mna tofauti ndogo sana na mnyama nyumbu kiakili.

nimetiririka kwa kiswahili, wewe unajibu kwa kibagladesh,

MAHAKAMA:-

USHAHIDI UMEJITOSHELEZA.

Ndoto mbaya sana jamani hili dubwasha hapa juu linaota liko mhakamani huku lenyewe ndo jaji,mwendesha mashitaka,mtuhumiwa halafu eti limeshinda kesi na linashangilia.....duh!
 
dr.slaa ana kadi ya ccm na anailipia, chadema ikifa anarudi zake ccm
 
wewe kama mtoto wa KIONGOZI WA CCM ( HII NI KUTOKANA NA UTAFITI KWAMBA WATETEZI WA CCM HAPA JF NI WATOTO AU WAKE WA VIONGOZI ) KWANINI USIMUACHE SLAA AIUE CDM BADALA YA KUMTONYA ? ILI NYINYI MUENDELEE KURITHI VYEO VYA BABA ZENU KAMA MTOTO WA MGIMWA !


kodi zetu zinatuuma sana
 
CCM wamewanunua ndio. Hata Dr Slaa asingesema ningesema mimi...
Hivi huwezi kutumia kichwa chako kufikiri mawazo mbadala hata siku moja tu!maana always wewe ndo waleee "tunaunga mkono maamuzi ya kamati kuu..."
 
sasa kama Slaa anaua chama si ndio vizuri mfurahi?
 
Back
Top Bottom