Babu hana sera kwa sasa unadhani asema nini jukwaani?
Anakiuaje chama ambacho kilishajifia siku nyingi zilizopita?
Kwa nini watu wenu wengi wanakuwa wananunulika?Kama viongozi wenu wengi wananunulika,mnataka kuwaambia watanzania wasiwe na imani na CDM tena kwani wakishika uongozi wa nchi hii watanunuliwa na kufanya madudu yaleyale tunayoyaona sasa hivi chini ya magamba?Hivi kweli kama ni kweli wananunuliwa na magamba,hamjaweza kupata chanzo chake kweli na kuzuia hii tabia?CCM wamewanunua ndio. Hata Dr Slaa asingesema ningesema mimi...
Ni muda mfupi tu tangu Madiwani wawili CHADEMA wa Shinyanga mjini watangaze kujiuzulu na kuhamia CCM,Dr Slaa ameibuka na madai mazito kwamba Chama Cha Mapinduzi wamehusika na mchezo mchafu wa kuwanunua Madiwani wake ili kukidhohofisha CHADEMA.
Dr. Slaa alitoa madai hayo wakati akiwa katika za kumnadi Mgombea Ubunge wa Chadema Bi Tendega.Madai ya Dr Slaa yanashangaza kwakweli na inaonyesha ni jinsi gani Viongozi wa juu wa Chama wanavyopenda kutoa kauli nyepesi kuhusiana na matatizo yanayoikabili CHADEMA.
Bahati mbaya sana tatizo hili la Viongozi wa CHADEMA kupenda kuiingiza CCM kila wanapokabiliwa na matatizo ya ndani limeonekana kuwaambukiza Wafuasi wake pia.
Hivi ni nani asiyejua kuwa CHADEMA wamegawanyika japo Viongozi wanatumia nguvu kubwa kuionyesha Dunia kuwa hakuna mgawanyiko wowote?Pamoja na Dr. Slaa kujaribu kuficha hali halisi iliyoko ndani ya Chama lakini mwisho wa siku akaonekana kukiri kiaina kuwepo kwa mgawanyiko pale alipodai milango iko wazi kwa yeyote anayetaka kuhama CHADEMA.
Dr. Slaa unaua CHADEMA.
Kwa nini watu wenu wengi wanakuwa wananunulika?Kama viongozi wenu wengi wananunulika,mnataka kuwaambia watanzania wasiwe na imani na CDM tena kwani wakishika uongozi wa nchi hii watanunuliwa na kufanya madudu yaleyale tunayoyaona sasa hivi chini ya magamba?Hivi kweli kama ni kweli wananunuliwa na magamba,hamjaweza kupata chanzo chake kweli na kuzuia hii tabia?
Mnataka kutuaminisha kuwa kila anayetoka CDM basi ni Yuda Iskariote?Kweli mnashindwa kufanya "VETTING" kwa viongozi wenu,mtaweza kufanya "VETTING" kwa viongozi wa taifa kama mkipewa ridhaa ya kuongoza nchi?Mbona CDM ndio wapiga kelele wa kwanza kuwa vyombo vya serikali havifanyi 'VETTING' kwa viongozi mbalimbali wanaoteuliwa?
Kwa nini watu wenu wengi wanakuwa wananunulika?Kama viongozi wenu wengi wananunulika,mnataka kuwaambia watanzania wasiwe na imani na CDM tena kwani wakishika uongozi wa nchi hii watanunuliwa na kufanya madudu yaleyale tunayoyaona sasa hivi chini ya magamba?Hivi kweli kama ni kweli wananunuliwa na magamba,hamjaweza kupata chanzo chake kweli na kuzuia hii tabia?
Mnataka kutuaminisha kuwa kila anayetoka CDM basi ni Yuda Iskariote?Kweli mnashindwa kufanya "VETTING" kwa viongozi wenu,mtaweza kufanya "VETTING" kwa viongozi wa taifa kama mkipewa ridhaa ya kuongoza nchi?Mbona CDM ndio wapiga kelele wa kwanza kuwa vyombo vya serikali havifanyi 'VETTING' kwa viongozi mbalimbali wanaoteuliwa?
sasa kama Slaa anaua chama si ndio vizuri mfurahi?