Mhe. Mbowe akiwa Mbeya alikiri wazi kuwa CHADEMA kwa miaka yote tangu kuanzishwa kwake kimekuwa ni chama cha HARAKATI... Lakini nilifurahi kusikia akiwaomba wenzake kuwa sasa ni wakati wa kukibadili Chama chao kutoka chama cha harakati na kuwa sasa chama cha SIASA.
Sasa ni karibu miezi mitano tangu atangaze na kuwasilisha ombi hili kwa wenzake lakini kwa masikitiko makubwa wenzake mmempuuza mwenyekiti wenu, badala ya kukibadilisha chama sasa mnakifanya cha harakati zaidi mpaka sasa mnapanga na kutekeleza kudhuru watu hasa wasiowaunga mkono.
Kumpuuza Mbowe kwenye wito wake huo ni kifo chenu na hivyo kuathirika kwa demokrasia nchini. Uwepo wenu umeleta joto zuri kwenye siasa na demokrasia nchini ukiachilia mbali vibweka vya baadhi ya viongozi wenu. Lakini nadhani sio tatizo la chama bali la viongozi wachache waliofanya CHADEMA kichaka cha kufichia rangi zao halisi.
MTAKAO CHANGIA PUNGUZENI MAPOVU NA MATUSI MJENGE HOJA.
Nnepi Nauye,
Huna hoja hapa. Hizi lugha za kuwa CHADEMA ni chama cha wana HARAKATI mbona zimezoeleka kwenye masikio ya Watanzania?Hizi ni lugha za chama Twawala, chama cha Mafisadi na Magaidi-CCM kinachoteka,kuumiza na kuwadhuru Watanzania kwa kutaka kuiaminisha jamii ya Watanzania kuwa ni kazi za CHADEMA!!
Bwana Nnepi kiukweli huwezi kuwathibitishia kuwa CDM ni chama cha HARAKATI na huna sababu za msingi za kuthibitisha hilo. Naamini kabisa ndani ya dhamiri yako unajua ukweli kuhusu CHADEMA kuwa si chama cha HARAKATI baali ni chama cha SIASA. kukuthibitishia hilo nakupa mfano ulio hai kuthibitisha kuwa CHADEMA ni chama cha SIASA.Kwa sasa Tanzania tupo kwenye mchakato wa kupata KATIBA MPYA na mchakato huu kubali usikubali UMEANZISHWA NA CHADEMA. Sasa sijui kwa upeo wako finyu bado unaweza kuendelea kung'ang'ania kuwa CDM ni wanaharakati!!!
CHADEMA ni chama cha SIASA kilichosajiliwa kwa mujibu wa sheria na kinafanya kazi za siasa kwa umakini mkubwa kuliko hata CCM yenyewe. Hili liko wazi kabisa hata Bungeni michango ya CHADEMA inaonekana! Ndiyo maana Watanzania wansema kwa sasa Mbunge 1 wa CHADEMA ni sawa na Wabunge 20 wa CCM.
Kinachoonekana hapa ni mkakati uleule wa CCM wa kutaka kuimaliza au kuiua CDM katika miaka 2 kama mlivyotamka kwa kauli zenu wewe,Mwigulu Nchemba na kiongozi wenu mkuu anayejulikana kama Dume la Nyani toka Hifadhi ya Gombe Bwana Steven Masato Wassira. Mmejiwekea makakti huu kwa vile msipoiua na kuimaliza CDM kitawapa shida sana kweny Uchaguzi wa 2015 kama mlivyotolewa kamasi mwaka 2010. Kilichowaokoa ni Tume ya Uchaguzi-NEC na UWT vinginevo CCM msingeliiona Ikulu. Huo ni ukweli mchungu.
Bwana Nnepi hoja zako ni dhaifu sana. Hata hili la kudai CDM inaendeleza uana harakati na kuumiza watu si la kweli hata kidogo. Swala la KUTEKA NA KUUMIZA WATU mnalitengeneza watu wa CCM ukiwemo wewe Nnepi,Mwigulu Nchemba,Steven Wassira mkishirikiana na UWT,kwa maana ua Usalama wa Taifa na siyo Umoja wa Wanawake Tanzania!!
Bwana Nnepi kumbuka kuwa kwa sasa CCM mnapitia wakti mgumu sana katika uhai wenu wa Chama. Hamjawahi kupata challenges(changamoto)katika wakti wowote zaidi ya wakti huu!!Kwamba Watanzania wa sasa siyo wale wa kizazi cha Baba zenu kina Mosses Nauye waliokuwa wakitamba na sera za Chama kimoja. Huo wakti haupo tena. Kwa sasa CCM lazima mjue mna-deal na Watanzania waliokwenda shule na wemye uelewa mkubwa kuliko hata mlioko madarakani!!
Kwa kumaliza niseme kuwa CCM mnapoteza muda wenu kutaka kuichafua CHADEMA. Kinachotokea ni kwamba badala ya kuichafua CDM nyie ndiyo mnazidi kuchafuka zaidi na zaidi. Swala kama la VIDEO YA LWAKATARE LIMEWAACHA UCHI na kujidhalilisha kusikomithilika. Mahakama Kuu juzi imetupilia mbali madai yenu ya Lwakatare wa CHADEMA ni Gaidi wakti nyie na Mwigulu Nchemba mliongea kwa jazba kwenye mikutano na Bungeni huku mkidai kuwa na ushahidi ambao mo tayari kuutoa popote hata Kuzimu(siyo Mbinguni) ikibidi!!!!
Swali langu kwako Bwana Nnepi na Mchembe ni: Je, baada ya Mahakma Kuu kutupilia mbali madai yenu ya Lwakatare kuwa ni gaidi mbona hampeleki huo USHAIHIDI ili kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu???